Ni faida gani ataipata Mungu kwa kuwachoma moto binadamu siku ya mwisho?

KWANINI MOTO WA JEHANAMU NI ILLUSION???

1.Ule moto hatujaambiwa unatumia fuel ya aina gani e.g petrol,gas, kerosene, au mkaa.

2.Ziendazo huko ni roho.Roho hazina sensory cells, so watakaoenda huko hawatahisi maumivu.

3.Chanzo cha roho ni pumzi aliyopuliziwa Adam na Mungu, ile pumzi ndio tunayo ibreath in and out, nayo ni oxygen...oxygen kazi yake ni kusapoti moto uwake. So roho zitakazokwenda jehanamu zitakuwa na kazi ya kusapoti combustion.

SWALI: NINI KAZI YA MOTO WA JEHANAMU???...Wafiadini majibu tafadhali.
 
Kweli bwana muulize
 
Hakuna kitu kama hicho ni nadharia tu ambazo watu kama wewe walizianzisha na kuwaaminisha watu kuwa kuna kuchomwa moto kwa watenda dhambi siku ya mwisho Ili kupunguza madhambi kwa kiasi fulani
Imani yako tuu hiyo ndo inayokufanya usimwamini muumba wako
 
Kwanini unakimbilia mahubiri badala ya kustick kwenye swali? Ama umeamua kuongeza maswali yako kufanya mtihani uwe na maswali mengi zaidi?
Acha figsu figsu jibu bwana unajua kumuamini kuna kufanya uwe mtiifu angalia wale wanaomtii bwana Kama ni majambazi au wezi au magaidi
 
swali lingekuwa anapata faida gani kwa sisi kuwepo 'duniani' kabla ya kufa na kufata mengineyo,,
 
Hakuna moto wa milele.
soma Mwanzo 3:19
Mhubiri 9:5,6,10
Zaburi 146:3,4
Yeremia 7:31
 
Hakuna kitu kama hicho ni nadharia tu ambazo watu kama wewe walizianzisha na kuwaaminisha watu kuwa kuna kuchomwa moto kwa watenda dhambi siku ya mwisho Ili kupunguza madhambi kwa kiasi fulani
Wewe sio wa kwanza kuzikataa/kupinga..
Walikuwepo waliopinga kinadharia kamaa ww.
Mwisho wa siku walipotea kinadharia.
Cha kufurahisha ni kwamba Mungu katupa zawadi nzuri ambayo hawezi kutunyang'anya..
Zawadi ya uhuru wa kuchagua..Ukiwa hai.
Unaweza ukachagua kumkubali au kumpinga kwa namna yeyote ile kama ww ufanyavyo.
Ku mwamini au kutokumwamini.
MUNGU SI DICTATOR.
Hata ukimtukana matusi makubwa makubwa au ya kinadharia.
Sawa tu.

LKN
Katika yote hayo..Siku utakapokuwa mbele yake.
Maneno yako hayatabadilisha kitu..
Kwamba ulikuwa huamini..
uliamini ni nadharia ya watu..hayata saidia kitu.
Kilio na machozi yako..haya badiliaha msimamo wake.

Neno moja kwako.
Mungu anakupenda.
Mlango uko wazi,bado nafasi unayo kwa sasa anaweza akakusamehe..akakufanya kuwa mwana wake
 
Acha figsu figsu jibu bwana unajua kumuamini kuna kufanya uwe mtiifu angalia wale wanaomtii bwana Kama ni majambazi au wezi au magaidi

Kutii jambo usilolijua kunajenga woga, woga, na woga hujenga hofu na hofu ikikua inajenga mazoea ambayo huitwa imani, na ukiisha kuamini ni kutarajia mambo yanayosemekana yanakuja tokea adamu ambayo kimsingi hayatakuja, tukubaliane ama kutokubaliana kwamba aliyeleta dhana hii ya uungu ni mbunifu wa hali ya juu, ambaye ana elimu kubwa ya maarifa yaliyomzidi mwanadamu wa kawaida na kwa kiwango kikubwa kachangia dunia kuwa sehemu salama ya kuishi kwa kuvuruga akili za wanadamu!
 


Kwanza lazima utambue kuwa akili za Mungu hazichunguziki;
Kwani asipowachoma anapata hasara gani?
Unachoshindwa kujua unadhani wewe ni wa thamani sana machoni pa Mungu.
Kwa Mungu mwanadamu ni udongo na yeye ni mfinyanzi.
Mfinyanzi anapofinyaga gae (Kigae) harafu kikawa kibovu akikibomoa utamuuliza kwa nini kakibomoa?
Kwa mantiki hiyo, huwezi kupata ujasiri wa kumhoji Mungu kama huwezi kumtii yeye aliyekufinyanga.
 
moto utachoma nini wakati mwili umeshaoza kaburini!
 
Tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Tofauti na malaika binadamu tuna free will. Baada ya Yesu Kristo kufa msalabani ili tuhesabiwe haki, basi imebaki ni machaguo yako tu uende mbinguni au motoni. Si Mungu anayekupeleka. Yes binadamu ni dhaifu na wadhambi, lakini hakuna mtu atakayekulazimisha (hata Mungu) kukiendea kiti che rehema cha Mungu kutubu. Hivyo Mungu hapendi (mungu anapenda) mtu yoyote apotee bali wote tuiendee toba.
 

Kwa ufahamu wangu:-
1. Mungu sio mwanadamu hata aanze kutafuta faida kwa maamuzi anayoyafanya, akiamua amemaliza.
2. Kukaa motoni milele ni sawa na kukaa katika uzima wa milele Mbinguni, kwa sababu nyati hizo kifo hakitakuwepo. Mauti itakuwa imefungwa
3. ni vema kuyachunguza maandiko ili upate kuyatii na kuyafuata, na sio kwa lengo la kuyakosoa maana utapotea na roho ya ukengeufu inaweza ikakuvaa.

Wasalaam,
 
jiandae kujibiwa ni "fumbo la imani"

Hahhahaa....mkuu umenichekesha sana....watakimbilia "Fumbo la Imani",kama ulikuwepo vile....

Hawa hawa ndio walewale wanaosema "Usinichukie mimi,Zichukie dhambi zangu"...yaani haya majitu hayana aibu....hawa wanafanya hii dunia wanadamu wengine ni mataahira yaani[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…