Ni kauli gani uliwahi kuambiwa na baba, mama au mlezi wako ambayo baadae kabisa ndio ulikuja kuielewa?

Ni kauli gani uliwahi kuambiwa na baba, mama au mlezi wako ambayo baadae kabisa ndio ulikuja kuielewa?

Kwema wakuu?

Binafsi nilikulia kwenye familia ambayo wazazi wanazingatia sana kuhusu watoto wao, nikimaanisha ni watu wenye kufuatilia Kwa ukaribu sana mienendo yetu, sio watu waliotuachaniza kufanya mambo Kwa kujiamulia.

Kipindi nasoma nilikuwa na rafiki zangu ambao wazazi wao walikuwa tofauti kidogo na wa kwangu, yaani ni aina za familia ambazo mtu unaweza kutoka hata ukalale huko huko hakuna mtu atakuuliza. Kiufupi walikuwa huru sana.

Katika urafiki wetu Kuna muda nilikuwa nashindwa kuenjoy sababu nashindwa kufanya baadhi ya mambo Kwa kuhofia muda au jambo husika huenda likazalisha maswali mengi Kwa wazazi wangu ilhali Kwa wenzangu sio issue hata kidogo, hakuna wa kuwafuatilia.

Familia ilikuwa na uwezo wa wastani TU hakuna kitu tuliomba tukakosa.

Siku moja tukiwa shule wale jamaa zangu walikuja na kusema wamepata kazi kiwanda Fulani wanaingia usiku na kutoka asubuhi kisha wanaunganisha kuja shule, mshahara 70000 Kwa mwezi, na Wana siku ya pili tangu waanze. Kwa wakati ule na umri ilikuwa ni pesa nzuri TU, nikawa naona jamaa zangu wanaenda kutoboa kimaisha tukiwa bado tunasoma. Kwa wakati huo sikuweza hata kuwaza kuhusu ugumu wa kazi pamoja na kupata muda wa mapumziko sababu kiuhalisia ni ngumu kuhandle mambo hayo within 24 hrs pasipo mapumziko ya kutosha.

Kichwa kilipata moto sana, Kuona rafiki zangu wana-make na shule wanakuja. Kwakuwa nyumbani siwezi kujiondokea tu ikabidi nijaribu kulifikisha Kwa mzee nikitegemea ataruhusu kwakuwa ni wazo chanya kabisa. Nililifikisha kwake lakini ikawa kinyume na matarajio. Mzee alinigombeza sana na kunielekeza mambo mengi sana, nilikumbana na maswali magumu ambayo majibu sikuwa nayo ila kubwa aliniambia "Jifunze kufanya mambo Kwa wakati, MAISHA YAPO TU SIO YA KUKIMBILIA"

Kiukweli moyoni mwangu sikuridhika, nikaona mzee kanionea. Nikawa najutia kuwa kwenye familia kama Ile ya kukaa wanatubana. Nikahisi mzee hataki kabisa nifanikiwe, ila ndio sikuwa na namna ikawa nimepigwa marufuku.
Jamaa wale hata wiki mbili hazikuishaga wakaacha kule tukabaki kusoma TU.

Sasa Kuna kipindi hayo yote yaliisha, mambo ya elimu, utu uzima Sasa nikiwa najisimamia mwenyewe niliwahi kupigwa na maisha mtaani, kila nlichogusa ilikuwa hola. Nikaamua kwenda kiwanda Fulani, kazi ni ngumu halafu msimamizi katuweka watatu TU ili apunguze cost halafu mashine haizimwi, aisee... Niliishia nusu siku nikatema Bungo hata hela sikuwahi kuiomba.

Alhamdulillah Mungu alibariki, nikavuka kote huko, maisha yamekuwa poa, nimepiga kazi Home Tanzania hadi nilipopata Connection ya kazi Jamhuri ya Czech kwenye moja ya makampuni makubwa ya ujenzi ambapo ndipo nilipo na Watanzania wengine wawili miezi takribani mitatu

Kweli maisha hayakimbiliwi.

One Love...
Kua uyaone mwanangu.
 
Soma sana,itakuja kukuuma siku moja,watu ambao uliwaacha nyuma wanasoma halafu wanakuja kuwa mabosi wako...
 
Katika maisha yako jitahidi ujifunze kuishi maisha ya namna zote ,hii itakusaidia katika kipindi cha furaha na tabu
 
Nakumbuka Mama yangu Mlezi alikuwa ananihamsha asubuhi saa Tisa kufanya kazi za ndani na kulala saa Sita Usiku na alikuwa akiniambiaga utakiona cha mtema kuni yaan nyumba hii mpk uhame ila cha ajabu kahama yeye na Yale mateso kwangu yamenifunza jinsi ya kuishi na walimwengu like hata siku wife akivinuna napiga usafi ndani na nje ya nyumba yangu napika msosi wangu napiga na Vi serengeti vyangu viwili nalala
 
Hapana alikua mtu poa sana. Ila maneno yake tulikuja kuyaelewa baadae sana na tabu tulizipata hasa.
Katika watu wanaoona.mbali kwa watoto wao ni baba, na akiona mwenzake (mkewe) ana msikiliza atamwambia mengi kuhusu kila mtoto na maisha yake ya baadae, mama akijifanya yeye ndiye mwenye uchungu na watoto ana nyamaza anakufa nalo
 
Back
Top Bottom