Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

umenikumbusha kitu hapa
nilipanga pahala, maji ni dawasco na kila mtu mita yake
nilikua nalipa 40k kila mwezi, baada ya miezi 5 nakuja kustuka kuna leakage, tena sehem ya outlet ya bomba bafuni, na ni ngumu kugundua, maji yana 'chururu' kimya kimya mno yakiambaa ukutani mpaka chini , inaambaa na kona za sakafu, yalee mpaka kwenye kashimo, yaani chururu huioni mpaka uweke macho karib kabisa na ukuta(una tiles), nikapata jibu kwanini ukuta wote wa upande wa pili(kuna room) ulikua unapukutika

nikafunga koki kubwa ya nje, ikawa nikitaka kuchota najaza jaba na ndoo then nafunga koki, bili ya maji ilikuja 8000 kwa miezi iliyobaki
Hii ya leakage usipojua utaumia sanaa.. Sisi bili ilikuja laki mzee lakini kila tuliamgalia hatuoni maji yanatumika wapi...!!
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Kujenga kidogo kidogo siyo sababu, itakuwa yeye kakulia kwenye maisha ya vyoo vya nje, kama kakukia kwenye nyumba ya vyoo vya ndani lazima na yeye angejenga choo ndani tu, kama anamke basi huyo mke wake jamii moja na yeye wamelelewa kwenye nyumba ya vyoo vya nje au kwao walikuwa wana jisaidia vichakani uko vijijini kwao
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Niite nikushauri.

Ua chumba kimoja. Kulingana na ramani ya nyumba Ilivyo toavyoo viwili ita fundi aweke system ya mabomba kutoa taka nje kwenye shimo la nje.

Nimuhim kuangalia location ya chumba atakachokiua na shimo lilipo.

Upata vyoo vya kisasa. Fundi ataweka mtandao huu
Screenshot_20221230-092937.jpg
Screenshot_20221230-092836.jpg
Screenshot_20221230-092820.jpg
Screenshot_20221230-092732.jpg
Screenshot_20221230-092655.jpg
Screenshot_20221230-092639.jpg

Hakikisha mfumo wa maji taka nje unakuwa wa kisasa wa kupoteza maji ardhini.
 
Unarudiaje mkuu, bati mpya au unatoa zile zilizopo then wanarekebisha afu unarudisha zile zile?
Mm naona nirudie upya zote maaana kwanza kench ipo juu pia ukuta hawakutanguliza plaster mwanzoni so zinakanyagwa kanyagwa sana zinakuwa na kasoro

Napenda baada ya kumalizana na kila kitu kinacho husu ukuta pasiwe na mtu wa kupanda tena juu ya bati ili niwe na Imani na kilicho fanyika
 
Mm naona nirudie upya zote maaana kwanza kench ipo juu pia ukuta hawakutanguliza plaster mwanzoni so zinakanyagwa kanyagwa sana zinakuwa na kasoro

Napenda baada ya kumalizana na kila kitu kinacho husu ukuta pasiwe na mtu wa kupanda tena juu ya bati ili niwe na Imani na kilicho fanyika

Bati ni 40 nimezilaza hidden roof
Hujaeleweka
 
Hiyo mkuu imenitokea mimi, nilinunua kiwanja 2010...nikaja kujenga 2015.. siku magufuli anaapishwa ndo nahamia kwangu,, ila sahiv nimezungukwa na waswahili wasiojielewa hata pakupitisha kigari hapapo...nikija kununua gar itabid ilale (CCM.) Natamani kuuza kwa bei ya kutupa nijenge sehemu nyingine..Kijumba chenyewe cha kawaida ila unaishi na watu wenye wivu balaa....

Makosa niliyoyafanya nilijenga kwa haraka haraka lengo nihamie kwangu kutokana kugombana gombana na mwenyenyumba..
Haraka haraka haina baraka..!!

Maisha ndio yalivyo mkuu,umetoka kugombana na wenye nyumba sasa hivi unagombana na majirani [emoji276]mwendo ni haste haste hakuna kupumzika
 
Kuamini mafundi nikiambiwa cement imeisha napiga simu tu inapelekwa bila kufatilia. Kuna siku fundi anapiga simu kuwa wamesimama kazi kwa kuwa cement imeisha inabidi ipelekwe haraka.

Ikabidi niende mwenyewe kuangalia kazi imefikiaje hadi cement kuisha hivo, nilivyofika mafundi wakastuka sana maana hawakutarajia kuniona kwa wakati huo. Ikawa kila ninapoingia kukagua jamaa kama ananizuga ili niache nimsikilize yeye. Nikahisi kitu nikaongeza umakini kuangalia chumba hadi chumba.

Bwana weee! Si nikakuta kuna mifuko 9 ya cement haijatumika wameificha kwenye chumba chooni. Asee jamaa alibabaika sana akakosa la kusema.
Hukufukuza majambazi hayo?
 
Hiyo mkuu imenitokea mimi, nilinunua kiwanja 2010...nikaja kujenga 2015.. siku magufuli anaapishwa ndo nahamia kwangu,, ila sahiv nimezungukwa na waswahili wasiojielewa hata pakupitisha kigari hapapo...nikija kununua gar itabid ilale (CCM.) Natamani kuuza kwa bei ya kutupa nijenge sehemu nyingine..Kijumba chenyewe cha kawaida ila unaishi na watu wenye wivu balaa....

Makosa niliyoyafanya nilijenga kwa haraka haraka lengo nihamie kwangu kutokana kugombana gombana na mwenyenyumba..
Haraka haraka haina baraka..!!

Shukuru upo kwako Mkuu
 
Mnaejenga mijumba mikubwa mjitafakari mambo yamebadilika siku hizi hakuna kutembeleana ovyo wala kuishi kwa ndugu kama zamani na watoto wakikua wanakimbilia sehemu nyingine kutafuta maisha ,kwahiyo utabaki na jumba kubwa kama msikiti peke yako
😂😂😂😂😂😂😆😆
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.

Kuweka choo ndani inawezekana.. aue chumba kimoja aweke choo ndani. Na hata chumba chake kugeuza master kinawezekana
 
Back
Top Bottom