Uchaguzi 2020 Nguvu mpya, kasi mpya, ari mpya ya Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Nguvu mpya, kasi mpya, ari mpya ya Tundu Lissu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Adhabu ya kifungo cha kutofanya kampeni imemalizika jana saa tano na dakika 59 usiku, kwa hiyo kuanzia asubuhi hii ya leo ya tarehe 9 yuko huru kuendelea na kampeni zake.

That punishment wasn't a fair play in political grounds lakini waswahili wanasema kumpiga chura teke ni kumwongezea hatua kwakuwa tembea ya chura ni ya kurukaruka.

Lissu aliamua kukubaliana na uamuzi wa tume pamoja na kuwa adhabu husika haikuwa sahihi...lakini akatumia muda huo kujiachia na kufanya mengi ambayo kama si adhabu husika asingeyafanya kamwe.

Mengi aliyoyafanya yalikuwa burudani tosha kwake na kwa jamii lakini pia yakamuongezea umaarufu na ufahamu mpya wa maisha ya mtanzania wa kawaida huko mitaani na huko uswazi.

Matukio yake yote yametengeneza headlines na kufunika matukio mengine yote ya kiserikali kwa wiki hii yote ya adhabu. Tukio la ufunguzi wa stand mpya Mbezi lilidoda na kudorora kuliko tukio la Lissu kuzuiwa kuingia mkoa wa Pwani pale eneo la Gogoni.

Kuna ufunuo wa ajabu kwa CHADEMA na LISSU. Japo mamlaka na wapinzani wa Lissu na Chadema hawawezi kulikubali hili,lakini huo ndio ukweli mchungu. Lissu is unbeatable. CHADEMA is unconquered.

Mitandaoni, vijiweni, makazini, sehemu za starehe, majumbani na kila mahali ni mijadala ya Lissu na Chadema. Mfano hai ni hapa JF. Asilimia 90 ya habari za siasa ni Lissu na Chadema, bila hivi vitu viwili ni kama hakuna mijadala ama mijadala inakuwa imepoa na kupooza kabisa.

Kuna maono makubwa sana kwa CHADEMA NA LISSU, umaarufu wao umefika kileleni na kuvunja rekodi kupindukia. Ni ukweli mchungu kwenye masikio ya wapinzani wao.

Ujasiri wa ajabu wa Lissu umeipeleka Chadema next level, umewapa Wananchi mwamko mpya lakini wakati huohuo umepeleka ganzi kubwa CCM yote juu mpaka chini.

Ukufunzi wake mahiri wa sheria za uchaguzi kwenye majukwaa ya kampeni ni kigezo kingine kinachoongeza mvuto na ufuasi mkubwa kila alikopita.

Kibonzo cha DW kinamuonesha Lissu kama nyani mzee aliyekwepa mitego mishale na vizingiti vingi, lakini kiroho kinatoa tafsiri pana zaidi ya MBEBA MAONO. Kumbuka sterling hafi, mbeba maono hafi.


JamiiForums844291276.jpg
 
Wakija wale wenye hoja nyepesi watakuambia ni msaliti mara sio mzalendo utafikiri hiyo mikataba ya madini alisaini yeye kwa hati ya dharura huko bungeni.

pia wanasahau wakati Lissu akipambania wananchi wa Nyamongo enzi za Mkapa wapate haki zao kwenye madini Jiwe alikuwa kwenye baraza la Mawaziri akila anasa tuu lakini sasa hivi kageuka kuwa mzalendo kwavile hajui kiingereza lakini ana Phd.
 
"We suppose to focus according our direction, according our environment, that's only way we can help our peoples. No body should come and say that his there to save the problems of our peoples, we are the one we are leader we suppose to change the direction
From Birmingham palace!?[emoji848][emoji30][emoji2960][emoji2827]
 
Wakija wale wenye hoja nyepesi watakuambia ni msaliti mara sio mzalendo utafikiri hiyo mikataba ya madini alisaini yeye kwa hati ya dharura huko bungeni . pia wanasahau wakati Lissu akipambania wananchi wa Nyamongo enzi za Mkapa wapate haki zao kwenye madini Jiwe alikuwa kwenye baraza la Mawaziri akila anasa tuu lakini sasa hivi kageuka kuwa mzalendo kwavile hajui kiingereza lakini ana Phd
Hiki kibonzo kina tafsiri pana sana
JamiiForums1106629257.jpg
 
