Nguvu ya Biashara ya Forex, Ujasusi na yaliyo nyuma ya pazia

Nguvu ya Biashara ya Forex, Ujasusi na yaliyo nyuma ya pazia

Yaani mtu anacopy maandishi ya wengine na kuyatafsiri bila ya kuwa acknowledge then wewe unakuja hapa kunitaka nimuheshimu? Na ndio maana nikasema angeweka hiyo link tusome wenyewe na kuweka maoni yake juu ya Forex Trading...maana anachoandika kuhusu huyu bwana Geogre Soron kiko exactly kama kilivyoelezwa kwenye hiyo link neno kwa neno kasoro Lugha
Wengine tuna-appriciate mchango wake wa kutafuta nondo na kuzitafsiri kisha kutulisha maarifa. Ninavyojua elimu hutolewa kwa wasiojua. Ukiona ulikuwa unajua, pita kushoto, tuache tusiojua tufaidi. By the way, hata elimu ya darasani tuliyofundishwa ni copy and paste kutoka vitabu mbalimbali vya wa-magharibi. Au kuna yeyote aliyeandika kitabu hapa Tanzania aliandika from his/her own brain? Think more na uache ushamba wa kujitia unajua.
 
Yaani mtu anacopy maandishi ya wengine na kuyatafsiri bila ya kuwa acknowledge then wewe unakuja hapa kunitaka nimuheshimu? Na ndio maana nikasema angeweka hiyo link tusome wenyewe na kuweka maoni yake juu ya Forex Trading...maana anachoandika kuhusu huyu bwana Geogre Soron kiko exactly kama kilivyoelezwa kwenye hiyo link neno kwa neno kasoro Lugha
Kinachokusumbua ni wivu na roho mbaya....sasa bila kuandikwa sehemu ye angejua wapi si lazima kiwe kimeandikwa ye ndo akapekue na kutuletea sababu sio wote wenye ujuzi,maalifa na uelewa wa kupekua huko na kuelewa kila mstari (hiyo inasababishwa na sababu nyingi kama kutokujua Lugha ya malkia,uvivu,uelewa wa haraka na pia kujitoa)....Sasa mtu kapekua huko katuletea hapa tena kwa Lugha yetu mama we unamkosoa basi ungeleta wewe (Ngoja niache kuandika maana kila navyozidi kuandika nazidi kukereka)
 
Yaani mtu anacopy maandishi ya wengine na kuyatafsiri bila ya kuwa acknowledge then wewe unakuja hapa kunitaka nimuheshimu? Na ndio maana nikasema angeweka hiyo link tusome wenyewe na kuweka maoni yake juu ya Forex Trading...maana anachoandika kuhusu huyu bwana Geogre Soron kiko exactly kama kilivyoelezwa kwenye hiyo link neno kwa neno kasoro Lugha

Mbweha wewe sasa nan kakuita uje kusoma kama katafsiri wewe unapungukiwa nin au we ndo George Soros Acha ubibi wewe punguza wivu The bold ana chama lake lina wana wengi utakufa kwa wivu shenzi kakuibia kazi yako.????
 
Mbweha wewe sasa nan kakuita uje kusoma kama katafsiri wewe unapungukiwa nin au we ndo George Soros Acha ubibi wewe punguza wivu The bold ana chama lake lina wana wengi utakufa kwa wivu shenzi kakuibia kazi yako.????
taratibu bas ucje kula ban tukakukosa tena jukwaa LA kikubwa
 
Si Angeweka tu link tusome wenyewe kisha aje na conclusions zake kuhusu hiyo biashara ya Forex
We mbona hukuweka,, binadamu bwanaaa, wivu utawaua jifunze kutoa credits binadamu hatuezi fanana jamaa yupo beyond your knowledge
 
BLACK WEDNESDAY: NGUVU YA BIASHARA YA FOREX, UJASUSI NA YALIYO NYUMA YA PAZIA

de483a8db03b3e42aa7355d44dbe9ac3.gif


SEHEMU YA TANO


"…uwekezaji unahitaji subira. Ni kama vile kupaka rangi nyumba na kusubiri ikauke. Au kupanda mmea na kuusubiri ukue. Kama wewe ni mtu mwenye kupenda furaha ya haraka haraka chukua elfu kumi yako nenda 'coco beach'.!"


- The Bold, 2018



'Dili' ya Karne

Katika sehemu iliyopita nilieleza namna ambavyo George Soros alianza kutengeneza position yenye thamani ya zaidi ya bilioni 10 za Marekani. Lakini pia tuliangalia kwa mapana maana ya 'short sell' katika soko la hisa na soko la fedha duniani.

Katika sehemu hii ya tano twende taratibu hatua kwa hatua tuone namna amnavyo George Soros alishort Paundi ya Uingereza na kuifilisi benki Kuu.

Karibu…

Usiku wa kuamkia tarehe 16 Septemba 1992 wakati ambao ulimwengu mzima umelala George Soros kupitia Quatumn Fund alikuwa anaazima na kuuza Paundi ya Uingereza kuzidi katika kiwango kikubwa na cha kutisha. Alikuwa anaazima kutoka kwa kila benki na mashirika makubwa ambayo yalikuwa tayari kumpatia.
Naamini mpaka sasa wote tunaelewa kwa upana maana ya short sell na hivyo tunaelewa kwa nini Soros alikuwa anaazima na kuiuza Paundi.

Katika ulimwengu wa masoko ya fedha duniani, wafanyabiashara wa fedha wana tabia kama mbwa mwitu. 'Hawalali' muda wote wakiwinda fursa za kuuza au kununua sarafu fulani.
Kwa hiyo kitendo hiki cha George Soros kuuza kwa kasi Paundi na kwa kiwango kikubwa mawimbi yake yaliwafikia pia Hedge Funfmds nyingine na wafanyabiashara wengine wa soko la fedha. Japokuwa kama nilivyoeleza huko awali kwamba katika kipindi hiki Soros bado hakuwa Bilionea maarufu kama tumjuavyo sasa lakini wafanyabiashara wengi wa soko la fedha walikiwa wanamfahamu yeye na kampuni yake na walifahamu na kuheshimu umahiri wake hasa hasa kwenye uchambuzi wa masoko ya Ulaya.

Hivyo basi baada ya kusikia kuwa George Soros alikuwa akiazima Paundi kwa kiwango kikubwa na kuziuza, karibia soko lote la fedha duniani likaanza kuuza Paundi ya Uingereza.

Mpaka kufikia muda ambao London Market inafunguliwa mida ya asubuhi, maafisa wa serikali waliianza siku kwa kushuhudia mabilioni ya Paundi yakiwa yameuzwa tayari. Kama ambavyo nilieleza kuwa sarafu fulani ikiwa inauzwa sana thamani yake kwenye soko inashuka. Ikinunuliwa sana, thamani yake inapanda.
Kwa hiyo kitendo cha Paundi kuwa inauzwa sana kilisababisha kuwe na presha ya kuitaka thamani yake ishuke. Kilichokuwa kinasaidia pekee ni ile hali ya serikali kuzingatia sharti kwamba Paundi isiuzwe chini ya 2.78 DM.

Lakini kitendo cha serikali kung'ang'ana kwamba thamani ya Paundi ibaki pale pale kilikuwa kinaumiza zaidi sarafu yao. Hakuna mfanyabiashara wa fedha ambaye alikuwa tayari kuinunua kwa thamani hiyo huku akijua fika kwamba kuna mabilioni kwa mabilioni ya Paundi yanauzwa na hii ikiashiria kwamba thamani ya Paundi inaelekea kuporomoka kwa kasi ya radi.

