voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,545
- 11,935
Wanabodi JF!,
Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).
Nimefuatilia mijadala mbalimbali ambayo imekuwa ikiendelea kwenye social platforms,takriban muda wa wiki moja na ushei sasa.
Kuna wachangiaji ambao wamegawanyika katika pande mbili tofauti.
Upande mmoja ni wale wanaoitetea jamii ya wamaasai kuendelea kuishi wao pamoja na shughuli zao za ufugaji.
Pamoja na kuendelea kuongezeka ndani ya eneo la hifadhi hiyo kama ilivyo kwa sasa.
Kundi la pili ni wale ambao wanatetea uhifadhi maliasili ya wanyama pori na Ikolojia viumbe hai,vilivyo ndani ya eneo hilo muhimu na maarufu Duniani kwa utalii.
Mimi ninasimama upande wa watetezi wa Mazingira na Maliasili za wanyama pori na uoto wa asili,katika hifadhi ya Ngorongoro.
Ni ukweli usiopingika kwamba eneo hilo limekuwa likikaliwa na jamii ya kabila la kifugaji la wamaasai kwa asili.
Lakini inapokuja suala la uchumi wa kitaifa na pato la taifa kama nchi.
Eneo hilo na mengineyo mengi nchini yanayohusiana na utalii,yanabakia kuwa muhimu kwa upatikanaji wa fedha za kigeni.
Ambazo huingia na kuchangia maendeleo ya nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu na afya ya jamii.
Na hivyo kulifanya eneo hilo kutazamwa kwa maslahi mapana ya kitaifa na kimataifa.
Ikizihusu pia taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa zinazojihusisha na utunzaji mazingira na viumbe hai Duniani.
Ikiwemo UNESCO.
Kuna kundi la watu wamechangia kwa kumshambulia Moja kwamoja #Maulidkitenge.
Kwa ile tu kunyoosha ukweli wake na kutoa maoni yake baada kile alichokishuhudia kule Ngorongoro.
Pia kuna waliochangia kwa kuwa wanatokana na jamii husika zinazokabiliwa na kadhia ya moja kwa moja ya kutakiwa kuhamishwa toka Ngorongoro hifadhini.
Lakini pia kuna wachangiaji ambao wameligeuza suala hili kuwa kama mtaji wao wa kisiasa zaidi.
Na hii niseme kuwa ni kwa maslahi binafsi ya wanasiasa hao.
Na hapa kuna wanasiasa wa pande zote mbili za kisiasa Toka upinzani na chama tawala CCM.
Mimi nachangia kama mtanzania ambaye nimefanyia kazi katika eneo hilo,kwa ukaribu na kwa muda mrefu sasa.
Nimeziona athari zinazoikumba hifadhi ya Ngorongoro katika kila hatua.
Kuongezeka kwa idadi ya wakazi na muingiliano wa shughuli za kiutalii.Ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.
Kwa ujumla ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi au utatuzi wa mapema.kabla halijageuka na kuzaa mgogoro mkubwa baadae.
Endapo tu,halitachukuliwa maamuzi sahihi na kwa wakati stahiki.
Ebu tujiulize kwa kina!
Kama idadi ya wafugaji wa kimasaai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inaongezeka kwa kasi.
Kama ilivyo kwa watanzania wote.
Je inakuwaje kuhusu upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama,Elimu, Zahanati na maji kwa matumizi ya binadamu na mifugo yao?
Katika eneo zima la Ngorongoro. Je kama wakipewa huduma zote na miji yao kutambulika kisheria...kutakuwa na kitu kinaitwa hifadhi ya Ngorongoro?
Ukizingatia kuwa jiografia ya eneo kubwa la Ngorongoro ni lenye kiwango cha chini cha mvua katika msimu wa mwaka mzima na hivyo suala la upatikanaji wa maji inakuwa moja ya changamoto kubwa kuwaathiri wakazi hao pamoja na mifugo yao.
Jambo linaloilazimu mamlaka ya hifadhi kuwasaidia ili kuwanusuru na maafa hayo.
Je, serikali inalo fungu la kuendelea kuwahudumia kwa muda woote,pamoja na idadi yao kuzidi kuongezeka kila uchao?
Je, watetezi wa wafugaji hao wanaelewa kwamba.
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na kupelekea kubadilika kwa mifumo ya maisha katika jamii nyingi.
