Ngorongoro inaangamia, tuache Siasa kwenye ukweli

Ngorongoro inaangamia, tuache Siasa kwenye ukweli

Watanzania ni wanafiki sana au tuna undumilakuwili kwenye mambo sensitive kwenye maisha yetu.

Wakati miti karibu milion 2 inakatwa selous national park kule tunakojenga mradi wa stiegler hakuna mtu aliepiga kelele na hata kutoa hoja za kwanini tusikate hiyo miti badala yake wengi sana walipongeza mradi bila kuangalia postive na negative effect.

Kwa mtazamo wangu, nadhani suala ni kuwaelimisha jamii husika iliyopo NCAA jinsi ya kuishi na wanyama pori na serikali ku-control namba ya watu na mifugo ili isizidi kiwango ambacho kinaweza kuleta athari kwa wanyamapori.

Kwa hio kwa sababu tuliharibu selous tuharibu na ngorongoro ?
Kucontrol watu ni kazi ngumu sanaa bora wapewe eneo jingine wahame.
Mbna watu wanapisha ujenzi wa miundombinu kila siku kwani wao maasai ni kina nani hadi wasihame ?
 
Ila nikiisoma hii post ninazidi kuamini kwamba hela inatafutwa haswa
 
Watu ni wa ajabu sana ...yaani wanazungumzia watu wameongezeka sana lakini wanashau na wanyama wameongezeka maradufu na wanaolinda hao wanyama ni jamii ya kifugaji.kama kuna wavamizi ambao siyo jamii ya wafugaji waondolewe...hivi binadamu na wanyama wanaoishi pamoja sio kivutio cha utalii?
 
Wewe unapaelewa vizuri kabisa.
Wapo wengi wanajadili hili suala bila hata kuijuia Ngorongoro wala wakazi wake.
Mimi ni mhifadhi huru. Na eneo tajwa ni miongoni mwa maeneo nimefanya kazi na kupata uzoefu mkubwa na hisia mchanganyiko.
Ni hivi: NGORONGORO inakufa kwa mengi.
Na zisipofanyika jitihada za makusudi kuendeleza uhifadhi mle ndani tutapoteza ikolojia muhimu sana pamoja na kipokwa sifa zote tulizo nazo kwenye utalii.
Tufikirie kuhusu:
  • Kudhibiti idadi ya ng'ombe.
  • Kudhibiti idadi ya watu.
  • Kudhibiti makazi na shughuli za watu.
  • Kudhibiti ujenzi wa hoteli na kambi za kitalii.
Aidha nitoe tu angalizo: kwa tabia zetu hizi za kutokujali uhifadhi wa mazingira huko mbele ya safari tutaendeleza harakati za kugombania access ya maeneo nyeti kwenye uhifadhi.
 
Wanabodi JF!,

Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).

Nimefuatilia mijadala mbalimbali ambayo imekuwa ikiendelea kwenye social platforms,takriban muda wa wiki moja na ushei sasa.



Maendeleo hayana chama.
Wewe ni mjinga kama Kitenge. Toka lini Ngorongoro inapata mvua kidogo mwaka mzima? Ngorongoro ni ukanda wa juu unaopata mvua sawia kila mwaka. Tena mvua nyingi kuliko sehemu nyingi nchini.

Hatua ya kwanza iwe ya kuivunja hiyo NCAA mnayoitumia kujitajirisha kwa kufisadi na kujilipa posho kubwa kubwa.
Eneo likabidhiwa kwa TANAPA ili iwe national park. Utalii wa utamaduni umekwisha. Eneo la NCA liwe mbuga ya Taifa chini ya Tanapa kama ilivyo Serengeti, Tarangire au lake Manyara.
 
Kwani wewe wanyama pori wanakusaidia nini. Wapambanieni wazungu kwani kuhifadhi mlipanga mlipangiwa.
 
Wanabodi JF!,

Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).
Njoo uchukue teni,wanyama kukaa na binadamu mnaona ajabu wakti wamekaa nao enzi na enzi...tarangire wanyama yanakaa na watu miaka,minjingu pundamilia wanashinda kwenye makazi ya watu na kuku hamshangai...tunajua macho kumchuzi anataka kuwapa OBC eneo zaidi pia yeye na waarabu wa granmelia wanataka kujenga hotel
 
Watanzania ni wanafiki sana au tuna undumilakuwili kwenye mambo sensitive kwenye maisha yetu.