Kwa hiyo kulikuwa na njia mbili za kuhakikisha kwamba thamani ya Paundi inabaki juu. Njia ya kwanza ilikuwa ni kuhakikisha inaanza tena kununuliwa kwa kiwango kikubwa. Na njia ya Pili ilikuwa ni kuanza kucheza na Interest Rates.
Njia zote mbili hizi zilikuwa na changamoto zake.
Njia ya kwanza ya kuhakikisha inaanza tena kununuliwa ilikuwa haiwezekani kwa maana ya kwamba wafanyabiashara wakubwa wote walikuwa wanafuata kile ambacho Soros alikuwa anakifanya. Walikuwa wanauza kila Paundi waliyonayo na ile ambayo waliweza kuazima.
Njia ya Pili ya kuongeza Interest Rates ilikuwa ni hatari zaidi kwa kuwa nchi ilikuwa imetoka kwenye mdororo wa kiuchumi, kwa hiyo walihitaji kuhakikisha kuna spending kubwa kwa wananchi ili uchumi uendelee kuchangamka.


Ndio hapa inaturejesha tena kwenye kikao cha Waziri Mkuu John Mayor na wasaidizi wake nyumbani kwake Whitehall siku hiyo hiyo ya Septemba 16, 1992.


Nyumbani kwa Waziri Mkuu

Hali ya kikao ilikuwa tete kweli kweli. Wanasema siku ya kufa nyami miti yote inateleza. Ndicho ambacho kilikuwa kinawakuta serikali ya Uingereza. Kila suluhisho ambalo walikuwa wanalijadili na kulipendekeza lilikuwa haliwezekani kiutekelezaji.
Ndipo hapa wakafikia uamuzi ambao walikuja kuujutia baadae.

Kwa kuwa hakukuwa na mfanyabiashara mkubwa au shirika lolote la fedha au mabenki ambao walikuwa tayari kununua Paundi ya Uingereza (kila mtu alikuwa anauza) serikali ya Uingereza ikafikia uamuzi kwamba wao wenyewe kama serikali waanze kuinunua Paundi.
Kitu ambacho nataka ukumbuke ni kwamba, unaponunua sarafu fulani maana yake ni kwamba unatoa/unauza sarafu nyingine. Yaani kwa mfano ukisema unataka kununua sarafu ya kitanzania yenye thamani ya bilioni moja. Maana yake unatakiwa utumia mfano dola kama laki nne na nusu hivi kuinunua bilioni moja ya kitanzania. Ndio hapa tinasema unakuwa umenunua shilingi na umeuza dola.

Kwa hiyo kitendo cha serikali ya Uingereza kufikia uamuzi wa kutaka kuanza kuinunua Paundi maana yake ni kwamba walikuwa wanatumia akiba yao ya fedha za kigeni (Foreign Reserve) kuinusuru Paundi. Kama ikitokea George Soros akashinda vita hii maana yale ni kwamba watapata hasara mara mbili, sarafu yao kushuka thamani na watakuwa wamepoteza kiwango kikubwa cha akiba ya fedha za kigeni.

Mida ya saa 8:40 AM serikali ya walijibu mapigo ya Soros kwa kununua Paundi Bilioni moja!

Ajabu ni kwamba hakukuwa na muitikio wowote ule chanya katika soko. Bado watu waliendelea kuuza Paundi kwa kasi ya radi.

Ndipo hapa ambapo serikali ya Uingereza ikaanza mchezo mchafu wa propaganda.
Waziri wa Fedha wa Uingereza Bw. Norman Lamont akafanya kikao na waandishi wa habari na kueleza kwamba kuna mfanyabiashara (George Soros) ambaye alikuwa amedhamiria kuubomoa uchumi wa Uingereza. Waziri Lamont akajiapiza kwamba watatumia misuli yao yote kupambana na 'dhalimu' huyo ili kutetea uchumi wa Uingereza na akaweka hadharani mpango wa Serikali kutumia dola bilioni 15 kuitetea Paundi.

Kwa wale ambao wanafanya biashara ya Forex nadhani wanajua ni kwa kiasi gani ambavyo 'News' zinaathiri soko la fedha. Leo hii Trump hata akitweet tu tayari kwenye soko utaona athari zake. Ukisikia Mario Draghi, Rais wa Benki ya Ulaya anaongea na kama unahold 'pair' fulani yenye Euro ndani yake basi presha inakupanda. Ukisikia mwanamama Janet Yellen, Mwenyekiti wa Federal Reserve ya Marekani ana mkutano na waandishi wa habari alafu wewe unaifanyia biashara pair yenye USD ndani yake unaweza kuzimia. Ni kwa sababu hicho kitakachoongelewa eidha kitakupa faida ambayo itakufanya utabasamu mpaka koromeo lidondoke au habari hiyo itakupa kilio cha uchungu kufanana na msiba.
Binafsi naweza kusema katiba biashara ya fedha (forex) News ndio factor kubwa zaidi inayoamua uelekeo wa thamani ya sarafu. Na factor ya pili ni kubwa ni 'market markers' (hawa tutawaongelea huko mbele saikolojia yao na namna wanavyocheza na masoko ya fedha).

Kwa hiyo mkutano huu na vyombo vya habari ulilenga mambo mawili. Moja ni kutaka kuingiza hali ya uzalendo kwa mabenki ya Uingereza kuitetea Paundi ili kupambana na 'dhalimu' wa kimarekani ambaye anataka kuuzamisha uchumi wa Uingereza, na pili ni kujaribu kuiokoa Paundi kwa factor ya 'positive news' (nadhiri ya kutumia dola bilioni 15 kuitetea Paundi) maana yake thamani ya Paundi iende juu.

cd0ced9f8c8bb59fad15983e74e6777b.jpg

George Soros na Girlfriend wake Adrianna Ferreyr mcheza sinema kutoka Brazil


George Soros anajulikana kwa namna ambavyo yuko 'notorious' kwenye kutake risk za kibiashara.
Baada ya kusikia kuwa serikali ya Uingereza wanatumia dola bilioni 15 ya akiba yao ya fedha ya kigeni kuitetea Paundi, naye akaongeza position yake kutoka dola bilioni 10 mpaka dola bilioni 15.

Kwa hiyo kile kikao cha Waziri Lamont na waandishi wa habari pamoja na nadhiri ya kutumia dola bilioni 15 kuitetea dola haikuwa na matokeo yoyote chanya kwenye soko. Paundi iliendelea kuuzwa kwa kasi na kwa kiwango kikubwa katika soko la fedha la dunia.

Serikali ya Uingereza hawakuishia hapo tu. Japo walitangaza kutumia dola bilioni 15 kuitetea Paundi lakini walijikuta wanatumia fedha za kigeni zenye thamani ya Puandi bilioni 27 kuinunua Paundi.

Lakini misuli ya Soros ilionekana ngangari zaidi yao. Ulimwengu ulikuwa na imani zaidi na Soros kuzidi serikali ya Uingereza. Soros aliendelea kuhold position yake dhidi ya Puandi na ulimwengu mzima wa soko la fedha ulikuwa nyuma yake kwa kuendelea kuiuza Puandi kwa mabilioni na mabilioni.

Serikali ya Uingereza ilishikwa na kiwewe zaidi.

Kila mti ulikuwa unateleza.

Mbele yao walikiwa na silaha moja ya mwisho… Interest Rates.

