Ni kitu gani kimebadilika katika elimu Tanzania? Tukiendelea kuwaacha wajinga watuongoze watu wenye akili ni hatari

Ni kitu gani kimebadilika katika elimu Tanzania? Tukiendelea kuwaacha wajinga watuongoze watu wenye akili ni hatari

Na pia alisoma Trinity college na King' School huyo mwalimu nadhani walikuta Cambridge college thou sina hakika.
Isaac Barrow naye alisoma charterhouse according to wikipedia
Unafikiri nini kifanyike katika elimu ili vijana wetu wawe kama kina Isaack Newton?
 
Labda niulize sisi tuliosoma miaka ya nyuma na sasa kuna kitu gani kimebadirika?

Tulisoma bila kuwa na vitabu, hatukujuwa sylubus yoyote, Primary tuliwahi namba SAA 12 asubuhi na SAA 8 mchana ni mwisho wa masomo na kurudi nyumbani na wengi hatukusoma masomo ya ziada tuition lakini kulikuwa na vipanga balaa.

Sasa uvumilivu umenishinda, nina kitoto ni one of dependant wangu anaamka Saa 10 usiku saa 12 asubuhi anaanza tuition ya lazima shuleni anaendelea na masomo mpaka Saa 12 jioni kisa eti ni darasa la saba.

Sasa nimepitia repoti yake leo asubuhi hii ya annual examination sijafurahishwa nayo lakini remarks za class teacher ameandika Good.

Nimejiuliza sana darasa la Watoto 60 mtoto anakuwa wa 50 hii good inatoka wapi? OK average B lakini kutesa kote huku Watoto haya ndio matokeo yake? Na ieleweke wazi hii ni private school.

Sasa labda Mimi nimepitwa na wakati naomba mnielimishe huku ndio tulikofikia?

Ifike sasa Wazazi hasa kina mama tuache ushamba, ni bora kutafuta shule ya umma nzuri mtoto asome huko umuwekee usimamizi mzuri tu kuliko huu Utapeli tunaofanyiwa na hizi private school.

Anyway nisiwachoshe lakini sijafurahishwa kwakweli.
Kama mnaweza kuruhusu darasa la saba kuingia bungeni, then we are doomed! Bungeni mijadala yake ni rocket science kwa msukuma! huyu aende achuuze afanye biashara zake za guest, siyo majadiliano ya bunge!
 
Ifike sasa Wazazi hasa kina mama tuache ushamba, ni bora kutafuta shule ya umma nzuri mtoto asome huko umuwekee usimamizi mzuri tu kuliko huu Utapeli tunaofanyiwa na hizi private school.
Huko shule za umma kusikie tu labda kidogo vidato vya juu kuliko huko shule za msingi, bora angalau huko primary school.

Mtafutie shule nzuri karibu na nyumbani ili angalau apate muda mzuri wa kulala na kuwahi nyumbani.
 
Unafikiri nini kifanyike katika elimu ili vijana wetu wawe kama kina Isaack Newton?
Tuache kuwafundisha kukalili tu bila kureason na ndiyo maana tunayojifunza darasani hatuwezi kuyatumia ku impliment chochote kwa wengi wetu. Na elimu itufunze kwanza kutatua changamoto zetu mfano kutengeneza zana za kilimo bora kwa kutumia material zilizopo kwenye maeneo yetu na ambazo kila mtu anaweza kujifunza na kutengeneza kama walivyofanya wachina mwanzo
 
Akili zako hazikutoshi, Mimi ni mlezi siyo mzazi, mtoto amefiwa na mzazi wake nimebeba jukumu la kumlea.

Acha this hash language, kuna maana gani ya maprivate school tunalipa mamimilion kama huwezi kupandisha uwezo wa mwanafunzi?
Hata kama hujamzaa huyo tayari ni mwanao, acha kumkana huyo mtoto.
 
Huko shule za umma kusikie tu labda kidogo vidato vya juu kuliko huko shule za msingi, bora angalau huko primary school.

