Ni kivumbi huko kigali rwanda yanga vs el merrikh & apr

Soloma TV Online

Senior Member
Joined
Jun 26, 2023
Posts
104
Reaction score
291
Timu ya soka ya Yanga inakwenda kuandika Historia yake ndani ya jiji la Kigali Rwanda kunako michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika. Iko hivi siku ya kesho Jumamosi ya tarehe 16.9.2023 wageni Yanga watavaana na wenyeji wao El Merrikh katika kusaka nafasi ya kutinga hatua ya Makundi ya michuano hiyo, furaha itaendelea tena ndani ya jiji hilo lenye mvuto wa kipekee barani Afrika siku ya Jumapili ya tarehe 17.9.2023 pale ambapo Mchezaji wao kipenzi Fiston Mayele na Pyramid yake watawavaa washika mitutu wa nchi hiyo APR. Na hapa nikutonye tu kuna uwezekano mkubwa kwa Uongozi wa Yanga kuwanunulia tiketi maelfu ya Mashabiki wao waliojazana nchini humo kwenda kumshuhudia Mayele wao.

NA HII TUNAIITA NI YANGA DHIDI YA EL MERRIKH & APR
 
Mayele ana nyota ya timu zinazovaa jezi za kijani...

AS Vita -> Yanga -> Pyramids
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…