Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Kwa bahati nzuri nilibahatika kuhudhuria maziko ya dosa pale mlandizi,nilisikitika kwa mengi lakini kubwa hata kula na vaa yake ilikuwa shida mno.alisahaulika kabisa.huyu hakuna dereva bali mtu mwenye uwezo wake,enzi hizo alimiliki malori kadhaa,alijitoa kifedha mno mpaka kuuza baadhi ya mali zake ili kusaidia uhuru.
 
Atalipwa mbinguni na Allah!
 
Cc Mohamed said.
 
Nyerere alikuwa mwanamikakati hodari sana.
 
Nyerere alikua kichwa na smart sana,kuunganisha watanzania sio suala dogo.
 
Nyerere alikua kichwa na smart sana,kuunganisha watanzania sio suala dogo.
Jiwe...
Historia ya uhuru wa Tanganyika imeathirika sana kwa watu kutia fikra zao binafsi badala ya kuweka yale yenye ithibati ya utafiti.

Ndiyo sababu leo mimi niandikapo historia ya TANU wasomaji huwa wanasoma upya historia ya uhuru wa Tanganyika.

Viongozi wa TANU majimboni wengi wao wakitokea TAA ndiyo waliomjulisha Mwalimu kwa wanachama wao na si kinyume chake.

Soma historia yote hii vipi TANU iliingia majimboni utakuta hakuna aliyemjua Nyerere majimboni sikwambii Dar es Salaam.

Tanganyika wananchi hawakuwa wamehasimiana.

Walikuwa wamoja.
 
Nyerere alikuwa mwanamikakati hodari sana.
Yoda,
Unaijua historia ya Hamza Mwapachu (1913 - 1962) na aliyofanya kuwapata vijana wasomi kupigania uhuru wa Tanganyika?
Soma hapo chini:

MWALIMU WA MWALIMU:
HAMZA KIBWANA MWAPACHU (1913 - 1962)
Balozi Mwapachu afichua barua ya Shujaa Hamza
Na Bakari Mwakangwale

BALOZI Juma Hamza Mwapachu, ameiweka hadharani barua ya baba yake Mzee Hamza Kibwana Mwapachu, aliyomwandikia Mwalimu Julius K. Nyerere, mwaka 1949.

Barua hiyo imewekwa hadharani Watanzania wakielekea kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa Rais wa kwanza wa Tanganyika na baadae Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius K. Nyerere, aliyefariki dunia Oktoba 14, 1999.

Akizungumzia barua hiyo, mtafiti na mwandishi wa vitabu vya historia sahihi ya Tanganyika, Mohammed Said Salum, amesema barua hiyo karibu sasa itafikia miaka 70, tokea kuandikwa kwake.

Akitoa maoni yake Mohamed Said, alisema anadhani sababu ya kuiweka barua hiyo hadharani wakati huu, pengine ni kutaka kuwazindua Watanzania kuhusu kupotoshwa kwa historia ya wananchi wa Tanganyika katika kujikomboa kutoka katika makucha ya ukoloni wa Waingereza.

“Kumekuwa na tatizo kubwa katika kutafiti na kuandika kwa usahihi historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika, sasa naona Balozi Juma Mwapachu ameiweka hadharani barua ya baba yake Hamza Kibwana Mwapachu (1913 1962) aliyomwandikia Julius Nyerere, mwaka wa 1949, ili pengine kulizindua Taifa.
Amesema Mzee Said.

Akifafanua Mohamed Said amesema, mengi yaliyoandikwa kuhusu historia ya Tanganyika, yamemtaja Julius Nyerere, peke yake kiasi cha kufanya iaminike kuwa kabla yake hapakuwa na wanasiasa wala hapakuwapo na watu waliofanya juhudi zozote za kutaka kuikomboa Tanganyika kutoka kwa wakoloni, isipokuwa Mwalimu Julius Nyerere peke yake hali iliyopelekea nchi kukosa kuwatambua mashujaa wake.

Alisema, barua hiyo imedhihirisha ukweli kuwa historia ya uhuru wa Tanganyika, ipo katika vichwa vya watu na wengi wao wameshatangulia mbele ya haki na hata nyaraka nyingi zinazoonyesha mawasiliano ya kudai uhuru wakati huo pia zipo mikononi mwa watu binafsi.