Mtafutie shule nzuri karibu na nyumbani ili angalau apate muda mzuri wa kulala na kuwahi nyumbani.
Kwa sisi Watoto wa mjini Olympio ndio choice, ile ni English medium ya serikali, ni bora ukampa tip head teacher mtoto akasoma pale ukawa unalipia school bus kuliko haya mamilion tunayopigwa na hizi private school halafu hakuna maajabu yoyote.

Washkaji zangu kadhaa wanajimudu lakini Watoto zao wako pale na wanafanya vizuri tu, hili swala la shule Wazazi tunajichanganya sana.

Nina kijana wangu amemaliza form four form five nataka aende shule ya serikali, hata selection bado mama yake huyo tayari kashachukuwa fomu private hivi ninavyokwambia yupo boarding anasoma pre form five, je ni kweli form five anahitaji hizo Pre? Kama siyo Utapeli ni nini?
 
Tuache kuwafundisha kukalili tu bila kureason na ndiyo maana tunayojifunza darasani hatuwezi kuyatumia ku impliment chochote kwa wengi wetu. Na elimu itufunze kwanza kutatua changamoto zetu mfano kutengeneza zana za kilimo bora kwa kutumia material zilizopo kwenye maeneo yetu na ambazo kila mtu anaweza kujifunza na kutengeneza kama walivyofanya wachina mwanzo
Ni wazo zuri, je ni nani wa kulianzisha?
 
Kwa sisi Watoto wa mjini Olympio ndio choice, ile ni English medium ya serikali, ni bora ukampa tip head teacher mtoto akasoma pale ukawa unalipia school bus kuliko haya mamilion tunayopigwa na hizi private school halafu hakuna maajabu yoyote.

Washkaji zangu kadhaa wanajimudu lakini Watoto zao wako pale na wanafanya vizuri tu, hili swala la shule Wazazi tunajichanganya sana.

Nina kijana wangu amemaliza form four form five nataka aende shule ya serikali, hata selection bado mama yake huyo tayari kashachukuwa fomu private hivi ninavyokwambia yupo boarding anasoma pre form five, je ni kweli form five anahitaji hizo Pre? Kama siyo Utapeli ni nini?
Bilashaka nafasi changamoto maana ni kitonga tayari hicho, kila mmoja asie na kitu ndio kimbilio kwake
 
kuna maana gani ya maprivate school tunalipa mamimilion kama huwezi kupandisha uwezo wa mwanafunzi?
Kuna jamaa alisema mwanao ni kilaza. Mimi napingana nae isipokuwa nadiriki kusema wewe ndio kilaza.

Mtoto amefaulu kwa wastani wa B wewe unataka nini zaidi. Huo ufaulu unauona mdogo. Mbona ni ufaulu ni mzuri tu.
 
Elimu ya bongo, unasoma ili ukalili na upate misifa ya kijinga ya kufaulu mitihani ya kushindania ukalili bora.

Elimu ya bongo ni takataka, basi tu hatujapata viongozi sahihi.

Kuna topics+masomo yalitakiwa kufutwa, pia kuna Coz vyuoni zinatakiwa kufutwa, bila kusahau hata baadhi ya shule+vyuo vofutwe maana havina faida zaid ya kuzalisha ujinga mpya.

Kama uko vzur kiuchumi, somesha watoto zako shule za kawaida, yaan wasome bila mateso ya matwishen na kuwahishwa asubuh bila sababu za maana, then mwanao akijua kusoma na kuandika inatosha muachishe shule, mpeleke short-coz za kujifunza lugha ngeni za kimataifa mfano kiingereza, kifaransa, kijerumani, kiispania, kichina, kihindi n.k, then mpe muda atulize akili huku ukimpa motivation za maisha, BELIEVE ME baada ya muda utakuja kunishukuru.

Au
[emoji116] mwanao akimaliza kidato cha 4, achana na mashule ya A-level sjui wapi mpeleke vyuo vya kati akajifunze coz za kompyuta+ufundi ikiwezekana ajikite huko maisha yake yote, baada ya muda utakuja kunishukuru, tuendako huko hawa watu watahitajika sana, zaidi ya hizo takataka tunazowakalilisha wanafunzi.

