Ngorongoro inaangamia, tuache Siasa kwenye ukweli


Hivi ukimpa mtu offer ya kumhamishia mahali ambapo maisha yake yatakuwa qualitatively better kuliko yalivyo pale alipo sasa atakaa kweli?

Sidhani kama Serikali imenadi mpango wowote wa maana kwa hii jamii ya Wamaasai.
 
Kwani zamani kulikuwaje? Ngorongoro ndio imevumbuliwa hivi karibuni ama
Waache Wamasai waishi hizi project zinakuja oh tunatunza mazingira ni scheme kama scheme zingine tu
Shida ni 10% inasumbua sana
Mwarabu kwao hakuna miti ndio waje kutufundisha kutunza miti this is a joke....
 
Kuna watu wengi wanafaidika na uwepo wa wamasai Ngorongoro. Ngorongoro peke yake ina NGO zaidi ya 60. Hizi ni NGO ambazo mmasai akiondoka Ngorongoro zote hazitakuwa na cha kufanya.

Bahati mbaya kuna watu wanasikiliza utetezi wa hizi NGO na kudhani ni kweli wana lengo zuri kwa wamasai kumbe wana tetea ugali wao.

Kimsingi kuishi na wanyama siyo fahari, ni shida. Ni kitu unachoweza kukifanya kama huna alternative yoyote.

Kuna sababu nyingi za kwa nini wamasai wanatakiwa kuondoka au kupunguzwa ngorongoro.

1. Idadi yao imeongezeka sana. Na kama tunavyojua watu wanapoongezeka wanyama wanapungua na hatimaye kutoweka kabisa.
2. Wamasai pia wanahitaji kuendelea. Wanataka shule nzuri, umeme, na wafanye shughuli zao zingine kisasa zaidi. Mle ngorongoro wame minywa sana.
3. Ngorongoro ni cash cow kwa Taifa. Hivyo ni lazima ilindwe. Ku relocate watu kwa sababu za kimaendeleo ni jambo la kawaida..na mara nyingi tu watu wamehamishwa maeneo yao kupisha shughuli.za maendeleo. So wamasai ni nani hadi wasihamishwe?
 
Wamasai na wasukuma ni jamii haribifu sana kwa mazingira,mwenyewe huwa napata hasira sana Tanzania INA maeneo mengi yaliyo wazi kwa nini Watu wanakwenda kuharibu ecology ya wanyama-hata hiyo Hotel ya Loliondo ni ya kubomolewa.

Yani ingekuwa Mimi ndio Rais,a see wiki mmoja kubwa wote wangetoka.
 
Hivi ukimpa mtu offer ya kumhamishia mahali ambapo maisha yake yatakuwa qualitatively better kuliko yalivyo pale alipo sasa atakaa kweli?

Sidhani kama Serikali imenadi mpango wowote wa maana kwa hii jamii ya Wamaasai.
Hii ndio ilitakiwa kuwa hoja sasa, kuhusu wanakopelekwa, sio kubishana kuhusu kuhama. Kuhama lazima wahame, kama wameona hawapelekwi sehemu nzuri waseme tujadili
 
Hakuna namna, Ngorongoro lazima tuilinde kwa gharama yeyote ile.

Haiwezekani eneo tunalolitegemea kwa kuingiza fedha za kigeni kwa ajiri ya maendeleo ya Tanzania nzima tuliache likiangamia mbele ya macho yetu.

Ngorongoro ikiangamia, Serengeti itaangamia, nilikuwa Ngorongoro mwaka 2020, hali ni mbaya na hadi wale Tour Guides wanakiri kuwa shughuli za kibidamamu zinakimbiza wanyama mbali. Na Mimi mwenyewe nilijionea kwa Jinsi gani shughuli za kibinadamu zimekimbiza wanyama mbali.

Suluhisho kwa Ngorongoro ni kwamba hela zinazotumika katika kuwalisha hao wamasai takribani bilioni 3 kwa mwaka zitumike kuwajengea makazi ya kudumu eneo lingine na wahamishiwe huko
 
Tanzania inambuga nyingi kiufup zipunguzwe
Kweli nimeamini kichaa si lazima aokote makopo,
Pia kuna usemi usemeo hata wapumbavu wanazeeka,
unaweza ona mtu ana mvi kichwani lakini akili zake hamnazo.
Sor sijamtaja mtu!
 
Mkuu
Unahitaji kueleweshwa kidogo kuhusiana na hili.

Hapa haiongelewi Ngorongoro ya Loliondo,huko ndio kuna mwarabu.

Bali inaongelewa tarafa ya Ngorongoro ambalo ni eneo linaloihusu Crater ya Ngorongoro na vijiji kadhaa vya kuizunguka hiyo crater.
 
