Ni kwa jinsi gani Katiba Mpya inaweza kushusha bei za vyakula?

Ni kwa jinsi gani Katiba Mpya inaweza kushusha bei za vyakula?

powercert_Tz

Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
45
Reaction score
44
Kumekuwa na hoja kutoka siasa za upinzani, wakidai kwamba kuna uwezekano wa bei za vyakula kushuka iwapo tu tungekuwa na Katiba Mpya.

Hii ni hoja inayowavutia sana wananchi ila hakuna hata kiongozi mmoja wa upinzani aliewahi kueleza ni kwa jinsi gani jambo hili linawezekana.

Tafadhali kama una maoni yanayo weza kutusaidia kuthibitisha kuwa jambo hili ni kweli au lah, unakaribishwa kwa faida ya wengi.
 
Jibu maswali haya mawili:

1. Wewe una elimu ya kiwango gani kwanza?

2. Na wewe unafikirije kwani? Katiba (Kwa maana ya mfumo wa wananchi kujitawala na kujiamulia mambo yao; mfano namna ya kupata viongozi, mgawanyo wa rasrimali nk) uko connected vipi na maisha yao (yetu) ya Kila siku?

NB: Ukiwa mkweli wa nafsi yako na ukajibu maswali haya kwa uaminifu wote, huhitaji kuelezwa au kufundishwa na mtu ili uelewe ni kwa jinsi gani mfumo wa mzuri au mbaya wa kujitawala watu uliotengenezwa na kijitabu kinachoitwa "katiba" katika jamii fulani unaweza kuathiri maisha yao ya Kila siku Kwa namna hasi au chanya..
 
Jibu maswali haya mawili:

1. Wewe una elimu ya kiwango gani kwanza?

2. Na wewe unafikirije kwani? Katiba (Kwa maana ya mfumo wa wananchi kujitawala na kujiamulia mambo yao; mfano namna ya kupata viongozi, mgawanyo wa rasrimali nk) uko connected vipi na maisha yao (yetu) ya Kila siku?
Mimi nimeishia darasa la saba, na hili swala silielewi ndio maana nimeuliza. Mimi ni Mtanzania na naishi hapa hapa nchini. Bei za vyakula imepanda ila nashindwa kuelewa ni kwanamna gani katiba niliyo nayo sasa inaweza kusababisha mambo hayo, kiasi kwamba tukiwa na katiba mpya tutakua na unafuu kwenye mambo kama haya.
 
Nacho kiona kwenye hizi harakati za katiba mpya, ni maswala ya madaraka tu. Kwamba wapinzani wameshagundua hawawezi kushika dola kama katiba itaendelea kua hii, hivyo wanajaribu kahakikisha tunaichukia hii katiba tuliyo nayo ili tupate hiyo nyingine itakayo wapa wao mwanya wa kupenya kwenye dola.

Ila kiukweli harakati hizi sio kwa maslahi ya wananchi, hawa watu hua wanatanguliza maslahi yao mbele tu sikuzote. Hata ukichunguza kilicho sababisha mchakato wa kwanza kutofikia muafaka utakuta changamoto ilikua ni maslahi ya upinzani hayakutimizwa.
 
Nilitegemea swali lako liwe, je hii katiba ya sasa inachangiaje kupandisha gharama za maisha au mfumuko wa bei? mfano kuna ulazima gani kila nafasi nyeti lazima ateuliwe badala ya kuomba na kuchaguliwa kwa mchakato huru kwa kuzingatia vigezo? ie sasa hivi watu wote wanaoteuliwa kigezo kikuu ni kuwa kada badala ya kuangalia uzoefu na utaalamu kwenye eneo husika hii ingeongeza weledi na ufanisi kwenye kujibu changamoto mbalimbali katika nchi yetu
 
nilitegemea swali lako liwe, je hii katiba ya sasa inachangiaje kupandisha gharama za maisha au mfumuko wa bei? mfano kuna ulazima gani kila nafasi nyeti lazima ateuliwe badala ya kuomba na kuchaguliwa kwa mchakato huru kwa kuzingatia vigezo? ie sasa hivi watu wote wanaoteuliwa kigezo kikuu ni kuwa kada badala ya kuangalia uzoefu na utaalamu kwenye eneo husika hii ingeongeza weledi na ufanisi kwenye kujibu changamoto mbalimbali katika nchi yetu
Kwa inavyo onekana umeelewa swali ila huna majibu ya kujitosheleza ndio maana unajitikita katika kutengeneza maswali unayotaka. Ulipaswa kueleza ni kwanamna gani ya sasa inasababisha gharama za maisha kama unaona swali lilipaswa kuulizwa hivyo kisha ueleze ni kwa namna gani mpya itatatua hizo changamoto. Inawezekana umesoma na unaakili ila umeendekeza ubishi. Kama unamajibu ya swali bro toa majibu, kama huna kaa tulia.
 
Kumekuwa na hoja kutoka siasa za upinzani, wakidai kwamba kuna uwezekano wa bei za vyakula kushuka iwapo tu tungekuwa na Katiba Mpya.

Hii ni hoja inayowavutia sana wananchi ila hakuna hata kiongozi mmoja wa upinzani aliewahi kueleza ni kwa jinsi gani jambo hili linawezekana.

Tafadhali kama una maoni yanayo weza kutusaidia kuthibitisha kuwa jambo hili ni kweli au lah, unakaribishwa kwa faida ya wengi.
Wewe unafaidika nini na kutokuwa na katiba mpya?

Sasa tukiwa na katiba mpya tutapata viongozi wanaotekeleza matakwa yao na siyo hawa wanaojaza matumbo yao na kusababisha mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali vikiwemo vyakula!
 
Kwa inavyo onekana umeelewa swali ila huna majibu ya kujitosheleza ndio maana unajitikita katika kutengeneza maswali unayotaka. Ulipaswa kueleza ni kwanamna gani ya sasa inasababisha gharama za maisha kama unaona swali lilipaswa kuulizwa hivyo kisha ueleze ni kwa namna gani mpya itatatua hizo changamoto. Inawezekana umesoma na unaakili ila umeendekeza ubishi. Kama unamajibu ya swali bro toa majibu, kama huna kaa tulia.
Nilichokieleza hapo % kubwa ndio kinachangia hali ya maisha ya mtz mfano mawaziri wote walioteuliwa hakuna anayekuja na suluhu ya gharama za maisha kupanda zaidi ya kusingizia covid na vita kitu kinachoonyesha uwezo mdogo wa mawazo kwa wateule mfumo unaotokana na katiba hii tuliyonayo
 
powercert_Tz Katiba mpya itatufanya tusipate tena viongozi walafi kama shetani Magufuli ambaye kwa kushirikiana na Biswalo wamehamisha mabilioni ya fedha kwenda China na kusikojulikana, tusipate mtu kama shetani Magufuli aliyehamisha hazina ya nchi kupeleka Chato na kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa usio na kazi, kujenga referral hospital bila utaratibu, kujenga benki kubwa bila kuzingatia uchumi wa wana Chato kutaka kuifanya Chato kuwa mkoa, kukopa katika mabenki ya biashara yenye riba kubwa na kununua ndege kwa cash na hivyo kuongeza deni la Taifa na kusababisha wananchi kubebeshwa mzigo mkubwa wa kodi na matozo lukuki.

Katiba mpya itawezesha wananchi kutopata viongozi kama Mpango aliyepora mabilioni ya fedha kutoka bureau de change za watu na kupeleka kusikojulikana, tusipate watu kama Makonda waliowabakikizia watu madawa ya kulevya na kuwapora fedha zao, kuua watu, tusipate watu kama Sabaya muuaji na aliyepora mali na fedha za watu.

Katiba mpya itawezesha wananchi kutopata viongozi watakao ingiza nchi katika mgogoro wa kiuchumi kiholela, kupanda kwa gharama za maisha kiholela, kuzuia wizi wa fedha za umma unaofanywa na viongozi walafi kama shetani Magufuli na kuzuia majanga mengi yanayosababishwa na viongozi wabovu!
 
Mimi nimeishia darasa la saba, na hili swala silielewi ndio maana nimeuliza. Mimi ni Mtanzania na naishi hapa hapa nchini. Bei za vyakula imepanda ila nashindwa kuelewa ni kwanamna gani katiba niliyo nayo sasa inaweza kusababisha mambo hayo, kiasi kwamba tukiwa na katiba mpya tutakua na unafuu kwenye mambo kama haya.
Lada wewe ni mkweli na sio mpiga "propaganda pumbazo" kama wale chawa wengine..

Kama ndiyo hivyo, basi pole sana na mimi nakuchukulia hivyo kuwa hujui na Kwa maana hiyo najitolea kukupa shule/ tuition isiyo na malipo kabisa hapa hapa..

