Kumekuepo na hadaa za wanasiasa matapeli kuhubiri mabadiliko ya sheria za uchaguzi nnje kabisa ya wakati wa mabadiliko ya sheria na katiba, kana kwamba hayo ndiyo mahitaji muhimu zaidi kwa wananchi wa Tanzania kuliko maji, afya, elimu, kilimo, ufugaji, uvuvi, biashara, miundombinu, usafirishaji n.k
Lakini pia,
matapeli hao wa kisiasa nchini wanaendelea kuhadaa wananchi zaidi kwamba hitaji la waTanzania ni vyeo na mamlaka. Kwamba wananchi wanahitaji sana matapeli hao wa kisiasa wapate vyeo, kuliko mahitaji yao muhimu ya kila siku.
Na ndio maana,
agenda kubwa za wanasiasa hao waliofilisika hoja zimekua ni kujadili umri wa makamu mwenyekiti wa CCM bara, na na ubaguzi dhidi ya ukanda anakotoka rais Dr. Samia Suluhu Hassan na jinsia yake, kana kwamba ukiwa kiongozi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka upande wa Zanzibari Bara, ni kosa na ni anasa kubwa mno, huku wakijua wazi kabisa kua hakuna mtu anaweza kupata uongozi wa kitaifa Tanzania bila waZanzibari.
Ni vizuri kama wanasiasa kuibua hoja zenye mashiko kwa wakati sahihi na muafaka, kuliko kubwekabweka na kuwahadaa wananchi kwa vimisemo vitakavyowaathiri wenyewe na kuwakosesha fursa na haki zao za msingi, ikiwa ni pamoja na haki ya kupiga kura kuchagua viongozi ambao wanawataka kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi.
Kumbuka,
hata mtua aimbe, alie, acheke, acheze au abwekebweke namna gani, uchaguzi mkuu wa kihistoria Tanzania upo pale pale, ni Oct.2025
Mungu Ibariki Tanzania