Ni kuandika Katiba Mpya au Kurekebisha Sheria za Chaguzi?

Ni kuandika Katiba Mpya au Kurekebisha Sheria za Chaguzi?

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
12,096
Reaction score
15,393
Kuna ufafanuzi unaohitajika kwa wanaoyaelewa vizuri haya maswala ya Katiba na sheria. Ni matumaini yangu kwamba baada ya uchangiaji wa mada hii wengi wetu ambao hatuna ufahamu vizuri juu ya mambo yahusuyo kazi hii inayokusudiwa kuanza, sote tutakuwa tumepata uelewa wa kutosha, na haitakuwa tena kama swala zima linatumika kuwachanganya wananchi wasijue kinachofanyika.

Kuna habari kwamba pesa inawekwa, kiasi cha Tsh 9 bilioni kiasi kitacho ombwa na Wizara ya Sheria katika Bajeti ya 2023/2024 ili pesa hiyo itumike katika kuandaa Katiba Mpya, na kurekebisha sheria kadhaa zihusuzo maswala ya uchaguzi, kama vile Tume Huru, na chaguzi za serikali za mitaa (2024) na ule wa 2025.

Hili linachanganya kidogo kwa tusioelewa hizi taratibu za kisheria.

Nidhanivyo mimi, ni kwamba jambo muhimu linalotakiwa kufanyika kwanza ni kuandika Katiba Mpya, ambayo, hiyo Katiba Mpya, ndiyo itakayoweka mwongozo wa kupata sheria zitakazoshughulikia maswala ya Uchaguzi na mambo mengine.

Kinachonichanganya sasa hivi, ni hili la kusema fungu hilo la pesa litatumika pia, mbali ya kutengeneza Katiba Mpya, litarekebisha sheria zihusuzo maswala ya uchaguzi.

Mtu anaweza kudhani hakuna mkanganyiko, kwa sababu Katiba Mpya ndiyo itakayotengenezwa kwanza, lakini ukiangalia vizuri, hili siyo linalonuiwa kufanyika mara moja. Ni "urekebishaji wa sheria" ndilo nuio la kwanza.

Mkanganyiko huu unaongezeka, pale inapokumbukwa kwamba kuna ile Tume iliyotoa mapendekezo yake kwamba Katiba Mpya itaanza kushughulikiwa baada ya 2025, na CCM inaliafiki hilo lilivyo.

Hapa nadhani kuna kuvungavunga kwa maksudi kunakofanywa na serikali. Lengo la fungu hili, siyo Kuandika Katiba Mpya; bali ni kurekebisha sheria zilizopo sasa hivi zinazolenga Tume ya Uchaguzi na maswala mengine ya uchaguzi, ambayo bado yanatokana na Katiba hii iliyopo sasa.

Kwa nini pawepo na ubabaishaji katika swala kama hili? Akina Zitto walishaafiki swala hilo, wanaogopa kuwauza CHADEMA walioapa kwamba bila Katiba Mpya hakuna uchaguzi?
 
Mkuu kinachokuja ni Katiba Mpya full stop ! haya mengine ni lugha tu ya namna ya uwasilishaji wa Taarifa .

Nafahamu wasiwasi ulionao , lakini nakutoa mashaka , hatujawahi kukosea .

La mwisho , naomba unipongeze kwa kuteuliwa kwenye Jukwaa hili
 
Mkuu kinachokuja ni Katiba Mpya full stop ! haya mengine ni lugha tu ya namna ya uwasilishaji wa Taarifa .

Nafahamu wasiwasi ulionao , lakini nakutoa mashaka , hatujawahi kukosea .

La mwisho , naomba unipongeze kwa kuteuliwa kwenye Jukwaa hili
Mkuu 'Erythro', unajuwa mimi sina mashaka na wewe, kama wewe hili lipo wazi siku zote.
Na nina uhakika unaelewa mashaka yangu yalipo kuhusu CHADEMA.

Huu mstari wa mwisho, niseme sijapata taarifa, lakini hilo halinizuii kamwe "Kupongeza" bila hata kujuwa sababu yenyewe, kwani msimamo wako hauyumbi kwa unayoyatetea. Kwa hiyo PONGEZI zangu zinalalia huko huko.

Umepambana sana, tokea nikufahamu humu humu JF.
Pongezi kwako, mkuu 'Erythrocyte'.

Mapambano "Yaendelee! (Naiga lugha).
 
Mkuu 'Erythro', unajuwa mimi sina mashaka na wewe, kama wewe hili lipo wazi siku zote.
Na nina uhakika unaelewa mashaka yangu yalipo kuhusu CHADEMA.

Huu mstari wa mwisho, niseme sijapata taarifa, lakini hilo halinizuii kamwe "Kupongeza" bila hata kujuwa sababu yenyewe, kwani msimamo wako hauyumbi kwa unayoyatetea. Kwa hiyo PONGEZI zangu zinalalia huko huko.