Na nakuunganisha na ndugu huyu aitwaye Binadamu Mtakatifu Kwa sababu comment yake hapo juu kama si Kwa makusudi, basi inaonesha hata yeye haelewi chochote kiasi cha kulinganisha mambo ya U.S.A na Tanzania kwa kuwa tu anasikiaga watu wakisema au kuona kwenye TV au kusoma mahali..

SASA TUANZE TUISHENI YETU KWA NAMNA HII;

Kwamba, ili ujue uhusiano wa KATIBA YA NCHI na maisha ya kila siku ya wananchi hao, sharti kwanza uelewe "Nini maana ya Katiba"

KATIBA YA NCHI NI NINI?

JIBU
: Ni sheria mama ya nchi (makubaliano ya wananchi wenyewe) yanayoweka misingi mikuu ya kisiasa, madaraka, wajibu na majukumu ya serikali. Aidha, katiba huonesha na kuainisha bayana HAKI na WAJIBU wa raia wa nchi hiyo kwao wenyewe, kwa nchi yao na kwa serikali yao inayowaongoza ambao kimsingi wao wananchi ndiyo wameiweka kwa njia ya uchaguzi ulio HURU, wa WAZI na wa HAKI..

KATIBA YA NCHI HUPATIKANAJE?

Kama inavyoelezwa katika maana ya Katiba, Kwamba ni makubaliano ya watu wenyewe jinsi watakavyojiongoza na kusimamia mambo yao, basi jibu la swali hili moja kwa moja ni kuwa, KATIBA hupatikana Kwa makubaliano ya wananchi wenyewe kwa umoja wao Kwamba, hiki kiwe/kitakuwa hivi, na kile hivi nk nk..

KATIBA YETU YA TANZANIA (JMT) YA MWAKA 1977 ILIPATIKANAJE?

Haikupatikana Kwa njia kama inavyoelezwa hapo juu. Ni kikundi tu cha watu wachache tu chini ya Baba wa Taifa hili hayati Mwl. Julius K. Nyerere kilikaa na kuamua nchi hii iongozwe vipi. Na kimsingi hiki ndicho chanzo kikuu cha matatizo ya nchi hii mpaka leo na ukielewa hili, utakuwa mwanzo mzuri kwako kuanza kupata majibu ya maswali yako..

Ili uelewe zaidi, nikuulize swali moja rahisi sana.

Kwamba, assume kuwa wewe ni baba wa familia. Kisha ukawa unajifanyia tu mambo yako bila kuwashirikisha watoto wako na mke wako ndani ya nyumba. Unadhani nyumba hiyo itakuwa ya namna gani?

Bila shaka, watasema Duuh, Dingi huyu ni dikteta sana. Ndivyo ilivyo Tanzania ya leo..!

NINI UHUSIANO WA SI TU KUPANDA AU KUSHUKA KWA BEI VYAKULA NA VITU VINGINE, BALI UHUSIANO WAKE KATIKA MFUMO MZIMA WA MAISHA YA KILA SIKU YA WATU KATIKA NCHI?

Kwa ufupi sana;

✓ Katiba ndiyo imeweka utaratibu wa kuweka na kuwatoa (kuwawajibisha) viongozi wanaoongoza serikali kwa niaba ya wananchi..

✓ Katiba kupitia serikali yao waliyoiweka madarakani ndiyo inayotoa mwelekeo wa KISERA, KISHERIA, MIPANGO ya kiuchumi na kimaendeleo ya nchi..


KWANINI MAMBO YAKO HIVI? KWANINI MATATIZO HAYA YANAHUSIANISHWA NA KATIBA HII ILIYOPO? JE, KWELI KATIBA MPYA ITKUWA TIBA YA CHANGAMOTO HIZI?

1. Nimekupa historia ya katiba ya Tanzania ya 1977 Kwamba, si makubaliano ya wananchi wote. Utaratibu uliowekwa na watu wachache kwa ajili ya wengi siku zote hupingwa na huwa haukubaliki. Labda katiba hii ya 1977 ilifaa kwa wakati ule wakati nchi ikiwa chini ya mfumo wa chama kimoja na population isiofika hata 10M leo tuko zaidi ya 60M na nchi iko chini ya mfumo wa vyama vingi.

KWA HIYO JIBU LA SWALI #1 NI:

✓ Mambo yako hivi Kwa sababu walioitengeneza katiba hiyo ndiyo walio na serikali tangu wakati huo hadi sasa.