Na jamii ya wamaasai wakiwa mojawapo ya wahanga wa mabadiliko hayo.
Kutokana na baadhi yao kupoteza kiasi kikubwa cha mifugo yao kutokana na maradhi au tabia nchi.
Imewalazimu pia kuanza kula vyakula ambavyo hapo awali havikukubalika kama chakula rasmi na ilikuwa ni marufuku kwao kuvila.
Ikiwemo Nyama Pori,Samaki na kuku.
Baada ya maisha kuwabadilikia na vijana wengi wa kimaasai kuingia mijini na kuchanganyika na jamii zingine katika jitihada za kutafutia maisha.
Leo hii wamekuwa walaji wakubwa wa vyakula vingi ambavyo hapo awali haikuwa kwenye orodha yao ikiwemo Chips Mayai nk.
Na ni katika mtindo huo,tabia hizi zinaambukizwa taratibu hadi huko kwenye asili zao.
Ngorongoro ikiwa muhanga mojawapo ya eneo husika.
Mifugo Tegemezi .
Tofauti na mifugo kama Ng'ombe,Punda,Mbuzi na kondoo inayofugwa na wamaasai hao wa Ngorongoro (na idadi yao pia ikiongezeka kwakasi).ambayo kiasili wanakula majani sambamba na wanyama wengine wa porini.
Kuna wanyama kama Mbwa ambao wafugaji wanawafuga na kuwategemea kama nyenzo muhimu kwa ulinzi wa mifugo yao,nyakati za usiku dhidi ya wanyama pori walao nyama kama Simba,Chui na Fisi.
Je! wao hao mbwa ambao kila kaya,lazima inawamiliki kwa idadi ya wastani usiopungua mbwa watano kila kaya.
Je, Wanakula nini kila siku ilhali chakula cha maasai wa asili ni mchanganyiko wa maziwa na mahindi almaarufu kama Roshoroo.?
Ambacho si chakula kinacholiwa na hao mbwa wa asili ya wamaasai.
Ikumbukwe kuwa nyama ya mbuzi ambayo huchinjwa na maasai hao mara chache katika maboma yao,huwa ni kidogo kuliko mahitaji rasmi ya kutosheleza jamii husika wakiwemo watoto wadogo.
Jambo ambalo hupelekea mgawanyo usio sawia kati ya wanaume
(Morani na wazee) na upande wa wanawake (kina mama,vikongwe na watoto wadogo).
Hapo humlazimu mbwa kujitafutia riziki zao na watoto wao.
Kwa mbinu asilia za kuwinda wanyama pori kama vile Sungura,Swala, watoto wa nyumbu na punda.
Na saa ingine hadi watoto wachanga wa Twiga.
Tukio ambalo mimi binafsi, niliwahi kulishuhudia na kulitolea taarifa pale Seneto gate kwa maaskari wa Ngorongoro.
Je, Hatujiulizi kwamba kuna idadi ngapi? au kiasi gani cha wanyamapori kinapotea kila mwaka kwa kuliwa na idadi kubwa ya mbwa wanaomilikiwa na wamaasai.?
Wakati tukiwatetea wamasai wa Ngorongoro,pia vema tuelewe kwamba,wao wanaishi pale ndiyo.
Lakini Ngorongoro inabeba maisha ya watanzania wengi kutokana na pato linaloingizwa kupitia sekta pekee ya utalii.
Na hivyo tunapotetea haki ya wamaasai wakaazi wa Ngorongoro kutohamishwa.
Pia ni vema tukumbuke na madhara yanayoweza kupatikana endapo jamii hiyo itaachwa kuzagaa na kuongezeka bila udhibiti sahihi kwa manufaa ya wengi nchini.
Na kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.
Hapo sijaongelea kero zinazowasibu wakazi hao kwa uduni wa maisha kutokana na kutoruhusiwa kulima mazao ya chakula kisheria.
Na hivyo kupelekea baadhi ya familia zinazoishi pembezoni mwa shughuli za kitalii,kugeuka omba omba mabarabarani jambo linaloiwekea Tanzania [emoji1241] taswira mbaya kimataifa.
Pindi watalii hao wanaporudi makwao na kusimulia walichokiona ikiwemo pamoja na picha za video na mgando.
Tuacheni siasa na malumbano yasiyo na tija.
Watanzania tubadilike linapokuja suala la ukweli na tuache tabia ya kutanguliza maslahi binafsi mbele.
Maendeleo hayana chama.
