NHIF yasema baadhi ya hospitali huwaandikia wagonjwa wenye bima dawa zisizo sahihi. Hii ni hatari kwa afya, ni sawa na kuwanywesha sumu

NHIF yasema baadhi ya hospitali huwaandikia wagonjwa wenye bima dawa zisizo sahihi. Hii ni hatari kwa afya, ni sawa na kuwanywesha sumu

Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mh Konga amesema Taasisi yake imebaini madaktari wanawaandikia Wagonjwa dawa zisizo sahihi na huu ni uhujumu uchumi.

Konga amesema mtu anapokunywa dawa isiyostahili anakuwa amekunywa sumu hivyo hospital zinazofanya mchezo huu zitashughulikiwa na Wizara.

Aidha Konga amesema hospital hizo zitalazimika kurudisha Fedha zote walizolipwa isivyo halali.

Source ITV
Ndo madhara ya sisi kushinda kula Chakula kama dawa na kujikuta tunakula dawa kama chakula
 
NIHF waache uhuni, wao suyo madaktari. Na wala siyo kazi yao kukosoa kazi za madaktari hapa nchini.

Wasitafute visibgizio bali waeleze kwann wanaiba hela za wateja wao kwa kuweka masharti kandamizi?
 
NHIF wanchojua Ni Kulipana mamishaha makubwa na posho tu.

Lakini huu MFUko Ni TAKATAKA KABISA.

Hata private wanaopokea huu UBARO nawaomea huruma tu
 
Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mh Konga amesema Taasisi yake imebaini madaktari wanawaandikia Wagonjwa dawa zisizo sahihi na huu ni uhujumu uchumi.

Konga amesema mtu anapokunywa dawa isiyostahili anakuwa amekunywa sumu hivyo hospital zinazofanya mchezo huu zitashughulikiwa na Wizara.

Aidha Konga amesema hospital hizo zitalazimika kurudisha Fedha zote walizolipwa isivyo halali.

Source ITV
Hesabu huwa hazidanganyi, wameanza kuumbuka sasa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Tanzania tunalishwa very damn news reports

Kwamba madaktari ni wezi au hawajui madawa au ni vipi yani?

Kwa nini yeye NHIF ndio anajua zaidi madwa, yeye ni healthcare regulator?

If anything WAO NHIF ndio wana masharti kwa madaktari kuandika dawa cheap and cheesy
Mchezo wa kuwaandikia wagonjwa dawa zisitumika sana, upo tangu zahanati binafsi zilipoanzishwa wakati huo haikuwepo bima ya afya.
 
Tanzania tunalishwa very damn news reports

Kwamba madaktari ni wezi au hawajui madawa au ni vipi yani?

Kwa nini yeye NHIF ndio anajua zaidi madwa, yeye ni healthcare regulator?

If anything WAO NHIF ndio wana masharti kwa madaktari kuandika dawa cheap and cheesy
Labda Kama wewe ni Daktari unajaribu kutetea yanayofanyika ila katika hili uchunguzi wa kina unahitajika ili kutafuta suruhu ya kudumu.

Hospitali nyingi hasa hizi policlinic wanatabia hiyo ya kurundika madawa kwa mgonjwa ilimradi tu NHIF bill isome kubwa

Binafsi nakubaliana na NHIF katika hili kwasababu kwanza nimwanachama wa NHIF hivyo napata huduma kupitia bima yao.

Nimeshuhudia mengi katika matibabu yangu na familia yangu. Swala la kurundikiwa dawa lipo wazi sana si kwa watoto hata watu wazima

Kuna taasisi kabisa zimejiwekea minimum amount ya mtu wa NHIF kutibiwa! Na hata ukipima vipimo vya maabara vikakukuta hauna tatizo lazima utaandikiwa dawa tuu!?

Labda mkurugenzi wa NHIF anachotakiwa kufanya ni kuweka watu mtaani wamsaidie kukusanya taarifa ndani ya mwezi mmoja tu halafu majibu yawekwe hadharani uone Kama watu hawatashika tama
 
Wanaokatwa hela za bima ya NHIF ni wengi uklinganisha na wale wanaoitumia huduma ya bima kupata matibabu kwa mwezi husikaaa... shirika linajihujumuu lenyewe waache janja janjaa
 
Wanaokatwa hela za bima ya NHIF ni wengi uklinganisha na wale wanaoitumia huduma ya bima kupata matibabu kwa mwezi husikaaa... shirika linajihujumuu lenyewe waache janja janjaa
Uongozi unapaswa kubadilishwa
 
Hili ni zao la mmomonyoko wa maadili katika jamii. Kila sehemu ni uozo, udanganyifu na wizi. Hakuna anayejali lile ovu analofanya lina athari gani kwa wengine.
 
Haya matatizo wanapata NHIF tu? Ifike muda watu tupewe choice ya kujiunga na medical scheme/insurance inayompendeza.
 
Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mh Konga amesema Taasisi yake imebaini madaktari wanawaandikia Wagonjwa dawa zisizo sahihi na huu ni uhujumu uchumi.

Konga amesema mtu anapokunywa dawa isiyostahili anakuwa amekunywa sumu hivyo hospital zinazofanya mchezo huu zitashughulikiwa na Wizara.

Aidha Konga amesema hospital hizo zitalazimika kurudisha Fedha zote walizolipwa isivyo halali.

Source ITV
Ni kweli kabisa, Hospital za private wanauza dawa tu kwa kweli. Unaumwa mafua lakini utapewa dawa karibu aina tano.
 
Nhif utadhan walikuwa usingizini, na hili ndilo shirika pekee la uma lililonaki kufanya dhuruma mbele ya uso wa mama yetu, tunatambua mama ni mpenda haki , tunaomba basi ateue team nje ya bima ifanye utafiti ajue nini kinachoendelea. Kiukweli kuna mgongano mkubwa sana dhidi ya watoahuduma na wakubwa wa nhif, mama kodolea macho shirika hili, dhuruma juu ya dhuruma na mwisho wa siku nikudhoofisha sekta binafsi na kwa ujumla hali ni mbaya sana sana, hospitali zina miezi zaidi ya mitano hazijalipwa. nhif mungu anawaona isee.
 
Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mh. Konga amesema taasisi yake imebaini madaktari wanawaandikia wagonjwa dawa zisizo sahihi na huu ni uhujumu uchumi.

Konga amesema mtu anapokunywa dawa isiyostahili anakuwa amekunywa sumu hivyo hospital zinazofanya mchezo huu zitashughulikiwa na wizara.

Aidha Konga amesema hospital hizo zitalazimika kurudisha fedha zote walizolipwa isivyo halali.

Source: ITV
Asitutishe
 
NHIF wanafata muongozi wa tiba ambao umethibitishwa na wizara , wizara imetoa tiba kila ugonjwa utibiwe vipi kuanza dispensary mpaka national hospital , na daktari wa level ya kuanzia chini mpaka juu dawa gani anaruhusiwa kutoa

Kwenye field ni tofauti na muongozo wa makaratasi
 
Back
Top Bottom