Kwanza watu wakumbuke kuwa lengo la mashindano ni fund raising kwa african clubs
Baada ya hapo, nijuavyo mimi vigezo ni hiv;
1. Timu shiriki lazima ziwe nane tu.
2. Nchi moja isiwe na timu zadi ya moja.
3. Ukanda mmoja usiwe na timu zaidi ya tatu.
4. Timu iwe ni bingwa wa CAFCL kati ya 2015 hadi 2022 (miaka 8)
5. Mafanikio ya club katika 5 years ranking ya CAF.
6. Umaarufu wa club kwenye soka la africa.
Namna timu zilivyopatikana
1. Kigezo namba 4 kilitoa timu tano tu ambazo ni Al ahly, wydad, esperence, mamelo na Tp mazembe.
2. Vigezo namba 2 automatically kilicoincide na kigeno namba 4
3. Ukanda wa kaskazini ulitoa timu 3 (ahly, wydad na esperence) kwa kigezo cha 4 pekee na kubanwa na vigezo vya 2 na 3.
4. Ukanda wa kusini mashariki ulitoa timu 1 kwa kigezo namba 4 (mamelod) na timu moja kwa kigezo namba 5 (simba)
5. Ukanda wa kati magharibi ulitoa timu 1 kwa kigezo cha 4 (mazembe) na timu 1 kwa kigezo cha 5 (petro atletico)
6. Mpaka hapo zikawa timu 7, bado moja, ukiangalia kusini mashariki hakukuwa na timu nyingine iliyokidhi vigezo hivyo ikawa ukanda wa kati magharibi ndio utoe timu ya 8
7. Kwa kuangalia vigezo vyote hivyo kuanzia 1 mpaka 6, kigezo namba 6 kikampa nafasi enyimba na kumuacha horoya.
Sent from my TECNO RC6 using
JamiiForums mobile app