✓ Katiba hiyo kwa kifupi haiwapi wananchi mamlaka ya kuchagua na kuwajibisha viongozi wa serikali yao. Yaani viongozi wa serikali wana nguvu ya maamuzi kisiasa na kiuchumi kuliko wenye nchi yaani umma..

✓ Ushahidi ni uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 na ule wa Rais, wabunge na udiwani mwaka 2020. Na Ushahidi mwingine ni kauli za kubeza na kutweza wananchi zinazotolewa na viongozi dhidi ya wananchi.

Mfano, kauli waziri wa fedha Mwigulu Nchemba ya "asiyetaka kulipa tozo na KODI za serikali ahamie nchi ya Burundi".

Kwanini alitoa kauli hii?

Ni kwa sababu tu wananchi walilalamikia mzigo wa tozo na kodi mwaka jana 2022!!

Lakini mpaka leo hii mtu huyu yupo na anashikilia madaraka ya uwaziri wa fedha na wananchi hamna lolote la kufanya Kwa sababu hamkumpa ninyi cheo cha uwaziri wa fedha!!

JIBU LA SWALI #2 NI;

Kila kitu kinahusiana na katiba.

Ukiwa na kiongozi mwenye maamuzi na mamlaka na hatumii mamlaka yake kuja na maamuzi sahihi ya SERA ZA KIUCHUMI RAFIKI (bei za bidhaa na huduma), SERA za kijamii na SERA za maendeleo na huku akiwa anajua kabisa wananchi hawawezi kumwajibisha Kwa vyovyote, tegemeeni maumivu na kilio..!

Angalia serikali yote iliyopo sasa. Anzia Kwa wenyeviti wa serikali za vitongoji/vijiji/mitaa, madiwani, wabunge na Rais. Nani aliwachagua mwaka 2019 na 2020?

JIBU NI: Walijichagua wenyewe kwa msaada wa dola chini ya Rais Magufuli wakati huo. Hawapo Kwa ridhaa ya wananchi!!

Na kama ndiyo hivi, ni obviously, hawa hawawajibiki Kwa wananchi, wanawajibika kwa Rais aliyewaweka na serikali yake...

Na mtalia na kupiga kelele sana juu ya kupanda kwa gharama za maisha tokana na sera mbaya za kifedha na uchumi, lakini hakuna wa kuwasikiliza na hamuwezi kuwatoa kwenye nafasi zao Kwa njia za kikatiba Kwa sababu hazipo na kama zipo ni ngumu kwelikweli...!


JIBU SWALI #3 NI;

Yes, suluhuhisho ni katiba ya nchi iliyo bora inayowapa mamlaka kamili wananchi ya kuchagua viongozi na kuwatoa iwapo wanaboronga na wanaposhindwa ku - meet matarajio Yao bila sababu za msingi kama ilivyo leo..

Hebu angalia bunge hili la sasa. Lina tija yoyote kweli au wapo pale kwa maslahi yao tu? Lilifanya Nini kiasi cha Mafuta ya petrol kufikia karibu TZS 4,000 Kwa Lita Kwa interval ya mwaka mmoja tu toka March, 2021 ambalo bei ilikuwa TZS 1,800 Kwa Lita?

Unajua kisingizio kilikuwa Nini? Vita ya Ukraine na Urusi..!!

Haya, leo VYAKULA kama mahindi, Mchele, Maharage bei haishikiki, iko juu na maisha ya watu mijini na vijijini ni magumu. Je, kisingizio ni vita ya Ukraine na Urusi tena?

JIBU NI HAPANA...

Tatizo liko Kwa vyombo vya kuisimamami serikali kama Bunge nk kushindwa kufanya kazi na WAJIBU wake wa kikatiba kwa sababu hawawajibiki kwenu wananchi maana hamkuwachagua nyie...!!

TUFANYEJE SASA?

1. NDIYO. Kwa sbb ya kelele za kina Tundu Lissu na CHADEMA zinazoendelea kupigwa, serikali na CCM wameshahituka na kuona hatari iliyopo mbele yao iwapo hawatachukua hatua. Na ni kweli kwa sababu wananchi wengi wameshaanza kuamka na kuona tatizo lilipo..

Kwa hiyo, tayari tumeshaanza kudanganywa na kupumbazwa na "mikakati ya muda mfupi" tu ya kukabiliana na hali ngumu ya kiamisha.