Wakati miti karibu milion 2 inakatwa selous national park kule tunakojenga mradi wa stiegler hakuna mtu aliepiga kelele na hata kutoa hoja za kwanini tusikate hiyo miti badala yake wengi sana walipongeza mradi bila kuangalia postive na negative effect.

Kwa mtazamo wangu, nadhani suala ni kuwaelimisha jamii husika iliyopo NCAA jinsi ya kuishi na wanyama pori na serikali ku-control namba ya watu na mifugo ili isizidi kiwango ambacho kinaweza kuleta athari kwa wanyamapori.
Umeongea point ya msingi sana "ku-control namba ya watu na mifugo" na nadhani hili ndilo litakalofanyika na NCAA wameanza wao kama wao kuchukua hatua ya kuhamisha ofisi na makazi kupeleka karatu. Hatua itakayofuata nadhani ni kupunguza idadi ya wamasai walioko ndani ya hifadhi na siyo kuwahamisha wote maana wamasai wana haki ya asili na kisheria ya kuwa kule.

Hifadhi imeharibika sana na ujenzi wa nyumba za tofali na bati umeongezeka kwa kasi.
 
Hiyo nembo inamaana gani?

View attachment 2113934

Ni sahihi kabisa maoni yako kuhusu nembo.
Lakini mambo yamebadilika, hali zimebadilika, watu wamebadilika n.k. sasa kwa nini na sisi tusiende kulingana na mabadiliko hayo?? Hiyo nembo siyo msaafu (ambayo imeandikwa ukithubutu kubadilisha chochote kwenye hiyo, utapewa mapigo kulingana na ulichofanya) inaweza ikabadilishwa. Ukweli ni kuwa watu wanazaliana na kuongezeka sana. Pia desturi za wanaoishi kule ndani wanaenda kuchukuana hata wengine kutoka nchi jirani. Kuna siku nimeona hapa JF mpaka nyumba za bati zimejengwa kwenye hifadhi.
 
Mimi sihitaji kusoma tafiti ya mtu wakati binafsi nina miaka zaidi ya thelathini nikiwa katika eneo husika.

Hao watafiti huja kuandika kwa kuhoji watu kwa kipindi fulani na kuondoka lakini mimi ninielewa eneo hilo kuanzia Loduare mpaka Wasso kule Loliondo.

Ninaijua milima yote na nimeipanda kwa miguu yangu ukiwemo huo wa Le Magurut

Nimezitembelea crater zote kuanzia Ngorongoro, Olmoti na Empakai.

Nimepanda mpaka kileleni mwa mlima pekee wenye volcano [emoji291] hai...Oldoinyo Lengai.

Nimetembelea na kufanya kazi katika ziwa pekee lenye mazalia ya flamingo Lake Natron.

Nimewatembelea mpaka machifu maarufu wa Ngorongoro akiwemo marehemu Birkaa na Ole Mereiya.

Utafiti gani zaidi nauhitaji #Lukubuzo ramsis!

Labda watafiti ndio wanitafute ili niwatafiti.
A man himself !!

wewe Ni mtu muhimu Sana,. Ngorongoro inakuhitaji Ni wakati wako wa kuitetea sasa
 
Waacheni masai waishi maeneo yao ya asili bhana, kama vipi hamishieni hao wanyama serengeti, selous au mikumi nchi hii imejaa hifadhi kila mahali............hivi ni nani anatakiwa kupewa kipaumbele kati ya binadamu na mnyama kuishi mahali?
 
Kama wakipatiwa huduma zote za kijamii basi ujue Neno la hifadhi litakufa kabisaa... wakati mnajua toplist ya nchi zinaongiza kwa utalii duniani, tanzania nayo imekuwa ya kwanza kwahyo kwa mimi nachoomba wamasai waendelee kujirecord na tik tok watoboe maisha waache kuwinda wanyama na kugoma kutoka kwenye hifadhi
 
Swala la Ngorongoro liko wazi kabisa.kua jamii ya wafugaji wanapaswa kuondoka eneo la hifadhi .Kinacholeta huu msuguano ni serikali yenyewe kutaka vyote vyote.Serikali inapokosa kauli moja thabiti ndo kunapelekea hizi siasa uchwara zinazoendelea sasa.Na hii danadana imeanza kitambo sasa serikali isipokaa chini nakuchukua hatua sasa hivi kukiwa bado na hili vuguvugu iko siku tutajutia.
 