Umepambana sana, tokea nikufahamu humu humu JF.
Pongezi kwako, mkuu 'Erythrocyte'.

Mapambano "Yaendelee! (Naiga lugha).
Asante sana
 
Mkuu kinachokuja ni Katiba Mpya full stop ! haya mengine ni lugha tu ya namna ya uwasilishaji wa Taarifa .

Nafahamu wasiwasi ulionao , lakini nakutoa mashaka , hatujawahi kukosea .

La mwisho , naomba unipongeze kwa kuteuliwa kwenye Jukwaa hili
Katiba mpya haitokamilika kabla ya 2025, kinachoanza ni mabadiliko ya sheria ya uchaguzi.
 
Katiba mpya haitokamilika kabla ya 2025, kinachoanza ni mabadiliko ya sheria ya uchaguzi.
Hata mimi nadhani ni hivyo, lakini wahusika (serkali) ndiyo inayopotosha kwa kutumia lugha ya kilaghai.

Waseme moja kwa moja, kwamba haya ni marekebisho ya sheria zilizopo, zilizotungwa kwa mwongozo wa Katiba iliyopo sasa, ambayo itakoma hapo Katiba Mpya itakapokamilishwa (sijui lini).

Na sheria mpya zinazohusiana na chaguzi zitatungwa upya chini ya hiyo katiba mpya ili kutumiwa katika chaguzi baadae baada ya 2025.

Na umuhimu wa kulielewa hili jambo ni kwamba, hayo marekebisho ya sheria zilizopo, zinazotokana na katiba hii tuliyo nayo, bado sheria hizo zitakuwa zikiheshimu katiba ambayo inampa mteuzi (Rais) madaraka makubwa sana yasiyokuwa na kikomo. wala kuhojiwa popote; mahakamani kwa mfano.

Shria hizi zikirekebishwa zitakuwa na uwezo wa kumpunguzia Rais madaraka aliyonayo?

Hizi sheria zitarekebishwa ziseme matokeo ya uchaguzi ya rais yakishatangazwa hakuna wa kuyapinga?

Sheria hizi zitaruhusu Mgombea asiye na chama? n.k., n.k.,.

Usisahau ni nani anayerekebisha hizo sheria. Hilo ni Bunge la CCM! Sijui kama ni sahihi kuwatambua wabunge wa ACTWazalendo, kama wapunge wa upinzani.. Hata kama ni wa upinzani, kura zao hazisaidii chochote.
 
Tunabidi sisi wasomi na wazalendo wa kweli , Mama atulipe ili tuingie Mtaani kutoa Elimu kuhusu, Katiba mpya
 
Kuna ufafanuzi unaohitajika kwa wanaoyaelewa vizuri haya maswala ya Katiba na sheria. Ni matumaini yangu kwamba baada ya uchangiaji wa mada hii wengi wetu ambao hatuna ufahamu vizuri juu ya mambo yahusuyo kazi hii inayokusudiwa kuanza, sote tutakuwa tumepata uelewa wa kutosha, na haitakuwa tena kama swala zima linatumika kuwachanganya wananchi wasijue kinachofanyika.

Kuna habari kwamba pesa inawekwa, kiasi cha Tsh 9 bilioni kiasi kitacho ombwa na Wizara ya Sheria katika Bajeti ya 2023/2024 ili pesa hiyo itumike katika kuandaa Katiba Mpya, na kurekebisha sheria kadhaa zihusuzo maswala ya uchaguzi, kama vile Tume Huru, na chaguzi za serikali za mitaa (2024) na ule wa 2025.

Hili linachanganya kidogo kwa tusioelewa hizi taratibu za kisheria.

Nidhanivyo mimi, ni kwamba jambo muhimu linalotakiwa kufanyika kwanza ni kuandika Katiba Mpya, ambayo, hiyo Katiba Mpya, ndiyo itakayoweka mwongozo wa kupata sheria zitakazoshughulikia maswala ya Uchaguzi na mambo mengine.

Kinachonichanganya sasa hivi, ni hili la kusema fungu hilo la pesa litatumika pia, mbali ya kutengeneza Katiba Mpya, litarekebisha sheria zihusuzo maswala ya uchaguzi.

Mtu anaweza kudhani hakuna mkanganyiko, kwa sababu Katiba Mpya ndiyo itakayotengenezwa kwanza, lakini ukiangalia vizuri, hili siyo linalonuiwa kufanyika mara moja. Ni "urekebishaji wa sheria" ndilo nuio la kwanza.

Mkanganyiko huu unaongezeka, pale inapokumbukwa kwamba kuna ile Tume iliyotoa mapendekezo yake kwamba Katiba Mpya itaanza kushughulikiwa baada ya 2025, na CCM inaliafiki hilo lilivyo.

