JOYOPAPASI
JF-Expert Member
- Jan 10, 2016
- 250
- 409
#NGORONGORO SIO SEHEMU YA MAKAZI YA BINADAMU BALI NI HIFADHI YA WANYAMA POLI Naa Joseph #Yona
Mwaka 1960 Ngorongoro Ilikuwa na Tembo zaidi ya 2000! Ila leo hii Tembo waliobaki Ngorongoro ni 30! Moja ya utajiri wa kipekee duniani ni kuwa na wanyama Mwitu kama hawa ambao sisi wabongo tunawachukulia poa sana!
Ila wana thamani kubwa katika ulimwengu huu! Dunia nzima kwa sasa inateigemea zaidi Tanzania kuhusu wanyama pori. Tanzania ndio wenye wanyama wengi tuliobaki duniani. Ila mbali na hilo wanyama wamekuwa wakiangamizwa kwa speed ya kutisha na sisi wenyewe Watanzania na sasa kuna wanyama ambao wapo kwenye Hatari ya kuangamia kabisa katika uso wa dunia.
Muhimu kuanza kuchukua hatua stahiki kuinusulu Hifadhi adimu Duniani kwa vivutio vya utalii.
MADAI YA WATU KUISHI HIFADHI YA NGORONGORO NA WANYAMA POLI KUWA NI KUVUTIA UTALII NI UJINGA NA UPUUZI
Hivi karibuni kumezuka mijadala mingi juu ya uwepo wa zaidi ya watu zaidi ya laki Moja kuishi hifadhi ya Ngorongoro kuwa ni njia Moja wapo ya KUVUTIA UTALII ni ujinga na upuuzi usio vumilika hata kidogo.
Tumeshudia Waandishi wa habari Maulid Kitenge na Oscar Oscar Mzee wa Kaliua wakiwa wanaripoti kutoka Hifadhi ya Ngorongoro na kueleza ualisia unaoendelea hapo Hifadhini kumejitokeza, kundi la wajinga flani kwa maslahi yao binafsi bila kuangalia hali ilivyo wameanza kampeni ya kuwashambulia waandishi hao, bali tuangalie uhalisia, taarifa ni kuwa kuna jamii ya watu wachache ni wanufaika na shida za watu walio wengi maskini, huko Ngorongoro Tuendako watoto wanakufa, hakuna barabara, hakuna huduma za kijamii nk ndo maana MECIRA tunasema hatua za haraka zichukuliwe kuondoa hali ya hatari zaidi baadaye na sasa.
Shida inayoonekana hapo ni wafugaji kuingilia hifadhi, kwa ajili ya malisho na Taifa linaweza kukosa watalii kwani watakuwa wanafika kwenye hifadhi badala ya kuona pundamilia, au Twiga wanakutana na Ng'ombe na Taifa kukosa mapato yatokanayo na utalii, lakini pia kizazi Cha Sasa kitaona mazingira rafiki kwa malisho ni kwenye hifadhi kwani kitaona hakuna katazo lolote kama wanahabari tunapaswa kuishauri serikali njia sahihi za kuepukana na hili tatizo, kazi iendelee.
Hakika mapendekezo ya Kitenge na Oscar* yanatakiwa kuchukuliwa haraka hatua za makusudi kwa ajili ya kuokoa kizazi ambacho kinaishi maisha hatarishi, na kuokoa hifadhi kuondokana na hatari ya kuwa jangwa.
#PazaSauti
#KataaMakaziYaWatuNgorongoro
Mwaka 1960 Ngorongoro Ilikuwa na Tembo zaidi ya 2000! Ila leo hii Tembo waliobaki Ngorongoro ni 30! Moja ya utajiri wa kipekee duniani ni kuwa na wanyama Mwitu kama hawa ambao sisi wabongo tunawachukulia poa sana!
Ila wana thamani kubwa katika ulimwengu huu! Dunia nzima kwa sasa inateigemea zaidi Tanzania kuhusu wanyama pori. Tanzania ndio wenye wanyama wengi tuliobaki duniani. Ila mbali na hilo wanyama wamekuwa wakiangamizwa kwa speed ya kutisha na sisi wenyewe Watanzania na sasa kuna wanyama ambao wapo kwenye Hatari ya kuangamia kabisa katika uso wa dunia.
Muhimu kuanza kuchukua hatua stahiki kuinusulu Hifadhi adimu Duniani kwa vivutio vya utalii.
MADAI YA WATU KUISHI HIFADHI YA NGORONGORO NA WANYAMA POLI KUWA NI KUVUTIA UTALII NI UJINGA NA UPUUZI
Hivi karibuni kumezuka mijadala mingi juu ya uwepo wa zaidi ya watu zaidi ya laki Moja kuishi hifadhi ya Ngorongoro kuwa ni njia Moja wapo ya KUVUTIA UTALII ni ujinga na upuuzi usio vumilika hata kidogo.
Tumeshudia Waandishi wa habari Maulid Kitenge na Oscar Oscar Mzee wa Kaliua wakiwa wanaripoti kutoka Hifadhi ya Ngorongoro na kueleza ualisia unaoendelea hapo Hifadhini kumejitokeza, kundi la wajinga flani kwa maslahi yao binafsi bila kuangalia hali ilivyo wameanza kampeni ya kuwashambulia waandishi hao, bali tuangalie uhalisia, taarifa ni kuwa kuna jamii ya watu wachache ni wanufaika na shida za watu walio wengi maskini, huko Ngorongoro Tuendako watoto wanakufa, hakuna barabara, hakuna huduma za kijamii nk ndo maana MECIRA tunasema hatua za haraka zichukuliwe kuondoa hali ya hatari zaidi baadaye na sasa.
Shida inayoonekana hapo ni wafugaji kuingilia hifadhi, kwa ajili ya malisho na Taifa linaweza kukosa watalii kwani watakuwa wanafika kwenye hifadhi badala ya kuona pundamilia, au Twiga wanakutana na Ng'ombe na Taifa kukosa mapato yatokanayo na utalii, lakini pia kizazi Cha Sasa kitaona mazingira rafiki kwa malisho ni kwenye hifadhi kwani kitaona hakuna katazo lolote kama wanahabari tunapaswa kuishauri serikali njia sahihi za kuepukana na hili tatizo, kazi iendelee.
Hakika mapendekezo ya Kitenge na Oscar* yanatakiwa kuchukuliwa haraka hatua za makusudi kwa ajili ya kuokoa kizazi ambacho kinaishi maisha hatarishi, na kuokoa hifadhi kuondokana na hatari ya kuwa jangwa.
#PazaSauti
#KataaMakaziYaWatuNgorongoro