Ni jambo gani huwezi kulisahau kwa mara ya kwanza ulipoanza kazi.

Ni jambo gani huwezi kulisahau kwa mara ya kwanza ulipoanza kazi.

Watu kama nyie ndio hua mnaharibu thd hapa JF,huo upuuzi nenda pm ukaongee nae huyo mwenzako,acha kuharibu thd kwa kutuletea upuuzi upuuzi hapa.
wanazingua sana wanaleta mazungumzo binafsi kwenye threads za watu alafu hata aibu hawaoni watu wanachangia mada wao wanaleta story gani sijui alafu hata hazieleweki hazina faida kwa wengine kwanini wasiende pm kupiga story hizo wanadandia nyuzi za watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi waiter. Naanza asubui shati jeupe balaa,jioni lilikua limeloa michuzi batiki muruašŸ¤—
Motel Agip pale nikaondoka na vi tip km 3000 hivi Miaka Hiyo Ndio tu shing mia coin tunatoka km dhahabu.mzungu anachukua ka mia anakuachia vilivyobaki.
Basi ikawa game, cashier anakuja na vi ndururu mia mia kibao,mzee wakilipa buku 50 blue tena 5 enzi hizo change zao buku tatu unapeleka ndururu za 100,30 wanaona hatubebi huu mzigo.wanachukua ka coin kamoja wakaonyeshe kwao. 2900 unalamba ila usisahau wahenga. Mnashare hapo restaurant manager na chef wana chao cashier anajua.
Kwa siku buku 3 au 1.5 lazima, ukirudi mtaani sasa na hivyo vi mia mia ilikua tabu sana. 🤣
 
Daah mkuu hongera miaka 21_ulikuwa umeshamaliza chuo
Mara ya kwanza walijua ni mtoto wa boss kaja maana mi ndio nilikua kadogoooo, halafu tukawa tumeongozana na HR. Walikua wananituma tuma saaaana ila kiukweli niliingia nikiwa mdogo miaka 21 et officer [emoji3][emoji3]kimtindo namimi nikawa natumia advantage hiyo hiyo nikikosea nasema mtoto ndo anajifunza ruksa kukosea!

Sasa mimi ndo nikawa nawahi kila siku, naogea vizuri tu kwenye story za hapa na pale nachangia kwa adabu kabisa kumbe kila kitu nilikua location tu najibana tu wanizoee kidogo. Baada ya kujua jua kazi na kunizoea walinikoma sasa maana kiukweli mimi sijawahi kuwahi kwa chochote tangu secondary mpka U.E mi nachelewaga tu yani kila kitu mi nilikua mzee wa deadline, kwenye story mi ndo naongea pumba kuliko, yaani mimi ndo ikawa naongoza kwa zile excuse za ugonjwa, ikafika kipindi hata ofisini nafika tu kusaini naend akukaa nje kwa mlinzi mpaka time ya kutoka.Mungu sio Athumani bana wakanichoka bhana kilichonikuta nadhan mnaelewa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani makazini ukiwa systematic unaonekana unajipendekeza sijui kwa nini kuna husda sana
Kwa mara ya kwanza kabisa naonja kuajiriwa na kuanza kazi rasmi nilikuwa najituma sana na mwenye weledi nadhani kwasababu ya kimuyemuye cha kazi,sikutaka kabisaa ujinga kwenye ishu za kazi,.kazi ilikuwa ndio mpenzi wangu mahabuba,.lakini siji kusahau nilipomsikia supervisor wangu akiniteta ofisini "fulani (mimi)anajifanya kupenda sana kazi ee anataka kuonekana bora au anautaka yeye uboss,kujishaua tuu...ngoja aizoee kazi tuone" na maneno mengine mengi mengi,.daaaahhh niligwayaaa nguvu zikaniisha looh[emoji17]nikakumbuka tuu usia wa mama yangu juu ya mambo ya makazini...

Nilijipa moyo lakini nilijiona kabisaa kiutendaji naanza kuwa mnyonge,sikuwa na hamu na kazi tena...nikajisemea mtu huyu kuna siku anaweza kuni recommend vibaya hata bila kujua,.baada ya mwaka mmoja nili resign na kufanya ustaarabu mwingine..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipoanza kazi sitasahau kuna dada mmoja wa makamo nilimpa shikamoo na nilikua namuheshimu sana, ila nilipokaa kdg ilitokea safari ya morogoro kule mtibwa sugar, tulifikia hotel flani nimesahau jina la kijiji nahisi mazizini, usiku kama saa nne kila mmoja yuko chumban kwake mm nilitoka nje nikawa napiga stori na mlinzi huku tukila konyagi, ghafla yule dada akaja anadai amekosa usingizi akajiunga kwenye konyagi, kilichofuata nilijikuta niko kwenye room ya yule dada, tulifanya mengi mno hadi tunarudi ofisini tukaendelea kimya kimya kumbe yule dada ni goma la mkuu probation period ilipoisha sikupewa mkataba kisa mahusiano mabovu eneo la kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom