Neymar Jr amekurupuka kwenda PSG

Neymar Jr amekurupuka kwenda PSG

Tatizo wabongo wajuaji sana....mtoa mada maisha yako yote hapa duniani akaunti yako bank haitakuja kusoma salio sawa na mshahara wa Neymar kwa wiki moja,funny enough unamzodoa kwa maamuzi yake juu ya fani yake na kipato chake!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We mleta mada n fala tu
Wa kawaida ukiamka,nawa
Uso ndo uingie jf

[Color= yellow]Triple A[/color]
 
Hii article nimeiona huko fesibuku...muwe mnatoa credit!
 
Haaa haa eti umemshauri kua bora angeenda Manure...[emoji23][emoji23] labda kama kutimiza ya kua mfalme wa kuuza jezi ila ufalme wa soka siku hizi haupatikani pale Manure yaani awe mfalme kwa kubeba EFL na YUROPA duh ni bora amefuata sarafu PSG kuliko wehu wa kwenda Manure maana hata UCL wanaenda kwa kuvizia.
Kila la heri Neymar kacheze soka mafanikio yako yapo miguuni mwako kama ni ufalme iko wazi hapo Barca hata ungebaki isingesaidia wanasema ligue 1 ni dhaifu na mambo kibao nenda kaifanye kua bora ndio ilivyo lazima kuwe na mtu wa kwanza.
 
Sidhani kama amekurupuka ila ki uhalisia NEYMAR kuna kitu anacho kitaka

Amesha chukua makombe tayari ambayo kuna baadhi ya wachezaji wanatamani....NEYMAR kwa mafanikio aliyo yapata Barca yana mtosha ikizingatiwa bado ana umri mdogo.....

NEYMAR anacho taka yeye ni kuonekana kisoka angarau hata siku moja na yeye aje kuwa mchezaji bora wa dunia...

CR7 na Mess wana elekea mwishoni sasa, sasa nani ataye weza kuchukua nafasi hizo ni NEYMAR...Uchezaji wa wake akienda PSG ata fanya vizuri sana tofauti akibaki Barcelona..

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli Neymar angeenda kuwa mfalme km ilivyosema mwisho wa CR7 na MESSI zinaenda ukingon,km angebak Barca kwel Neymar angekuwa bonge la mfalme ktk la liga,ila kitendo cha kwenda PSG labda ni kibiashara zaid si kutegemea kuwa mfalme wa soka dunian km akina CR7 na MESSI.

Ngoja tusubir tuone ufalme wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Miaka mitano ijayo dogo atakuwa na 30. SIJUI UNANIELEWA?
Pale barca lazima awe nyuma ya messi na umri unaenda, ukizingatia hujui kesho yako. Pale hawezi kuwa mfale mbele ya king leo SIJUI UNANIELEWA?
Kwenye mpira wa sasa ni kupata muda wa kucheza, kupata vikombe na mkwanja, angalia madogo kama kina lukaku wanavyogoma kukaa benchi, sababu ni nini? Wanataka wacheze na waache legacy, kama unajitambua utaitafuta kwa njia yoyote SIJUI UNANIELEWA?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta uzi unakadi number ngapi ya Barca
pili Pesa kitu nyingine brother

Kwanini tuna watu kama milioni hamsini na hatuwezi kuipa dunia mtu kama Neymar,, Messi au George Weah , Didier Drogba, Yaya Toure au Kalusha Bwalya. Senegal, Ivory Coast, Mali Ghana na Cameroon wana wana wananchi wadogo kuliko sisi, lakini kila mwaka wanaipa dunia wachezaji wazuri kabisa. Tatizo nini kwetu?
 
Kweli Neymar angeenda kuwa mfalme km ilivyosema mwisho wa CR7 na MESSI zinaenda ukingon,km angebak Barca kwel Neymar angekuwa bonge la mfalme ktk la liga,ila kitendo cha kwenda PSG labda ni kibiashara zaid si kutegemea kuwa mfalme wa soka dunian km akina CR7 na MESSI.

Ngoja tusubir tuone ufalme wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kikosi bora cha barca kwa sasa kinaelekea kufa angalia umri wa wachezaji kina mesi suarez etc.Jamaa kasepa kakwepa lawama ameenda kweny club yenye kiu na mipango kuliko barca.Saivi Madrid kwa laliga ndo inanguvu na itachkua muda kupotea kama miaka kadhaa ilopita.

Neymar kafanya uamuzi wa busara kwa sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amesajililiwa kwa dau La billion 500 ambapo atakua analipwa million 220 kwa siku moja

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio Mkuu,

Moja ya udhaifu wa redio nyingi katika vipindi vya mchezo huwa hawa ibadilishi fedha hiyo katika fedha ya kitanzania.


Sasa huwa nashindwa kuwaelewa wanadhani watu wote wanauelewa wa thamani ya fedha za kigeni,kumbe sio.


Hili inatakiwa walifanyie kazi..kwangu Mimi hizi (£,€ $)kidogo nipo na ulewa wa kutosha.
 