Saa 9:00 AM Waziri wa fedha wa Uingereza wa kipindi hicho, Norman Lamont akampigia simu Waziri Mkuu John Mayor akiwa na pendekezo la mwisho la kuinusuru Puandi. Kwamba waongeze Interest Rates.
Naamini tunakumbuka nilivyofafanua namna gani ukiongeza interest rates thamani ya sarafu yako inapanda kwa kuwa wafanyabiashara na mabenki watainunua ili waiuze kwa faida hiyo ya juu.
Lakini kwa mazingira ambayo Uingereza walikuwa wanapitia ilikuwa ni wendawazimu kuongeza Interest Rates. Nilieleza kwamba nchi ikiwa kwenye mdororo wa kiuchumi unapaswa kushusha interest rates ili kuchochea spending na mzunguko wa fedha. Na ikumbukwe kwamba ukiongeza interest rates watakaonufaika moja kwa moja ni wafanyabiashara ya fedha na mabenki na sio mwananchi wa kawaida. Lakini pia kama wangelifanya hivi kulikuwa na tishio la kuurejesha uchumi wa Uingereza kwenye mdororo ambao wametoka mwaka mmoja tu uliopita.

Kwa hiyo pendekexo hili la Waziri Lamont ilikuwa ni wendawazimu katika viwango vyote.
Lakini uwendawazimu huu ndio ilikuwa silaha yao pekee ambayo ilikuwa imebakia.

Mara hii ya kwanza saa tatu asubuhi Waziri Mkuu John Mayor alikataa katakata kuongeza Interest Rates.

Kwenye soko la dunia Paundi ilikuwa inauzwa kwa kasi zaidi.

Saa 10:00 AM Waziri wa Fedha Norman Lamont alipiga tena simu kwa Waziri Mkuu akimuomba akubali ombi lake la kuongeza Interest Rates. Waziri Mkuu John Mayor akakataa kwa mara nyingine.

Paundi ikaendelea kuuzwa zaidi kwenye soko la Dunia.

Saa 11:00 AM Lamont akapiga tena simu kwa Waziri Mkuu. Safari hii akimtaka Waziri Mkuu amwambie wafanye nini? Waziri Mkuu hakuwa na jawabu… wala hakuna mtu yeyote kwenye serikali ya Uingereza ambaye alikuwa na jawabu. Silaha pekee ambayo walibakiwa nayo ilikuwa ni Interest Rates.
Hivyo basi saa 11:30 AM Waziri Mkuu John Mayor alikubali ombi la Waziri wa Fedha kuongeza Interest Rates.

Kwa hiyo majira ya saa sita kasoro mchana, serikali ya Uingereza ilitangaza kuongeza Interest Rates kwa basis points 200… yaani kutoka 10% mpaka 12%.

Ilikuwa ni 'dili' nono ambayo ingewatoa mate wafanyabiashara wote wa fedha duniani. Lakini watu katika ulimwengu wa fedha walikuwa wanamuangalia Soros atafanya nini.
"Don't bite!" Ndilo jibu pekee ambalo Soros aliwajibu wafanyabiashara wenzake na mabenki ambao mate yaliaanza kuwatoka kutokana na kuongezwa kwa interest rates. Aliwaonya kwamba 'meli' inaelekea kuzama. Wasijitumbukize wakazama nayo.

6c9b5a857e54582c7393a3b054a884cc.jpg

Waziri Norman Lamont akiwa na mentee wake, David Cameroon kipindi akiwa kijana


Bundi aliendelea kulia mlangoni kwa serikali ya Uingereza… ulimwengu uliendelea kuuza Paundi kwa kasi. Licha ya kuongeza interest rates bado watu walikuwa na imani na kile ambacho Soros alikuwa anakiona akilini mwake. Anguko la Paundi la Kihistoria.

Ndipo hapa ambapo serikali ya Uingereza ikafanya jambo lingine la uwendawazimu zaidi.
Majira ya saa 04:00 PM Waziri Lamont alielekea nyumbani kwa Waziri Mkuu John Mayor maeneo ya Whitehall kuungana na wengine walioko huko kufanya mjadala nini zaidi kifanyike kuinusuru Paundi.
Baada ya majadiliano ya masaa kadhaa wakatoka na moja ya uamuzi wa ajabu zaidi kiuchumi kuwahi kufanyika.

Serikali ya Uingereza ikatangaza tena kuongeza Interesf Rates kutoka ile 12% waliyoongeza awali mpaka 15%..!!!

Ilikuwa ni ajabu kweli kweli hasa ukizingatia hali tete ya kiuchumi ambayo Uingereza walikuwa nayo kipindi hicho.
Naomba ieleweke kwamba mfano sasa hivi, serikali nyingi ulimwenguni huwa wanatangaza viwango vipya vya interest rates maro moja kwa mwezi. Kwa hiyo kitendo cha serikali ya Uingereza kutangaza interest rates na kuzipandisha mara mbili ndani ya siku moja kilikuwa ni kitu cha ajabu kuzidi maelezo ninayoweza kuyatoa.

Mabenki na wafanyabiashara wengi mate yalianza kuwatoka. Lakini macho yao yalikuwa kwa Soros. Atafanya nini?
Soros alikuwa na jibu moja tu… kwamba serikali ya Uingereza ilikuwa 'desperate'! Wanachokifanya si jambo la kawaida kiuchumi, na hii inaonyesha ni kiasi gani ambavyo walikuwa desperate na hawana mbinu yoyote waliyobakiwa nayo kuinusuru Paundi. Hii maana yake ni kwamba walikuwa wanaelekea kusalimu amri na kupiga magoti. Walikuwa wanapaparika kama kuku anayekata roho. Hawakuwa na ujanja. Walikuwa wamewashika 'sehemu nyeti' na muda si mwingi watasalimu amri.

Kwa hiyo Soros akawahamasisha wenzake… "sell it!! Sell it as much as you can get!! Sell the GBP! Sell it against any other currency… Sell it against the US Dollar, Sell it against AUD, sell CAD, sell it against chinese Yen, sell it against Korean Won… just sell it as much as you can and by the time we go to sleep today we will have a fortune.."

Paundi iliuzwa kama njugu kwenye soko la fedha la dunia. Kwa mabilioni na mabilioni zaidi. Na kwa kasi ambayo haijawahi kutokea.

Serikali ya Uingereza hawakuwa na ujanja tena. Hawakuwa na silaha nyingine yoyote ile. Mafuriko ambayo walikuwa wameyazuia kwa mikono kwa siku nzima yalikuwa yamewazidi nguvu. Ulikuwa ni muda wa kupiga magoti, kuelekea kibla na kuchinjwa.

Muda wowote ulimwengu ulikuwa unatarajia serikali ya Uingereza kutangaza kushusha thamani ya Paundi na kujitoa kwenye mpango wa ERM.

Wanasema kwamba kama unaweza kuona 'aura' ya binadamu unaweza kujua kabla kifo akija mpata. Kwamba ukiangalia mfano picha ya mwisho ya marehemu Tupac, machoni mwake unaweza kukiona kifo kabisa. Unaweza kuona woga ambao anao. Unaweza kuona hofu ndani ya nafsi yake. Unaweza kuona kabisa kifo kikiwa kinamnyemelea.

Ndivyo ambavyo aura ya Waziri Norman Lamont ilivyokuwa alipoingia kwenye ukumbi wa mkutano na waandishi wa habari mida ya saa 07:30 PM.
Chumba chote kilikuwa kimya. Kelele cha kamera tu ambazo zilikuwa zinafotoa picha ndizo ambazo zilikuwa zinasikika. Waziri Lamont aliingia akiwa ameongozana na wasaidizi wake kadhaa pamoja na watu wa benki kuu na hazina. Wananchi wa Uingereza ambao walikuwa wanafuatilia mubashara mkutano huu wa Waziri na waandishi wa habari hofu ilikuwa imewajaa mioyoni mwao. Ni mwaka mmoja tu wametoka kwenye mdororo wa kiuchumi na leo hii kitakachotamkwa na Waziri kinaweza kuirudisha Uingereza kwenye mdororo kama ule au zaidi.

