Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Mambo yote ambayo unafanya mara moja tu kama wiring na plumbing ni muhimu kutumia muda sana.

Ningekuwa najenga sasa, ngepiga fiber ku future proof network. In fact nime augment network yangu na fiber kwa sababu natumia 10Gbps routers/switches/ NASes.

Nikifikiria sana, kwa matumizi ya kawaida, ukiwa na powerful wireless router utaweza kufanya mambo mengi kwa wireless. Devices zenyewe siku hizi zinakuwa wireless. Wiki iliyopita nimepewa Thinkpad X1 mpya kazini, haina hata network slot for RJ45, ni wireless tu, na inafanya kazi vizuri tu.

Tatizo linaweza kuja kama unatumia NAS na file transfer processes zinazohitaji speed kubwa utahitaji fiber.
Kumbe Thinkpads zinakubalika hadi huko dunia ya kwanza?. Huwa nazichukulia kawaida sana.
 
Kumbe Thinkpads zinakubalika hadi huko dunia ya kwanza?. Huwa nazichukulia kawaida sana.
Thinkpad ndiyo laptops zinazotumika zaidi kwenye corporate world Marekani.

Thinkpad kama hii ya X1 Carbon ina specs nzuri sana tu kwa kazi za kawaida, na unaweza ku customize na Lenovo kwa matakwa yako.
 
Mnaejenga mijumba mikubwa mjitafakari mambo yamebadilika siku hizi hakuna kutembeleana ovyo wala kuishi kwa ndugu kama zamani na watoto wakikua wanakimbilia sehemu nyingine kutafuta maisha ,kwahiyo utabaki na jumba kubwa kama msikiti peke yako
Mwisho wa siku ndio utasikia nataka kupangisha
 
nimekosea mengi ila kuna hili la kumuweka kijana kipindi sijaamia bila kuwa na makubaliano yoyote, sasa nimeamia na kijana sijui namuamishaje....
Hii mie pia iliwahi kunitokea siku za nyuma kijana alikaa akapata mke na mtoto. Siku nataka kuhamia kwenye hiyo nyumba ikabidi nikamlipie chumba na sebule mwaka ili atoke kwangu
 
Usije ukatumia pesa yooote kwenye ujenzi ukakaa usubiri muijiza.

Kwa mfano una 2mil unataka uingiize kwenye ujenzi. Tumia 1.5 tu 500k iweke pembeni.

Au una 20 Mil. Weka 15mil kwenye jengo 5mil iweke pembeni. Utanielewa baadae
Ebu fafanua maana nataka kuanza ujenzi hapa nina million 60. So niingize ngapi kwa ujenzi nibakize ngapi na kwa nini?
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Yaani ata fundi alishindwa kumshauri
 
Nyumba inatakiwa kupewa muda wa kukauka. Unaweka msingi unasubiria kidogo ukauke na kunywa maji vizuri wakati unadadisi ni vitu gani ambavyo vinatakiwa kuwekwa hapo kwenye msingi kabla ya kupandisha ukuta.
Mkuu Zemanda shukurani sana kwa madini ya thamani uliyotoa, vipi ni muda wa siku gapi tangu msingi umejengwa ndipo ukuta wa tofali uanze kujengwa?
 
Namshukuru Mungu amenijaalia uwezo wa ku design ndani pangu paweje...

Ninaamini kwamba usipojali kiwanja unachojengea bati umepoteza.

Ukijenga nyumba ukawwka bati. Umefukia kiwanja.

Jenga floor mbili. Utakuwa umesave kiwanja.

Tunajenga nyumba zetu. Lakini tunasahau tunaziba viwanja juu kwenyer paa
 
Dirisha la jikoni kuwekwa baada ya kozi mbili ,matokeo yake wakati wa plumbing imekua ngumu kuweka sehemu ya sink, nimeingia hasara ya kutoa grill likakatwe na kupandisha kozi mbili tena ili kupatikane mahali pa kuweka sink la vyombo,sikutaka libanane kwenye kona

Fundi kutotoboa msingi ili nyumba ipumue,hapa nafikiria kutoboa hata kama nyumba imeshapanda.

Kujenga mashimo mawili ya choo badala ya moja,hii najutia mpaka kesho ,kila mtu site naona anajenga moja

Kupandisha kozi 11 badala ya 10 baada ya msingi,matokeo yake nyumba imekua ndefu sana
Nyumba ndefu si inakuwa zuri hasa ukanda huu wa mwambao wa pwani kutokana na misimu ya joto, kwani joto ndani ya nyumba linakuwa si kali tofauti na nyumba fupi au?
 
Nilisimamia ujenzi wa nyumba ya familia nikajifunza baadhi ya kanuni!!

1. Kugawanya ujenzi kwa phases, ambapo phase ya kwanza msingi, ya pili kupandisha na ya tatu kupaua hapo unakuja kwenye finishing hiyo ni phase ya nne yenye vipengele vidogo vidogo kama plambing, mabomba ya umeme, plasta, madirisha (grill) na n.k.