Kama serikali imeshindwa kubadili huu ujinga basi mtu mmoja mmoja upatapo uelewa wa haya mambo unatakiwa uyafanyie kazi, mabadiriko yanaanza na wewe, ndipo wengine hufuata.
 
Akili zako hazikutoshi, Mimi ni mlezi siyo mzazi, mtoto amefiwa na mzazi wake nimebeba jukumu la kumlea.

Acha this hash language, kuna maana gani ya maprivate school tunalipa mamimilion kama huwezi kupandisha uwezo wa mwanafunzi?
Huwa mnapata wapi muda wa kujibizana na hawa wajinga ambao JF wameijua juzi tu, mkuu hawa usiwe unawajibu wengi wao maisha yamewatandika so wanaingia mitandaoni kumalizia hasira kwa watu wasiowajua.

Wewe ushangai mtu kajiunga mwaka jana tu tayari kaanza kutukana Wakubwa zake humu waliojiunga kipindi yeye ananyonya vidole.

Wapuuze hao wajinga.
 
Labda niulize sisi tuliosoma miaka ya nyuma na sasa kuna kitu gani kimebadirika?

Tulisoma bila kuwa na vitabu, hatukujuwa sylubus yoyote, Primary tuliwahi namba SAA 12 asubuhi na SAA 8 mchana ni mwisho wa masomo na kurudi nyumbani na wengi hatukusoma masomo ya ziada tuition lakini kulikuwa na vipanga balaa.

Sasa uvumilivu umenishinda, nina kitoto ni one of dependant wangu anaamka Saa 10 usiku saa 12 asubuhi anaanza tuition ya lazima shuleni anaendelea na masomo mpaka Saa 12 jioni kisa eti ni darasa la saba.

Sasa nimepitia repoti yake leo asubuhi hii ya annual examination sijafurahishwa nayo lakini remarks za class teacher ameandika Good.

Nimejiuliza sana darasa la Watoto 60 mtoto anakuwa wa 50 hii good inatoka wapi? OK average B lakini kutesa kote huku Watoto haya ndio matokeo yake? Na ieleweke wazi hii ni private school.

Sasa labda Mimi nimepitwa na wakati naomba mnielimishe huku ndio tulikofikia?

Ifike sasa Wazazi hasa kina mama tuache ushamba, ni bora kutafuta shule ya umma nzuri mtoto asome huko umuwekee usimamizi mzuri tu kuliko huu Utapeli tunaofanyiwa na hizi private school.

Anyway nisiwachoshe lakini sijafurahishwa kwakweli.
Ukijiona wewe una akili na wakati huo huo unakiri kuongozwa na mjinga, inabidi ukapimwe maradhi ya kichwa (kichaa) .
 
Labda niulize sisi tuliosoma miaka ya nyuma na sasa kuna kitu gani kimebadirika?

Tulisoma bila kuwa na vitabu, hatukujuwa sylubus yoyote, Primary tuliwahi namba SAA 12 asubuhi na SAA 8 mchana ni mwisho wa masomo na kurudi nyumbani na wengi hatukusoma masomo ya ziada tuition lakini kulikuwa na vipanga balaa.

Sasa uvumilivu umenishinda, nina kitoto ni one of dependant wangu anaamka Saa 10 usiku saa 12 asubuhi anaanza tuition ya lazima shuleni anaendelea na masomo mpaka Saa 12 jioni kisa eti ni darasa la saba.

Sasa nimepitia repoti yake leo asubuhi hii ya annual examination sijafurahishwa nayo lakini remarks za class teacher ameandika Good.

Nimejiuliza sana darasa la Watoto 60 mtoto anakuwa wa 50 hii good inatoka wapi? OK average B lakini kutesa kote huku Watoto haya ndio matokeo yake? Na ieleweke wazi hii ni private school.

Sasa labda Mimi nimepitwa na wakati naomba mnielimishe huku ndio tulikofikia?

Ifike sasa Wazazi hasa kina mama tuache ushamba, ni bora kutafuta shule ya umma nzuri mtoto asome huko umuwekee usimamizi mzuri tu kuliko huu Utapeli tunaofanyiwa na hizi private school.

