Nguzo 7 za Mafanikio Kupitia Manifestation, Nguzo Kwanza ni Kuijua Asili ya Manifestation, Kuwa na Ndoto, Kutia Nia, Kuamini, Kuthubutu, na Kutenda

Nguzo 7 za Mafanikio Kupitia Manifestation, Nguzo Kwanza ni Kuijua Asili ya Manifestation, Kuwa na Ndoto, Kutia Nia, Kuamini, Kuthubutu, na Kutenda

Kushukuru sio kukubaliana na jambo baya, ni kusema kwamba wewe ni mkubwa kuliko jambo baya.

Unaposhukuru unatengeneza mtetemo chanya, na utavutia mambo mengine mengi yaliyo chanya.

we shukuru tu sema asante na itoke moyoni. It creates a unique positive charge which will attract more positivity and good things in your way.

Cc: min -me
Ni kweli ni muhimu Kushukuru kwa kukubaliana na hali halisi alafu ku move on, lakini sio kufurahia mabaya na kuchukulia poa.
 
hayo ulioandika yanalipa kwenye Christian western societies au jamii zinazofwata western philosophy i.e meritocracy, tanzagiza haifwati meritocracy hivyo hard work haiwi rewarded na hailipi wanaoafanikiwa (karibia)wote ni wezi, walaghai na wababaishaji btw rostamu is 8 billion dollars worth, how is that possible kwenye nchi masikini kabisa duniani kama tanzagiza?
Mafanikio ni Nini ?
 
Hizi mada Huwa nazikubali ila shida Bro Mayalla Huwa hammalizi code mnaenda Halaf mnatuacha njia ya panda

Fungua tu code zote tupate kila kitu 🙏🙏

Nipo seat ya mbele kusubiri nondo zijazo Big up Sana Kwa bandiko zuri
 
swali gumu kulijibu …
Huenda ungejibu hili.....

hayo ulioandika yanalipa kwenye Christian western societies au jamii zinazofwata western philosophy i.e meritocracy, tanzagiza haifwati meritocracy hivyo hard work haiwi rewarded na hailipi wanaoafanikiwa (karibia)wote ni wezi, walaghai na wababaishaji btw rostamu is 8 billion dollars worth, how is that possible kwenye nchi masikini kabisa duniani kama tanzagiza?
Usingesema haya..., Sababu technically kufanikiwa ni kufanikisha kile ambacho umekianza kwahio kama motive ni monetary basi kwenye jamii inayocheza rafu wewe kufanya fair ni vigumu kupata hizo material things..., lakini kama wewe ulichokianza ni kusaidia jamii yako basi hautafanikiwa kama ukiwaibia na kupata pesa wakati wao wanadumaa kwa kufanya hivyo utakuwa haijafanikisha ustawi wao bali umezidi kuwadidimiza...
 
Kilichoandikwa humu ndo ukweli mtupu. Mungu yuko ndani yetu na kupitia "postive thinking" ambayo mimi huwa naitafsiri kama "kuamini kupitia wewe/kujiamini na kujiamlia ufanye nini ili upate nini" ndo humuwezesha mtu kufanikiwa

Kitu kingine ambacho nakiona niku "focus" na unachoamini wewe wala sio mtu mwingine.

Hizi dini zipo na kwa asilimia kubwa sasa hivi zinatumiwa na wachache kwa maslahi yao binafsi. Jamii iliyojengwa kwa kumfanya mtu ajiamini yeye mwenyewe huwa inafanikiwa sana kuliko jamii iliyojengwa kwa kuamini miujiza na hofu ya kutoweza

Siku moja nilihudhuria ibada mahala fulani kanisani alikuwepo mgeni kutoka ulaya (Mzungu) ambaye naye alikuwa kiongozi wa dini. Katika salamu zake alishindwa kuficha mshangao wake kwa kuona kundi kubwa sana la vijana kanisani. Alishangaa sana na kusema kwao siku hizi wanaojaa kanisani ni watu wazima ambao sio "working age". Alisifia na kuwapongeza viongozi kwa kuwahamasisha vijana kuja kanisani. Waumini walishangilia kwa makofi na vigelegele sana.

