Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,880
Ni wapi Julius Nyerere aliwazidi "ujanja" wazee wa mjini,born town na Watoto wa K'koo? Wazee wake na gwiji wetu wa historia Mohamed Said

Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja DSM tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.

Maelezo mengi ya Wazee yanaonyesha Julius aliaminiwa mapema sana na kupewa madaraka ndani ya chama na hatimaye baadae kuja kuwa Rais wa TAA/TANU na hatimaye nchi.Vijana wenzake waliompokea mjini wakebaki kuwa wao wao watoto wao na wajukuu wao kuwa Julius baada ya Uhuru "aliwasahu"

Wazee wengi wanahisi Julius aliwazidi ujanja na kuwaweka kando baada ya kuchukua nchi.Mitaa ya Kata ya Ng'ambo Tabora,miaka kumi iliyopita nilipata kuwaona wazee wawili,wajanja wa mjini waliompokea Nyerere ktk harakati zake mkoa wa Tabora.Mzee mmoja akiitwa Pacha,akiishi eneo la "filter" pembeni ya kilabu moja maarufu ya pombe mjini Tabora.Mzee mwingine akiitwa Rehani.Huyu kwa heshima kuna mtaa Tabora uliopewa jina lake.Unaitwa mtaa wa Rehani.Kuna Rehani A na Rehani B.

Hawa wote ukikaa nao watakuambia "Julius ni mjanja sana,alituzidi maarifa".Ukija K'koo kuna wazee wengi wapo na malalamiko na wengine wamekufa nayo.Sikumbuki ni Sykes yupi kati ya hao naowasikia.Lkn miaka miwili au mitatu iliyopita...Jijini Nairobi,kwenye Uwanja mdogo wa ndege wa maarufu kama "Wlison Airport" majira ya adhuhuri kuelekea alasiri.Nakutana na Wanawake wawili.Moja Mama wa makamo na mwingine mdada wa umri wa juu kidogo.Huyu Mama bila shaka ni mke wa marehemu na huyu wa pili bintiye.

Hawa wanajiandaa kupakia mwili wa ndugu yao,ni marehemu.Maafisa wa Uhamiaji wanatazama passport zao za kusafiria na kuona ni pass za kidiplomasia. Wanatakiwa kuusafirisha mwili wa ndugu yao kuja Dsm.Wamekodi ndege ndogo aina ya C208. Yenye uwezo wa kubeba watu wanne tu.Lakn wale wanawake wakiwa na ndugu wengine wanakubaliana kubeba maiti na wao kuja DSM.

Ndege ndogo,ktk ubanano na majonzi ya msiba wale wamama wanabanana na maiti ikiwa ndani ya mkeka kuileta Dsm.Ndege ya C206 ni ndogo sana kwa umbali wa Nairobi to Dsm, tena ukiwa na maiti,na hasa kwa wanawake.Kuuliza kwa ndugu waliobaki pale Uwanjani kufanya mpango wa kwenda Jomo Kenyatta ili waje Dsm,wanasema huyo alipata kuwa mpigania uhuru wa Tz,balozi mashuhuri na mwanadiplomasia mbobezi.

Pale pale wanaanza kung'aka kuwa hawa ni wapigania uhuru waliosahaulika na nchi,ndio maana wanabebwa na ndege ndogo aina ya C206 kurudi kwao.Ni malalamiko tu ya "kusahauliwa" muda wote wa maongezi yao.

Akija humu Mzee wangu Mohamed Said, atakutajia kina Mshume Kiyate(?), atataja kina Dosa, mara kina Tewa Said Tewa na wengine wengi kuwa hawa nao hawakufaidi matunda ya Uhuru. Hivi kwani huyu Julius alikuwa na ujanja kiasi gani hawa wote akawaingiza "mjini" wakati wao ndio waliompokea?

Nilitembelea Kilwa,kule kuna Kilwa ya Kivinje na Kilwa Kipatini. Huku Kilwa Kipatini ndio kwao na Kingunge.Huku kuna Kanisa kongwe sana la miaka mingi walijenga Wajerumani. Kanisa hili ndipo alibatizwa Kingunge N. Mwiru. Wengi hudhanj Kingunge hakuwahi kuwa na dini kabisaaa. Kumbe huyu ni mbatizwa ktk Kristo, kabla ya kwenda Usoviet na kuachana na dini.Lkn kwa kubatizwa huyu anaitwa "Ambrose Ngombare Mwiru".

Huku Kivinje kuna watu nao wanasema "Julius alituzidi ujanja". Hivi huu "ujanja" waliozidiwa hawa wote ni kwa sbb ya nini? Ni kwanini walimpokea na kumpa uongozi halafu baadae walalamike?Kwanini wasingemnyima?Je baada ya Uhuru hawa "walalamishi" wote walitaka Julius afanye nini ili walidhike?