Anyway nisiwachoshe lakini sijafurahishwa kwakweli.
1. Ni ukatili kumuamsha mtoto saa 10 kisa shule. Okoa huyo mtoto unayemlea.

2. Mtoto anafaulu Kwa wastani wa 'B', mwalimu lazima aandike 'very good'. Kumbuka, A - Excellent, B - Very Good, C - Good na D - Poor/Weak. Si suala la nafasi ya dogo darasani, ni personal progress yake.

3. Wazazi wa Tanzania AMKENI, mmezubaa sana. Kwanini mmeacha shule za binafsi ziwafanye zinavyotaka?
Mzazi una jukumu la kulinda ustawi na maendeleo ya mwanao. Usikubali tu kila linalotoka shule.
  • Usilazimishwe kumuweka mtoto boarding
  • Mtoto asilazimishwe kufanya homework za kupindukia. Kataza.
  • Remedials ni option, si lazima.
  • Hoji kuhusu michango na mipango ya shule kuhusu taaluma ya mwanao.
 
1. Ni ukatili kumuamsha mtoto saa 10 kisa shule. Okoa huyo mtoto unayemlea.

2. Mtoto anafaulu Kwa wastani wa 'B', mwalimu lazima aandike 'very good'. Kumbuka, A - Excellent, B - Very Good, C - Good na D - Poor/Weak. Si suala la nafasi ya dogo darasani, ni personal progress yake.

3. Wazazi wa Tanzania AMKENI, mmezubaa sana. Kwanini mmeacha shule za binafsi ziwafanye zinavyotaka?
Mzazi una jukumu la kulinda ustawi na maendeleo ya mwanao. Usikubali tu kila linalotoka shule.
  • Usilazimishwe kumuweka mtoto boarding
  • Mtoto asilazimishwe kufanya homework za kupindukia. Kataza.
  • Remedials ni option, si lazima.
  • Hoji kuhusu michango na mipango ya shule kuhusu taaluma ya mwanao.
Mkuu umeandika kitu cha maana sana, sasa Kali kuliko huyu mtoto anaumwa ni siku ya tatu sasa, inabidi aende shule huku anaumwa, nimemuuliza wife kati ya shule na na afya kipi ni bora? jibu nililopewa wacha nibaki nalo moyoni tu, eti kisingizio darasa la saba wanajiandaa na mtihani wa moko.

Sasa naomba kuelimishwa hivi kama afya ya mwanafunzi aio sawa na akipona akaenda kufanya mtihani wa moko, je asipofanya vizuri moko inamzuia kufanya National examination?

Kituko zaidi tunawatesa Watoto kwa manufaa ya shule maana wakimaliza National examination na wanafaulu kwenda form one lakini Wazazi bado tunawapeleka private, sasa shida yote hii ni ya nini?
 
Mkuu umeandika kitu cha maana sana, sasa Kali kuliko huyu mtoto anaumwa ni siku ya tatu sasa, inabidi aende shule huku anaumwa, nimemuuliza wife kati ya shule na na afya kipi ni bora? jibu nililopewa wacha nibaki nalo moyoni tu, eti kisingizio darasa la saba wanajiandaa na mtihani wa moko.

Sasa naomba kuelimishwa hivi kama afya ya mwanafunzi aio sawa na akipona akaenda kufanya mtihani wa moko, je asipofanya vizuri moko inamzuia kufanya National examination?

Kituko zaidi tunawatesa Watoto kwa manufaa ya shule maana wakimaliza National examination na wanafaulu kwenda form one lakini Wazazi bado tunawapeleka private, sasa shida yote hii ni ya nini?
Pole sana.
Shule nyingi sana za binafsi zinatumia wanafunzi Kwa manufaa yao ya kibiashara tu; bla bla bla za A kama zote.
Kwa hivyo, ni jukumu la wazazi na walezi kuwatetea na kuwalinda watoto dhidi ya uonevu na udhalimu wa shule za binafsi.
 
Back
Top Bottom