Kwa upande wangu nilitikisa kichwa kuwashangaa waumini wenzangu walifurahia kitu gani? Afrika dini imeletwa na wazungu na ukisoma historia vizuri dini iliambatana na ukoloni na hakuna mahali wamisionari walioleta dini Afrika walikemea ukoloni au kujitenga nao. Kauli na mshangao wake nilielewa tofauti kabisa. Nilichokielewa nakijua Mimi mwenyewe acha nibaki nacho tu

Tuwafundishe watoto wetu kujiamini na kufanya vile wanavyoviwaza kwasababu mawazo mazuri yote ndo roho mtakatifu mwenyewe huyo hakuna Mungu mwingine zaidi ya kitu chema unachokiwaza moyoni mwako! Mungu alitupulizia pumzi ya uhai yaani roho na Mungu ni roho kwa hiyo roho hiyo ipo ndani yako.

Wakristu tunaamini tulivuviwa roho mtakatifu anayekaa ndani yetu siku zote, sasa kwanini tunahangaika kumtafuta sehemu nyingine wakati tuko naye ndani yetu??

Unajikuta kabisa unapanga jambo jema la maendeleo kwamba nitafanya hiki na hiki na hiki, halafu from no where unapuuzia kufanyia kazi kisha unakaa unaanza kuilaumu serikali, wazazi wako au kwenda kukesha makanisani ushushiwe miujiza, no way!

Muujiza unao wewe na unaweza kufanikiwa kwa kufanya kilichoko ndani ya mawazo yako

TAHADHARI: Hata sheteni nae ni roho vile vile hivyo zingatia mawazo chanya ambayo ni halali na si haramu
 
Na ile voices from within yako huwa ni manifestation yako? Au huwa unaambiwa na mtu fulani
 
Wanabodi,
Nipashe ya Leo 16/06/2024

View attachment 3018955
NGUZO 7 ZA MANISTATION
Hili ni bandiko mwendelezo wa wiki iliyopita. Kama hukulisoma bandiko la kwanza, anzia hapa Siri ya Mafanikio Kupitia Manifestation -1: Manifestation ni Nini?

Kwa wasomaji wapya, wiki iliyopita niliintruduce topic ya kitu kinachoitwa manifestation, kwa lugha rahisi ni kuweka nia na kudhamiria kwa dhati kufanikiwa, kwa kutumia nguvu za nia, zilizomo ndani yako. Nikataja manifestations ina nguzo kuu 7.
  1. Foundation: Msingi wa Manifestation
  2. Laws: Sheria za Manifestation
  3. Vibrations:Mitetemo ya Manifestation
  4. Intention: Kuweka Nia
  5. Visualization: Kuona kwa jicho la ndani
  6. Affirmations: Kutumia Imani Chanya ya Kufanikiwa
  7. Process: Utekelezaji wa Manifestation.
Nguzo kuu ya kwanza ni Foundation: Msingi mkuu wa Manifestation ni nia na imani ya kufanikiwa.

Kuna makundi makuu 5 ya watu waliofanikiwa.

1. The Inheritors: hawa ni watu waliozaliwa kwenye familia tajiri, wafalme na matajiri, na viongozi, mtoto wa familia hii anazaliwa na kujikuta amerithi utajiri, hata kama kichwani ni zero, huyu atahesabika amefanikiwa.

2. The Best Brains: Hawa ni watu wenye akili nzuri, wasomi, wataajiriwa kazi nzuri, na kulipwa mishahara, hivyo kupata maisha ya mafanikio, kundi hili ni la waajiriwa.

3. The Best Talent: Hili ni kundi la watu wenye vipaji, wanamuziki, wasanii, waigizaji, wacheza mpira, au watu wenye vipaji vyovyote vinavyowaletea maisha mazuri, wakiwemo waandishi wa habari, watangazaji, etc. Mwanamuziki Michael Jackson, hakusoma hata darasa moja!, huyu Daimond Platnum wetu, Hamonise ni darasa la saba tuu lakini wamefanikiwa kutokana na vipaji.

4. The Hard Workers: Wafanyakazi kwa bidii, hawa ni working class, ukifanyakazi kwa bidii, utafanikiwa, hili ni kundi la wanaofanikiwa kwa kutumia nguvu zao, “mtaji wa masikini ni nguvu zake”.

5. Fixers: Hili ni kundi la mwisho la wapiga domo!, humu ndio kuna wanasiasa, wanaweza wasiwe best brains, hawana talent yoyote, sio hard workers, lakini wanafanikiwa kwa kupiga deals, fix na kupiga domo.

Makundi yote hayo yanafanikiwa kwa kufanya manifestation kwa kujua au bila kujua.

