Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?



Mawazo ya akina Kingunge hayo!!!

Kumbe kweli! Jambo likirudiwa mara nyingi linageuka kuwa ukweli kwa baadhi ya watu!

Nawe una amini kwamba Serikali inatakiwa kuwa chini ya chama cha siasa? CCM? Serikali inatakiwa kuwa chini ya katiba ya nchi. Chama kinaweza, nasema tena kinaweza kikatumika kubadilisha katiba ya nchi kwa muelekeo wake. Lakini huwezi ukaongoza serikali chini ya chama.
 
Kuna wakati vikao vya chama vitaongozwa na Lipumba wa CUF, ama Mbowe wa CHADEMA, ama Mtikila wa DP tokea Ikulu. Wakati huo tutakuwa tumewapiga chini CCM.
 

Lakini some times its not too good to know too much. Hiyo katiba unayo isema ndugu kama ni ya Tanzania angalia ibara ya 39(1) c.

Mtu hata stahili kuchaguliwa kushika kiti cha urais wa Jamhiri ya Muungano isipokuwa tu kama ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa.

Kwa tafsiri ni kwamba kabla ya kiapo cha kutii katiba rais lazima awe ni mtiifu kwa chama. Hiyo ndiyo katiba yenu kama ulikuwa unadhani unaifahamu vizuri na ndio maana tunapopigia kelele mabadiliko ya katiba huwa hututumii hivi vijisababu kama rais kufanyia vikao ikulu bali tunaangalia mianya inayoweza kuleta hivyo vijimambo..aaaaaaaaaaaaaggggghhhhhhhhhrrrrrrrrrrrr!!!!!!!!!!
 
Mimi nadhani hamna tatizo vikao kufanyika Ikulu. Kwani Ikuku si makazi binafsi vile vile ya JK? sasa kuna kosa gani kuwaalika watu nyumbani kwake wakafanya mkutano kwenye sitting room yake?

Basi hicho kitakuwa si kikao bali watu wameenda kumtenbelea JK,hebu tuwe tunatafakari kabla ya kujibu.
 
[Snip]........ibara ya 39(1) c. Mtu hata stahili kuchaguliwa kushika kiti cha urais wa Jamhiri ya Muungano isipokuwa tu kama ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa. ...........!!!

Burn! Burn!
Weka mambo wima. Hiyo unayoisema ni minimum qualification. Baada ya hapo Katiba haisemi lengo la wewe kuwa mwanachamama wa chama cha siasa ni kukitumia kuendesha nchi.

Malengo ya hicho kifungu ni tofauti. Wengi hatukipendi lakini kuwepo kwake hakufanyi iwe sababu ya kusimama wima ukasema naongoza kwa kutumia CCM. Ndo maana nasema ni zile za akina Kingunge wanaosema hadi leo kwamba maslahi ya chama kabla ya Taifa. Labda ni uzee lakini hiyo ni Nonsense isiyokuweko ktk nchi yoyote ya maana!
 

Unachoshindwa kufahamu au kuweka wazi ni kwamba, mtu binafsi kufanya shughuli binafsi kama kutoa mwali na vikao vingine vya kibinafsi si sawa na Kikwete kufanya vikao vya CCM. Kikwete anaweza kumtoa mwali Ikulu, hiyo ni shughuli binafsi.Kikwete kufanya kikao cha CCM ikulu si sawa, kwa sababu hii ni shughuli ya chama, si shughuli binafsi ya Kikwete.

Ikulu si makao binafsi ya Kikwete, ni makao rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pale Kikwete hakai kwa kofia ya mwenyekiti wa chama, anakaa kama rais, bajeti ya Ikulu haitoki CCM, CCM hawalipii maji wala umeme wa Ikulu, serikali inalipia.

Sasa kwa nini CCM watumie resources za serikali? Kwa nini CCM wasifanye vikao vyao Lumumba au kwenye jengo linguine la CCM badala ya kufanya unyonyaji huu wa kutumia majengo na resources nyingine za serikali?

