Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Ujamaa...
Salum Abdallah babu yangu hakuwa manamba.
Sisemi kuwa manamba ni watu duni la hasha ili hakuwa manamba.

Kazi yake ilikuwa mfua chuma.
Aliajiriwa kwa kazi hiyo na Tanganyika Railways katika miaka ya 1920.

Hamza Mwapachu na Julius Nyerere walijuana Makerere.

(Ukiandika uhuni ''babu yake Dully Sykes'' kadha wa kadha unanipa shida kwani huu kwangu ni mjadala wa kistaarabu si mjadala wa kejeli).

Angalia post yangu ya mwisho vipi ninavyoandika na kueleza historia ambayo haikuwa inafahamika kabla.

Kwa nini Hamza Mwapachu hakutakiwa kuchukua uongozi wa TAA na kuunda TANU au kwa nini Abdul Sykes hakuchukua au kwa nini Chief Kidaha Makwaia hakuchukua hizi zote ni historia za kusisimua.

Historia hii hakuna aliyepata kuandika ila mimi baada ya kusoma Nyaraka za Sykes na kuandika kitabu.

Kuhusu NECTA nina mengi ambayo naweza nikayaweka hapa kwa ushahidi na sote tukanufaika kwa taarifa hizo hata kama wewe hutoamini.

Lakini ili tufanye mjadala wenye tija muhimu kwanza tukaheshimiana.

Swali langu lilikua ni Kwanini viongozi wasiwe babu zako maana unasema walikua wengi je ni nini kiliwafanya wampe mwalimu uongozi. Inamaana kwa kipindi hicho hawakua na uwezo. Unasema Nacte ilikuwa inahujumu shule zenu na ushahidi unao, sasa unasita nini kuuweka hapa ili watu waone, umesema kulikua na hujuma basi unalojukumu la kudhibitisha hizo hujuma hapa. Leo ni 2023 bado mnahujumiwa kama mnavyo dai ni juzi tu matokeo yametoka bado mnashika mikia mixa mizero kibao kwene shule zenu na majina yenu.
 
Swali langu lilikua ni Kwanini viongozi wasiwe babu zako maana unasema walikua wengi je ni nini kiliwafanya wampe mwalimu uongozi. Inamaana kwa kipindi hicho hawakua na uwezo. Sikosoi wala kupuuza mchango wa wazee hao na wengine wengi. Salum abdallah kwa kazi yake itoshe tu kusema alikua ni manamba maana kazi hizo zilifanywa na watu wa chini sana kwa ugumu wa kazi hizo. Unasema NECTA ilikuwa inahujumu shule zenu na ushahidi unao, sasa unasita nini kuuweka hapa ili watu waone, umesema kulikua na hujuma basi unalojukumu la kudhibitisha hizo hujuma hapa. Leo ni 2023 bado mnahujumiwa kama mnavyo dai ni juzi tu matokeo yametoka bado mnashika mikia mixa mizero kibao kwene shule zenu na majina yenu.
 
KIKAO CHA KUUNDA TANU NYUMBANI KWA HAMZA KIBWANA MWAPACHU NANSIO, UKEREWE 1953

Ilikuwa miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953 kabla ya kufika April, 1953.

Abdul Sykes Act. President na Secretary wa TAA akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) walikwenda Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu.

Abdul Sykes alikuwa anataka kupata kauli ya mwisho ya Hamza Mwapachu kuhusu Julius Nyerere kuingizwa katika uongozi wa juu wa TAA kwenye uchaguzi wa viongozi wa TAA uliokuwa ufanyike mwezi April.

Uchaguzi ulifanyika kama walivyokubaliana watu hawa watatu na TAA ikawa chini ya uongozi wa Julius Kambarage Nyerere kama ilivyo hapo chini:

J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias, Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer, Ally K. Sykes Assistant Treasurer.

Committee members: Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo, Patrick Aoko.

(Tanganyika Standard 19 June 1953)
 
Unaweza ukasema maneno meng sana na unaweza ukaja na theory nying sana ila kuna kitu kimoja kinaitwa(lucky) bahati

Leo messi na C7 sio kwamba ndio wachezaji bora dunia nzima kwa miaka10 ila ni bahati

Unaweza ukawa bora sana au unaweza ukawa mzr sana ila km huna bahati ni kaz sana kufika mbali na watu weng wamefanikiwa sio kwa juhudi zao ila ni lucky bahati
 
Hiki Kiswahili anachoongea Mohamed Said,inaonekana hata wazee waliomsaidia Nyerere ndio walichoongea-kimejaa ujanja ujanja mwingi-endapo Nyerere angekaa nao bega kwa bega,hii nchi ingemshinda mapema-ilibidi kwa manufaa ya nchi apige upanga mapema
Kwani Nyerere hii nchi aliiweza? Siyo yeye aliyetuingiza kwenye umasikini mkubwa na yeye ndiyo chanzo cha ufisadi nchi hii.
 
Unaweza ukasema maneno meng sana na unaweza ukaja na theory nying sana ila kuna kitu kimoja kinaitwa(lucky) bahati

Leo messi na C7 sio kwamba ndio wachezaji bora dunia nzima kwa miaka10 ila ni bahati

Unaweza ukawa bora sana au unaweza ukawa mzr sana ila km huna bahati ni kaz sana kufika mbali na watu weng wamefanikiwa sio kwa juhudi zao ila ni lucky bahati
Mkoko...
Ilikuwa unayajua haya?
 
