Ni kosa gani alilolifanya Aboud Jumbe kustahili 'kifungo cha maisha'?

Ni kosa gani alilolifanya Aboud Jumbe kustahili 'kifungo cha maisha'?

kwa sasa bado alhaj jumbe yuko mji mwema?
au ameshatangulia mbele ya haki? Na bado yuko kwenye kizuizi cha nyumbani?
Ni muda umepita

Jumbe bado yupo hai.

Miaka ya 2005 alikuwa karibu kila siku ya Ijumaa akivuka pale kwenye pantoni alienda kuswali swala ya Ijumaa upande wa mjini na alikuwa gari yake haikai kwenye foleni.

Mwaka wa 2000 kama sijakosea alikwenda Geita kulikuwa na Jitimai (maswala ya kiislam).

Sasa nashangaa kusikia kuwa yuko kwenye kifungo. eeh!!
 
Uzi safi unafundisha historia kamili ambayo wengi hatuijui. Hapa kuna umuhim wa kujenga tabia ya kujisomea maandiko ya kihistoria pia!

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Mbaya wa Aboud Jumbe si Nyerere, bali ni muungano wa wazenji kadhaa ambao hawakukubaliana na mwenendo wa Jumbe wa kujiweka mbali na muungano baada ya kuona kuwa umuhimu wa nafasi ya makamu wa rais ulikuwa unamweza na nafasi ya waziri mkuu wakati huo, yaani Sokoine. Kwa muda mrefu tangu mwaka 1974 nafasi ya Makamu wa Rais ilikuwa na umuhimu sana ambapo Jumbe alimwakilisha Nyerere katika shughuli mbalimbali za kitaifa na za kimataifa, na vile vile alitoa maamuzi mbalimbali kwa niaba ya Rais. Baada ya Sokoine kung'ara sana katika siasa za Tanzania, nafasi hiyo ya Makamu wa Rais ikawa kama imemezwa na nafasi ya Waziri mkuu, ndipo Jumbe alipojisikia vibaya na kutaka kuondoa Zanzibar kwenye Muungano, na kusababisha machafuko ya kisiasa ya 1983. Hatua hiyo ilipingwa na wazenji kadhaa wakiwemo akina Sharif Hamad, Mzee Thabit Kombo, Brigedia Natepe, na wengineo.

Baada ya nafasi yaje kuchukuliwa na Rais Mwinyi, Mzee yule aliendelea kupewa heshima zote kama rais mstaafu, na nadhani ndiye mtu pekee aliyelipwa na kuhudumiwa sana na watanzania bila kufanya kazi yoyote, kwani tangu mwaka 1983 hadi leo hii ni karibu miaka 30 na bado analipwa na kuhudumiwa kama Rais mstaafu. Sidhani kama kuna kiongozi mweingie aliyewahi kuhudumiwa namna hiyo.

Nadhani kuwa alikuwa kakurupuka sana kwa vile kama angekuwa msikivu kidogo, huenda baada ya Sokine kufariki mwaka 1984, yeye ndiye ambaye angeweza kuchukua nafasi hiyo ya urais baada ya Nyerere kustaafu mwaka 1985; nafasi ambayo baadaye ilichukuliwa na Mwinyi aliyekuwa amemrithi umakamu wa Rais.
Ni siasa tu. mwenyezi Mungu azide kampa nguvu.
 
Sidhani kama mzee Jumbe alikurupuka! Naamini alifikia maamuzi aliyofikia kwa kusukumwa na ufahamu wake wa habari yenyewe ya muungano. Hata kama angepewa pesa zote za bajeti ya serikali Tz bado haiwi mbadala wa yeye kuwa huru. Mbona kama kafutwa kabisa miongoni mwa watu waliolitumikia taifa hili? Hasikiki tena!? Hata chembe ya haya hamna? Inasikitisha sana h
 
Anaishi mjimwema alie mponza Shalifu Hamad ndio aliopeleka waraka kwa nyerere kwamba jumbe alitaka kuvunja mungano
 
Habari wakuu,

Naombeni kujuzwa, aliyekuwa Rais wa Zanzibar kipindi hiko, ndugu Aboud Jumbe ambaye yupo Kizuizini mjini Kigamboni kwa takribani miaka 31 kifungo chake alihukumiwa miaka mingapi?

Au ndio cha maisha? Mwenye kujua anaweza atujuze maana Mzee Jumbe amezeeka kweli lakini hakuna hata msamaha mpaka leo.
 
Dah....Naandaa makala kuhusu huyu jamaa nitarudi hapa baadae
 
Tuwaachie wazenji maana alikuwa raisi wao. Mzee Sheini kazi kwako
 
HABARI HIZI ZA UPOTOSHAJI ALIWAHI PIA KUZILETA TUNDU LISSU NA AKAPINGWA HATA NA EDWIN MTEI....

Ni habari za kizushi.... na nadhani hata ile sheria ya mitandao huenda isikuguse......
 
Ndio maana tunataka mabadiliko,inakuwaje mtu anatelekezwa nyumbani kwa miaka yote hiyo kwa matakwa ya mtu fulani?mawazo mhando in action!
 
CCM mnataka kusema mzee Aboud Jumbe Mwinyi hayuko kizuizini????? kwa hiyo amezeeka sana na ni mgonjwa hajiwezi ndio maana miaka yote hiyo hahudhurii sherehe za kitaifa!!!!!

Ee Mwenyezi Mungu tunusuru na balaa la CCM na dhulma zao na shari zao Aamin.
 
Kizuizini ili kuwa uhukumiwi bali unawekwa. Bila kupelekwa mahakamani
 
Back
Top Bottom