Kuwa na mikakati ya muda mfupi (Short terms strategies/solutions) ni sawa na siyo mbaya kabisa. Lakini tunahitaji suluhisho la kudumu...

2. Suluhisho hili ni KATIBA MPYA YA WANANCHI inayorekebisha kasoro zote zilizo kwenye katiba tuliyonayo ya 1977. Katiba itakayowapa wananchi mamlaka kamili ya KUWAWEKA na KUWAWAJIBISHA viongozi wao. Na pia kuondoa kimrundikia mamlaka mtu mmoja tu aitwaye "RAIS" anayeweza kufanya lolote bila kuulizwa wala kuwajibishwa na sheria yoyote..

Natumai umeelewa sasa. Kama una swali, uliza tu
 
Umeongea sana na kunitag kwako inaonekana wewe ndio huelewi kitu
Thibitisha kuwa mimi sielewi kitu..

Wewe umelinganisha USA na Tanzania. Unaielewa katiba ya USA wewe?

Unaelewa mfumo wa utawala wa USA wewe?

Hebu tujadiliane hapa hapa ili tupeane UFAHAMU wa mambo haya ili tusaidiane kwenye harakati za mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ya nchi yetu..

Mimi sijui, hebu nijulishe uyajuayo ya USA vs Tanzania..

Karibu
 
Nacho kiona kwenye hizi harakati za katiba mpya, ni maswala ya madaraka tu. Kwamba wapinzani wameshagundua hawawezi kushika dola kama katiba itaendelea kua hii, hivyo wanajaribu kahakikisha tunaichukia hii katiba tuliyo nayo ili tupate hiyo nyingine itakayo wapa wao mwanya wa kupenya kwenye dola. Ila kiukweli harakati hizi sio kwa maslahi ya wananchi, hawa watu hua wanatanguliza maslahi yao mbele tu sikuzote. Hata ukichunguza kilicho sababisha mchakato wa kwanza kutofikia muafaka utakuta changamoto ilikua ni maslahi ya upinzani hayakutimizwa.
Wewe nae ni G.O.A.T! wa kikweli kweli.
 
Lada wewe ni mkweli na sio mpiga "propaganda pumbazo" kama wale chawa wengine..

Kama ndiyo hivyo, basi pole sana na mimi nakuchukulia hivyo kuwa hujui na Kwa maana hiyo najitolea kukupa shule/ tuition isiyo na malipo kabisa hapa hapa..

Na nakuunganisha na ndugu huyu aitwaye Binadamu Mtakatifu Kwa sababu comment yake hapo juu kama si Kwa makusudi, basi inaonesha hata yeye haelewi chochote kiasi cha kulinganisha mambo ya U.S.A na Tanzania kwa kuwa tu anasikiaga watu wakisema au kuona kwenye TV au kusoma mahali..

SASA TUANZE TUISHENI YETU KWA NAMNA HII;

Kwamba, ili ujue uhusiano wa KATIBA YA NCHI na maisha ya kila siku ya wananchi hao, sharti kwanza uelewe "Nini maana ya Katiba"

KATIBA YA NCHI NI NINI?

JIBU
: Ni sheria mama ya nchi (makubaliano ya wananchi wenyewe) yanayoweka misingi mikuu ya kisiasa, madaraka, wajibu na majukumu ya serikali. Aidha, katiba huonesha na kuainisha bayana HAKI na WAJIBU wa raia wa nchi hiyo kwao wenyewe, kwa nchi yao na kwa serikali yao inayowaongoza ambao kimsingi wao wananchi ndiyo wameiweka kwa njia ya uchaguzi ulio HURU, wa WAZI na wa HAKI..

KATIBA YA NCHI HUPATIKANAJE?

Kama inavyoelezwa katika maana ya Katiba, Kwamba ni makubaliano ya watu wenyewe jinsi watakavyojiongoza na kusimamia mambo yao, basi jibu la swali hili moja kwa moja ni kuwa, KATIBA hupatikana Kwa makubaliano ya wananchi wenyewe kwa umoja wao Kwamba, hiki kiwe/kitakuwa hivi, na kile hivi nk nk..

KATIBA YETU YA TANZANIA (JMT) YA MWAKA 1977 ILIPATIKANAJE?

