Ni aibu kuandaa sherehe za kupokea ndege

Ni aibu kuandaa sherehe za kupokea ndege

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
Tangu awamu ya tano tumekuwa na kasumba ya kuandaa sherehe kupokea ndege au kupokea miradi lakini kwa mtizamo wangu mimi mtu wa chini ninaona kama fedheha fulani.

Nilitegemea serikali kuona kitu kama ununuzi wa ndege ni kitu kidogo ambacho hakihitaji kuandaliwa sherehe ya kuhudhuriwa na mkuu wa nchi.

Tunayo safari ndefu na hapa tulipo tutatakiwa kujivunia mambo gani? Miaka ya 60 labda ndiyo miaka ya mkuu wa nchi kupokea ndege kwa sherehe.

Nikitazama nchi yetu naona tunayo miaka mamia kabla ya kupiga hatua za uhakika kwa sababu tunaweka magoli yetu kwenye mambo mambo madogo na kuyashangilia hayo.

Mfano Leo hii nikipita nchi nzima kumejaa wakandarasi wa kichina wakijenga miradi mbalimbali na ukingiia kwenye miradi hii unakuta kazi zote wanafanya wachina wenyewe. wameajiriwa vijawa wachache kutoka vyuo vyetu vya ufundi na hawa hawafanyi kazi za ujenzi wa miradi bali ni kutafuta vibali, kwenda tanroad kufanya tests za materials, kuandaaa orodha za wafanya kazi n.k

Ujenzi huu wa kichina umekuwepo nchini kwa miaka na bado hatujafanikiwa kujifunza chochote lakini kila mwaka viongozi huandaa sherehe za kupokea miradi. utaendelea kuwepo kwa miaka kadhaa ijayo maana hatuna plan ya watu wetu kujifunza na kuanza kufanya.

Binafsi ningependa kuona zama hizi tunatoka kwenye kasumba au fikra za viongozi wetu wa miaka ya 60 na tunajikita katika kutafuta watanzania leo hii wafanye nini ili kuwa washindani katika dunia na haya ndiyo tuandae sherehe kubwa kusherehekea.
 
Ndiyo ununuzi wa ndege kinaonekana ni kitu kidogo kwa nchi lakini kina maana kubwa sana miaka ya hivi karibuni hasa baada ya miaka takribani 20 ya kufa kwa kila kitu kilichotambulisha nchi yetu kitaifa na kimataifa.

Viwanda vyote vilivyotengeneza Made in Tanzania waliviua.
Usafiri wa treni uliosafirisha bidhaa za kilimo kwa gharama nafuu toka pande zote za Tanzania mliziua.
Usafiri wa ndege kupitia ATCL nazo mkaziua.
Hadi shule zetu kongwe kidogo mziue.

Ni baada ya JPM kuingia na kuanza takribani kuamsha roho ya utaifa na kuanza kufufua karibu kila kitu.

Kwa muktadha huu kusheherekea hakuepukiki.
 
Ndiyo ununuzi wa ndege kinaonekana ni kitu kidogo kwa nchi lakini kina maana kubwa sana miaka ya hivi karibuni hasa baada ya miaka takribani 20 ya kufa kwa kila kitu kilichotambulisha nchi yetu kitaifa na kimataifa...
hii approach yako ni very wrong kabisa. ni sawa na kusema kama hukucheza michezo ya kupika pika na sasa umezeeka basi inabidi uicheze.

Yes hakuna anayekataaa kuwa kila kitu kilikuwa kimekufa lakini fikra zetu za leo ziendelee kuwa za kisasa. tusidumazwe na ucheleweshaji tulioupitia huko nyuma
 
Tangu awamu ya Tano tumekuwa na kasumba ya kuandaa sherehe kupokea ndege au kupokea miradi lakini kwa mtizamo wangu mimi mtu wa chini ninaona kama fedheha fulani...
NI AIBU KUBWA Siku TRENI la UMEME likifika LITAZUNGUSHWA NCHI NZIMA KAMA MWENGE wa UHURU
 
Hakuna aibu pale inapokelewa na ndio sherehe yenyewe ndege si jaba la maji kwamba unaweza nunua ukaingia nalo geto kimyakimya
CHADEMA funguweni vichwa vyenu
 
Back
Top Bottom