Ni chakula gani hupendi, mimi sipendi ndizi za kupika

Ni chakula gani hupendi, mimi sipendi ndizi za kupika

Wewe ndizi huzijuwi,ulikula ndizi wanazo tumia. kupika pombe, Siku utapokula ndizi,zikapata mpikani,hutatamani chakula kingine
 
kuna makande yanapikwa kama pilau achana na hayo maharage yaani ukipikiwa na wataalam kama sisi utahamia.
ujue hakuna chakula kibaya sema ni mapishi na ulle mpangilio wa kula .chakula chochote ukila kila siku unakinai .chakula kilekile mapishi yale yale ndo tatizo la waafrica

Na wewe utakua ni mpare tu, maana si kwa kwa kupenda huko makande ,umeyasifiaa,mi nikila sishibi,nasikia njaa mara moja.
 
Binafsi siupendi Ugali na haijalishi kuna mboga gani, nakula Ugali tu kama sina jinsi lkn siupendi na hata kama ukipigwa marufuku kwangu poa tu na kamwe siwezi kuumiss!
kama mm mkuu sipendi ugali haijalishi mboga
 
chakula ambacho sipendi.
WALI KUKU
NYAMA CHOMA
MAYAI YA KUKU.

swissme
 
Waaooh yaani nikiona ndizi za kijani gengeni ninachanganyikiwa, ninaweza kuanza na mtori asubuhi machalari mchana na jioni bila matatizo.
wow! wew ungekuw dada angu tungeelewan sana apo kwny mlo huu
 
Mimi sipendi wali,pilau,chips,ugali sembe bali napenda dona,mboga za majani,matunda,viazi vya kuchemsha,majimbi ya kuchemsha, ndizi nyama,asali,juice ya mchanganyiko wa mboga za majani na matunda,maziwa e.t.c
 
Kusema kweli ndizi nazipenda zilizoiva tu nakula kama tunda ila sio ndizi za kupika.

Ndizi za kupika nakula tu kuzuia kifo panapokua hakuna chakula kingine.

Katika chakula nisichokipenda zaidi Duniani ni ndizi za kupika.
Tumefanana
 
Me njugumawe jamani. Zimenishinda kabisa.
Vengine vote napeleka kama sina akili vizuri.
[emoji39][emoji39][emoji39][emoji39][emoji39]
Huo msosi hata mimi nimeushidwa nikila nyungu mawe baada ya muda nikipumua naisikia harufu yake puani
 
Back
Top Bottom