Waacheni masai waishi maeneo yao ya asili bhana, kama vipi hamishieni hao wanyama serengeti, selous au mikumi nchi hii imejaa hifadhi kila mahali............hivi ni nani anatakiwa kupewa kipaumbele kati ya binadamu na mnyama kuishi mahali?
Kwani ni lazima binadamu aishi porini?.Kila kitu kinategemeana ndo maana vikawepo.Uharibifu wa mazingira utakapokithiri hata binadamu atakua hatarini.kwahiyo kama binadamu anayejielewa lazima tubalance haya mambo.Binadamu ni mhimu ila pia ni mnyama mwaribifu ndo maana tukawekeana sheria.tukisema kwasababu ni binadamu aachwe tu iko siku futatafuta mazingira rafiki yakuishi kwa tochi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwani ni lazima binadamu aishi porini?.Kila kitu kinategemeana ndo maana vikawepo.Uharibifu wa mazingira utakapokithiri hata binadamu atakua hatarini.kwahiyo kama binadamu anayejielewa lazima tubalance haya mambo.Binadamu ni mhimu ila pia ni mnyama mwaribifu ndo maana tukawekeana sheria.tukisema kwasababu ni binadamu aachwe tu iko siku futatafuta mazingira rafiki yakuishi kwa tochi.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Nch hii ina mbuga nyingi sana na zenye eneo kubwa sana kuweza kuhamisha kabila ambalo limedumisha mila na tamaduni zake kwenye maeneo yao ya asili na hivyo kuwa kivutio kwa wageni, acheni kuleta maslahi binafsi kwenye hili swala.......
 
Hiyo nembo inamaana gani?

View attachment 2113934
Hii nembo ilitengenezwa miaka hiyo kulipokua na sheria ya matumizi mseto ya ardhi ila haya ni mambo yanayoweza kubadilika muda wowote.kwahiyo hata hii nembo naamini itakuja kubadilika kwasababu sasa hivi wizara ya maliasili iko na mchakato wa mfumo wa jeshi usu la uhifadhi ambalo litabadili mambo mengi yakiutendaji na utambulisho.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nashukuru kwa hilo mkuu,watu hawapendi ukweli.
Umeandika vizuri, lakini ukaweka ukweli nusu. Unatakiwa ukamilishe taarifa yako.
Yapo mambo ambayo hayabishiwi.
La kwanza ni kwamba Ngorongoro ina hali mbaya.
La pili ni kwamba Ngorongoro ni ya kipekee kwa kuhifadhi Wafugaji na Wanyamapori.
Tatu ni kwamba Hifadhi hii ya Wafugaji na Wanyamapori inaingiza pesa za kutosha kila mwaka. Takribani zaidi ya Bilioni 150 kila mwaka.
NNE ni kwamba Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imeshindwa kuitunza hiyo Hifadhi, pamoja na makusanyo makubwa sana kila mwaka.
TANO ni kwamba kila anayezungumzia uharibifu wa Ngorongoro anakwepa kumtaja MTUHUMIWA halisi, ambaye ni Ngorongoro Conservation Area Authority, yaani Mamlaka ya Hifadhi hii, badala yake anaelekeza lawama kwa Wafugaji, ambao ni sehemu ya Uhifadhi huu.
Na mwisho tunatakiwa tuungane kuiokoa Ngorongoro kwa kuwaweka Kitimoto Mamlaka ya Hifadhi watueleze wanalofanya katika hiyo Hifadhi wakati mazingira yanaendelea kudorora.
Kuna kila dalili kuwa rushwa inatembea katika hizi harakati.
Viongozi wa Mamlaka ya Hifadhi wanaweza kuwahonga watu wachache, lakini hawawezi kutuhonga Watanzania wote, tena kwa kutumia pesa zetu za Umma.
Sijaona anayeuliza utaratibu wa kutoa Vibali vya Ujenzi ndani ya Hifadhi na madhara yake kwa Uhifadhi.
Madhara ya Majengo makubwa na Mahoteli yanavuruga 'ecosystem' ya Ngorongoro.
Mamlaka ya Hifadhi ndilo tatizo la Ngorongoro.
 
Iangamie tu, unadhani hao wanaowafurusha wamasai ni kwa maslahi ya Taifa?
 
Wanabodi JF!,

Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).

Nimefuatilia mijadala mbalimbali ambayo imekuwa ikiendelea kwenye social platforms,takriban muda wa wiki moja na ushei sasa.

Kuna wachangiaji ambao wamegawanyika katika pande mbili tofauti.