Lakini kwa upande wa Soros hii ulikuwa ni wakati ambao amekuwa anausubiri kwa zaidi ya miezi miwili tangu aanze kujenga position yake ya mabilioni dhidi ya Paundi. Na wakati huo ndio ulikuwa umewadia.
Yeye pamoja na vijana wake walikuwa wamejikusanya mbele ya runinga ofisini kwao New York wakifuatilia mubashara kabisa mkutano huu wa Waziri Lamont na wanahabari.

Wakati wa kujua mbivu na mbichi ulikuwa umewadia.



Stay here… narudi!


The Bold - 0718 096 811 (WhatsApp Only)
To Infinity and Beyond

Pls: Follow, subscribe and nifuate WhatsApp
Gud 1
 
BLACK WEDNESDAY: NGUVU YA BIASHARA YA FOREX, UJASUSI NA YALIYO NYUMA YA PAZIA



SEHEMU YA PILI


"…maisha hayajali kama uko sahihi au hauko sahihi. Bali maisha yanajengwa na kiasi gani cha faida unapata pale unapokuwa sahihi na kiasi gani cha hasara unapata pale unapokuwa hauko sahihi.."

- The Bold, 2017



GENESIS

Unapochunguza tukio lolote lile, usikimbilie kwenye hitimisho. Kwa sababu hata siku moja hakuna hitimisho linalotoa jawabu. Kila hitimisho ni muitikio akisi ya mjengeko wa chanzo au mizizi. Kwa hiyo ili kufahamu uhalisia wa suala lolote lile ni vyema kutazama matokeo yake lakini ni jambo la weledi zaidi kama ukizama na kufukua mzizi wake.

Kwa hiyo kabla sijaeleza namna ambavyo George Soros aliweza kuipigisha magoti nchi nzima ya Uingereza, kisa ambacho nitakitumia kujenga hoja zangu na maoni yangu juu ya biashara ya Forex ambayo imejizolea umaarufu hivi karibuni, kwanza kabisa nataka kutumia fursa hii kufukua mzizi wa tukio la Septemba 16, 1992 ambalo kwenye sehemu ya kwanza nilieleza kwamba Waziri Mkuu alikuwa ameitisha mkutano wa dharura nyumbani kwake Whitehall.

Ni kwamba,

Baada ya vita kuu ya pili ya Dunia, nchi za Ulaya ziliazimia kuunganisha uchumi wao kwa pamoja kwa mkazo zaidi.
Ikumbukwe kwamba ni miongo kama mitano tu nyuma kulikuwa kumemalizika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Vita hizi zote zilikuwa na hasara kubwa sana za kiuchumi. Kwa hiyo lengo kuu la kwanza la dhamira hii ya nchi za Ulaya kuunganisha chumi zao ilikuwa ni kujaribu kuzuia kutokea kwa vita kuu nyingine kwa maana ya kwamba, chumi hizi kama utatengenezwa mfumo wa kuziunganisha maana yake ni kwamba zitakuwa zinategemeana. Na kama zikitegemeana maana yake ni kwamba kila nchi itakuwa inawajibika zaidi kuepuka kutokea kwa vita nyingine ili kulinda uchumi wa nchi zao (yaani nchi yoyote katika jumuiya hiyo ikiingia vitani maana yake chumi za nchi nyingine zote ndani ya jumuiya nazo zitaathirika).
Kwa hiyo hill lilikuwa ni lengo kuu la kwanza kabisa.

Lengo la pili lilikuwa ni hatimaye kupatikane Umoja rasmi wa kisiasa na kidiplomasia ambao utachochea zaidi mshikamano wa nchi za Ulaya kiuchumi na hatimaye kuwa na uchumi ambao unaweza kushindana na nchi ya Marekani.

Wengi tunaifahamu EU (European Union) ya sasa ambayo ilianzishwa rasmi mwaka 1999. Lakini kwa kipindi hicho cha miaka baada ya Vita kuu ya pili ya Dunia, yaani mwaka 1957, nchi za Ulaya walianzisha chombo kinachoitwa European Economic Community (ECC). Kama ambavyo nilieleza awali, chombo hiki lengo lake kuu lilikuwa ni 'economic intergration.' Kujenga mafungamano ya kiuchumi baina ya nchi zote za Ulaya.

Sasa basi, mojawapo ya sera za kukumbukwa zaidi chini ya chombo hiki ilikuwa ni uanzishwaji wa mfumo wa ERM (European Exchange Rate Mechanism). Sera hii ilianza kutekelezwa rasmi mwaka 1979.

Kipindi ambacho nchi hizi ziliungana kuanzisha chomo hiki cha uchumi kulikuwa na pendekezo la kuwa na sarafu moja. Lakini nchi nyingi hazikuwa tayari kuachilia sarafu zao na kuanza kutumia sarafu mpya.
Kwa hiyo mwaka huu 1979 walipoanzisha sera ya ERM walikubaliana kwamba kila nchi itaweka thamani ya sarafu yake kulingana na thamani za sarafu za nchi nyingine ndani ya Ulaya.

Kwa kawaida, thamani ya sarafu ya nchi inatokana na namna 'inavyoperform' kwenye soko kwa kuzingatia kanuni za 'demand and supply'. Thamani yake itapanda au kushuka kutokana na namna inavyohitajika na upatikanaji wake.


Lakini nchi za Ulaya zenyewe kipindi hicho kwa kuona wingi wao wa nchi wanachama, walidhamiria kulinda thamani za sarafu zao.

Sasa basi, kwa kuwa Ujerumani ndio ambayo ilikiwa na uchumi mkubwa zaidi na imara, kwa hiyo sarafu za nchi zote kwenye jumuiya zilitakiwa kuweka thamani yake kulingana na thamani ya fedha ya Ujerumani ambayo kipindi hicho walikuwa bado wanatumia Deutschmark (DM).

Kuna jambo moja la muhimu ambalo tunapaswa kuliweka akilini. Pale ambapo serikali inakuwa inaamua kufuata mfumo huu wa kuweka 'fixed exchange rates' inapaswa pia kushiriki moja kwa moja kwenye soka la biashara ya fedha. Kivipi?
Unapoacha sarafu yako 'ifloat' kwenye soko, maana yake ni kwamba soko ndilo litaamua kiwango cha 'exchange rate' ya sarafu yako dhidi ya sarafu za nchi nyingine. Hii ni tofauti kabisa na kama ukiamua kuwa na 'fixed exchange rate'. Unapswa kujihusisha muda wote kwenye soko ili kuhakikisha 'exchange rate' inabaki pale ambako unataka.

Hii ikoje?

Tuseme kwa mfano nchi imeweka 'exchange rate' yake katika kiwango fulani. Sasa kuna namna mbili ambazo serikali (benki kuu) ambayo imeamua kuwa na fixed exchange rate wanakuwa wanafanya ili kiwango hicho kibakie pale.

