Nguruwe wangu anatatizo la kukojoa mfululizo mara tu baada ya kunywa maji hayakai tumboni anayakojoa yote papo hapo

gimmy's

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2011
Posts
3,312
Reaction score
3,345
Wanajukwaa wenzangu kama yupo mwenye majibu ya tatizo naomba maelekezo,

Ukweli tanzania tunasafari ndefu kwani ukosefu wa maabara za mifugo umewafanya ma afisa mifugo kuwa wapiga ramli chonganishi kwenye matibabu ya mifugo yetu.

Natanguliza shukrani!
 
Mie sina majibu ya tatizo lako, ila nimekuwa interested Tu na hiyo issue

Yani anakunywa maji na anayakojoa muda huo huo? Au Mie ndio sijaelewa
 
Kwa faida ya wafugaji wenzangu wa nguruwe,
Nilibahatika kupata ufumbuzi wa tatizo la nguruwe wangu na nashukuru sasa anaendelea vema,

Dr ameniambia nguruwe wangu alikua akisumbuliwa na moja ya matatizo yafuatayo ambayo yote yanamahusiano na utendaji kazi wa figo,
1)Kisukari
2)bacteria wanaoshambulia figo

Dr amenieleza dawa nzuri kwa tatizo ni sulphar,
Nimemchoma sulphar na kwa sasa mnyama anaendelea vizuri.

Note:
Dr alishauri licha yakuwa OTC inauwezo wakutibu tatizo hili lakini alishauri kutotumia OTC kabisa kwani moja ya side effect ya OTC hupelekea mkusanyiko wa kemikali kwenye figo ambayo tayari inatatizo.
Asanteni.
 
Hongera mkuu.
 
Hawa jamaa wanapata mpaka UTI na mawe kwenye figo
 
Mpeleke msikitini akapigiwe dua la maana jombaa🤣🤣🤣😁😄😃😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…