View attachment 2124772
Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).
Nimefuatilia mijadala mbalimbali ambayo imekuwa ikiendelea kwenye social platforms,takriban muda wa wiki moja na ushei sasa.
Kuna wachangiaji ambao wamegawanyika katika pande mbili tofauti.
Upande mmoja ni wale wanaoitetea jamii ya wamaasai kuendelea kuishi wao pamoja na shughuli zao za ufugaji.
Pamoja na kuendelea kuongezeka ndani ya eneo la hifadhi hiyo kama ilivyo kwa sasa.
Kundi la pili ni wale ambao wanatetea uhifadhi maliasili ya wanyama pori na Ikolojia viumbe hai,vilivyo ndani ya eneo hilo muhimu na maarufu Duniani kwa utalii.
Mimi ninasimama upande wa watetezi wa Mazingira na Maliasili za wanyama pori na uoto wa asili,katika hifadhi ya Ngorongoro.
Ni ukweli usiopingika kwamba eneo hilo limekuwa likikaliwa na jamii ya kabila la kifugaji la wamaasai kwa asili.
Lakini inapokuja suala la uchumi wa kitaifa na pato la taifa kama nchi.
Eneo hilo na mengineyo mengi nchini yanayohusiana na utalii,yanabakia kuwa muhimu kwa upatikanaji wa fedha za kigeni.
Ambazo huingia na kuchangia maendeleo ya nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu na afya ya jamii.
Na hivyo kulifanya eneo hilo kutazamwa kwa maslahi mapana ya kitaifa na kimataifa.
Ikizihusu pia taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa zinazojihusisha na utunzaji mazingira na viumbe hai Duniani.
Ikiwemo UNESCO.
Kuna kundi la watu wamechangia kwa kumshambulia Moja kwamoja #Maulidkitenge.
Kwa ile tu kunyoosha ukweli wake na kutoa maoni yake baada kile alichokishuhudia kule Ngorongoro.
Pia kuna waliochangia kwa kuwa wanatokana na jamii husika zinazokabiliwa na kadhia ya moja kwa moja ya kutakiwa kuhamishwa toka Ngorongoro hifadhini.
Lakini pia kuna wachangiaji ambao wameligeuza suala hili kuwa kama mtaji wao wa kisiasa zaidi.
Na hii niseme kuwa ni kwa maslahi binafsi ya wanasiasa hao.
Na hapa kuna wanasiasa wa pande zote mbili za kisiasa Toka upinzani na chama tawala CCM.
Mimi nachangia kama mtanzania ambaye nimefanyia kazi katika eneo hilo,kwa ukaribu na kwa muda mrefu sasa.
Nimeziona athari zinazoikumba hifadhi ya Ngorongoro katika kila hatua.
Kuongezeka kwa idadi ya wakazi na muingiliano wa shughuli za kiutalii.Ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.
Kwa ujumla ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi au utatuzi wa mapema.kabla halijageuka na kuzaa mgogoro mkubwa baadae.
Endapo tu,halitachukuliwa maamuzi sahihi na kwa wakati stahiki.
Ebu tujiulize kwa kina!
Kama idadi ya wafugaji wa kimasaai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inaongezeka kwa kasi.
Kama ilivyo kwa watanzania wote.
Je inakuwaje kuhusu upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama,Elimu, Zahanati na maji kwa matumizi ya binadamu na mifugo yao?
Katika eneo zima la Ngorongoro. Je kama wakipewa huduma zote na miji yao kutambulika kisheria...kutakuwa na kitu kinaitwa hifadhi ya Ngorongoro?
Ukizingatia kuwa jiografia ya eneo kubwa la Ngorongoro ni lenye kiwango cha chini cha mvua katika msimu wa mwaka mzima na hivyo suala la upatikanaji wa maji inakuwa moja ya changamoto kubwa kuwaathiri wakazi hao pamoja na mifugo yao.
Jambo linaloilazimu mamlaka ya hifadhi kuwasaidia ili kuwanusuru na maafa hayo.
Je, serikali inalo fungu la kuendelea kuwahudumia kwa muda woote,pamoja na idadi yao kuzidi kuongezeka kila uchao?
Je, watetezi wa wafugaji hao wanaelewa kwamba.
Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na kupelekea kubadilika kwa mifumo ya maisha katika jamii nyingi.
Na jamii ya wamaasai wakiwa mojawapo ya wahanga wa mabadiliko hayo.
