Ni aibu kwa klabu kubwa Kama Simba Sc kupiga magoti na kuanza kubembeleza mchezaji

Suala la Chama si suala la kuchekea bali ni suala la udhariri kwa timu kubwa Kama Simba Sc kubembeleza mchezaji.

Hii haileti picha nzuri kuanzia benchi la ufundi mpaka kwa wachezaji, ni suala ambalo linaharibu saikolojia ya wachezaji kwa ujumla...
Hakuna ubaya wowote timu kukaa na kuelewana na mchezaji, ni vyema pia timu kutambua mchango wa mchezaji na kuondoa tofauti.

Viongozi weledi huchukua maamzi yasiyokuwa na gharama.
 
Nyie mlivo Tuma wazee washirikina kumroga mayele asiondoke, hapo mnaona ni sawa tu
 
Unaendelea na vichekesho vyako...kwani vile vikao vya wiki mzima na Mayele na viongozi wenu vilikuwa vya nini? Mmebembeleza sana sema yeye alikuwa anawabana kwenye malipo..na alisema ANAPENDA PESA KULIKO YANGA.....
 
Mpira ni ajira kama zingine.Kama kuna mambo mwajiriwa anaona hayako sawa kwake ni haki yake kufwatilia hali kadhalika kwa upande wa mwajiri.Tuache ukondoo kwenye mambo tunayoona ni haki yetu kuyapatia ufumbuzi.Unachokileta wewe ni ushabiki mandazi uliopitwa na wakati,wakati hio wewe uko kwenye shughuli zako mambo yanaenda ila kwa wengine unaleta ushabiki mandazi.
 
KIKWETE ASHINDWA KUMBAKISHA MAYELE.

VIONGOZI WA YANGA walipambana kadri walivyoweza wakatumia HADI ushawishi wa RAIS mstafu lakini wapi.
 
Vipi suala la pre season, kwenda kwa mafungu,kocha mkuu wala msaidizi kutokuwepo, nayo iigwe na timu zingine?
Kwa sasa timu ipo kwenye mazoezi ya viungo ili kurudisha fitness za wachezaji kutoka likizo fupi.
Baada ya hapo ndo yataanza mambo ya training kiufundi na kimifumo uwanjani sasa hapo ndo ni muhimu makocha wote wawepo kujua udhaifu wa wachezaji wao kiwanjani katika nyanja tofauti kama vile fitness n.k, na kuwafanyia training zaidi katika eneo aliloonesha/walililoonesha mapungufu.
 
Bangala kasepa.Aziz Ki,Aucho na Diara kamatieni hapohapo,Mungu fundi sana,,😅😂
haaa,,burudaaani kabisa,,,raha sana😅
 
Vipi suala la pre season, kwenda kwa mafungu,kocha mkuu wala msaidizi kutokuwepo, nayo iigwe na timu zingine?
Unashindwa kuhoji HabarI za Aziza , Duara , Dada Joyce na nguchilo wako wapi wewe unaanza kupiga madomo kuhoji HabarI za timu isiyo kuhusu. Luc Eymael hakukosea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…