Moja ni kushiriki na kwa kuuza na kununua sarafu yao kwenye soko. Serikali inaweza kuamua kuweka fixed exchange rate lakini soko nalo linatoa presha kwa kiwango hicho kilichowekwa eidha kama ni kikubwa sana au kidogo sana kwa kuzingatia kanuni ya 'demand and supply' ya sarafu husika. Kwa hiyo mara kadhaa soko la fedha la dunia litatoa presha kwa kiwango hiki fixed kiweze kubadilika. Sasa serikali wanachofanya ni kuuza au kuinunua sarafu yao. Kwa mfano kama kukiwa na presha ya sarafu kushuka chini ya kiwango kile cha exchange rate ambacho wamekiweka, serikali itatumia hazina yake ya fedha ya kigeni kuinunua sarafu yake. Hii itasababisha thamani ya sarafu husika kupanda kutokana na 'supply' kuwa ndogo na hatimaye kiwango cha exchange rate kubaki pale ambako serikali imeweka.

Pia ikitokea kwamba kuna presha ya exchange rate kupanda kuzidi pale ambapo serikali wameweka, kinachofanyika serikali yenyewe inaanza kuiuza sarafu yake. Hii itafanya thamani ya sarafu husika kushuka kutokana na 'supply' kuwa kubwa na hivyo exchange rate inarudi pale ambako serikali inataka.

Njia ya pili ambayo serikali ambayo inayoweka fixed exchange rate wanashiriki kwenye soko ili exchange rate ibaki pale pale ni kwa kucheza na Interest Rates.
Kwa mfano serikali ikitaka sarafu yake ipande thamani wanachoweza kufanya ni kuongeza Interest Rates. Unapoongeza Interest Rates maana yake ni kwamba mabenki, mashirika makubwa ya fedha na wenye mitaji mikubwa watanunua zaidi sarafu yako ili waweze kuikopesha kwa faida kubwa (umeongeza interest rates). Lakini pia kama ukitaka thamani ya sarafu yako ishuke, unachofanya unaweza kushusha interest rates. Maana yake ni kwamba mabenki na wenye mitaji mikubwa ya fedha watapunguza kununua sarafu yako na kwenda kununua sarafu nyingine zenye rates za juu. Hii itafanya sarafu yako kushuka thamani.

Huu mchezo wa kucheza na interest rates ni adhimu sana kwa serikali zote duniani. Ni moja ya turufu adhimu zaidi ambayo serikali wanayo ili kurekebisha uelekeo wa kiuchumi. Kwa mfano kama nchi ikiwa kwenye mdororo wa kiuchumi, serikali inaweza kushusha interest rates ili kuchochea uwekezaji na matumizi (spending). Au kwa mfano kukitokea mfumuko mkubwa wa bei (inflation), serikali inaweza kuongeza interest rates ili kupunguza mzunguko wa fedha na hivyo kuongeza demand ya sarafu yao na kufanya inflation kwenda chini.


Nadhani unapata picha walau kidogo ni namna gani pale serikali ikiamua kuwa na 'fixed exchange rates' inapaswa kuhusika kwa kiwango kikubwa mno katika soko la dunia la fedha. Ni suala ambalo kama serikali halitalifanya kwa makini, kosa dogo tu linaweza kuzamisha uchumi wa nchi.

d08fed72cfb6ce6eabb0566a8a2a1c5d.jpg

Waziri Mkuu Margaret Thatcher na Rais Regan wa Marekani


Hii inatupeleka mpaka mwaka 1990. Katika kipindi hiki nchi ya Uingereza ilikuwa inapitia kwenye moja ya vipindi vigumu zaidi vya kiuchumi. Mfumuko wa bei ulikuwa mkubwa, uzalishaji umeshuka kwa kiwango kikubwa na uuzaji wa bidhaa nje umeporomoka. Mbaya zaidi serikali ilikuwa inaonekana kwamba hawakuwa na uwezo wa kutatua mdororo huu wa kiuchumi.

Ikumbukwe kwamba mpaka kipindi hiki, nchi ya Uingereza bado ilikuwa haijajiunga na mpango wa ERM. Kwa hiyo zilianza kelele nyingi za wanasiasa kushinikiza serikali waingie kwenye mpango wa ERM kama ilivyo kwa nchi nyingine za Ulaya na labda inaweza kusaidia kufufua kwa kasi tena uchumi wa nchi yao.

Waziri Mkuu wa Uingereza wa kipindi hicho Bi. Margaret Thatcher alikuwa anapinga vikali mpango huu wa ERM. Alikuwa anaamini kwamba viwango vya exchange rate vinapaswa kujiweka vyenyewe kutokana muelekeo wa soko badala ya serikali kuingilia na kuweka viwango 'fixed.'
Ubaya ni kwamba hali ya kiuchumi haikuwa nzuri na wananchi wa Uingereza hawakuwa na imani na serikali kama walikuwa na uwezo wa kuwaondoa kwenye mdororo huo.

Kwa kifupi Bi. Margaret Thatcher hakuwa na 'mtaji' wa kisiasa kushawishi wananchi na hata mawaziri wake kwamba Uingereza isiingie kwenye mpango wa ERM. Kulikuwa na sauti nyingi sana za watu wazito lakini sauti ambayo ilikuwa kinara zaidi katika kushinikiza Uingereza kuingia kwenye mpangobwa ERam alikuea ni Waziri wa Fedha wa kipindi hicho Bw. John Major (huyu ndiye alikuja kuwa Waziri Mkuu baadae) yeye na wenzake wote walitaka Uingereza kuingia kwenye mpango wa ERM.
Kutokana ma msukumonwa kisiasa na uchumi kuendelea kudorora hatimaye mwezi Octoba, 1990 nchi ya Uingereza ikaingia kwenye mpango wa ERM.

Kama ambavyo nilieleza pale awali kwambwa kwa kuwa uchumi wa Ujerumani ulikuwa ndio mkubwa na imara kuliko chumi nyingine zote kwa hiyo thamani za sarafu zote za nchi zote wanachama vilipewa thamani kutokana na Deutsh Mark (DM) ya Ujerumani.
Uingereza yenyewe ilipojiunga Paundi yake ilipewa thamani ya 2.95 DM. Yaani Paundi moja ya Uingereza ni sawa na 2.95 DM za Ujerumani. Pamoja na hilo serikali ya Uingereza walitakiwa wahakikishe kuwa kwa kipindi chote thamani ya Paundi haitoki kati ya 2.78 DM mpaka 3.13 DM.

Haukupita muda mrefu, John Mayor ambaye ndiye alikuwa mstari wa mbele kushawishi Uingereza kuingia kwenye mpango wa ERM alishika madaraka ya Uwaziri Mkuu kuchukua nafazi ya Bi. Margaeret Thatcher.

Muda si muda mambo yaakanza kwenda sawia. Hiyo ilikuwa ni mwaka mwishoni mwa 1990 na mwaka 1991 na mwanzoni mwa mwaka 1992.
Mfumuko wa bei ulishuka, interest rest zikaaa kwenye mstari na kiwango cha wasio na ajira kilikuwa chini kabisa kwenye kiwango cha kihistoria. Kwa kifupi mambo yalikuwa swadakta kabisa. Waziri Mkuu mpya Mhe. John Mayor akaonekana shujaa machoni kwa Waingereza na kiongozi wa kupigiwa mfano duniani.

13773d5f3b00ee5520b4d1b459dd1c81.jpg

Waziri Mkuu John Major


Wakati huo huo, Jijini New York

Kuna msemo wa waswahili wanasema kwamba, wewe ukijua ya mbele, wenzako wanajua ya pembeni… na wewe ukijua ya pembeni basi wenzako wanajua ya nyuma.

Hiki ndicho ambacho kilikuwa kinatokea

Jijini New York nchini Marekani katika ofisi maridadi za Kampuni ya Quatumn Fund alikuwa ameketi mtu ambaye kwa sasa hakuna ambaye alikuwa qnamjua au anamfuatilia kwa sasa. George Soros alikuwa anafuatilia hatua kwa hatua kile ambacho kilikuwa kinaendelea nchini Uingereza.

