Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 49,390
- 152,301
Moja ya mambo yatayoigharimu CCM hii ya Magufuli, ni hiki kitendo cha mikutano ya Lissu inayovuta maelfu ya Wananchi kusambaa mitandaoni huku kwenye mainstream Media kama vile tv na redio mikiutano hii hairipotiwi wakati wananchi wanategemea kuiona ikiripotiwa katika vyombo hivi vya habari lakini inakuwa kinyume chake.
Hali hii inazidi kumfanya Lissu akubalike zaidi, huku wale wanaotuhumiwa kuzuia Media zisiripoti habari za Lissu, wakiendelea kupoteza mvuto mbele ya wananchi na hili jambo halina tofauti kabisa na kile kitendo cha kuzuia mikutano ya siasa ya vyama vya upinzani kwa miaka mitano huku CCM wakiwa wako huru kuendesha siasa, ambapo leo hii, wameanza kuvuna walichopanda kwa kuzuia mikutano ya siasa ya wapinzani na kama ambavyo watavuna wapandacho sasa kwa kuzuia habari za Lissu.
Na Lissu mjanja sana kwani ameshajua jambo hili linakera Wananchi hivyo analitumia kisiasa na ndio maana hivi karibuni alitamka wazi kuwa media haziripoti habari za mikutano yake kwasababu media zinamuogopa "mtu mmoja"(hakumtaja ila anaelewaka na ndio maana hata wananchi walishangilia kauli hiyo).
Kutotangaza habari za Lissu, ni hatari kisiasa, na kuzitangaza pia ni hatari kisiasa kwa wahusika.Sasa najiuliza, wanachomokea wapi wenzetu hawa?
Mwaka huu wataomba poa.
Hali hii inazidi kumfanya Lissu akubalike zaidi, huku wale wanaotuhumiwa kuzuia Media zisiripoti habari za Lissu, wakiendelea kupoteza mvuto mbele ya wananchi na hili jambo halina tofauti kabisa na kile kitendo cha kuzuia mikutano ya siasa ya vyama vya upinzani kwa miaka mitano huku CCM wakiwa wako huru kuendesha siasa, ambapo leo hii, wameanza kuvuna walichopanda kwa kuzuia mikutano ya siasa ya wapinzani na kama ambavyo watavuna wapandacho sasa kwa kuzuia habari za Lissu.
Na Lissu mjanja sana kwani ameshajua jambo hili linakera Wananchi hivyo analitumia kisiasa na ndio maana hivi karibuni alitamka wazi kuwa media haziripoti habari za mikutano yake kwasababu media zinamuogopa "mtu mmoja"(hakumtaja ila anaelewaka na ndio maana hata wananchi walishangilia kauli hiyo).
Kutotangaza habari za Lissu, ni hatari kisiasa, na kuzitangaza pia ni hatari kisiasa kwa wahusika.Sasa najiuliza, wanachomokea wapi wenzetu hawa?
Mwaka huu wataomba poa.