Neymar afikisha miaka 30 leo. Dunia ya soka bado inamdai huku muda ukiwa unamuacha

Neymar afikisha miaka 30 leo. Dunia ya soka bado inamdai huku muda ukiwa unamuacha

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Neymar Jr mchezaji wa PSG na timu ya taifa ya Brazil, leo ametimiza miaka 30.

Wakati Neymar akisheherekea kutimiza miaka 30 ya kuzaliwa kwake, Dunia ya soka bado ina deni kwake.

Tuliaminishwa na gwiji wa soka wa Brazil Pele kuwa Neymar atakuja kufuta ufalme wa Messi na Ronaldo na atatwaa Ballon D'or za kutosha.

Lakini nikiangalia saa yangu mkononi, naona kabisa muda ukikataa kuhusu kauli ya Pele. Sioni ni kwa namna gani Neymar ambaye ameshachoka na kushuka uwezo kushinda hata hao akina Messi na Neymar.

Neymar ambaye kila ikifika February kwenye hatua ya mtoano ya Uefa Champions League, Neymar ni lazima awe majeruhi au ajitafutie kadi nyekundu ili apate nafasi ya kwenda kuhudhuria birthday ya dada yake huko Brazil.

Happy birthday Neymar, lakini dunia ya soka bado haijafaidi na kujionea kipaji chako licha ya kukimbia Barcelona na kwenda PSG lakini bado umefeli bro!

BA65EEF9-25A3-4685-97AA-8831AD2EE783.jpeg
 
2022 brazil inaenda kuchukua ndoo la dunia kule quatar ,na ndipo imefika zamu ya neymar kuchukua ballon dor
 
Back
Top Bottom