Wakati Waingereza wakiwa wanafurahi na kushangilia uchumi wao kutengamaa… huko jijini New York, kulikuwa na sisila, George Soros ambaye mpaka muda huu pengine ndiye alikuwa mtu pekee duniani aliyeona 'loop hole' katika hali hii ya "kutengemaa kwa uchumi" kwa Uingereza. Alikuwa ameusoma mchezo wote hatua kwa hatua… kwa hiyo ndio maana wakati Waingereza wakishangilia na Dunia ikimpongeza Waziri Mkuu John Mayor, wakati ambao hata watu wa serikali wenyewe, baraza la mawaziri na wataalamu wao wakiona neema na kuwafamya wapongezane kwa kugongesha glass… yeye George Soros hakuona 'kushamiri kwa uchumi' bali aliona 'limbo', shimo refu la giza… na alidhamiria kutengeneza mpango maridhawa kabisa na kuitumbukiza nchi ya Uingereza kwenye shimo hilo. Pia alitaka kutumia fursa hii kuandika jina lake kwenye vitabu vya historia kwa vizazi na vizazi kwa karne kadhaa zijazo.



Chiefs, tupate kifungua kinywa kwanza… tutaendelea.


The Bold
To Infinity and Beyond
Noma sana
 
Aisee Mkuu Hongera Nyingi Kwako, Ni Elimu Moja Kubwa Sana, Na Hii Inasaidia Kwa Namna Moja kujua Kwa Mapana Yake kuhusu hiyo Biashara Ya Foreign Exchange, Kubwa Ambalo Naamini THE BOLD upo sahihi sana na Kwa Unalofanya Ujakoseaa tena Kubwa Zaidi pengine Baada Ya kutafsiri na kuiweka hapa Umepunguza Baadhi ya Propaganda Za Kwenye Uandishi kutuleletea Kitu very short but Clear Na Yenye kueleweka Zaidi, Lakini Pia Msaada Kwa Sisi ambao Tunaitaji Kuijua biashara ya Forex ila Vitabu vyake vina Lugha ambayo ukivisoma Inabidi Uwe na Panadol pembeni bila Kusahau KAMUSI ya kiingereza Na Inapelekea page moja Kuisoma Masaa Matatu, Ila Wewe mkuu daa Yani Unatufanya Tusome Page Mia (100) kwa Dakika Chache tu...BIG UP and Thenx To You
 
the bold safi sana. but nimekutext wassup kitambo..but kimya.
 
Si Angeweka tu link tusome wenyewe kisha aje na conclusions zake kuhusu hiyo biashara ya Forex
Link zipo tangu zamani ila shule ndo tatizo kwa wantanzania walio wengi, unafikir wametumia ligha ya kwenu, pia kuna maneno ya kitaalam ya biashara kama umesoma engineering huwez elewa so jamaa anapoteza muda wake kukinyumbulishia kila kitu wewe unateleza unaona rahisi,
 
Link zipo tangu zamani ila shule ndo tatizo kwa wantanzania walio wengi, unafikir wametumia ligha ya kwenu, pia kuna maneno ya kitaalam ya biashara kama umesoma engineering huwez elewa so jamaa anapoteza muda wake kukinyumbulishia kila kitu wewe unateleza unaona rahisi,
Tatizo sio shule tu tatizo kubwa n lugha" tukubali tukatae watz wengi lugha imetukataa haswa hasa hizi article za wenzetu wanatumia lugha ngumu kama lugha yenyew rasha rasha kama yangu hapa hamna kitu utaelewa zaidi ya kuhamia insta kwenye umbea wa kina mange
 
Aisee Mkuu Hongera Nyingi Kwako, Ni Elimu Moja Kubwa Sana, Na Hii Inasaidia Kwa Namna Moja kujua Kwa Mapana Yake kuhusu hiyo Biashara Ya Foreign Exchange, Kubwa Ambalo Naamini THE BOLD upo sahihi sana na Kwa Unalofanya Ujakoseaa tena Kubwa Zaidi pengine Baada Ya kutafsiri na kuiweka hapa Umepunguza Baadhi ya Propaganda Za Kwenye Uandishi kutuleletea Kitu very short but Clear Na Yenye kueleweka Zaidi, Lakini Pia Msaada Kwa Sisi ambao Tunaitaji Kuijua biashara ya Forex ila Vitabu vyake vina Lugha ambayo ukivisoma Inabidi Uwe na Panadol pembeni bila Kusahau KAMUSI ya kiingereza Na Inapelekea page moja Kuisoma Masaa Matatu, Ila Wewe mkuu daa Yani Unatufanya Tusome Page Mia (100) kwa Dakika Chache tu...BIG UP and Thenx To You

Vitabu rahis vipo kibao ila kwa ushauri kama upo Dsm kaanze pale TMT usome ndio mambo mengine utaelewa kwa mapana..... ila kumbuka sio kila mtu lazma afanye forex ingawa leo watu wengi wamepata pesa mingi wengine mpaka $12,000
 
BLACK WEDNESDAY: NGUVU YA BIASHARA YA FOREX, UJASUSI NA YALIYO NYUMA YA PAZIA

90221c19b7041e730383a45a5f4f3397.jpg


SEHEMU YA SITA


Waziri wa fedha Norman Lamont alikwenda moja kwa moja mpaka mahala pa kuzungumza ambako alikuwa ameandaliwa.

Muda mchache uliopita alikuwa amemaliza kikao na Waziri Mkuu John Major, Waziri wa mambo ya nje Douglas Hurd, Rais wa Bodi ya Biashara nchini Uingereza Bw. Michael Heseltine na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Kenneth Clarke. Alikuwa amefika hapa kutangaza uamuzi ambao ulikuwa umefikiwa na kikao hicho cha dharura.

Baada ya waandishi wa habari kutulia, Waziri Lamont kwanza alianza kueleza namna ambavyo kuna hali ya dharura ya kiuchumi ambayo imeikumba Uingereza. Kwamba uchumi umeanza kwenda kombo tofauti na ambavyo walikuwa wanatarajia. Pia alieleza namna ambavyo sarafu yao ilikuwa kwenye msongo mkubwa wa kushindwa kuwezesha biashara kufanyika na kuchochea uwekezaji kutokana na kuonekana thamani yake iko juu zaidi tofauti na uhalisia.

Hivyo basi kutokana na Uingereza kuwa ndani ya mpango wa ERM ambao unatoa sharti la kuweka thamani ya Paundi kati ya 2.78 DM na 3.31 DM, kwa hiyo kwa masikitiko makubwa Waziri Lamont alitangaza kwamba Uingereza inajitoa kwenye mpango wa ERM na kufloat sarafu yake (kuacha thamani ya sarafu iamuliwe na soko la fedha).
Waziri Lamont alieleza pia kuwa interest rates inashushwa mpaka 12% (kesho yake ilishushwa tena kurudi 10%).

Kimya cha woga kilitawala kwenye chumba cha mkutano wa habari, lakini huko jijini New York kwenye ofisi za Quatumn Fund pamoja na ofisi nyingine zote za hedge funds na wafanyabiashara wa fedha kulitawaliwa na vifijo na nderemo.

George Soros na wote walioamini katika kile ambacho alikuwa anakiona kwa muda wa miezi miwili iliyopita walikuwa wameshinda ushindi wa kishindo.

Dakika chache tu baada ya Waziri Lamont kutangaza kuwa Uingereza wanajitoa kwenye mpango wa ERM na kufloat sarafu yao, thamani ya Paundi ilishuka kwa 25% dhidi ya dola.

