Nguo ya ndani inabidi ivaliwe kwa miezi mitatu tu na itupwe. Kina dada acheni kununua sidiria za mitumba

Asiye na uwezo afanyeje ?kinachotakiwa ni usafi wa hali ya juu , na uwe na za kutosha , hata mwaka inaonekana kama mpya
 
Watu tunatumia £30 kununua bra moja Marks and Spenser halafu unatwambia tutupe baada ya/// Zile Bra na chupi kama ni mtunzaji hata miaka 10 unavaa. Wewe ungewaambia wavaa mitumba lakini siwezi kwenda M&S ninunue chupi halafu nitupe!!!!! Sisemi zaidi.
 
Inategemea unazo ngapi. Wengine wana 50+ akirudi a ni baada ya zaidi ya mwezi. Ninavhofahamu ni kuwa nguo yeyote inayovaliwa next to the skin inatakiwa kubadilishwa kila siku.
Pichu
Socks
Vest
Sidiria
How are you, wish you a very happy and blessed weekend
 
Nina boxers 15. Kama unajua kujumlisha na kugawanya utajua kwa mwezi inavaliwa mara mbili, kwa miezi mitatu inavaliwa mara 6. Kwahio nitupe nguo baada ya kuivaa mara sita? Hapo sijazungumzia wenye underwear 50!
 
Bra za mtumba ni the best, za dukani hazikai vizuri, hazibani nyonyo, zinakua mama nibebe yani huku mgongoni inapanda juu, mikanda imelegea, mi siziwezi.
Za mitumba zilikuwa dukani kabla ya wewe kununua kama mtumba.
 
Nina boxers 15. Kama unajua kujumlisha na kugawanya utajua kwa mwezi inavaliwa mara mbili, kwa miezi mitatu inavaliwa mara 6. Kwahio nitupe nguo baada ya kuivaa mara sita? Hapo sijazungumzia wenye underwear 50!
Km unazo nyingi. Sawa
 
Yeye mwenyewe aliyeandika ana boxer ina 4yrs
 
Chupi nivae miezi 3 kisha niitupe?
Ahhh wapi!!
Kwahiyo kama nitanunua dazani January ikifika March zote nazitupa afu mwendo wa chukuchuku tu.
Chaaaa!!!!
 
Inategemea unazo ngapi. Wengine wana 50+ akirudi a ni baada ya zaidi ya mwezi. Ninavhofahamu ni kuwa nguo yeyote inayovaliwa next to the skin inatakiwa kubadilishwa kila siku.
Pichu
Socks
Vest
Sidiria
Mimi kubadili socks ni mpaka dole gumba liniambie.

Yaani ni mpaka pale linapochomoza kwenye socks ndio najua mambo yamekuwa mambo.
 
Mtoa mada unapaswa ujue pia kuwa tupo wenye 100+ means rotation ya kurudia inafika hata miez miwili na nusu Ebooh
 
Cha kutupa baada ya miezi 3 ni mswaki, maana wautumia si chini ya mara moja kwa siku.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…