Ni faida gani ataipata Mungu kwa kuwachoma moto binadamu siku ya mwisho?

Ni faida gani ataipata Mungu kwa kuwachoma moto binadamu siku ya mwisho?

Salaaam..

Kwanza kabisa naomba niweke msimamo wangu kiimani, mimi naamini mungu yupo na ndie muweza wa yote.

Turudi kwenye mada..nacho jua mimi adhabu huwa inatolewa ili iwe funzo kwa mkosaji au kwa watu wanao mzunguka huyo mkosaji..adhabu hii huwa ni fundisho kwa mkosaji ili asirudie tena kosa pia ni funzo kwa wengine ili wasifanye kosa hilo.

Haya sasa binadam wote watakao kufa wakiwa na dhambi wameahidiwa moto wa milele kule jehanamu kama adhabu..lakini pia tuna ambiwa kuwa baada ya adhabu hiyo hakuta kuwa na kifo tena wala dhambi na watu watakao kuwa na dhambi watabaki motoni milele..

SWALI:

je adhabu hiyo ya moto itakua ni funzo kwa nan??

Na je ni faida gani mungu ataipata kwa kuwa choma moto viumbe alio waumba mwenyewe..

Je shetani alipangwa ili maisha yawe hivi??

Yesu alikufa msalabani kwa sababu ya dhambi zetu wanadam ambazo chanzo chake ni shetani..je shetani hawezi kudhibitiwa na kupewa adhabu kali kwa kuharibu ulimwengu???maana watu wanajaa kwenye anasa kuliko kwenye nyumba za ibada takatifu..


Nawasilisha..karibuni
Nikosoe kama nitakosea...
Kuna mfano niliwahi kupewa nikiwa mdogo naomba nikupe na wewe.
"Kuna Mtu alikua anahoji na kutafakari sana utemdaji kazi wa MUNGU. Alitaman sana kujua chanzo mipango na mengi kuhusu MUNGU. Siku moja akiwa pembeni ya ufuko wa bahari aliona katoto kadogo kamechimba shimo kando ya bahari, na kanafanya kazi ya kwenda kuchota maji baharini kuyaleta kujaza kwenye shimo lake. Alishindwa kuvumilia na kumuuliza yule mtoto unafanya nini?
Mtoto akajibu "nataka kuhamisha maji ya bahari niyajaze hapa kwenye shimo langu"
Alimcheka sana yule mtoto na kumuona mpumbavu kisha akaondoka na kitudi alipokua amekaa. Alipofika akageuka hakumuona yule mtoto"


[emoji120] moral of the story ni kwamba, ubongo wa mwanadamu ni kale ka shimo na UMUNGU ni ile bahari. Haviwezi kutoshana.
Stay humble and your GOD will have mercy on your soul at the end of time
 
Kama unaweza wasiliana naye ajupe jibu.ukisoma maandiko inaonekana kama atawaacha wasio wake bila msaada.kwakuwa patakuwa hakuna kufa tena watakaobaki nje watajijua wenyewe.sidhan kama ni moto as moto ila kuachwa na Mungu si jambo zuri kabisa
 
Salaaam..

Kwanza kabisa naomba niweke msimamo wangu kiimani, mimi naamini mungu yupo na ndie muweza wa yote.

Turudi kwenye mada..nacho jua mimi adhabu huwa inatolewa ili iwe funzo kwa mkosaji au kwa watu wanao mzunguka huyo mkosaji..adhabu hii huwa ni fundisho kwa mkosaji ili asirudie tena kosa pia ni funzo kwa wengine ili wasifanye kosa hilo.

Haya sasa binadam wote watakao kufa wakiwa na dhambi wameahidiwa moto wa milele kule jehanamu kama adhabu..lakini pia tuna ambiwa kuwa baada ya adhabu hiyo hakuta kuwa na kifo tena wala dhambi na watu watakao kuwa na dhambi watabaki motoni milele..

SWALI:

je adhabu hiyo ya moto itakua ni funzo kwa nan??

Na je ni faida gani mungu ataipata kwa kuwa choma moto viumbe alio waumba mwenyewe..

Je shetani alipangwa ili maisha yawe hivi??

Yesu alikufa msalabani kwa sababu ya dhambi zetu wanadam ambazo chanzo chake ni shetani..je shetani hawezi kudhibitiwa na kupewa adhabu kali kwa kuharibu ulimwengu???maana watu wanajaa kwenye anasa kuliko kwenye nyumba za ibada takatifu..


Nawasilisha..karibuni
Hakuna cha moto wala nini, hayo ni mafundisho ya kipagani.
 
Vitakuwa vilianza sawa.
Sijakuwelewa, unamaanisha viumbe vilikuwepo kipindi universe inaanza na wakaanza pamoja? Kwa kuwa hauamini uwepo wa mungu hii nadharia yako inajipinga hata theory ya evolution. Oxygen iliibukia miaka 2bilion iliyopita sasa mwanadamu na viumbe vingine kipindi universe inaanza walitumia hewa gani kuadapt mazingira? Mkuu au we unaamini katika ubudha?.
 
Wewe sio wa kwanza kuzikataa/kupinga..
Walikuwepo waliopinga kinadharia kamaa ww.
Mwisho wa siku walipotea kinadharia.
Cha kufurahisha ni kwamba Mungu katupa zawadi nzuri ambayo hawezi kutunyang'anya..
Zawadi ya uhuru wa kuchagua..Ukiwa hai.
Unaweza ukachagua kumkubali au kumpinga kwa namna yeyote ile kama ww ufanyavyo.
Ku mwamini au kutokumwamini.
MUNGU SI DICTATOR.
Hata ukimtukana matusi makubwa makubwa au ya kinadharia.
Sawa tu.

LKN
Katika yote hayo..Siku utakapokuwa mbele yake.
Maneno yako hayatabadilisha kitu..
Kwamba ulikuwa huamini..
uliamini ni nadharia ya watu..hayata saidia kitu.
Kilio na machozi yako..haya badiliaha msimamo wake.

Neno moja kwako.
Mungu anakupenda.
Mlango uko wazi,bado nafasi unayo kwa sasa anaweza akakusamehe..akakufanya kuwa mwana wake
Yupi sasa kati ya Allah, Yesu, Yehova, Buddha, Haile ssalasi[emoji32]
 
Mungu hamchomi Mtu ,moto ndio unachoma , moto umewekwa kwa ajili ya shetani wewe unayekwenda jehanum ni kiherehere chako tu , acha dhambi nenda mbinguni hutaki utaenda jehanum tu Na huko huchomwi nu Mungu ni wewe mwenyewe umejipeleka kwa kutotiii Amri za Mungu ,
 
sasa mtoa mada nawe jiulize kuna faida gani anayoipata hakimu baada ya kumfunga mwalifu? hayo yote yamewekwa ili Neno litimie
 
Back
Top Bottom