Kutokana na baadhi yao kupoteza kiasi kikubwa cha mifugo yao kutokana na maradhi au tabia nchi.
Imewalazimu pia kuanza kula vyakula ambavyo hapo awali havikukubalika kama chakula rasmi na ilikuwa ni marufuku kwao kuvila.
Ikiwemo Nyama Pori,Samaki na kuku.
Baada ya maisha kuwabadilikia na vijana wengi wa kimaasai kuingia mijini na kuchanganyika na jamii zingine katika jitihada za kutafutia maisha.
Leo hii wamekuwa walaji wakubwa wa vyakula vingi ambavyo hapo awali haikuwa kwenye orodha yao ikiwemo Chips Mayai nk.
Na ni katika mtindo huo,tabia hizi zinaambukizwa taratibu hadi huko kwenye asili zao.
Ngorongoro ikiwa muhanga mojawapo ya eneo husika.
Mifugo Tegemezi .
Tofauti na mifugo kama Ng'ombe,Punda,Mbuzi na kondoo inayofugwa na wamaasai hao wa Ngorongoro (na idadi yao pia ikiongezeka kwakasi).ambayo kiasili wanakula majani sambamba na wanyama wengine wa porini.
Kuna wanyama kama Mbwa ambao wafugaji wanawafuga na kuwategemea kama nyenzo muhimu kwa ulinzi wa mifugo yao,nyakati za usiku dhidi ya wanyama pori walao nyama kama Simba,Chui na Fisi.
Je! wao hao mbwa ambao kila kaya,lazima inawamiliki kwa idadi ya wastani usiopungua mbwa watano kila kaya.
Je, Wanakula nini kila siku ilhali chakula cha maasai wa asili ni mchanganyiko wa maziwa na mahindi almaarufu kama Roshoroo.?
Ambacho si chakula kinacholiwa na hao mbwa wa asili ya wamaasai.
Ikumbukwe kuwa nyama ya mbuzi ambayo huchinjwa na maasai hao mara chache katika maboma yao,huwa ni kidogo kuliko mahitaji rasmi ya kutosheleza jamii husika wakiwemo watoto wadogo.
Jambo ambalo hupelekea mgawanyo usio sawia kati ya wanaume
(Morani na wazee) na upande wa wanawake (kina mama,vikongwe na watoto wadogo).
Hapo humlazimu mbwa kujitafutia riziki zao na watoto wao.
Kwa mbinu asilia za kuwinda wanyama pori kama vile Sungura,Swala, watoto wa nyumbu na punda.
Na saa ingine hadi watoto wachanga wa Twiga.
Tukio ambalo mimi binafsi, niliwahi kulishuhudia na kulitolea taarifa pale Seneto gate kwa maaskari wa Ngorongoro.
Je, Hatujiulizi kwamba kuna idadi ngapi? au kiasi gani cha wanyamapori kinapotea kila mwaka kwa kuliwa na idadi kubwa ya mbwa wanaomilikiwa na wamaasai.?
Wakati tukiwatetea wamasai wa Ngorongoro,pia vema tuelewe kwamba,wao wanaishi pale ndiyo.
Lakini Ngorongoro inabeba maisha ya watanzania wengi kutokana na pato linaloingizwa kupitia sekta pekee ya utalii.
Na hivyo tunapotetea haki ya wamaasai wakaazi wa Ngorongoro kutohamishwa.
Pia ni vema tukumbuke na madhara yanayoweza kupatikana endapo jamii hiyo itaachwa kuzagaa na kuongezeka bila udhibiti sahihi kwa manufaa ya wengi nchini.
Na kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.
Hapo sijaongelea kero zinazowasibu wakazi hao kwa uduni wa maisha kutokana na kutoruhusiwa kulima mazao ya chakula kisheria.
Na hivyo kupelekea baadhi ya familia zinazoishi pembezoni mwa shughuli za kitalii,kugeuka omba omba mabarabarani jambo linaloiwekea Tanzania [emoji1241] taswira mbaya kimataifa.
Pindi watalii hao wanaporudi makwao na kusimulia walichokiona ikiwemo pamoja na picha za video na mgando.
Tuacheni siasa na malumbano yasiyo na tija.
Watanzania tubadilike linapokuja suala la ukweli na tuache tabia ya kutanguliza maslahi binafsi mbele.
Maendeleo hayana chama.
View attachment 2124772