Upande mmoja ni wale wanaoitetea jamii ya wamaasai kuendelea kuishi wao pamoja na shughuli zao za ufugaji.

Pamoja na kuendelea kuongezeka ndani ya eneo la hifadhi hiyo kama ilivyo kwa sasa.

Kundi la pili ni wale ambao wanatetea uhifadhi maliasili ya wanyama pori na Ikolojia viumbe hai,vilivyo ndani ya eneo hilo muhimu na maarufu Duniani kwa utalii.

Mimi ninasimama upande wa watetezi wa Mazingira na Maliasili za wanyama pori na uoto wa asili,katika hifadhi ya Ngorongoro.

Ni ukweli usiopingika kwamba eneo hilo limekuwa likikaliwa na jamii ya kabila la kifugaji la wamaasai kwa asili.

Lakini inapokuja suala la uchumi wa kitaifa na pato la taifa kama nchi.
Eneo hilo na mengineyo mengi nchini yanayohusiana na utalii,yanabakia kuwa muhimu kwa upatikanaji wa fedha za kigeni.
Ambazo huingia na kuchangia maendeleo ya nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu na afya ya jamii.

Na hivyo kulifanya eneo hilo kutazamwa kwa maslahi mapana ya kitaifa na kimataifa.

Ikizihusu pia taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa zinazojihusisha na utunzaji mazingira na viumbe hai Duniani.
Ikiwemo UNESCO.

Kuna kundi la watu wamechangia kwa kumshambulia Moja kwamoja #Maulidkitenge.
Kwa ile tu kunyoosha ukweli wake na kutoa maoni yake baada kile alichokishuhudia kule Ngorongoro.

Pia kuna waliochangia kwa kuwa wanatokana na jamii husika zinazokabiliwa na kadhia ya moja kwa moja ya kutakiwa kuhamishwa toka Ngorongoro hifadhini.


Lakini pia kuna wachangiaji ambao wameligeuza suala hili kuwa kama mtaji wao wa kisiasa zaidi.

Na hii niseme kuwa ni kwa maslahi binafsi ya wanasiasa hao.

Na hapa kuna wanasiasa wa pande zote mbili za kisiasa Toka upinzani na chama tawala CCM.

Mimi nachangia kama mtanzania ambaye nimefanyia kazi katika eneo hilo,kwa ukaribu na kwa muda mrefu sasa.

Nimeziona athari zinazoikumba hifadhi ya Ngorongoro katika kila hatua.

Kuongezeka kwa idadi ya wakazi na muingiliano wa shughuli za kiutalii.Ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.

Kwa ujumla ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi au utatuzi wa mapema.kabla halijageuka na kuzaa mgogoro mkubwa baadae.
Endapo tu,halitachukuliwa maamuzi sahihi na kwa wakati stahiki.

Ebu tujiulize kwa kina!

Kama idadi ya wafugaji wa kimasaai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inaongezeka kwa kasi.
Kama ilivyo kwa watanzania wote.

Je inakuwaje kuhusu upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama,Elimu, Zahanati na maji kwa matumizi ya binadamu na mifugo yao?

Katika eneo zima la Ngorongoro. Je kama wakipewa huduma zote na miji yao kutambulika kisheria...kutakuwa na kitu kinaitwa hifadhi ya Ngorongoro?

Ukizingatia kuwa jiografia ya eneo kubwa la Ngorongoro ni lenye kiwango cha chini cha mvua katika msimu wa mwaka mzima na hivyo suala la upatikanaji wa maji inakuwa moja ya changamoto kubwa kuwaathiri wakazi hao pamoja na mifugo yao.

Jambo linaloilazimu mamlaka ya hifadhi kuwasaidia ili kuwanusuru na maafa hayo.

Je, serikali inalo fungu la kuendelea kuwahudumia kwa muda woote,pamoja na idadi yao kuzidi kuongezeka kila uchao?


Je, watetezi wa wafugaji hao wanaelewa kwamba.

Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na kupelekea kubadilika kwa mifumo ya maisha katika jamii nyingi.

Na jamii ya wamaasai wakiwa mojawapo ya wahanga wa mabadiliko hayo.
Kutokana na baadhi yao kupoteza kiasi kikubwa cha mifugo yao kutokana na maradhi au tabia nchi.

Imewalazimu pia kuanza kula vyakula ambavyo hapo awali havikukubalika kama chakula rasmi na ilikuwa ni marufuku kwao kuvila.
Ikiwemo Nyama Pori,Samaki na kuku.

