Nyumba kubwa lina raha yake. Kama una pesa bora ujenge nyumba kubwa. Sebule mbili, chumba cha kusomea/ofisi. Self contained bed rooms 4, jiko kubwa etcKutumia pesa nyingi kufanya ujenzi wa jumba kubwa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nyumba kubwa lina raha yake. Kama una pesa bora ujenge nyumba kubwa. Sebule mbili, chumba cha kusomea/ofisi. Self contained bed rooms 4, jiko kubwa etcKutumia pesa nyingi kufanya ujenzi wa jumba kubwa
Yeye hana uzoefu, nadhani ndio anataka kuanza kujenga nyumba yake ya kwanza, kwa hiyo anatafuta uzoefu.Ungeanza wewe ingependeza
Kwani nyaya si zilezile hapo si kuongeza inverterKutoweka wiring system ya solar! Mnaojenga saivi hili nalo mlitizame..
Lakini ninadhani hiyo unaweza kuiweka muda wowoteAisee mimi sijui, ila fundi aliniambia tulisahau wiring ya solar, sasa alichomaanisha ni nini hapo?
Duuh pole sanaa... Huyo jamaa yako mwizii naee kweli anashirikiana na mafundiKuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.
Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.
Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Mimi sikujua kabisa mkuu, lakini kwa mfumo huo si inabidi uweke solar panel kubwa, battery kubwa ili kuweza kumudu appliances za umeme wa 220V(huu wa taaaanesco)Kwani nyaya si zilezile hapo si kuongeza inverter
So long hakuna kutindua nyumba hapo hakuna shida mkuu, hakuna kitu inakera kama kutindua nyumba.Lakini ninadhani hiyo unaweza kuiweka muda wowote
Kiukweli, sikumfanya chochote maana kwa jinsi alivyotetemeka kwa uoga ilikuwa ni adhabu tosha. Na aliendelea na mifuko ile ile, na kesho yake nikapeleka mdogo wangu akasimamie.Eeeheehe ukafanyaje sasa hapo?
Asante chief, alikuwa ni huyo fundi mwenyewe ila kesho yake nikampeleka mdogo angu akasimamie.Duuh pole sanaa... Huyo jamaa yako mwizii naee kweli anashirikiana na mafundi
Ukitaka maisha yasiokua na mawazo tumia wiring mbili kwenye nyumba.Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?
Somo la solar haijanikaa vizuri.
Ilishauzwa boss sikuipenda, kwa muonekano waweza sema ina vyumba hata 5 mpaka sita ukiwa njee ndani sasa ni sawa viukumbi vidogo dogoSasa boss kama mavyumba makubwa si utafute fundi urekebishe, uweke zote self
Kuanza kujenga kwa pesa za pension baada ya kustaafu.
Mzee wangu baada ya kustaafu alifanya hicho kitu. Ni hatari kupita maelezo. Kwanini?
1. Mhusika hashauriki, anataka tu kujenga kwa sababu ana pesa mfukoni.
2. Anachokijenga huwa hakieleweki au hakikamiliki. Anaamini pesa yake ya pension inatosha kufanya chochote au kila kitu kitawezekana. Anaokota ramani popote anataka kujenga.
comment #98 imejibu vizuri, pasi, jiko na vifaa vyenye Watts Nyingi (300W au zaidi) ni msala kwa Solar ( japo kama uko vizuri kifedha inawezakana )Asante kwa maelezo mazuri. Na solar yenye ukubwa gani naweza kufunga ili kutumia kwenye vifaa vya kawaida kama pasi, TV nk? Umesema hapo nikifunga invertor sina sababu ya kubadilisha taa, maana yake hata vifaa vingine naweza kutumia kwa hiyo solar?
Somo la solar haijanikaa vizuri.
Ni kweli ndugu,, ndo maana tunapeana uzoefu hapa ilikupunguza makosa yasitokee kwa wingiAlways makosa ya kawaida hayaepukiki na sometimes huja kugundulika ujenzi ukiwa umeshakamilika
Kushinda site ni muhimu sana mkuuThough sijawahi kuwa na nyumba wala kujenga ila kosa ambalo siwezi kufanya ni kuachia upenyo wowote, nitajipanga vizuri na hela yao yote cash na nitakuwa nao site kufuatilia kila hatua huku nikiwa na nguo za kazi ikibidi kusaidiana nao kabisa.
Inavuja?Kujenga nyumba bati kufichilia ndani(hidden roof) kwakweli maisha yamekuwa ya wasiwasi kipindi hiki cha mvua nakaa ndani utafikiri nimejificha chini ya mwembe.