Ni kujidanganya kwa mashabiki wa Yanga na Simba kuwaza kuchukua kombe la Club Bingwa badala ya kombe la Shirikisho

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Sisemi mengi:

Kwa uwekezaji tunaofanya kwa vilabu vyetu vya Yanga na Simba kulinganisha na miamba ya soka Afrika kwa upande wa vilabu, ni kujidanganga kuwaza kuchukua kombe la club bingwa barani Afrika badala ya kuwaza kwanza kuchukua kombe la shirikisho.

Hata kuvuka hatua ya robo fainali kwa timu zetu bado ni ndoto. Timu vibonde huishia hatua ya makundi.

Tunaloliita kombe la looser, ndio size, yetu na ndio linaweza kutupa heshima katika soka la Afrika kwa sasa lakini sio kujidanganya na Kombe la Mabingwa Afika.

Habari ndio hio.
 
Wa kuelewa wameelewa na wasioelewa wataelewa katika hatua inayofuata pale mmoja anapoweza kuingia nusu fainali(akijipanga vizuri), na mwingine kuishia robo fainali hata akijipanga mwaka mzima kwa kikosi alichonacho.
Suala sio kujipanga vizuri au kujiandaa mwaka mzima bali muda mwingine shirikisho na champions inategemea umekutana na nani knock out stage lakini ukweli kote ni kwa moto.

Ule msimu simba alitolewa na Kaizer kwa yale matokeo ya jumla sio kwamba simba alitakiwa ajiandae mwaka mzima ili amtoe Kaizer ukweli ni kwamba alijichangaya kidogo.

Kuna timu zinaitwa AS FAR na USM alger. Hizi timu ziko shirikisho. AS FAR anaongoza ligi yao mbele ya wydad aliyeko champions. USM alger yuko nafasi ya 5 kwenye ligi yao na anamzidi JS kabylie alieko mkiani points 15. JS kabylie yuko champions na anaongoza kundi.

Kwa hiyo sio rahisi kuelezea ugumu atakao kutana nao simba dhidi ya Wydad au JS kabylie au dhidi ya ugumu atakao kutana nao yanga dhidi ya USM alger au AS FAR.
 
Sasa utafanyaje ikiwa timu zetu zinapata nafasi ya kushiriki klabu bingwa Afrika? tujitoe makusudi kwa kuogopa kushindana na vigogo?
Nashangaaa hapo.[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wa kuelewa wameelewa na wasioelewa wataelewa katika hatua inayofuata pale mmoja anapoweza kuingia nusu fainali(akijipanga vizuri), na mwingine kuishia robo fainali hata akijipanga mwaka mzima kwa kikosi alichonacho.
Ngoja muda uje utoe majibu
 
Tunaloliita kombe la looser, ndio size, yetu na ndio linaweza kutupa heshima katika soka la Afrika kwa sasa lakini sio kujidanganya na Kombe la Mabingwa Afika.
ni Manara ndio ameliita hivyo, usituchafue wananchi halisi. Yule yuko pale kibiashara zaidi wala hatufai, na hata alifikia hatua ya kutuita wote hamnazo isipokuwa wawili tu
 
Na Yanga msipochukua hilo kombe LA loser mashabiki wenu watakufa kwa pressure
 
Wa kuelewa wameelewa na wasioelewa wataelewa katika hatua inayofuata pale mmoja anapoweza kuingia nusu fainali(akijipanga vizuri), na mwingine kuishia robo fainali hata akijipanga mwaka mzima kwa kikosi alichonacho.
Kufika robo fainali ya CAF champions League ni sawa na kuchukua kombe la Shirikisho CAF

Hebu fikiria timu zilizofika robo fainali ya UEFA CL kama vile Madrid, Bayern, Man City, Napoli n.k kwa ubora wao zingekuwa EUROPA lazima zingechukua kombe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…