Haikupatikana Kwa njia kama inavyoelezwa hapo juu. Ni kikundi tu cha watu wachache tu chini ya Baba wa Taifa hili hayati Mwl. Julius K. Nyerere kilikaa na kuamua nchi hii iongozwe vipi. Na kimsingi hiki ndicho chanzo kikuu cha matatizo ya nchi hii mpaka leo na ukielewa hili, utakuwa mwanzo mzuri kwako kuanza kupata majibu ya maswali yako..

Ili uelewe zaidi, nikuulize swali moja rahisi sana.

Kwamba, assume kuwa wewe ni baba wa familia. Kisha ukawa unajifanyia tu mambo yako bila kuwashirikisha watoto wako na mke wako ndani ya nyumba. Unadhani nyumba hiyo itakuwa ya namna gani?

Bila shaka, watasema Duuh, Dingi huyu ni dikteta sana. Ndivyo ilivyo Tanzania ya leo..!

NINI UHUSIANO WA SI TU KUPANDA AU KUSHUKA KWA BEI VYAKULA NA VITU VINGINE, BALI UHUSIANO WAKE KATIKA MFUMO MZIMA WA MAISHA YA KILA SIKU YA WATU KATIKA NCHI?

Kwa ufupi sana;

✓ Katiba ndiyo imeweka utaratibu wa kuweka na kuwatoa (kuwawajibisha) viongozi wanaoongoza serikali kwa niaba ya wananchi..

✓ Katiba kupitia serikali yao waliyoiweka madarakani ndiyo inayotoa mwelekeo wa KISERA, KISHERIA, MIPANGO ya kiuchumi na kimaendeleo ya nchi..


KWANINI MAMBO YAKO HIVI? KWANINI MATATIZO HAYA YANAHUSIANISHWA NA KATIBA HII ILIYOPO? JE, KWELI KATIBA MPYA ITKUWA TIBA YA CHANGAMOTO HIZI?

1. Nimekupa historia ya katiba ya Tanzania ya 1977 Kwamba, si makubaliano ya wananchi wote. Utaratibu uliowekwa na watu wachache kwa ajili ya wengi siku zote hupingwa na huwa haukubaliki. Labda katiba hii ya 1977 ilifaa kwa wakati ule wakati nchi ikiwa chini ya mfumo wa chama kimoja na population isiofika hata 10M leo tuko zaidi ya 60M na nchi iko chini ya mfumo wa vyama vingi.

KWA HIYO JIBU LA SWALI #1 NI:

✓ Mambo yako hivi Kwa sababu walioitengeneza katiba hiyo ndiyo walio na serikali tangu wakati huo hadi sasa.

✓ Katiba hiyo kwa kifupi haiwapi wananchi mamlaka ya kuchagua na kuwajibisha viongozi wa serikali yao. Yaani viongozi wa serikali wana nguvu ya maamuzi kisiasa na kiuchumi kuliko wenye nchi yaani umma..

✓ Ushahidi ni uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2019 na ule wa Rais, wabunge na udiwani mwaka 2020. Na Ushahidi mwingine ni kauli za kubeza na kutweza wananchi zinazotolewa na viongozi dhidi ya wananchi.

Mfano, kauli waziri wa fedha Mwigulu Nchemba ya "asiyetaka kulipa tozo na KODI za serikali ahamie nchi ya Burundi".

Kwanini alitoa kauli hii?

Ni kwa sababu tu wananchi walilalamikia mzigo wa tozo na kodi mwaka jana 2022!!

Lakini mpaka leo hii mtu huyu yupo na anashikilia madaraka ya uwaziri wa fedha na wananchi hamna lolote la kufanya Kwa sababu hamkumpa ninyi cheo cha uwaziri wa fedha!!

JIBU LA SWALI #2 NI;

Kila kitu kinahusiana na katiba.

Ukiwa na kiongozi mwenye maamuzi na mamlaka na hatumii mamlaka yake kuja na maamuzi sahihi ya SERA ZA KIUCHUMI RAFIKI (bei za bidhaa na huduma), SERA za kijamii na SERA za maendeleo na huku akiwa anajua kabisa wananchi hawawezi kumwajibisha Kwa vyovyote, tegemeeni maumivu na kilio..!

Angalia serikali yote iliyopo sasa. Anzia Kwa wenyeviti wa serikali za vitongoji/vijiji/mitaa, madiwani, wabunge na Rais. Nani aliwachagua mwaka 2019 na 2020?

JIBU NI: Walijichagua wenyewe kwa msaada wa dola chini ya Rais Magufuli wakati huo. Hawapo Kwa ridhaa ya wananchi!!