Leo ninaomba majibu, nijue, ni wapi Julius, kijana wa Kizanaki aliwazidi "ujanja" hawa vijana wa mjini wa K'koo?
Cc Ngongo UncleBen Barbarosa Ritz
 
Julius alipewa uongozi wa TAA kwa sababu alikuwa msomi, na kwa asilia jamaa alikiwa ana ka nguvu ka ushawishi , pia aliwazidi ujanja ndio we mtu alikuwa ashenda uganda, ashenda ulaya hasa kwa nini asiwazidi.

Pia haiwezekani nchi ika mkumbuka kila mtu, wengine walifanya kwa uzalendo na utaifa wao si mpaka wajengewe nyumba

*Nyerere mwenyewe alikufa ni kama hana kitu, zaidi ya jina kubwa tuu, muacheni apumzike tu baba wa Taifa

*Ila wenye uwezo wa kiwakumbuka wengine nao waruhusiwe wafanye hivo.
 
Ni wapi Julius Nyerere aliwazidi "ujanja" wazee wa mjini,born town na Watoto wa K'koo? Wazee wake na gwiji wetu wa historia Mohamed Said

Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja Dsm tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.

Maelezo mengi ya Wazee yanaonyesha Julius aliaminiwa mapema sana na kupewa madaraka ndani ya chama na hatimaye baadae kuja kuwa Rais wa TAA/TANU na hatimaye nchi.Vijana wenzake waliompokea mjini wakebaki kuwa wao wao watoto wao na wajukuu wao kuwa Julius baada ya Uhuru "aliwasahu"

Wazee wengi wanahisi Julius aliwazidi ujanja na kuwaweka kando baada ya kuchukua nchi.Mitaa ya Kata ya Ng'ambo Tabora,miaka kumi iliyopita nilipata kuwaona wazee wawili,wajanja wa mjini waliompokea Nyerere ktk harakati zake mkoa wa Tabora.Mzee mmoja akiitwa Pacha,akiishi eneo la "filter" pembeni ya kilabu moja maarufu ya pombe mjini Tabora.Mzee mwingine akiitwa Rehani.Huyu kwa heshima kuna mtaa Tabora uliopewa jina lake.Unaitwa mtaa wa Rehani.Kuna Rehani A na Rehani B.

Hawa wote ukikaa nao watakuambia "Julius ni mjanja sana,alituzidi maarifa".Ukija K'koo kuna wazee wengi wapo na malalamiko na wengine wamekufa nayo.Sikumbuki ni Sykes yupi kati ya hao naowasikia.Lkn miaka miwili au mitatu iliyopita...Jijini Nairobi,kwenye Uwanja mdogo wa ndege wa maarufu kama "Wlison Airport" majira ya adhuhuri kuelekea alasiri.Nakutana na Wanawake wawili.Moja Mama wa makamo na mwingine mdada wa umri wa juu kidogo.Huyu Mama bila shaka ni mke wa marehemu na huyu wa pili bintiye.

Hawa wanajiandaa kupakia mwili wa ndugu yao,ni marehemu.Maafisa wa Uhamiaji wanatazama passport zao za kusafiria na kuona ni pass za kidiplomasia.Wanatakiwa kuusafirisha mwili wa ndugu yao kuja Dsm.Wamekodi ndege ndogo aina ya C208.Yenye uwezo wa kubeba watu wanne tu.Lakn wale wanawake wakiwa na ndugu wengine wanakubaliana kubeba maiti na wao kuja Dsm.

Ndege ndogo,ktk ubanano na majonzi ya msiba wale wamama wanabanana na maiti ikiwa ndani ya mkeka kuileta Dsm.Ndege ya C208 ni ndogo sana kwa umbali wa Nairobi to Dsm,tena ukiwa na maiti,na hasa kwa wanawake.Kuuliza kwa ndugu waliobaki pale Uwanjani kufanya mpango wa kwenda Jomo Kenyatta ili waje Dsm,wanasema huyo alipata kuwa mpigania uhuru wa Tz,balozi mashuhuri na mwanadiplomasia mbobezi.

Pale pale wanaanza kung'aka kuwa hawa ni wapigania uhuru waliosahaulika na nchi,ndio maana wanabebwa na ndege ndogo aina ya C208 kurudi kwao.Ni malalamiko tu ya "kusahauliwa" muda wote wa maongezi yao.

Akija humu Mzee wangu Mohamed Said,atakutajia kina Mshume Kiyate(?),atataja kina Dosa,mara kina Tewa Said Tewa na wengine wengi kuwa hawa nao hawakufaidi matunda ya Uhuru.Hivi kwani huyu Julius alikuwa na ujanja kiasi gani hawa wote akawaingiza "mjini" wakati wao ndio waliompokea?

