Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Kuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.

Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.

Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Duuh pole sanaa... Huyo jamaa yako mwizii naee kweli anashirikiana na mafundi
 
Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?

Somo la solar haijanikaa vizuri.
Ukitaka maisha yasiokua na mawazo tumia wiring mbili kwenye nyumba.
 
Kuanza kujenga kwa pesa za pension baada ya kustaafu.
Mzee wangu baada ya kustaafu alifanya hicho kitu. Ni hatari kupita maelezo. Kwanini?

1. Mhusika hashauriki, anataka tu kujenga kwa sababu ana pesa mfukoni.

2. Anachokijenga huwa hakieleweki au hakikamiliki. Anaamini pesa yake ya pension inatosha kufanya chochote au kila kitu kitawezekana. Anaokota ramani popote anataka kujenga.

Kuhusu hii kitu, nina ushuhuda wa wazee wangu wawili waliostaafu jeshi.

Walifanya huo ujinga.
 
Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?

Somo la solar haijanikaa vizuri.
comment #98 imejibu vizuri, pasi, jiko na vifaa vyenye Watts Nyingi (300W au zaidi) ni msala kwa Solar ( japo kama uko vizuri kifedha inawezakana )

Solar hasa inahitaji vifaa laini (Watts Ndogo) kama taa, friji, TV, nk

ukiweka Inverter utatumia vifaa vyote vile vinavyoendeshwa na tenesco isipokua vile vikubwa pasi, jiko, nk

fundi anaweza weka udhibiti kwenye mfumo wa Solar ( mbele ya Inverter ), mathani fyuzi ambayo itakata pale mtu atakapochomeka vyombo vizito kama pasi kwenye soketi wakati mfumo wa Solar ukiwa unaopareti

kuhusu size ya mfumo weka vifaa ulivyonavyo, mie au mtu mwingine anawezasaidia pia

ila kwa ushauri tu juu ya tech ya vifaa (ni swala la ufanisi) nashauri hivi:

1. Solar Panel, chagua ya panel ya Mono badala ya Poly , soma zaidi hapa, bei zimechangamka

2. Charge Controller, chagua MPPT badala ya PWM, soma zaidi hapa , bei zimechangamka

3. Battery , wanasema zile za Minara ziko poa

3. Inverter, chagua yenye kutoa Pure Sine Wave, hii itaendesha vizuri ile vifaa vya umeme vyenye mota ndani kama friji, feni, mashine ya kunyolea, nk



 
Kujenga nyumba sehemu yenye water tables bila kutumia dawa za kuta matokeo yake fungus ukutani. Nilipata hasara isiyomithilika. Ilikua ujenzi wa kwanza.

Nilitumia fundi wa slope kitonga kama waswahili wanavyopenda duka linalozidisha chenji.
 
Though sijawahi kuwa na nyumba wala kujenga ila kosa ambalo siwezi kufanya ni kuachia upenyo wowote, nitajipanga vizuri na hela yao yote cash na nitakuwa nao site kufuatilia kila hatua huku nikiwa na nguo za kazi ikibidi kusaidiana nao kabisa.
Kushinda site ni muhimu sana mkuu
Mafundi wengine wanaenda nje kabisa ya makubaliano,, anaamua kukujengea atakavyo yeye kama anajenga kibanda cha kuku nyumbani kwake.
 
Back
Top Bottom