Na kama ndiyo hivi, ni obviously, hawa hawawajibiki Kwa wananchi, wanawajibika kwa Rais aliyewaweka na serikali yake...

Na mtalia na kupiga kelele sana juu ya kupanda kwa gharama za maisha tokana na sera mbaya za kifedha na uchumi, lakini hakuna wa kuwasikiliza na hamuwezi kuwatoa kwenye nafasi zao Kwa njia za kikatiba Kwa sababu hazipo na kama zipo ni ngumu kwelikweli...!


JIBU SWALI #3 NI;

Yes, suluhuhisho ni katiba ya nchi iliyo bora inayowapa mamlaka kamili wananchi ya kuchagua viongozi na kuwatoa iwapo wanaboronga na wanaposhindwa ku - meet matarajio Yao bila sababu za msingi kama ilivyo leo..

Hebu angalia bunge hili la sasa. Lina tija yoyote kweli au wapo pale kwa maslahi yao tu? Lilifanya Nini kiasi cha Mafuta ya petrol kufikia karibu TZS 4,000 Kwa Lita Kwa interval ya mwaka mmoja tu toka March, 2021 ambalo bei ilikuwa TZS 1,800 Kwa Lita?

Unajua kisingizio kilikuwa Nini? Vita ya Ukraine na Urusi..!!

Haya, leo VYAKULA kama mahindi, Mchele, Maharage bei haishikiki, iko juu na maisha ya watu mijini na vijijini ni magumu. Je, kisingizio ni vita ya Ukraine na Urusi tena?

JIBU NI HAPANA...

Tatizo liko Kwa vyombo vya kuisimamami serikali kama Bunge nk kushindwa kufanya kazi na WAJIBU wake wa kikatiba kwa sababu hawawajibiki kwenu wananchi maana hamkuwachagua nyie...!!

TUFANYEJE SASA?

1. NDIYO. Kwa sbb ya kelele za kina Tundu Lissu na CHADEMA zinazoendelea kupigwa, serikali na CCM wameshahituka na kuona hatari iliyopo mbele yao iwapo hawatachukua hatua. Na ni kweli kwa sababu wananchi wengi wameshaanza kuamka na kuona tatizo lilipo..

Kwa hiyo, tayari tumeshaanza kudanganywa na kupumbazwa na "mikakati ya muda mfupi" tu ya kukabiliana na hali ngumu ya kiamisha.

Kuwa na mikakati ya muda mfupi (Short terms strategies/solutions) ni sawa na siyo mbaya kabisa. Lakini tunahitaji suluhisho la kudumu...

2. Suluhisho hili ni KATIBA MPYA YA WANANCHI inayorekebisha kasoro zote zilizo kwenye katiba tuliyonayo ya 1977. Katiba itakayowapa wananchi mamlaka kamili ya KUWAWEKA na KUWAWAJIBISHA viongozi wao. Na pia kuondoa kimrundikia mamlaka mtu mmoja tu aitwaye "RAIS" anayeweza kufanya lolote bila kuulizwa wala kuwajibishwa na sheria yoyote..

Natumai umeelewa sasa. Kama una swali, uliza tu
mfano rahisi ni bunge wanaongeza tozo na Kodi kwenye bidhaa muhimu ie mafuta ili kuongeza mapato lakini hapo hapo hawafikirii kupunguza matumizi mfano kila mwaka bunge linapitisha bajeti ya kununua magari mapya lakini hawafikirii iyo gharama/fedha zingepelekwa kwenye luzuku ya mafuta ingesaidia sana kupunguza mfumuko wa bei na gharama za maisha kwa watu wote
20220610_094227.jpg
 
Katiba mpya itawasaidiaje wapinzani kupata madaraka au kushika dola?
Nacho kiona kwenye hizi harakati za katiba mpya, ni maswala ya madaraka tu. Kwamba wapinzani wameshagundua hawawezi kushika dola kama katiba itaendelea kua hii, hivyo wanajaribu kahakikisha tunaichukia hii katiba tuliyo nayo ili tupate hiyo nyingine itakayo wapa wao mwanya wa kupenya kwenye dola. Ila kiukweli harakati hizi sio kwa maslahi ya wananchi, hawa watu hua wanatanguliza maslahi yao mbele tu sikuzote. Hata ukichunguza kilicho sababisha mchakato wa kwanza kutofikia muafaka utakuta changamoto ilikua ni maslahi ya upinzani hayakutimizwa.
 