Watu wa CUF na CHADEMA nao wakisema wanataka kufanya vikao vyao Ikulu kama wanavyofanya CCM,ikulu itakubali?

Kwamba Kikwete ameshinda uchaguzi kwa tiketi ya CCM na kuunda serikali ya CCM ahaina maana CCM inaweza kutumia resources za serikali itakavyo, si sawa, si haki, ni unyonyaji, ni utovu wa maadili, kuna conflict of interest, kuna double standard.

Kama nilivyosema mwanzo, usuluhishi mzuri ungekuwa kufanya rais na mwenyekiti wa CCM kuwa watu wawili tofauti.
 
Issue: Je, si kuvunja sheria kutumia mali na muda wa watumishi wa umma kwa manufaa ya chama kimoja? [KUMBUKA mkutano huu yasemekana umefanyika Ikulu] na Je, hawa wawakilishi wa Zanzibar, huwa hawana mavazi ya chama chao au ni kamgomo baridi[hii sasa imezoeleka kwa hawa jamaa wa Zanzibar kutokuvaa 'jezi' za timu yao. Manazi wa chama tawala hili limekaaje? Kaa chini, tafakari ....
 
nimejiuliza hili swali pia, kuwa kazi za chama ndani na may be kwa gharama za serikali, mmh sijui wenye kuelewa hii inasemaje watupe msaada ktk tuta! but sio sahihi naamini hivyo!
 
Hivi na mweshimiwa chenge ni mjumbe? au ni macho yangu tu? Haya kwa wale wanaofikiria kuwa ktk chama cha Mapinduzi kutatokea mabadiliko miaka ya karibuni wameliwa.
 
Hivi na mweshimiwa chenge ni mjumbe? au ni macho yangu tu? Haya kwa wale wanaofikiria kuwa ktk chama cha Mapinduzi kutatokea mabadiliko miaka ya karibuni wameliwa.

Mkuu Rafikikabisa, labda wakereketwa wa CCM watatupatia jibu
 
npo na gazet la mwananchi naiona hii picha na habari nkashtuka, mi nahsi c harari coz pale unatumika mda na raslimali za serikali badala ya kutumia za chama.
 
Mkapa, Dr. Mwinyi, Vuai, Karume wana aleji na Mashati ya kijani?
 

Labda ndio maana ya chama kushika hatamu za utamu.
 
Nafikiri hii ni sawa na kufanya biashara Ikulu.

Ile ni sehemu inayotakiwa kuwa mbali kabisa na vyama vya Siasa. Hii kuvaa shati za kijani na kuitisha mkutano hapo na mpiga picha wa Rais akimpiga picha Mwenyekiti wa CCM na genge lake la CCM, sidhani kama ni sawa.

Maadamu nchi ni MALI yao, mtawafanya nini?
 
Kweli mnashangaa? Basi jueni kuwa Chama ndio Serikali yenyewe na ukiisema Serikali basi unakisema Chama! Nani leo hii anaweza kutofautisha shughuli za chama na za serikali kuanzia ngazi ya taifa hadi kijiji. Ndugu zangu muuone ukweli kwamba CCM ni chama dola na dalili zote zinaonyesha kwamba kitaendelea hivyo kwa muda mrefu kwa kadiri Watanzania watakavyoendeleza u-kilaza wa kushabikia pilau, fulana na capelo za kijani na njano na kutoa ushindi wa kishindo. Hapo Ikulu hao wakulu wako jumbani kwao.
 
Hivi na mweshimiwa chenge ni mjumbe? au ni macho yangu tu? Haya kwa wale wanaofikiria kuwa ktk chama cha Mapinduzi kutatokea mabadiliko miaka ya karibuni wameliwa.

Usisahau pia kuwa ni mwenyekiti wa kamati ya chama ya maadili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…