Ngorongoro ilindwe kwa gharama yoyote ile

Wamasai hao wa wanaotetewa leo wakishaharibu mazingira ya hapo watahama na kwenda kuharibu kwingine mwishowe tutaikosa Ngorongoro na wamasai pia tutawakosa
 
True [emoji106] said mkuu iMind.
Yaani umetembea kwenye ukweli mtupu bila kuuma uma maneno.

Jana nimeona kwenye luninga ya ITV wamekodi vijana mamluki wa kimaasai eti wanaongea kwa kumtuhumu #Maulid kitenge.
Kwamba anatumika.

Lakini ukweli ni kwamba huu mgogoro unakuzwa na watu wa genge lenye maslahi binafsi.wakiwemo wanasiasa na hizo NGO's za mifukoni.
Toka huko Loliondo.

Na baadhi zimehusishwa na raia wa kigeni walioweka makazi yao Kenya [emoji1139].
 
Kinachotokea Ngorongoro ni mojawapo ya tragedy of the commons.
Ukweli ni kuwa ukiacha eneo la Crater (shimoni), maeneo mengine yote yameharibiwa kikamilifu.
Wewe unapaelewa vizuri kabisa.
 
Hii ndio ilitakiwa kuwa hoja sasa, kuhusu wanakopelekwa, sio kubishana kuhusu kuhama. Kuhama lazima wahame, kama wameona hawapelekwi sehemu nzuri waseme tujadili
Kweli kabisa!
 
.... Ngorongoro imezalisha mabilioni ya fedha kwenye uchumi wa nchi; wamasai wakiwa sehemu ya vivutio vya utalii. Badala ya matumizi ya nguvu, serikali iwape motisha ili wahame kwa hiari. Kwa mfano, serikali ijenge flats maeneo fulani kama zile za JWTZ zilizojengwa maeneo mbalimbali nje ya miji then wahusika wahamishiwe huko. Mbona vijiji vya ujamaa enzi za Nyerere na Kawawa (Simba wa Vita) iliwezekana?

Atakayegoma kuhama huyo sasa atakuwa na jambo lake na haitakii mema nchi yetu hapo sasa nguvu inaweza kutumika. Ila kuwafukuza bila kuwaandalia makazi ni kuwaonea; ni unyanyasaji wala sio haki hata kidogo!
 
Mkuu logic yako ni nzuri. Solution ni lipi hapo...... sasa
Solution ni wao baadhi ya wamaasai kukubali kuhamishiwa katika eneo wanalofidiwa na serikali.

Zoezi hilo lifanyike kwa usawa bila upendeleo ili kutoleta manung'uniko baina ya wao kwa wao.

Na pia ikibidi ibaki idadi ya jamii ya hao wafugaji ambayo itaweza kubalance na mazingira ya uhifadhi bila madhara.

Hapa wanaweza kuanza na wale ambao wanamiliki idadi kubwa ya mifugo pamoja na kaya kubwa kubwa ambazo zina mahitaji makubwa ya huduma za kijamii ikiwemo Chakula, Shule na Matibabu.

Lakini pia waweke ukomo wa maeneo ya malisho kwa mifugo itakayobaki ndani ya hiyo hifadhi badala ya sasa ambapo wanazagaa kila sehemu ikiwemo njia kuu za kitalii huku wale watoto wachungaji wamekuwa wakiomba omba chakula toka kwenye magari yanayopita na watalii.
 
Kwa mtazamo wangu ili kuilinda na kuidumisha ngorongoro ufanyike udhibiti wa kuzuwia ongezeko la jamii ya masai na mifugo yao kwa kuwahamishia maeneo mengine ya nchi pili iangaliwe kwa marejeo idadi ya masai na mifugo waliokuwepo wakati ngorongoro inaanzishwa ili ziada ihamishwe na kuzuwia kutokuvuka idadi jambo hilo linaweza kutungiwa sheria kwa ajili ya uhifadhi na usalama wa jamii ya masai vinginevyo ni kweli ngorongoro inaangamia naunga mkono hoja
 
Watanzania ni wanafiki sana au tuna undumilakuwili kwenye mambo sensitive kwenye maisha yetu.

Wakati miti karibu milion 2 inakatwa selous national park kule tunakojenga mradi wa stiegler hakuna mtu aliepiga kelele na hata kutoa hoja za kwanini tusikate hiyo miti badala yake wengi sana walipongeza mradi bila kuangalia postive na negative effect.

Kwa mtazamo wangu, nadhani suala ni kuwaelimisha jamii husika iliyopo NCAA jinsi ya kuishi na wanyama pori na serikali ku-control namba ya watu na mifugo ili isizidi kiwango ambacho kinaweza kuleta athari kwa wanyamapori.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…