nilitegemea swali lako liwe, je hii katiba ya sasa inachangiaje kupandisha gharama za maisha au mfumuko wa bei? mfano kuna ulazima gani kila nafasi nyeti lazima ateuliwe badala ya kuomba na kuchaguliwa kwa mchakato huru kwa kuzingatia vigezo? ie sasa hivi watu wote wanaoteuliwa kigezo kikuu ni kuwa kada badala ya kuangalia uzoefu na utaalamu kwenye eneo husika hii ingeongeza weledi na ufanisi kwenye kujibu changamoto mbalimbali katika nchi yetu
Wakishaomba wakapata ndo bei ya chakula inashuka??
 
nilitegemea swali lako liwe, je hii katiba ya sasa inachangiaje kupandisha gharama za maisha au mfumuko wa bei? mfano kuna ulazima gani kila nafasi nyeti lazima ateuliwe badala ya kuomba na kuchaguliwa kwa mchakato huru kwa kuzingatia vigezo? ie sasa hivi watu wote wanaoteuliwa kigezo kikuu ni kuwa kada badala ya kuangalia uzoefu na utaalamu kwenye eneo husika hii ingeongeza weledi na ufanisi kwenye kujibu changamoto mbalimbali katika nchi yetu
H0: Katiba iliyopo haiathiri gharama za maisha.
H1: Katiba iliyopo inaathiri gharama za maisha.

Gharama za maisha ni zipi?
 
Wakishaomba wakapata ndo bei ya chakula inashuka??
maelezo yako wazi ila wewe umechagua kutumia kalio kufikiria na ndio shida yenu nyie watu maana apo mama yenu akikubali mchakato wa katiba uanze mtakuja hapa kushangilia😃😃
 
powercert_Tz Katiba mpya itatufanya tusipate tena viongozi walafi kama shetani Magufuli ambaye kwa kushirikiana na Biswalo wamehamisha mabilioni ya fedha kwenda China na kusikojulikana, tusipate mtu kama shetani Magufuli aliyehamisha hazina ya nchi kupeleka Chato na kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa usio na kazi, kujenga referral hospital bila utaratibu, kujenga benki kubwa bila kuzingatia uchumi wa wana Chato kutaka kuifanya Chato kuwa mkoa, kukopa katika mabenki ya biashara yenye riba kubwa na kununua ndege kwa cash na hivyo kuongeza deni la Taifa na kusababisha wananchi kubebeshwa mzigo mkubwa wa kodi na matozo lukuki.

Katiba mpya itawezesha wananchi kutopata viongozi kama Mpango aliyepora mabilioni ya fedha kutoka bureau de change za watu na kupeleka kusikojulikana, tusipate watu kama Makonda waliowabakikizia watu madawa ya kulevya na kuwapora fedha zao, kuua watu, tusipate watu kama Sabaya muuaji na aliyepora mali na fedha za watu.

Katiba mpya itawezesha wananchi kutopata viongozi watakao ingiza nchi katika mgogoro wa kiuchumi kiholela, kupanda kwa gharama za maisha kiholela, kuzuia wizi wa fedha za umma unaofanywa na viongozi walafi kama shetani Magufuli na kuzuia majanga mengi yanayosababishwa na viongozi wabovu!
hakuna katiba inapatikana jamii forum , whatapp na Facebook hata namba moja anajua akiigusa hii katiba atatupisha . Katiba mpya ni takwa la wanasiasa
 
Kumekuwa na hoja kutoka siasa za upinzani, wakidai kwamba kuna uwezekano wa bei za vyakula kushuka iwapo tu tungekuwa na Katiba Mpya.

Hii ni hoja inayowavutia sana wananchi ila hakuna hata kiongozi mmoja wa upinzani aliewahi kueleza ni kwa jinsi gani jambo hili linawezekana.

Tafadhali kama una maoni yanayo weza kutusaidia kuthibitisha kuwa jambo hili ni kweli au lah, unakaribishwa kwa faida ya wengi.
Una hakika halijatolewa ufafanuzi popote?
 
hakuna katiba inapatikana jamii forum , whatapp na Facebook hata namba moja anajua akiigusa hii katiba atatupisha . Katiba mpya ni takwa la wanasiasa
Wapumbavu kama wewe huwezi kuwakosa katika jamii kwa hiyo hushangazi!
 
Back
Top Bottom