Lugha nyingine ya manifestation is “making your dream come true”, kufanya ndoto yako kuwa kweli.

Msingi mkuu wa manifestation ni nia na imani ya kujiamini kuwa wewe una powers ndani yako na una uwezo wa kufanikiwa, kwa kutumia mawazo yako kutia nia ya kuzifungulia hizo powers zilizomo ndani yako zikuletee mafanikio ya kupata kitu unachokitaka

Manifestation ni kutumia the power of mind, through positive thinking to open the energy stored in your subconscious mind, ikupe chochote unachokitaka. Watu wote wenye mafanikio wanatumia manifestation kwa kujua au kutokujua, ila siri kuu ya kwanza ya mafanikio, ni kuwa na ndoto, wazo, nia, kisha kuifanyia kazi hiyo ndoto.

Kuna wengi wana mawazo mazuri tuu ya maendeleo, na kusema nikiwa mkubwa nataka kuwa pilot, daktari, polisi, tajiri, lakini wazo hilo linaishia hewani, kwasababu haulifanyii kazi. Ili uweze kufanikiwa, ni lazima ufanyie kazi ndoto yako. Kuota tuu ndoto ya unataka kuwa tajiri, halafu hauifanyii kazi hiyo ndoto, inaitwa ni “day dreaming”, yaani yaani kuota ndoto ya mchana, kama ile hadithi ya ndoto ya Alinacha kwenye hadithi za Alfu Lela Ulela.

Kwenye Nguzo 7 za Manifestation, Nguzo ya kwanza ni Asili ya Manifestation
Kuna wengi wanadhani manifestations ni jambo jipya, hapana, manifestation ni jambo la enzi na enzi toka enzi za Masiha, alifundisha “ombeni mtapewa", "tafuteni mtapata", "bisheni hodi, mtafunguliwa”, na akasema “hata ukiwa na imani ndogo kama chembe ya haradali, unaweza kuiambia milima iondoke na milima ikahama”.

Kitu kinachoitwa meditation, tafakuri jadidi au tahajudi, ni manifestation. Wakati wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Waislamu, wanatakiwa kunuizia kufunga kila siku kuwa kesho nitafunga. Kitendo cha kunuizia ni manifestation. Wakatoliki hufanya sala za novena ni manifestation. Sala za kujirudia rudia kama rozari ni manifestation, sala za tasbihi ni manifestations.

Mara nyingi enzi za ujana maji ya moto, mvulana akimuona msichana, akampenda, akadhamiria kumpata, hufanya juhudi mbalimbali, ili kumpata, hivyo kutumia manifestation bila kujijua, ila mwisho wa siku, hufanikiwa.

Ili kupata mafanikio kwenye jambo lolote, lazima kwanza, uwe na ndoto ya kufanikiwa, ndoto hiyo ni kuwa na mawazo chanya, kwa kizungu, “positive thinking”. Mawazo chanya haya yanakuwa yana nguvu ndani yake, inayoitwa “the power of positive thinking”. Kisha uweke nia thabiti na ya dhati ya kufanikiwa, tatu ufanye juhudi na bidii kulifanikisha hilo jambo lako. Ile power au nguvu iliyomo ndani yako, itafungua milango ya mafanikio, na utafanikiwa.

Kuna watu wanadhani kuna watu wana bahati tuu ya kufanikiwa na wengine wana laana ya umasikini, hapana!, Mungu alituumba binadamu wote tufanikiwe, ila kuna kanuni za mafanikio, ukizifuata na kuzipatia, ni lazima utafanikiwa.

Wiki itajayo nitakuletea nguzo ya pili ya manifestation yenye sheria 12 za mafanikio kupitia manifestation ambazo ukizifuata kikamilifu, utafanikiwa.

Paskali
Asante kaka kwa kutupa elimu adimu sana
 
Na ile voices from within yako huwa ni manifestation yako? Au huwa unaambiwa na mtu fulani
No ile sio manifestation, ile ni uwezo wa kusikia sauti kutoka ndani yako, inakuambia kitu fulani, bila kukupa sababu.

Sauti hiyo ni kutoka kwake YEYE aliye ndani yako, most of the times, huwa kweli. Hii ni baadhi ya mifano
- Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...

- Voices From Within: Je, wajua yuko Peponi, Mbinguni, Kwa Baba yake? Why kumshutumu, kumsakama na kumsimanga? Aachwe apumzike kwa amani

- "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia

P
 
Back
Top Bottom