Baada ya maisha kuwabadilikia na vijana wengi wa kimaasai kuingia mijini na kuchanganyika na jamii zingine katika jitihada za kutafutia maisha.

Leo hii wamekuwa walaji wakubwa wa vyakula vingi ambavyo hapo awali haikuwa kwenye orodha yao ikiwemo Chips Mayai nk.

Na ni katika mtindo huo,tabia hizi zinaambukizwa taratibu hadi huko kwenye asili zao.
Ngorongoro ikiwa muhanga mojawapo ya eneo husika.

Mifugo Tegemezi .

Tofauti na mifugo kama Ng'ombe,Punda,Mbuzi na kondoo inayofugwa na wamaasai hao wa Ngorongoro (na idadi yao pia ikiongezeka kwakasi).ambayo kiasili wanakula majani sambamba na wanyama wengine wa porini.

Kuna wanyama kama Mbwa ambao wafugaji wanawafuga na kuwategemea kama nyenzo muhimu kwa ulinzi wa mifugo yao,nyakati za usiku dhidi ya wanyama pori walao nyama kama Simba,Chui na Fisi.

Je! wao hao mbwa ambao kila kaya,lazima inawamiliki kwa idadi ya wastani usiopungua mbwa watano kila kaya.

Je, Wanakula nini kila siku ilhali chakula cha maasai wa asili ni mchanganyiko wa maziwa na mahindi almaarufu kama Roshoroo.?
Ambacho si chakula kinacholiwa na hao mbwa wa asili ya wamaasai.

Ikumbukwe kuwa nyama ya mbuzi ambayo huchinjwa na maasai hao mara chache katika maboma yao,huwa ni kidogo kuliko mahitaji rasmi ya kutosheleza jamii husika wakiwemo watoto wadogo.

Jambo ambalo hupelekea mgawanyo usio sawia kati ya wanaume
(Morani na wazee) na upande wa wanawake (kina mama,vikongwe na watoto wadogo).

Hapo humlazimu mbwa kujitafutia riziki zao na watoto wao.
Kwa mbinu asilia za kuwinda wanyama pori kama vile Sungura,Swala, watoto wa nyumbu na punda.

Na saa ingine hadi watoto wachanga wa Twiga.
Tukio ambalo mimi binafsi, niliwahi kulishuhudia na kulitolea taarifa pale Seneto gate kwa maaskari wa Ngorongoro.

Je, Hatujiulizi kwamba kuna idadi ngapi? au kiasi gani cha wanyamapori kinapotea kila mwaka kwa kuliwa na idadi kubwa ya mbwa wanaomilikiwa na wamaasai.?

Wakati tukiwatetea wamasai wa Ngorongoro,pia vema tuelewe kwamba,wao wanaishi pale ndiyo.
Lakini Ngorongoro inabeba maisha ya watanzania wengi kutokana na pato linaloingizwa kupitia sekta pekee ya utalii.

Na hivyo tunapotetea haki ya wamaasai wakaazi wa Ngorongoro kutohamishwa.

Pia ni vema tukumbuke na madhara yanayoweza kupatikana endapo jamii hiyo itaachwa kuzagaa na kuongezeka bila udhibiti sahihi kwa manufaa ya wengi nchini.

Na kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

Hapo sijaongelea kero zinazowasibu wakazi hao kwa uduni wa maisha kutokana na kutoruhusiwa kulima mazao ya chakula kisheria.

Na hivyo kupelekea baadhi ya familia zinazoishi pembezoni mwa shughuli za kitalii,kugeuka omba omba mabarabarani jambo linaloiwekea Tanzania [emoji1241] taswira mbaya kimataifa.

Pindi watalii hao wanaporudi makwao na kusimulia walichokiona ikiwemo pamoja na picha za video na mgando.

Tuacheni siasa na malumbano yasiyo na tija.

Watanzania tubadilike linapokuja suala la ukweli na tuache tabia ya kutanguliza maslahi binafsi mbele.

Maendeleo hayana chama.
Ebu tuache porojo maana jamii ya kimasaai haijaanza kuishi huko jana iyo population increase awakuiproject ao watu wa mazingira kwmb baada ya miaka kadhaa wataleta uharibifu kwenye mazingira wafanye namna mapema leo ndo wanaona mazingira yanaharibika, waacheni ao watu waishiiiii acheniiii porojo
 
Back
Top Bottom