Hapa nadhani kuna kuvungavunga kwa maksudi kunakofanywa na serikali. Lengo la fungu hili, siyo Kuandika Katiba Mpya; bali ni kurekebisha sheria zilizopo sasa hivi zinazolenga Tume ya Uchaguzi na maswala mengine ya uchaguzi, ambayo bado yanatokana na Katiba hii iliyopo sasa.

Kwa nini pawepo na ubabaishaji katika swala kama hili? Akina Zitto walishaafiki swala hilo, wanaogopa kuwauza CHADEMA walioapa kwamba bila Katiba Mpya hakuna uchaguzi?
Muda huu wa miaka 2 iliyobaki ya Mama Samia madarakani hautoshi kufanya mchakato wa katiba mpya, ila unatosha kufanya mabadiliko ya katiba yetu ili uchaguzi wa 2025 uwe ni uchaguzi huru na wa haki na hiki kinachokwenda kutokea ndicho hiki tulicho kishauri Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!

P
 
Muda huu wa miaka 2 iliyobaki ya Mama Samia madarakani hautoshi kufanya mchakato wa katiba mpya, ila unatosha kufanya mabadiliko ya katiba yetu ili uchaguzi wa 2025 uwe ni uchaguzi huru na wa haki na hiki kinachokwenda kutokea ndicho hiki tulicho kishauri Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!

P
Kwa hiyo, lugha sahihi hapo ni "Kurekebisha Katiba", na siyo "Kuandika Katiba Mpya" kama Wizara yenye wataalam wote wa sheria inavyopotosha watu kwa maksudi kabisa!

Hata hivyo, haya Marekebisho yanafanywa na CCM, ikiwa ni pamoja na Bunge lake!
Ushiriki katika kurekebisha katiba kwa wasiokuwa CCM ni lini na wapi?
 
Kwa hiyo, lugha sahihi hapo ni "Kurekebisha Katiba", na siyo "Kuandika Katiba Mpya" kama Wizara yenye wataalam wote wa sheria inavyopotosha watu kwa maksudi kabisa!
Yes ni marekebisho tuu ya katiba na sheria ndio yanaweza kufanyika ndani ya miaka 2 hii iliyobakia, unless kama tutaamua kuendelea na ule mchakato wa kuikamilisha ile bora katiba. Mchakato huu wa Katiba ni umasikini wetu. Tujikubali, tuukubali, tuupigie kura ya ndio
Hata hivyo, haya Marekebisho yanafanywa na CCM, ikiwa ni pamoja na Bunge lake!
Ushiriki katika kurekebisha katiba kwa wasiokuwa CCM ni lini na wapi?
Utaratibu utaandaliwa na kutakuwepo ushirikishaji wa kutosha wa wadau, ila CCM ndio chama tawala na ndio yenye upper hand!.

P
 
Yes ni marekebisho tuu ya katiba na sheria ndio yanaweza kufanyika ndani ya miaka 2 hii iliyobakia, unless kama tutaamua kuendelea na ule mchakato wa kuikamilisha ile bora katiba. Mchakato huu wa Katiba ni umasikini wetu. Tujikubali, tuukubali, tuupigie kura ya ndio

Utaratibu utaandaliwa na kutakuwepo ushirikishaji wa kutosha wa wadau, ila CCM ndio chama tawala na ndio yenye upper hand!.

P
"...upperhand" ikiwa na maana, ndiye refa/mwenyekiti wa shughuli zote. Neno lake ndilo la mwisho!

hapo inatakiwa "Nguvu ya Umma."

CHADEMA ingefaa waweke akili zao huko kungali mapema. ....' lakini tatizo lao linajulikana, inapokuja kwenye swala hilo la "supreme arbiter"; wana tatizo kubwa sana upande huo.
 
"...upperhand" ikiwa na maana, ndiye refa/mwenyekiti wa shughuli zote. Neno lake ndilo la mwisho!

hapo inatakiwa "Nguvu ya Umma."

CHADEMA ingefaa waweke akili zao huko kungali mapema. ....' lakini tatizo lao linajulikana, inapokuja kwenye swala hilo la "supreme arbiter"; wana tatizo kubwa sana upande huo.
Linapokuja suala la maslahi ya taifa, don't bank on partisan politics, kwenye hili Chadema are already done!, well taken care off, don't bank on them anymore!.
P
 
Linapokuja suala la maslahi ya taifa, don't bank on partisan politics, kwenye hili Chadema are already done!, well taken care off, don't bank on them anymore!.
P
Sikubaliani nawe.
"...swala la maslahi ya taifa" haliwezi kuwa nje ya 'partisan politics'.
Ni lazima pawepo na upande mbadala unaoongoza juhudi za wananchi.

Unaweka 'focus' yako kwa CHADEMA for your own partisan interests; but my reasons for them not being the right group for the leadership work are totally different from your own.
 
Back
Top Bottom