2. Kugawanya phases na kujengea mfukoni, unakwenda site na ramani yako unafanya makadirio na fundi ya gharama, nguvukazi na materials kwa phase ya kwanza. Unachofanya kadirio la fundi unaongeza na wewe kidogo (mafundi hawajui kukadiria). Unakusanya ile pesa.

3. Ukishakusanya pesa ya phase, unatafuta wiki au siku kumi za kazi ya phase 1. Mfano; ushaongea na fundi msingi utatumia siku nne, saa kumi na mbili upo site halafu wa mwisho kuondoka. Angalau utapunguza kupigwa na fundi na phase ya pili hivyo hivyo

4. Unapogawanya ujenzi kwa phase maumivu ni madogo sana. Mfano foundation m1.7 unatafuta m2 unasimamia show ukimaliza unaondoka na mahesabu ya kupandisha labda m4 unakwenda kuitafuta. Baada ya miezi ukirudi nyumba inapanda wiki tu mpaka inaisha japo ulisimama kwa miezi sita. Ukiondoka hapo na hesabu za kupaua na n.k.

NB: Ujenzi hakikisha unachorewa ramani tena mchoraji anafika site kuangalia eneo atakushauri vizuri sana
Asante sana kwa ushauri na mwongozo, Mungu azidi kukuweka.
 
M
KUANZA KUJENGA NA FUNDI ASIE JUA KUFANYA SETTING YA MSINGI!!!!!!! MSINGI HAUKUWA SQUARE NA ILIONGEZA GHARAMA KWANGU , LAZIMA UNAPOAANZA KUJENGA TAFUTA MTAALAMU UMLIPE, MALIPO INATEGEMEA NA AINA YA NYUMBA THEN NDIYO UENDELEE NA MAFUNDI WA KAWAIDA KAWAIDA. NAOMBA SANA MZIGATIE HILI NDG ZANGU MAANA NAJUA HUMU WAJUAJI WENGI 😀

Pia kuna kosa kubwa la kutokuwa na walewa mdogo wa plumber au maksudi kutaka urahisi Kwanza kwenye Bathroom kufanya setting choo, sehemu ya kuogea na wash basin vikae vipi? sasa unakuta fundi sehemu ya kuongea inakuwa ya kwanza ukifungua mlango tu then inafuata wash basin mwisho kwenye ukuta na juu kidirisha ndiyo sasa kinakaa choo , sasa ebu fikiria unavyooga maji ya shower yanaruka mpka mlangoni ndiyo sasa yanaelekea upande wa choo ndiyo yanatoka, ukimuuliza fundi anakwambia kutakuwa na slope kali haina shida!!!!! kimsingi kwenye set up unaanza na wash basin au choo then mwishoni unaweka sehemu ya kuogea (shower) kosa lingine ni plumber kuweka heater ndani ya bathroom badala ya kuiweka nje tena unakuta kila bathroom ina heater yake wakati inawezekana kuweka moja ikatumika hata bathroom tatu. AKSANTENI.
Mkuu asante sana ku share elimu, sorry naomba kuuliza je kwani mtu akishakuwa ni fundi ujenzi anaweza asiwe vizuri kwenye ujenzi wa msingi (Fondation)?
 
Dirisha la jikoni kuwekwa baada ya kozi mbili ,matokeo yake wakati wa plumbing imekua ngumu kuweka sehemu ya sink, nimeingia hasara ya kutoa grill likakatwe na kupandisha kozi mbili tena ili kupatikane mahali pa kuweka sink la vyombo,sikutaka libanane kwenye kona

Fundi kutotoboa msingi ili nyumba ipumue,hapa nafikiria kutoboa hata kama nyumba imeshapanda.

Kujenga mashimo mawili ya choo badala ya moja,hii najutia mpaka kesho ,kila mtu site naona anajenga moja

Kupandisha kozi 11 badala ya 10 baada ya msingi,matokeo yake nyumba imekua ndefu sana
Urefu wa kwenda juu ni mabati alivyopaua labda, lakini kozi moja iliyoongezeka haiwezi kufanya nyumba iwe ndefu kias Cha kusema "sana"
 
Naombeni ushauri kesho naenda kukutana na fundi ili anipigie gharama za kuanza msingi kwanza

Je kuna ulazima wa kuwa na vyoo viwili vya ndani kimoja master na kimoja cha public, nyumba ya vyumba viwili tu

Au nikiweka choo kimoja tu hicho cha public itakuwa good

Kibaraza cha jikoni hicho kina umuhimu wa kukaa hapo au nikiondoe

Na naomba mnisaidie kwenye upande wa ukubwa sebule inakuwa na ukubwa gani standard urefu na upanda(futi na meter)

Chumba cha master kinakuwa na ukubwa gani pia,chumba cha kawaida kinakuwa na ukubwa gani, choo kinakuwa na ukubwa gani na jiko la kawaida linakuwa na ukubwa gani.

Sitaki nyumba kubwa inisumbue kwenye kuimalizia, nataka iliyotulia standard isinitese kwenye vifaa vinavyoanzia na english huko
 

Attachments

  • IMG_20250214_110953.jpg
    IMG_20250214_110953.jpg
    549.1 KB · Views: 3
Back
Top Bottom