Mimi kuna siku mgeni kaja kunitembelea, sina hata mia mbovu, ndani nina mchele na nje kuna matembele, nikaandaa mboga kwa ajili ya kupika na kubandika wali, basi bwana mgeni amefika tunasubiri msosi uive mara gesi ikaisha ndio kwanza maji yanaanza kukaukia , matembele yako kwenye maji, mgeni kaja na njaa anategemea kula kwangu alikotoka hakula, yani nilibaki sina cha kufanya, nikatafutiza kasoda kalibaki kwenye friji ndo nikampa akanywa.. akaondoka na njaa yake. Umasikini mbaya sana.