Let..
Hapana sithubutu kuandika uongo katika historia ya uhuru wa Tanganyuika kwa sababu wenyewe waliopigania uhuru huo walikuwa hai.

Ngombale Mwiru alikuwa yu hai yeye aliingizwa TANU na Ally Sykes haya kaeleza mwenyewe.

Prof. Haroub hakuwa anajua ule udugu uliokuwapo kati ya Mwalimu na Abdul.

Prof. Haroub hakuamini hadi alipokwenda kumuuliza Ahmed Rashad yale ambayo yeye hakuyaamini.

Ahmed Rashad na Abdul Sykes walijuana 1936 wakiwa watoto wadogo na wakawa marafiki ndugu hadi Abdul alipofariki 1968.

Ahmed Rashaad alimweleza kila kitu Prof. Haroub kiasi akamwambia ikiwa wewe unashangaa kuambiwa kuwa Abdul Sykes ndiye aliyekuwa nguvu katika kuasisi TANU utashangaa pia nikikuambia kuwa African Association iliasisiwa na baba yake Abdul, Mzee Kleist Sykes mwaka wa 1929?

Mimi ndiye niliyepata mshangao mkubwa zaidi kuwa Prof. Haroub hakuwa anaijua historia ya TANU.

Nitakueleza kitu ujue kuwa Prof. Haroub hakuwa anazijua siasa na historia za watu wa Dar es Salaam.

Prof. Haroub alikuwa mshenga wa kutaka kuposwa bint ya Ahmed Rashaad.

Walipofika nyumbani kwa Ahmed Rashaad na shughuli imeanza Prof. akatoka barua kumpa Ahmed Rashaad na walikuwa wamekaa pamoja bega kwa bega na Abbas Sykes.

Ahmed Rashaad hakupkea barua hiyo akamwambia amkabidhi Abbas Sykes.
Prof. akaja kunieleza kisa hiki na kuniuliza kwa nini aliambiwa posa ile ipokelewe na Abbas Sykes?

Nikampa historia nzima ya Mzee Rashaad na Abdul Sykes na kuwa ule urafiki baada ya kifo cha Abdul ulihamia kwa Abbas.

Ndipo nikajua kuwa Prof. Haroub si mjuzi wa historia yetu.
Ningeandika uongo sasa hivi nishafedheheka.

View attachment 2559355
Kulia Sheikh Ahmed Islam, Ahmed Rashad Ali na Prof. Haroub Othman 1997​
kwahiyo Tanzania nzima mjuvi wa historia ya TANU ni wewe tu na ukoo wako? Mudi wacha urongo!

Prof.Haroub ni gwiji wa tafiti kuliko hivyo vipeperushi vyako.
 
kwahiyo Tanzania nzima mjuvi wa historia ya TANU ni wewe tu na ukoo wako? Mudi wacha urongo!

Prof.Haroub ni gwiji wa tafiti kuliko hivyo vipeperushi vyako.
Prof. Haroub ni mwalimu wangu.

Mimi kuijua historia ya TANU wala si jambo la kukuzwa.

Yeyote yule angezaliwa na watu hawa na katika kipindi kile angeijua historia ya TANU.
 
Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja DSM tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.


Pengine walikuwa waoga wa kutema madini...walikuwa wanaongelea vyumbani...alivyokuja Nyerere akaongea na kueleweka...kwani kule Zanzibar MAKOBAZI SI YALIJIFICHA mapaka JONI akafanya yake!!
 
Ukifuatilia historia na harakati za Uhuru,unaona kuwa huyu kijana wa Kizanaki,mtoto wa Chief na "mvaa kaptula" alikuja baadae sana Dsm wakati wenzake wakiwa mjini kitambo na harakati za kumuondoa Mkoloni.Wakati Julius anakuja DSM tayari harakati za Uhuru zilikuwa zimepamba moto.


Pengine walikuwa waoga wa kutema madini...walikuwa wanaongelea vyumbani...alivyokuja Nyerere akaongea na kueleweka...kwani kule Zanzibar MAKOBAZI SI YALIJIFICHA mapaka JONI akafanya yake!!
Make...
Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza Government Circular zilizokuwa zinatolewa na serikali kuhusu wafanyakazi wa serikali kujihusisha na siasa.

Inelekea huijui historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mambo makubwa yalifanyika kuanzia mwaka wa 1950 hadi kuundwa kwa TANU mwaka wa 1954.

Yote yalikuwa wazi na wananchi wakishiriki.

Kuhusu Okello soma kitabu cha Dr. Harith Ghassany, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," utaijua historia ya mapinduzi.

Halikadhalika utamjua John Okello.

Ama hili la "makobazi," hii ni kejeli na kejeli haraka mjadala utaharibika kwani tutawakaribisha watu hodari kutukana kukushinda.
 
Sahihi kabisa
Unaweza ukasema maneno meng sana na unaweza ukaja na theory nying sana ila kuna kitu kimoja kinaitwa(lucky) bahati

Leo messi na C7 sio kwamba ndio wachezaji bora dunia nzima kwa miaka10 ila ni bahati

Unaweza ukawa bora sana au unaweza ukawa mzr sana ila km huna bahati ni kaz sana kufika mbali na watu weng wamefanikiwa sio kwa juhudi zao ila ni lucky bahati
 
Back
Top Bottom