Huwezi amini nimejua kwamba Tanzania Kuna ugeni wa rais wa Malawi baada ya kusikia KINGEREZA CHA BABA JESKA kikijadiliwa otherwise Lissu ndio alitrend zaidi. I CAN'T REACH YOU.....!
Leo wana Tamasha la Fiesta pale Taifa tokea jana jioni mpaka saa hizi gari la matangazo linapita likitupigia kelele kwamba hata jiwe atakuwepo kwenye hiyo burudani kwahiyo tuende
 
"We suppose to focus according our direction, according our environment, that's only way we can help our peoples. No body should come and say that his there to save the problems of our peoples, we are the one we are leader we suppose to change the direction
Ongeza na hii mkuu kwenye hiyo para "so that to push the developments of our peoples!" Haaa, hiki Kibeberu au maneno ya Kibeberu? Eti naye Dr. anajitia aibu bure bora angekomaa na Kiswahili tu ili vyombo vimsaidie! Sijui Kibeberu 100% lakini cha huyu kimezidi!
 
Huwezi amini nimejua kwamba Tanzania Kuna ugeni wa rais wa Malawi baada ya kusikia KINGEREZA CHA BABA JESKA kikijadiliwa otherwise Lissu ndio alitrend zaidi. I CAN'T REACH YOU.
Nilikuwa Mbezi jana wakati wa ufunguzi. Tuweni wakweli na bila chembe ya unafique uzinduzi ulidoda magari ya serikali na chama yalikuwa chini kidogo ya idadi ya wahudhuriaji.
 
Nilikuwa Mbezi jana wakati wa ufunguzi. Tuweni wakweli na bila chembe ya unafique uzinduzi ulidoda magari ya serikali na chama yalikuwa chini kidogo ya idadi ya wahudhuriaji.
Nilikuwa Mbezi jana wakati wa ufunguzi. Tuweni wakweli na bila chembe ya unafique uzinduzi ulidoda magari ya serikali na chama yalikuwa chini kidogo ya idadi ya wahudhuriaji.
Na wewe Ulienda kuhudhuria ifunguzi?--- ulienda kumpa support stone?🤣
 
Adhabu ya kifungo cha kutofanya kampeni imemalizika jana saa tano na dakika 59 usiku...kwa hiyo kuanzia asubuhi hii ya leo ya tarehe 9 yuko huru kuendelea na kampeni zake....
Binafsi namkubali magufuri kwa kuboresha miundombinu, barabara ya kwenda kwetu kakonko-kasulu km 180 ipo kwenye ujenzi. Hivyo nimetangaza mara kadhaa kura yangu ni magufuri na familia yangu na wale wanaonitegemea nawashawishi wampigie kura JPM.

Lakini nikitafakari

1. Umuhimu wa katiba mpya
2. Lisu anavyo nyanyaswa kila kona. Kuna mahali ma dc wamejaribu kumpiga mawe, serngeti akazuiwa kupita maeneo muhimu, ukerewe kivuko kikaondoshwa wkt zilibaki dk 15 tu na nafasi zilikuwepo.
3. Kuzuiwa kufanya kampeni na tume
4. Wagombea wa upinzani kuengeliwa huku wa ccm wote wamepitishwa.
5. Kesi za kijinga alizo funguliwa
6. Maofisa wa polisi kuonesha u CCM wao (Shana-r.i.h, Kigondo, ocd hai, na wote walioleta figisu za kijinga

Frankly, natamani nimchague Lissu asaidie kuweka misingi ya democracy nchini. Hawa ma RC, DC, ded wanakaa na kupanga kuipitisha ccm, nachukizwa sana. Mambo haya hayana budi kukomeshwa.

Lkn JPM namkubali. Nina utata hakika

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Badala ya nyani sema paka.
Hiyo cartoon ni ya "nine lives of the cat".
[emoji818][emoji818][emoji818][emoji1536][emoji1536][emoji1548][emoji1548][emoji1548][emoji1534][emoji1534][emoji1545][emoji1545][emoji1545][emoji1545] Nilijaribu kufanya na kolabo ya nyani aliyekwepa mishale mingi
 
Back
Top Bottom