Nilitembelea Kilwa,kule kuna Kilwa ya Kivinje na Kilwa Kipatini.Huku Kilwa Kipatini ndio kwao na Kingunge.Huku kuna Kanisa kongwe sana la miaka mingi walijenga Wajerumani.Kanisa hili ndipo alibatizwa Kingunge N. Mwiru.Wengi hudhanj Kingunge hakuwahi kuwa na dini kabisaaa...Kumbe huyu ni mbatizwa ktk Kristo,kabla ya kwenda Usoviet na kuachana na dini.Lkn kwa kubatizwa huyu anaitwa "Ambrose Ngombare Mwiru".

Huku Kivinje kuna watu nao wanasema "Julius alituzidi ujanja"...Hivi huu "ujanja" waliozidiwa hawa wote ni kwa sbb ya nini?Ni kwanini walimpokea na kumpa uongozi halafu baadae walalamike?Kwanini wasingemnyima?Je baada ya Uhuru hawa "walalamishi" wote walitaka Julius afanye nini ili walidhik mengionenam e?

Leo ninaomba majibu,nijue,ni wapi Julius,kijana wa Kizanaki aliwazidi "ujanja" hawa vijana wa mjini wa K'koo??
Cc Ngongo UncleBen Barbarosa Ritz
Barafu,
Umeandika maneno mengi na mengine umeyarejesha kwangu kama ndiyo
nimeyasema wakati sijapatapo kufanya hivyo.

In Shaallah nitajitahidi kukujibu kadri Allah atakavyoniwezesha.

Umeanza na swali la ''ujanja,'' kuwa Nyerere aliwazidi ujanja na umesherehesha
kwa maneno mengi ya ''gwiji,'' ''born town,'' ''mvaa kaptula,'' nk.

Kwa bahati hizo si lugha zangu mimi.

Si lugha zangu kwa kuwa ndani ya maneno hayo kuna kebehi na ukipenda matusi ya rejereja.

Kwa bahati hizi si lugha zangu. Labda nikufahamishe.

Itabidi endapo utapenda tufanye mjadala unieleze khasa umekusudia nini kwa neno, ''ujanja.''

Baba yangu katika miaka ya 1950/60 akivaa kaptula na stocking kazini.

Halikadhalika Abdul Sykes akivaa kaptula na shati jeupe pale ofisini kwake akiwa Market Master, Kariakoo Market.

Nimeandika kitabu cha Abdul Sykes na sasa ni kitabu maarufu.

Maneno yangu yote niliyotaka kusema kuhusu historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika nimeyasema mle.

Niliandika kwa Kiingereza na kikachapwa London mwaka wa 1998 na tafsiri yake ikachapwa Nairobi mwaka wa 2002.

Kitabu hiki kilifanyiwa, ''serialisation,'' tatu na The East African mwezi December, 1998 na ''review,'' na wanahistoria mashuhuri katika African History kama John Iliiffe, Jonathon Glassman na James Brenan na hizo ''review,'' kuchapwa katika ''journals,'' maarufu mojawapo ikiwa Cambridge Journal of Africa History.

Kitabu hiki kimepata heshima yake na hivyo mwandishi kapewa hadhi aliyostahili
kwa kitabu hicho.

Umetumia neno, ''kusahau,'' kuwa Nyerere amewasahau wazee waliopigania uhuru.
Sijui kwa nini umeamua kuwataja wazee peke yao katika hili.

Sijui kwa nini hukuwataja na vijana ila wawili Dossa na Tewa na kusema kuwa nimesema
''hawakufaidi matunda ya uhuru.''

Sijapatapo popote kuzungumza kuhusu Dossa au Tewa na matunda ya uhuru.
Labda utanijibu kuhusu haya.

Mimi nimetaja neno ''kusahau,'' katika kitabu cha Abdul Sykes na kwengineko katika
maandishi yangu mengi.

Lakini nimetaja ''kusahau,'' pale Nyerere katika kueleza historia yake alipofika Dar es
Salaam aliposahau Abdul alikuwa na cheo gani katika TAA yeye alipopokelewa ndani
ya TAA na Abdul Sykes mwaka wa 1952.

Haya yalitokea mwaka wa 1985 Ukumbi wa Diamond siku alipokuwa anaaga.

Ikiwa kuna wazee ambao wewe umezungumzanao na wakakuambia, ''wamesahauliwa,''
mimi siwezi kuwajibia.

Naomba nimalize kwa kukueleza wazee wangu mimi walimaliza vipi maisha yao ya siasa.

Wazee wangu baada ya Nyerere kuvunja Baraza la Wazee wa TANU mwaka wa 1963
wao hawakutia tena mguu pale Ofisi ya TANU wala hawakugombana na yeyote yule.

Wazee hawa walikufa majumbani mwao na heshima zao na kuzikwa kimya kimya na
ndugu zao.

Hapakuwa na mizinga, bendera kufunikwa majeneza yao na wala watoto
wao hawakusikitika kwa wazee wao kukosa hayo.

Hayo mengine siwezi kuyajibu kwa kuwa wenyewe wapo na ikiwa watakusikia na
watapenda kukujibu watakujibu.
 
Barafu,
Umeandika maneno mengi na mengine umeyarejesha kwangu kama ndiyo
nimeyasema wakati sijapatapo kufanya hivyo.

In Shaallah nitajitahidi kukujibu kadri Allah atakavyoniwezesha.

Umeanza na swali la ''ujanja,'' kuwa Nyerere aliwazidi ujanja na umesherehesha
kwa maneno mengi ya ''gwiji,'' ''born town,'' ''mvaa kaptula,'' nk.

Kwa bahati hizo si lugha zangu mimi.

Si lugha zangu kwa kuwa ndani ya maneno hayo kuna kebehi na ukipenda
matusi ya rejereja.

Kwa bahati hizi si lugha zangu.
Labda nikufahamishe.

Itabidi endapo utapenda tufanye mjadala unieleze khasa umekusudia nini
kwa neno, ''ujanja.''

Baba yangu katika miaka ya 1950/60 akivaa kaptula na stocking kazini.

Halikadhalika Abdul Sykes akivaa kaptula na shati jeupe pale ofisini kwake
akiwa Market Master, Kariakoo Market.

Nimeandika kitabu cha Abdul Sykes na sasa ni kitabu maarufu.

Maneno yangu yote niliyotaka kusema kuhusu historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika nimeyasema mle.

Niliandika kwa Kiingereza na kikachapwa London mwaka wa 1998 na tafsiri
yake ikachapwa Nairobi mwaka wa 2002.

Kitabu hiki kilifanyiwa, ''serialisation,'' tatu na The East African mwezi December,
1998 na ''review,'' na wanahistoria mashuhuri katika African History kama John
Iliiffe
, Jonathon Glassman na James Brenan na hizo ''review,'' kuchapwa
katika ''journals,'' maarufu mojawapo ikiwa Cambridge Journal of Africa History.

Kitabu hiki kimepata heshima yake na hivyo mwandishi kapewa hadhi aliyostahili
kwa kitabu hicho.

Umetumia neno, ''kusahau,'' kuwa Nyerere amewasahau wazee waliopigania uhuru.
Sijui kwa nini umeamua kuwataja wazee peke yao katika hili.

Sijui kwa nini hukuwataja na vijana ila wawili Dossa na Tewa na kusema kuwa nimesema
''hawakufaidi matunda ya uhuru.''

Sijapatapo popote kuzungumza kuhusu Dossa au Tewa na matunda ya uhuru.
Labda utanijibu kuhusu haya.

Mimi nimetaja neno ''kusahau,'' katika kitabu cha Abdul Sykes na kwengineko katika
maandishi yangu mengi.

Lakini nimetaja ''kusahau,'' pale Nyerere katika kueleza historia yake alipofika Dar es
Salaam aliposahau Abdul alikuwa na cheo gani katika TAA yeye alipopokelewa ndani
ya TAA na Abdul Sykes mwaka wa 1952.

Haya yalitokea mwaka wa 1985 Ukumbi wa Diamond siku alipokuwa anaaga.

Ikiwa kuna wazee ambao wewe umezungumzanao na wakakuambia, ''wamesahauliwa,''
mimi siwezi kuwajibia.

Naomba nimalize kwa kukueleza wazee wangu mimi walimaliza vipi maisha yao ya siasa.

Wazee wangu baada ya Nyerere kuvunja Baraza la Wazee wa TANU mwaka wa 1963
wao hawakutia tena mguu pale Ofisi ya TANU wala hawakugombana na yeyote yule.

Wazee hawa walikufa majumbani mwao na heshima zao na kuzikwa kimya kimya na
ndugu zao.

Hapakuwa na mizinga, bendera kufunikwa majeneza yao na wala watoto
wao hawakusikitika kwa wazee wao kukosa hayo.

Hayo mengine siwezi kuyajibu kwa kuwa wenyewe wapo na ikiwa watakusikia na
watapenda kukujibu watakujibu.
Mkuu Mzee Mohamed Said kwanza cha kwanza ujue ninakuheshimu sana,hata kama sikuwahi kukutana na wewe,lkn mimi nimekuwa mmoja wa wanafunzi wako wazuri tu wa maandishi yako ya historia JF na nje ya hapa.Hata kama kuna mahali huwa sikubaliani nawe,lkn unabaki kwangu kuwa mtu muhimu na chanzo kizuri cha historia ya Uhuru na mtiririko wake.

Nimetumia alama hizi " na " kwenye maneno "ujanja" ,"mvaa kaptula" na "gwiji" si kwa maana mbaya!Wala sijakusudia kudhihaki iwe wewe au JK.Ni mtindo tu.Ulipokwazika kwa maandishi hayo UNIWIE RADHI mzee.Haikuwa na dhamira mbaya.Nlipata kukutana na Wazee waliovaa kaptula na stockings,na wao walikuwa wakisema hiyo ndio ilikuwa "fashion" ya vijana wa enzi hizo walio wajanja.

Swali langu limetokana na maandishi yako mengi mzee.Ikiwa moja wapo la siku Nyerere aliposahau Cheo cha Sykes wakati wa TANU ili hali wao ndio waliompokea.Jingine ni bandiko lako liliolelezea Dosa(kama nakumbuka vizuri) alivyoenda kuishi Mlandizi na baadae kuaga dunia bila hali yoyote ya kutambuliwa na Julius wakati yeye ndio alikuwa akimuendesha Julius kila jioni ya weekend kupitia kilipo chuo kikuu Dsm kumpeleka Pugu Secondary.

Mzee Rehani niliwahi kusoma maandishi yako baada ya kumuona.Ukielezea jinsi alivyowekwa kizuizini na Julius,Rehani alivyotofautiana na Mwalimu juu ya uanzishwaji wa BAKWATA toka ule umoja wa East Africa wa Waislam.Namna alivyomkemea Nyerere ukumbi wa Agha Khan na kuzua ugomvi.Kiasi cha Rehani kumwambia Julius bila sisi utapata shida kuongoza.

Mjumuiko wa haya yote ndio msingi wa swali..Kwamba kwanini Mwalimu ni kama "aliwazidi wenzie waliomkaribisha?"Kwanini na wao wamekuwa wakisema kuwa kuna mambo hawaridhiki kwa kuenguliwa kwao baada ya Uhuru?Mpaka ikafikia kina Sykes kusema mmoja wao alitaka Cheif Makwaia ndio awe Rais wa TANU na si Mwalimu?

Samahani mzee..Neno "ujanja" halikudhamilia kuwadhalilisha watu au kukebehi..Kama uliza yangu imekukwaza niwe radhi.Naendelea kujifunza toka kwako.Karibu!
 
Mkuu Mzee Mohamed Said kwanza cha kwanza ujue ninakuheshimu sana,hata kama sikuwahi kukutana na wewe,lkn mimi nimekuwa mmoja wa wanafunzi wako wazuri tu wa maandishi yako ya historia JF na nje ya hapa.Hata kama kuna mahali huwa sikubaliani nawe,lkn unabaki kwangu kuwa mtu muhimu na chanzo kizuri cha historia ya Uhuru na mtiririko wake.

Nimetumia alama hizi " na " kwenye maneno "ujanja" ,"mvaa kaptula" na "gwiji" si kwa maana mbaya!Wala sijakusudia kudhihaki iwe wewe au JK.Ni mtindo tu.Ulipokwazika kwa maandishi hayo UNIWIE RADHI mzee.Haikuwa na dhamira mbaya.Nlipata kukutana na Wazee waliovaa kaptula na stockings,na wao walikuwa wakisema hiyo ndio ilikuwa "fashion" ya vijana wa enzi hizo walio wajanja.

Swali langu limetokana na maandishi yako mengi mzee.Ikiwa moja wapo la siku Nyerere aliposahau Cheo cha Sykes wakati wa TANU ili hali wao ndio waliompokea.Jingine ni bandiko lako liliolelezea Dosa(kama nakumbuka vizuri) alivyoenda kuishi Mlandizi na baadae kuaga dunia bila hali yoyote ya kutambuliwa na Julius wakati yeye ndio alikuwa akimuendesha Julius kila jioni ya weekend kupitia kilipo chuo kikuu Dsm kumpeleka Pugu Secondary.

Mzee Rehani niliwahi kusoma maandishi yako baada ya kumuona.Ukielezea jinsi alivyowekwa kizuizini na Julius,Rehani alivyotofautiana na Mwalimu juu ya uanzishwaji wa BAKWATA toka ule umoja wa East Africa wa Waislam.Namna alivyomkemea Nyerere ukumbi wa Agha Khan na kuzua ugomvi.Kiasi cha Rehani kumwambia Julius bila sisi utapata shida kuongoza.

Mjumuiko wa haya yote ndio msingi wa swali..Kwamba kwanini Mwalimu ni kama "aliwazidi wenzie waliomkaribisha?"Kwanini na wao wamekuwa wakisema kuwa kuna mambo hawaridhiki kwa kuenguliwa kwao baada ya Uhuru?Mpaka ikafikia kina Sykes kusema mmoja wao alitaka Cheif Makwaia ndio awe Rais wa TANU na si Mwalimu?ya
Samahani mzee..Neno "ujanja" halikudhamilia kuwadhalilisha watu au kukebehi..Kama uliza yangu imekukwaza niwe radhi.Naendelea kujifunza toka kwako.Karibu!
Barafu,
Kwanza ningependa kukufahamisha kuwa Dossa hakuwa anamuendesha
Nyerere.

Kumwendesha mtu ni kuwa dereva kaajiriwa.

Dossa hakuwa dereva wa Nyerere bali Dossa alikuwa na gari ya kutembelea
na gari hiyo ndiyo aliyokuwa akipanda Nyerere.

Kuhusu uhusiano wa Chief Kidaha Makwaia na Abdul Sykes huu uhusiano
ulikuwapo hata Abdul hajamjua Nyerere.

Uhusiano huu ulikuwa wakati Chief Kidaha ni mjumbe wa Legico na Abdul ni
Rais wa TAA.

Hiki ndicho kipindi alichomtaka Chief Kidaha ajiunge na harakati za kuunda TANU.
Si kama habari hizi zilikuja kusemwa baadae na watu kuelezwa baada ya ''ujanja,''
wa Nyerere.

Historia hii haikupatapo kujulikana hadi mimi nilipoiandika baada ya kuelezwa na mke
wa Abdul Sykes, Mama Daisy.

Kuhusu ''ujanja,'' msome Abdul Sykes utafahamu uwezo wake si wa kufadhili chama
tu bali hata ''intellect,'' yake.

Angalia ni watu gani Abdul alikuwa anasubihiananao wakati ule kuanzia akina Chief
Kidaha, Chief Marealle, Chief Fundikira, Earle Seaton
nk.

Huyu ni kijana aliyepata ''admission,'' ya Makerere 1942 na Princeton University 1953.

Huyu ni kijana ambae aliweza kuunda TANU ndani ya ubongo wake kuanzia 1945 akiwa
vitani Burma na kukamilisha ndoto yake 1954.

Huyu ni kijana aliyekuwa ana uwezo wa kuandika shajara (diary) zake aidha kwa ''long
hand,'' au kwa ''hati mkato,'' (short hand).

Huyu ni kijana aliyeweza kuwaunganisha vijana wenzake dhidi ya ukoloni katika chama
alichoasisi baba yake 1929.

Abdul ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kumtia katika, ''circle.''

Kuhusu hayo unayosema katenda Nyerere ''ujanja,'' dhidi ya historia hii mimi sina haja
ya kuyarejea hapa.

Kuna wakati Abdul Sykes hakuwa ananasibishwa na TANU wala na historia ya
uhuru wa Tanganyika wala na Nyerere.

Hili jambo sasa haliwezekani tena.
Kwangu mimi kazi ya kuandika historia ya wazee wangu imekamilika.

Mwaka wa 2011 Abdul na Ally Sykes katika kuadhimisha miaka 50 ya uhuru
wa Tanganyika, ndugu hawa wawili walitunukiwa medali kutambua mchango
wao katika uhuru wa Tanganyika.

Kama yupo mtafiti anataka kuandika, ''ujanja,'' wa Nyerere na afanye hivyo na hakika
atakuwa kaongeza elimu katika kuijua historia ya Tanganyika.

Ingia hapo chini kuangalia picha:
Mohamed Said: KUTOKA JF: ''UJANJA,'' WA NYERERE
 
Hahahaha aiseee mkuu barafu hapa ni maji marefu kwangu ,nimekaa pembeni nafuatilia kwa makini

Ila shida ya fasihi simulizi inapoteza uhalisia wake ,

Hivyo wacha nifuatilie mjadala halafu mwisho na mimi nitajiongeza maana kunakuwa na uongo mwingi na ukweli
 
Hahahaha aiseee mkuu barafu hapa ni maji marefu kwangu ,nimekaa pembeni nafuatilia kwa makini

Ila shida ya fasihi simulizi inapoteza uhalisia wake ,

Hivyo wacha nifuatilie mjadala halafu mwisho na mimi nitajiongeza maana kunakuwa na uongo mwingi na ukweli
Ha ha ha ha Mkuu UncleBen karibu sana jukwaani.Nilikuwa nataka kupata majibu ya moja kwa moja toka kwa Mzee wetu,maana ni kama kumekuwa na hali ya "sintofahamu" kwa muda mrefu sana juu ya Mwalimu Nyerere na makomrade wenzake wapigania Uhuru.

Sasa unapopate jukwaa kama hili,ambapo watu huongea kwa Uhuru,basi unakuwa ni wakati muafaka wa kupata nini hasa huyu kijana wa Butiama aliwazidi wale waliomkaribisha mjini.Sehemu kadhaa ukipita,hasa mikoa ya Tabora,Kigoma,Tanga,Lindi,Mtwara na Dsm unakutana na aina hiyo ya maneno.Nimeona majibu ya Mzee Mohamed Said
 
Ha ha ha ha Mkuu UncleBen karibu sana jukwaani.Nilikuwa nataka kupata majibu ya moja kwa moja toka kwa Mzee wetu,maana ni kama kumekuwa na hali ya "sintofahamu" kwa muda mrefu sana juu ya Mwalimu Nyerere na makomrade wenzake wapigania Uhuru.