BINAFSI sitamsamehe Neymar. Katika umri wa miaka 25, nyakati unazotamani kuona akielekea juu kabisa ya kilele cha ubora duniani, anachagua kuondoka Barcelona na kwenda PSG.

Kwa mchezaji wa aina yake mwenye uwezo kama wake, unatokaje kirahisi katika ligi bora duniani na kuchagua kucheza Ligue 1, ligi namba 5 kwa ubora barani Ulaya?

Tatizo ni nini? Pesa au ni kweli amechoshwa kuwa nyuma ya kivuli cha Lionel Messi? Labda sababu ya kwanza, vijana wa Amerika Kusini mioyo yao haijapishana sana na Waafrika.

Dhiki kali walizokumbana nazo utotoni zilishaichoma mioyo yao na kuiacha ikiwa na hasira kali ya kimaisha. Ilipo pesa, walipo wao.

Hapa kwenye kukimbia kivuli cha Leo Messi, ndiko kunakonipa shaka kidogo. Hapa Neymar anatudanganya, tena uongo mbaya wenye kukera.

Sikatai, kivuli cha Messi kimemficha sana. Ubora wake hauzungumzwi tena. Neymar yule tuliyemsikia akiwa Santos, si huyu wa sasa tuliyenaye hapa Nou Camp.

Chochote atakachofanya kimeshafanya na Messi tayari. Barca wana mfalme mmoja tu, La Pulga pekee. Kwa alipofika Neymar alitakiwa kuondoka Barca.

Lakini kama kweli sababu ni kusaka ufalme wa soka duniani, Neymar alitakiwa kujiuliza mara mbili, ni wapi anaweza kwenda na kutengeneza ufalme wa dunia?

Unakimbiaje kivuli cha Messi kwa kwenda PSG? Dunia ya sasa inaanza vipi kutoa mfalme wa soka katika ligi dhaifu kama ile ya Ligue 1?

Mtazame Zlatan Ibrahimov. Ni mfalme wa PSG. Ni mfalme wa Paris, ni gwiji wa Ligue 1, lakini yuko mbali na hadhi ya wafalme wa dunia. Neymar analijua hili?

Kwa miaka 10 sasa Ligue 1 imeendelea kuwa ligi kubwa ya kawaida duniani. Haisisimui kabisa. Wachezaji bora hudumu kwa msimu kadhaa kisha huamua kusaka malisho sehemu nyingine.

Eden Hazard amepata heshima aliyonayo baada ya kucheza Premier League. N’golo Kante pia. Hivyo hivyo kwa Riyad Mahrez na Didier Drogba.

Mtazame tena Kylian Mbappe? Pamoja na ubora wake, dunia imekuwa na mashaka naye bado. Wengi hawaamini kama ni mkali kama takwimu zinavyosema. Kwanini? Ni takwimu za Ligue 1.

Watu hawaiamini sana ligi ile, ni ngumu sana kuona akiibuka mfalme wa dunia maeneo yale. Neymar asiendelee kutudanganya. Kivuli cha Messi hakiwezi kufutwa kwa nyota anayevaa jezi ya PSG. Ni uongo huu.

Kama kweli Cristiano Ronaldo alimshauri kufikiria mara mbili kabla hajatoka Barcelona, basi CR7 ni mkubwa sana kifikra katika dunia ya soka ya sasa. Tusishangae anavyozidi kufanikiwa.

Ni klabu mbili tu ambazo Neymar angeweza kwenda na kuupata ufalme anaoutaka. Real Madrid na Manchester United. Lakini tayari Madrid wanaye Ronaldo, chaguo sahihi kwake lilikuwa Old Trafford.

Neymar angeweza kusimama na kugombea ufalme wa dunia akiwa na jezi ya Manchester. Pale ndipo mahala anakoweza kushindana na kina Leo Messi na Ronaldo, si PSG.

Ukweli mchungu unaofichwa na Neymar na baba yake ni huu, kinachowakimbiza Barcelona ni pesa tu. Hizi stori za Ufalme ni uongo tu.

Neymar hana shida na mataji tena, hana shida na tuzo ya Ballon d’Or. Shida yake ni pesa tu. Na kwa PSG amekutana na wendawazimu wa biashara, watampatia.

Tayari kuna ofa ya mshahara wa pauni 500,000 kwa wiki. Atapimwa afya katika hospitali ya kifahari kule Qatar, kisha atatambulishwa pale uliposimama mnara wa Paris maarufu kama mnasa wa Eiffel. Maisha yanataka nini tena zaidi?

PSG wanamhitaji Neymar kibiashara. Hawana shida ya miguu yake, wana shida na sura yake. Neymar ndiye mtu pekee duniani atakayeweza kukaa kwenye matangazo ya ndege zao na wakafanya biashara kubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaezekana hujui ulisemalo ndugu! Pale Barcelona, Neymar ameisha maliza makombe yote, acha aangalie kiwanja kipya tena kwa mkwanja uliovunja rekodi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom