NHIF matatani, kilio cha wamiliki wa hospitali binafsi kukatwa mabilioni ya fedha chaibuka

NHIF matatani, kilio cha wamiliki wa hospitali binafsi kukatwa mabilioni ya fedha chaibuka

NHIF hawako consistent kwenye makato wanayoyafanya, which inashusha credibility yao na kuonekana wahuni.

Kuna kipindi flani tuliambiwa tusifanye USS unless mteja ni mjamzito. Mwezi uliofuata tukafanya kama walivyotuambia, lakini cha ajabu walikata USS karibu nusu. Tulipolalamika, wakasema hamuwezi kuwa na wagonjwa wengi kiasi hiki. Tukawaambia basi angalieni mafaili ya wagonjwa, wakatishia kutufungia. Ikabidi tuwe wapole.
 
Kweli, umemaliza mkuu. Daktari kaona mgonjwa na kumpima ,NHIF wanasema Daktari hakupaswa kufanya hivyo vipimo, sasa kama hawataki watu watibiwe si waache kuchukua fedha za watu.

Sema hospitali private nao wanapiga hela kupitia NHIF. Mi niliwahi andikiwa risiti ya magongo ya miguu ila sikutapata na pesa najua hospitali walichukua
 
Hapa ni kuwashikisha adabu wote; NHIF na wamiliki wa Hospitali na hata maduka ya madawa. NHIF ni wapenda rushwa! Miaka yote kuiba kupitia hospitali, Hospitali nao wakawa ni sehemu ya wizi huo, mbali na kushirikiana na maafisa wa NHIF wakaanza kuongeza gharama za kipuuzi kabisa na kuandika hata vipimo ambavyo havikufanyika kwa mgonjwa.

Pharmacy nao wako hivyo wakishirikiana na madaktari wanapojaza fomu za NHIF, inaachwa mwanya wa kuongeza hata madawa ambayo mgonjwa hakuyatumia. Unapewa dawa unazostahili, halafu zinaongezwa zingine za gharama kubwa ambazo hata hukuzitumia na hata pharmacy haina.

Ni nchi inayohitaji mkono wa chuma bado! Tusilalamike kwa niaba ya wengine. Kila mtu anafahamu uaminifu mbovu alionao ingawa kamanda wa yote hayo ni NHIF!
 
Kweli, umemaliza mkuu. Daktari kaona mgonjwa na kumpima ,NHIF wanasema Daktari hakupaswa kufanya hivyo vipimo, sasa kama hawataki watu watibiwe si waache kuchukua fedha za watu.
Kwahiyo hawataki watu wapimwe tena mbona makubwa haya.
 
Sema hospitali private nao wanapiga hela kupitia NHIF. Mi niliwahi andikiwa risiti ya magongo ya miguu ila sikutapata na pesa najua hospitali walichukua
Eti kuna hospitali zinatoza laki 6 kama gharama ya kitanda kwa usiku mmoja! Utadhani uko 5-star hotel yenye heated swiming pool!
 
Yote hii ni kwa sababu ya matumizi ya paper work mpaka leo miaka zaidi ya 50 ya uhuru. NHIF anatakiwa awe na mfumo aachane na kutegemea karatasi ambazo hospitali wanaweza kuziedit
 
Wakati mwingine kadi ya NHIF haina tofauti sana na kitambulisho cha machinga.... takataka tu.
 
NHIF matatani, kilio cha wamiliki wa hospitali binafsi kukatwa mabilioni ya fedha chaibuka

WAMILIKI wa hospitali na zahanati binafsi mkoani Mwanza wameingia katika mvutano mkubwa na mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) kuhusu makato ya fedha wanazokatwa kila mwezi zinazotokana na matibabu wanayotoa kwa wateja wa mfuko huo.

NHIF mkoa wa Mwanza inatuhumiwa kuendesha utaratibu feki wa makato ya fedha kwa hospitali na zahanati binafsi mkoa wa Mwanza na kusababisha hasara na kilio kikubwa kwa wamiliki wa hospitali hizo.

Kilio cha wamiliki wa hospitali hizo kinatokana na NHIF kufanya makato ya fedha zinazotokana na matibabu yaliyofanywa na hospitali hizo ( mfano hospitali A imefanya matibabu ya Tsh. Milioni 70 kwa mwezi lakini NHIF inakata Milioni 20 )

Pia NHF inalalamikiwa na wadau hao wa afya mkoani mwanza kufanya makato hayo wanayodai sio halali.

NHF mkoa wa Mwanza imekuwa na utaratibu ambao sio rasmi wa kukata fedha bila utaratibu kwa kisingizio kuwa hospitali hizo zimetoa matibabu kwa wagonjwa waliopo kwenye mfuko huo bila utaratibu (yaani wamefanya vipimo kwa mgonjwa ambavyo havikutakiwa kufanyika).

Mmiliki wa zahanati moja jijini Mwanza (jina limehifadhiwa) amesema NHIF wamekuwa na utaratibu huo ambao unawaumiza wamiliki wa zahanati na hospitali binafsi.

Amesema NHIF chini ya meneja wa mkoa wa Mwanza, JARALTH MUSHASHU kwa kipindi cha miaka miwili yaani 2019 na 2020 wamezidi kuwanyanyasa watoa huduma ya afya wa hospitali binafsi jambo ambalo limekuwa ni kilio kwao.

Amemtaja msimamizi wa kitengo cha malipo DK. JULIETH MUHANIKA ambaye ndiye kikwazo na anayeongoza mchezo huo ambao umesababisha wamiliki hao kushindwa kutoa huduma stahiki kwa wagonjwa.

Amesema.Dk JULIETH anafanya hivyo kwa lengo la kuwatisha wamiliki wa hospitali na zahanati kutengeneza mazingira ya "Rushwa" jambo ambalo wameona hawewezi kutoa fedha kwa kuwa wanachokidai ni haki yao.

Mmiliki huyo ameeleza kuwa, ukipeleka malipo ya milioni 17 NHIF wanakata kiasi cha milioni mbili au zaidi fedha hizo, jambo ambalo amedai limeonesha kuna njia inayotumika isiyo halali kwao.

"Kwa mfano mimi kwa mwezi uliopita kunaa fedha malipo niliandika ili nilipwe na NHIF cha kushangaza kiasi cha fedha ambazo nimeandika nikashangaa nakatwa fedha bila kupewa ufafanuzi kwanini nimekatwa.

"Unaweza kupeleka fomu 1000 za wateja waliotibiwa hapa zikakatwa fomu 200, sasa kwa hali hiyo tayari wamenipa hasara na kila nikijaribu kupeleka malalamiko yangu sipewi majibu.

"Kuna makato ambayo yanafanyika ambayo hayaeleki, mimi kwa miaka hii miwili kwa hesabu za haraka nimekatwa zaidi ya milioni 40 na hiyo ni hesabu ndogo ambayo nimepiga ni zaidi ya hiyo nikikaa nikapiga vizuri.

"Ukipiga hesabu za haraka haraka kwa miaka hii miwili mitatu ambayo makato yamekuwa makubwa, hospitali zote makato yaliofanyika ni mabilioni ya fedha kwa kuwa kuna hospitali moja mwezi ulioisha wamekatwa kama Tsh. milioni 100.

"Zamani kulikuwa na makato ya kawaida sana ambayo tulikuwa tunayavumilia lakini kwa miaka hii tumeona tuanze kuamka na kulalamika kwa sababu imekuwa ni kikwazo kikuwa kwetu licha malalamiko yetu hayafanyiwi kazi.

"Shida iliyopo wanataka tuwafuate tuzungumze nao, wanachokifanya ni ktengeneza mazingira ya rushwa kwetu, sasa hatuwezi kutoa rushwa kwa mtu wakati tunachokipa ni kidogo sana.

"Pia utaratibu huu wa makato unaofanyika ni kwa mkoa wa Mwanza pekee na mikoa mingine nimejaribu kuzungumza nao wamesema huo utaratibu haupo," mmiliki wa zahanati jijini Mwanza

Mmiliki huyo wa zahanati amesema, msimamizi wa kitengo cha malipo Dk. Julieth ndiye anayefanya mpango huo kwa kushirikiana na meneja wa mkoa huo ili waweze kupewa kitu kidogo.

Mmiliki huyo anasikitika na kueleza kwamba, wanakata fedha zao bila utaratibu kwa kisingizio kwamba hospitali au kituo cha afya kimefanya matibabu kwa mgonjwa kwa kufanya vipimo ambavyo sio sahihi.

"Mfano wamekuwa wakisema kwamba tumefanya vipimo kwa mgonjwa isivyo halali wakati mimi ndiye daktari ambaye nimekutana na mgonjwa na kumuangalia na kuona ni vipimo vipi anatakiwa kufanyiwa na dawa ipi nimpe lakini wao wanasema tumefanya makosa.

"Kama wana mashaka na sisi wanachotakiwa kufanya wao ni kuchukua taarifa za kila mgonjwa anayefika katika kila hospitali na kuzungumza nae kuona tulichofanya ni uongo au ni ukweli sio watu wanakaa na kukata fedha zetu bila sababu.

"Imefika mahala tunataka hata kujitoa NHIF lakini tukijitoa hatuwezi kupata wagonjwa kwa kuwa watu wengi sasa hivi wapo NHIF maanake.

Amesema wamekuwa wajipa matumaini kuwa suala hilo litapatiwa ufumbuzi lakini mpaka sasa tatizo limeendelea kukuwa na kuzidi kuumiza wamiliki wa hospitali na zahanati binafsi.

Kwa upande wake, Mmiliki mmoja wa hospitali kubwa binafsi jijini Mwanza ambaye aligoma kutajwa jina lake, amesema NHIF mkoa wa Mwanza imekuwa ni kikwazo kwa wamiliki wa hospitali mkoani humo.

Amesema suala hilo wameisha kutana na NHIF kuzungumza nao kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita lakini mpaka sasa hakuna mabadiliko yoyote yanayoonekana.

Amesema bima zote zina matatizo lakini NHIF imekuwa "sugu" kwa kuwa wameshindwa kuonesha mwanga wa namna ambavyo wataweza kutatua tatizo hilo.