Sasa unapopate jukwaa kama hili,ambapo watu huongea kwa Uhuru,basi unakuwa ni wakati muafaka wa kupata nini hasa huyu kijana wa Butiama aliwazidi wale waliomkaribisha mjini.Sehemu kadhaa ukipita,hasa mikoa ya Tabora,Kigoma,Tanga,Lindi,Mtwara na Dsm unakutana na aina hiyo ya maneno.Nimeona majibu ya Mzee Mohamed Said
Barafu,
Kuna vitabu ni muhimu sana mwanafunzi wa historia ya Tanganyika kuvisoma.
Kitabu cha kwanza ni cha Bergen (1981).

Kitabu cha pili ni cha Sivalon (1992)
Kitabu cha tatu cha Njozi (2002) lakini hiki kilipigwa marufuku na serikali.

Pia kuna tasnifu ya Kiwanuka (1973)
Mswada wa kitabu cha Tewa (unadated)

Hapa unazungumzia kusoma takriban kurasa 500 za kazi ya kitafiti.

Nimeepuka kwa sababu za wazi kabisa na kwa makusudi kabisa kuweka rejea
ambazo mimi ndiye mwandishi.

Katika rejea hizi utajifunza mengi.

Kitabu cha Bergen kilikuwa kikiiuzwa Cathedral Bookshop lakini baada ya
kugundua yale yaliyoandikwa kimya kimya kimeondolewa hali kadhalika na
kitabu cha Sivalon.

Kuna jopo la wasomi wa Kitanzani likiongozwa na Prof. Shivji hivi sasa wako
katika kutafiti na kuandika kitabu cha maisha ya Nyerere.

Nimefanyanao mahojiano mara tatu nyumbani kwangu.

Katika nyaraka walizoniomba niwapatie ni mswada wa Tewa na kitabu cha
Bergen.

Ingia hapa kuona picha:
Mohamed Said: KUTOKA JF: VITABU MUHIMU KUMUELEWA NYERERE NA HISTORIA YA TANGANYIKA
 
Barafu,
Kuna vitabu ni muhimu sana mwanafunzi wa historia ya Tanganyika kuvisoma.
Kitabu cha kwanza ni cha Bergen (1981).

Kitabu cha pili ni cha Sivalon (1992)
Kitabu cha tatu cha Njozi (2002) lakini hiki kilipigwa marufuku na serikali.

Pia kuna tasnifu ya Kiwanuka (1973)
Mswada wa kitabu cha Tewa (unadated)

Hapa unazungumzia kusoma takriban kurasa 500 za kazi ya kitafiti.

Nimeepuka kwa sababu za wazi kabisa na kwa makusudi kabisa kuweka reja
ambazo mimi ndiye mwandishi.

Katika rejea hizi utajifunza mengi.

Kitabu cha Bergen kilikuwa kikiiuzwa Cathedral Bookshop lakini baada ya
kugundua yale yaliyoandikwa kimya kimya kimeondolewa hali kadhalika na
kitabu cha Sivalon.

Kuna jopo la wasomi wa Kitanzani likiongozwa na Prof. Shivji hivi sasa wako
katika kutafiti na kuandika kitabu cha maisha ya Nyerere.

Nimefanyanao mahojiano mara tatu nyumbani kwangu.

Katika nyaraka walizoniomba niwapatie ni mswada wa Tewa na kitabu cha
Bergen.
Ninashukuru sana Mzee Mohamed Said na Mungu akupe maisha marefu ili maarifa yako ya kihistoria yawafae watu wengine.Unafikiri ni kwanini St.Joseph walivitoa hivyo vitabu ktk shelves za Bookshop yao?
 
Ni wapi Julius Nyerere aliwazidi "ujanja" wazee wa mjini,born town na Watoto wa K'koo? Wazee wake na gwiji wetu wa historia Mohamed Said

Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja Dsm tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.

Maelezo mengi ya Wazee yanaonyesha Julius aliaminiwa mapema sana na kupewa madaraka ndani ya chama na hatimaye baadae kuja kuwa Rais wa TAA/TANU na hatimaye nchi.Vijana wenzake waliompokea mjini wakebaki kuwa wao wao watoto wao na wajukuu wao kuwa Julius baada ya Uhuru "aliwasahu"

Wazee wengi wanahisi Julius aliwazidi ujanja na kuwaweka kando baada ya kuchukua nchi.Mitaa ya Kata ya Ng'ambo Tabora,miaka kumi iliyopita nilipata kuwaona wazee wawili,wajanja wa mjini waliompokea Nyerere ktk harakati zake mkoa wa Tabora.Mzee mmoja akiitwa Pacha,akiishi eneo la "filter" pembeni ya kilabu moja maarufu ya pombe mjini Tabora.Mzee mwingine akiitwa Rehani.Huyu kwa heshima kuna mtaa Tabora uliopewa jina lake.Unaitwa mtaa wa Rehani.Kuna Rehani A na Rehani B.