Nilieleza kwamba position ya Soros dhidi ya Paundi ilikuwa na thamani ya $ 15 Bilioni. Siku hiyo mara tu baada ya Waziri Lamont kutoa tangazo la kufloat Paundi, thamani ya position ya Soros ilipanda mpaka $ 19 Bilioni na wiki mbili baadae ikaongezeka mpaka $ 22 Bilioni. Au kwa maneno machache, George Soros na Quatumn Fund walitengeneza faida ya Dolla Bilioni saba.!!
Nilieleza kuwa Hedge Fund managers wanapata 20% ya kila trade ambayo inaleta faida kwenye kampuni. Kwa hiyo katika trade George Soros alipata kiasi cha dollar billion 1.4 za kimarekani.

Asili ya biashara ya fedha ni kwamba kama wewe ukipata faida maana yake kwamba kuna mtu anapata hasara. Na katika trade hii George Soros alipata faida hiyo ya kutisha huku Benki kuu ya Uingereza ikiingia kwenye hasara ya karibia Dollar Billion 10 za kimarekani. Pamoja na hasara hii pia Uingereza walikuwa wamepoteza mabilioni ya akiba ya fedha za kigeni siku hiyo walipokuwa wakijitahidi kuokoa thamani ya Paundi.

Mwanzoni kabisa mwa makala hii nilieleza kwamba kabla ya mwaka 1992 kipindi Margareth Thatcher alipokuwa Waziri Mkuu, alipinga vikali Uingereza kuingia kwenye mpango wa ERM na serikali kujihusisha kwenye kuweka exchange rate ya Paundi. Alitala thamani ya Paundi iamukiwe na soko. Lakini John Major na wafuasi wake walipambana vikali kutaka Uingereza kuingia kwenye mpango wa ERM.

c0d349044a22e950219fb68efba6aea2.jpg


Kwa kuwa kipindi kile Uingereza ilikuwa kwenye mdororo mkali wa Kiuchumi hakuna mtu ambaye alimsikiliza Margareth Thatcher.
Hatimaye John Major aliingia madarakani huku akitumia mpango wa ERM kama mtaji wake kisiasa. Kwa hiyo kitendo cha kutokea anguko kubwa hivi la thamani ya Puandi kushuka na Uingereza kujitoa kwenye mpango wa ERM kulimgharibu mno. Hakuwa tena na mtaji wa kisiasa na wananchi wa Uingereza walimuona kama yeye ndiye ambaye aliwatumbukiza kwenye shimo hilo. Kwa hiyo kwenye uchaguzi uliofuata John Major na chama chake waliondolewa madarakani.

Na siku hii ya 16 September 1992 ni siku ambayo watu wa Uingereza hawaisahau maisha yao yote kutokana na machungu ambayo waliyapata na ndipo hapa waliibatiza jina kwamba ni BLACK WEDNESDAY.!

Lakini siku hii ndiyo siku ambayo Soros aliandika jina lake kwenye historia ya Dunia na kujizolea umaarufu kwenye soko la fedha la dunia na kudhihirisha kwamba yeye ni moja ya traders bora zaidi wa soko la fedha kuwahi kutokea chini ya jua.


Chiefs, hiyo ndiyo nguvu ya biashara ya Forex. Trader mmoja tu, tena ambaye kipindi hicho hakuwa na umaarufu au ushawishi mkubwa… lakini alitunishiana misuli ya kibiashara na maarifa ya soko la fedha dhidi ya benki kuu ya nchi na nchi nzima na kuwashinda na kutengeneza utajiri ndani ya siku moja tu.


Mpaka hapa nimeongelea upande mmoja wa biashara ya Forex (Nguvu ya Biashara hiyo) bado upande wa pili (yaliyo nyuma ya pazia) ambapo inahusu 'market markers' namna wanavyofanya kazi na kuathiri soko la fedha na namna ya kukabiliana nao.
Kipengele hicho nitakuwa naweka taratibu taratibu kama vidokezo (kwenye Morning and Evening Bulletins) ila mpaka hapa niseme kamba Makala hii imefika mwisho.

Naamini kwamba kuna kitu umepata na kujifunza.

eda09faec7d4dc83d8aff9aa59f17d4c.jpg


My Personal Expirience with Forex

Binafsi mara yangu ya kwanza kusikia hili suala ilikuwa ni mwaka 2013. Nimewahi kufanya kazi 'maalumu' na Shirika la World Vision Tanzania hasa kwenye programu zao vijana. Kuna siku nilikuwa naandaa 'speech' kuna vijana wa sekondari nilialikwa kuzungumza nao. Nikiwa kwenye maandalizi hayo ya speech nikawa natafuta mfano mzuri wa kijana mdogo ambaye amefanikiwa kwa kiwango kikubwa kwenye sekta aliyopo, nikawa naperuzi mtandaoni kuona kama naweza kupata mifano mizuri, ndipo nikakutana na Makala kuhusu kijana Sandile Shezi wa Afrika Kusini ambaye nadhani ni moja ya watu waliofanikiwa zaidi barani Afrika kwenye biashara ya Forex. Kipindi kile naisoma ile makala alikuwa na kama miaka 21 tu au 22.

Nilivutiwa sana na stori yake. Kwa hiyo hata baada ya kuandika speech yangu na kuzungumza na wale wanafunzi niliendelea kumfuatilia Sandile na mambo ambayo alikuwa anayafanya.
Kwa hiyo kwa kipindi kirefu nilikuwa najua kuhusu forex na inahusu nini lakini sikudhani kama inawezekana kuifanya ukiwa Tanzania. Kwamba hakuna infrastructure ya kuwezesha mtu kufanya forex ukiwa Tanzania. Kwa hiyo nikawa nafuatilia tu wafanyabiashara ya Forex (hasa Sandile) kama hobby.

Mwaka jana 2017, Ontario akaandika makala kuhusu biashara hii na ndiye alinifumbua macho kwamba inawezekana kabisa kuifanya hata hapa Tanzania kwa urahisi. Kwa hiyo nilifutilia kwa karibu sana kile ambacho kilikuwa kinaendelea.
Baadae tukawasiliana na akanieleza ni namna gani itafanyika na kadhalika na kadhalika. Akanipatia na vitabu ambavyo yeye amevisoma ushauri mwingine mwingi tu.

Hatimaye mwezi October nikahisi kwamba niko tayari kuanza biashara hiyo, kwa hiyo nikajiandikisha pale ofisini kwake ili kupata mafunzo rasmi na kisha kuanza kutrade.
Kwa hiyo nikahudhuria mafunzo, nikamaliza, nikaingia sokoni.
Kwa kuwa mimi na yeye wote ni vijana wenye ndoto kubwa, huwa tunakutana mara kadhaa na huyu jamaa kujadili masuala kadha wa kadha nje ya Forex. Baada ya kumaliza yale mafunzo, tukionana nilikuwa namwambia kuwa nataka kuwa 'best forex trader' kwenye hii nchi. Naye akawa anadai kuwa nitakuwa best ila sio juu yake (yani labda niwe namba mbili). Basi tunacheka tunaendelea na mijadala mingine.

Lakini binafsi nilikuwa namaanisha kabisa kwamba nataka niwe 'kipanga' wa Forex.