Amesema pamoja na kukata fedha zao, lakini NHIF imekuwa ikikaa miezi miwili hadi mitatu bila kuwalipa hali zao wamiliki wa hospitali na zahanati binafsi.

Ameendelea kueleza kwamba asilimia 80 au 90 ya wagonjwa wanaoenda katika hospitali hiyo ni wateja wa NHIF na kwamba kibaya zaidi wanapolipa fedha hizo lazima wanazikata.

"Unakuta unapeleka milioni 70 kwa mwezi ili ulipwe wanachokifany wanakata milioni 10 au zaidi sasa imefika mahala tumeamua kuacha kuzungumza nao.

"Hata tukipiga kelele hakuna wanachokifanya maana hawatusikilizi, yaani wao wamekaa kwa kutuvizia ukifanya kakosa kidogo tu wanakukata.

"Hili suala tulishalipeleka kwenye chama chetu cha APHFTA (Chama cha watoa huduma za afya binafsi nchini) wakatukutanisha na NHIF lakini hakuna mabadiliko ambayo yalishafanyika sasa tumeona hii imekuwa kero,"amesema mmiliki huyo wa hospitali.

Amesema kwa uhalisia makato yanayofanyika sio sahihi, na sababu za kukata kwao fedha hizo hazina mashiko kutokana na daktari ndiye aliyemuona mgonjwa na kumpa matibabu baada ya kumfanyia vipimo.

"Jamani hospitali binafsi tunateseka sana hatuna pakukimbilia, tunapojaribu kulalamika tunapewa vitisho na hii inafanyika kwa mwanza pekee kwa nini inakuwa kwetu tu, ingekuwa ni nchi nzima hapo tungesema ni ajenda ya taifa.

"Hospitali hizi binafsi lengo kubwa ni kutoa huduma bora kwa mgonjwa na sio biashara lakini tukisema tuanze kufanya biashara hatutatoa huduma kwa wagonjwa lakini wao hawalioni hilo.

Kutokana na tatizo hilo ambalo limekuwa kero kwa hospitali hizo mkoani humo, wamiliki hao wameiomba serikali kuunda tume huru kuchunguza suala hilo ili kuangalia kama makato yanayofanywa na NHIF kama ni halali na kwamba endapo ikibainika sio halali walipwe fedha zao zilizokatwa kwa kipindi chote.

Pamoja na kulipwa makato ya fedha zao, wanashinikiza watumishi hao wa umma wachukuliwe hatua kali za kisheria ili kumaliza tatizo hilo.

View attachment 1635828
Nhif konyo sana!
 
Kubinywa kwa uhuru wa huduma na kutegemea kitu kimoja ndo madhara yake

Bima nyingine mbona zinalipa bila kukata

Ni muda sasa wananchi hasa watumishi waachwe wachague mfuko wakuchangia inaweza boresha hata huduma vituoni


Sio NHIF na apo unakuta baba mfanyakazi
Wanufaika
Mama mzazi na baba
Mke wake
Watoto wakuwazaa

Ni population kubwa Sana ambayo mwisho wa siku wanaopata shida ni wananchi kwa kukosa baadhi ya huduma
Na kifo cha hospital binafsi
 
nafikiri makato siyo vituo binafsi tu hata serkalini wanawapiga panga.tofauti ni kuwa hospitali za serikalini wao wafanyakazi wanalipwa na serkali kuu. kusema kweli kuna kipindi unatamani kulia maana unakuta wamekata 3 million ambayo ungeweza kuwalipa wafanyakazi.

Naikiri tukubariane kwamba daktari ndiye akatwe kwenye mshahara wake .kwa sababu dakatri ndiye centa wa kila kitu.so kama amesababisha makato kufanyika basi yeye ndiye akatwe kwenye mshahara ndipo yeye aende ofisi za NHIF kudai kurejeshewa hela hizo.

Mmiliki wa vituo tunaonewa sana yani inabidi ubebe makosa ya daktari wakati hukushiriki makosa

Too bad and too sad.
 
Kubinywa kwa uhuru wa huduma na kutegemea kitu kimoja ndo madhara yake

Bima nyingine mbona zinalipa bila kukata....
siyo kweli .kwa sasa wote wameiga ushetani wa NHIF sema tu gharama za matibabu kwenye hizo bima nyengine ni kubwa so unaweza ku compensate
 
siyo kweli .kwa sasa wote wameiga ushetani wa NHIF sema tu gharama za matibabu kwenye hizo bima nyengine ni kubwa so unaweza ku compensate
NHIF wanaa makato feki ambayo hata maelezo hayana nna mfano wa vituo

Wanakata Hadi nusu

Mtu kaomba. Mil 30 kapewa 16mil

Huu ni upuuzi na ni kwasababu ya monopoly ya huduma iyo
 
Na bado mtafyekwa Sana reli zijengwe na ndege zinunuliwe
 
NHIF hiyo tabia hawajaanza leo. Uliza wenye pharmacy Moshi au Morogoro watakupa habari yake
 
Back
Top Bottom