Hawa wote ukikaa nao watakuambia "Julius ni mjanja sana,alituzidi maarifa".Ukija K'koo kuna wazee wengi wapo na malalamiko na wengine wamekufa nayo.Sikumbuki ni Sykes yupi kati ya hao naowasikia.Lkn miaka miwili au mitatu iliyopita...Jijini Nairobi,kwenye Uwanja mdogo wa ndege wa maarufu kama "Wlison Airport" majira ya adhuhuri kuelekea alasiri.Nakutana na Wanawake wawili.Moja Mama wa makamo na mwingine mdada wa umri wa juu kidogo.Huyu Mama bila shaka ni mke wa marehemu na huyu wa pili bintiye.

Hawa wanajiandaa kupakia mwili wa ndugu yao,ni marehemu.Maafisa wa Uhamiaji wanatazama passport zao za kusafiria na kuona ni pass za kidiplomasia.Wanatakiwa kuusafirisha mwili wa ndugu yao kuja Dsm.Wamekodi ndege ndogo aina ya C208.Yenye uwezo wa kubeba watu wanne tu.Lakn wale wanawake wakiwa na ndugu wengine wanakubaliana kubeba maiti na wao kuja Dsm.

Ndege ndogo,ktk ubanano na majonzi ya msiba wale wamama wanabanana na maiti ikiwa ndani ya mkeka kuileta Dsm.Ndege ya C206 ni ndogo sana kwa umbali wa Nairobi to Dsm,tena ukiwa na maiti,na hasa kwa wanawake.Kuuliza kwa ndugu waliobaki pale Uwanjani kufanya mpango wa kwenda Jomo Kenyatta ili waje Dsm,wanasema huyo alipata kuwa mpigania uhuru wa Tz,balozi mashuhuri na mwanadiplomasia mbobezi.

Pale pale wanaanza kung'aka kuwa hawa ni wapigania uhuru waliosahaulika na nchi,ndio maana wanabebwa na ndege ndogo aina ya C206 kurudi kwao.Ni malalamiko tu ya "kusahauliwa" muda wote wa maongezi yao.

Akija humu Mzee wangu Mohamed Said,atakutajia kina Mshume Kiyate(?),atataja kina Dosa,mara kina Tewa Said Tewa na wengine wengi kuwa hawa nao hawakufaidi matunda ya Uhuru.Hivi kwani huyu Julius alikuwa na ujanja kiasi gani hawa wote akawaingiza "mjini" wakati wao ndio waliompokea?

Nilitembelea Kilwa,kule kuna Kilwa ya Kivinje na Kilwa Kipatini.Huku Kilwa Kipatini ndio kwao na Kingunge.Huku kuna Kanisa kongwe sana la miaka mingi walijenga Wajerumani.Kanisa hili ndipo alibatizwa Kingunge N. Mwiru.Wengi hudhanj Kingunge hakuwahi kuwa na dini kabisaaa...Kumbe huyu ni mbatizwa ktk Kristo,kabla ya kwenda Usoviet na kuachana na dini.Lkn kwa kubatizwa huyu anaitwa "Ambrose Ngombare Mwiru".

Huku Kivinje kuna watu nao wanasema "Julius alituzidi ujanja"...Hivi huu "ujanja" waliozidiwa hawa wote ni kwa sbb ya nini?Ni kwanini walimpokea na kumpa uongozi halafu baadae walalamike?Kwanini wasingemnyima?Je baada ya Uhuru hawa "walalamishi" wote walitaka Julius afanye nini ili walidhike?

Leo ninaomba majibu,nijue,ni wapi Julius,kijana wa Kizanaki aliwazidi "ujanja" hawa vijana wa mjini wa K'koo??
Cc Ngongo UncleBen Barbarosa Ritz
Hiki Kiswahili anachoongea Mohamed Said,inaonekana hata wazee waliomsaidia Nyerere ndio walichoongea-kimejaa ujanja ujanja mwingi-endapo Nyerere angekaa nao bega kwa bega,hii nchi ingemshinda mapema-ilibidi kwa manufaa ya nchi apige upanga mapema
 
Na alikuwa na bahati ya kuaminiwa na wenzake sasa kama kuna ubaya aliukusudia kwenye nafsi yake labda leo ndio unaitwa "Ujanja" atajuana na mungu wake.

Ki uhalisia kabisa Watu wengi wa pwani au waislamu hawana ningwa katika kuwaamini watu wawe wa imani tofauti au wawe wa makabila tofauti, wao wanawaamini sana na hupata hasara sana kwani wengi wao sio waaminifu. hata kwenye biashara watu wa bara ni mara chahche sana kuwa waaminifu. Hii ni hulka yao, hawakuanza leo.
 
Back
Top Bottom