Nikaanza kutrade. Nikaweka hela kidogo tu kwanza kupima upepo. Nikaweka dola 320.
Wiki ya kwanza ya kutrade nili double akaunti yangu. Wiki ya pili akaunti yangu ikakua mpaka kufikia dola 1600 na ushee. Nikapata kale kaugonjwa ambao wote kwenye forex wanakapata. Ukianza kupata faida tu unajihisi umekuwa Guru. Nilijihisi Guru kweli kweli na naelekea kweli kuwa best trader.
Nikaanza strategy za hatari hatari, kuna kitu kinaitwa Scalping. Nikaanza kufanya hiyo. Hii ni skill ambayo watu inawachukua miaka kuidevelop, lakini mimi wiki mbili nikajihisi nina mabavu ya kuscalp.

Wiki ya tatu akaunti yangu ya Forex ya dola 1600 na ushei ilishuka mpaka ikawa inasoma chini ya sifuri (negative). Kwenye forex wanasema nikaunguza akaunti.

Inauma. Inatia hasira. Inachukiza.

Lakini nikajifunza kitu. Kitu kikubwa sana. Kwamba forex is not a game… maana ilifika kipindi nilikuwa natrade kama vile nacheza gemu la nyoka. Nilijiamini kupitiliza.
Nikajifunza kwamba ni biashara ambayo inahitaji kutulia. Inahitaji kutafakari maamuzi yako. Inahitaji strategy. Inahitaji kujifunza kila siku.
Nikajifunza pia kutumia moja ya turufu yangu kuu ambayo Mwenyezi Mungu amenibariki… Utulivu wa ndani.

Nikapumzika kama wiki mbili hivi… nilitoka mpaka kwenye group zote za Forex. Walioko huko wanafahamu japo hawakuelewa kwa nini nilitoka. Baada ya wiki mbili nikarejea. Nikiwa na utulivu huku nikiapproach soko na strategies. Kwa utulivu na targets za nini ambacho nakitaka… sio sifa tu kuwa 'best trader'.
Na tangu nirejee alhamdullilah… nafanya vizuri kwenye soko kuzidi mara ya kwanza. Sipendi kuongelea ni kiwango gani natengeneza but ni kiwango cha kuridhisha kabisa. Natamani niweke screenshot hapa za moja ya trade yangu lakini sitaki kuonekana kwamba najikweza au kutafuta sifa au vinginevyo. But ukilipatia na kulielewa soko unaweza kutengeneza mishahara ya watu kadhaa ndani ya masaa machache tu.
Niseme tu alhamdulliah walau sasa naona uhalisia wa kumtimizia Cheupe wangu ndoto yake ya muda mrefu… BMW X6. Soon. Inshallah.!!

16e10d1423696469005d03456a1a977c.jpg

Hii risiti nilivyofund account mara ya kwanza


35721ae811d7a10e296d1ca1373c1205.jpg

FNB Gold Account Visa Card... hawa ndio wanatoa huduma bora zaidi kwa wafanyabiashara wa forex nchini


Ushauri wangu kwa wale wanaotaka kufanya Forex

Moja; tambua kwamba forex ni biashara… sio game au sehemu ya kupata utajiri haraka haraka. You need to work hard. Binafsi kuna siku nalala masaa matatu tu (mfano mzuri jana). Kila nikipata muda ambao niko free, yaani siandiki au siko kwenye majukumu mengine, nautumia kufanya analysis, kutafuta good entries, na kujielimisha zaidi kwa kusoma vitabu.

Mbili; Kwa kuwa hii ni biashara hivyo unatakiwa kuelewa kuwa kuna uwezekano ukapata hasara. Kwa hiyo unatakiwa kuiweka saikolojia yako sawa sawa. Hivyo basi unatakiwa kufanyia biashara ya forex fedha ambayo hata ukiipoteza haiwezi kuathiri maisha yako kuendelea kwenye mtiririko. Hivyo basi usitumie karo ya shule ya watoto au ada yako ya chuo au kuchukua mkopo ili ufanye forex. Wako waliofanya hivyo na wakafanikiwa (Mfano Sandile Shezi alitumia karo ya chuo kufund account take ya forex) but its too risk. Sikushauri.
Nimetoa mfano mimi nilipoteza dola 1600 (mtaji niliowekeza ulikuwa dola 320 ambayo ni kama laki saba unusu hivi) japo ni hela nyingi kwa vyuma vilivyokaza lakini bado haijafikia kiwango cha kuathiri mtiririko wa maisha yangu nikiipoteza. Ndio maaana niliipoteza na kisha nikarudi tena.

Tatu; mtu pekee ambaye anaweza kuamua kwamba wewe uwe trader successful au unsuccesful sio Ontario au TMT au JP Markets. Ni wewe mwenyewe. Wewe ndiye mwenye uwezo wa kuamua kama unataka kufanikiwa ndani ya forex au kupoteza hela. Its in your hands.

Nne; usifuate huu mkumbo wa watu, sijui ni mihemuko sijui nini wakianza kupata faida kwenye forex wanasema wanataka kuacha kazi wafocus kwenye forex. KEEP YOUR JOB.!
Listen, hizi hela tunatafuta tu ili kutufanya tuishe kwa fahari na kujitosheleza. Lakini lazima uwe na kitu ambacho kinaku-difine katika maisha. Ni lazima uweke lengo la kuacha legacy fulani hapa duniani. Unaweza kufanya forex na kufanya kazi yako ya siku zote. Kwa hiyo weka bidii na umahiri pia kwenye hicho ambacho unakifanya sasa. Kama ni daktari kuwa mahiri zaidi. Kama ni mwalimu kuwa mahiri zaidi. Kama ni mkulima, lima zaidi.
Kwa mfano mimi niseme kwamba kipato ninachokipata nje ya uandishi ni kikubwa kuliko ninachopata kwenye hii shuguli ya uandishi. Lakini kwa nini naandika?? LEGACY…

Siku mwenyezi Mungu akinichukua nataka Tanzania inikumbuke kama ambavyo tunamkumbuka Shaban Robert na wandishi wengine nguli. Nataka kizazi hicho wakumbuke kwamba aliwahi kuishi muandishi mahiri aliyeitwa The Bold. Ndio maana japo nina shughuli zinazonipa kipato zaidi, lakini shughuli hii ya uandishi naifanya kwa bidii kubwa na kwa umahiri. Sitaki kukumbukwa kama best trader, nataka nikumbukwe kama best writer. Its all about leaving a LEGACY!!
Kwa hiyo fanya forex and Keep your job… unless you hate your job!! Kama huipendi kazi yako unaifanya tu kwa kuwa hauna namna nyingine then i can understand.


Jambo la mwisho nakushauri kwamba… SOMA SOMA SOMA SOMA SOMA. Soma sana na jielimishe kila siku juu ya hii biashara. Jiongezee maarifa kila siku.
Pia hakikisha unakuwa na utulivu wa ndani. Maamuzi sahihi na stategies… and may be One day you and The Bold will be best forex traders in this country.


d19e71024b166b66a6dcdb0a02024891.jpg

Hii trade ilikuwa ni juzi... $1,200 profit locked in a day

Jibu la swali ambalo niliulizwa WhatsApp: Hahah chiefs, naomba nijibu hapa kwa faida ya wote (qns kutoka inbox)
Sio kwamba kila siku napata profits za dola elfu moja... hapana (japo wapo wanapata profits za dola elfu moja na zaidi kila siku). But kwangu jana was a BIG DAY with big profits.

Kwa hiyo kuna siku utapata profits za dola mia, kuna siku dola hamsini, siku dola mia mbili, kuna siku unahold tu trades without profits na siku nyingine ndio kama jana, huge profits!! Inategemea ukubwa wa akaunti yako, strategy zako na trading style yako.



The Bold - 0718 096 811 (Whatsapp only)

Pls: follow, subscribe and nifuate WhatsApp
 
Back
Top Bottom