Aidha Mohamed Said alisema, barua hiyo pia imefungua mlango na kuwawezesha watafiti wa historia ya Tanganyika kuchungulia ndani kusoma na kufahamu nini Mzee Hamza Mwapachu, alikuwa anasema kumwambia Mwalimu Nyerere, katika mipango ya kudai uhuru wa Tanganyika.

“Barua hii ni muhimu na kwa haraka iwekwe katika Makumbusho ya Taifa kwa faida ya vizazi vijavyo na naamini katika Maktaba ya Mh. Balozi Juma Mwapachu, yapo mengi mbali na aliyohifadhi kichwani kwake."
Amesema Mzee Said.

Akasema, Mtafiti yeyote katika historia ya uhuru wa Tanganyika, kama atakuwa makini hatoweza kumuepuka Mzee Hamza Mwapachu, kwani ni vigumu kumtaja Mwalimu Julius Nyerere na usimtaje Mzee Hamza Mwapachu.

Akiizungumzia barua hiyo alisema, hiyo (barua) ni matokeo ya barua ambayo Mwalimu Nyerere, alimwandikia Mzee Mwapachu, kuhusu mambo muhimu waliyozungumza siku za nyuma.

Alisema, katika barua hiyo, Mzee Mwapachu, ameorodhesha moja baada ya jingine katika yale waliyozungumza ambayo ni ''Trusteeship as compared to Protectorate and Mandate, White Paper 191, White Settlement in Tanganyika.''

Anafafanua zaidi Mohamed Said kuwa, katika ukurasa wa kwanza katika barua hiyo yenye kurasa tatu, unaonyesha mambo manane lakini kwa uchache ameyataja hayo matatu ambayo (kwa Kiswahili) ni udhamini wa Tanganyika chini ya Waingereza, Mjadala wa Afrika Mashariki na Ukazi wa Wazungu Tanganyika.

“Haya yalikuwa mambo mazito, makubwa na ya kuzungumzwa kwa siri sana baina ya Waafrika, sasa inawezekana vipi historia kama hii ikaachwa ipotee hivi hivi tu?''

Amesema na kuhoji mwanahistoria Mohamed Said.

Alisema, jambo la kusikitisha ni pale inapojaribiwa, ingawa kwa kuchelewa kuwaenzi mashujaa walio pambana na ukoloni, hujitokeza maswali mengi, ambayo hakuna awezaye kuyajibu kwa uhakika na kwa ithibati ya kuaminika.

Mathalani, akahoji kuwa inawezekana vipi kutolewa Medali ya Mwenge wa Uhuru kwa Abdulwahid na Ally Sykes, (ndugu wawili) waliokuwa kati ya waasisi 17 wa TANU, ukawaacha waasisi wengine kama Saadan Abdul Kandoro na Japhet Kirilo (kwa kuwataja wachache).

Mohamed Said akasema, itoshe tu kueleza kuwa medali hizo zimetolewa kwa kuchelewa miaka 50, kwani Ally Sykes, kapokea medali yake akiwa katika mwisho wa maisha yake akiwa mgonjwa, miaka miwili kabla ya kifo chake mwaka 2013.

“Lakini swali linakuja, vipi utawapa medali mashujaa hawa wa uhuru usimpe medali Mzee Hamza Mwapachu, ambae ushahidi wa historia unaonyesha kuwa ndiyo alikuwa, "mentor," wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Abdul Sykes?”

“Hawa wote waliokuja kudai uhuru katika nafasi zao tofauti na baada ya uhuru kupatikana wakaja kuwa viongozi wa Tanganyika huru."

Amesema Mzee Said.

Akichimbua zaidi kumbukumbu ya historia alisema kuwa Dr. Vedasto Kyaruzi, alipata kumwambia Juma Mwapachu, kuwa kama si mpango waliouweka Hamza Mwapachu na Abdul Sykes, basi Tanganyika isingepata uhuru wake mwaka wa 1961.

“Dr. Kyaruzi, akaongeza kwa kumwambia Juma Mwapachu, kuwa kule Nansio Kisiwani, alikopelekwa baba yake na Waingereza, ile ilikuwa ni jela ya kumtia kizuizini ili kumzuia asishiriki katika siasa.”

Akasema, wazalendo hao ndio waliochora ramani ya njia ipi ichukuliwe kuidai Tanganyika na kuitoa katika mikono ya Waingereza kwa salama.

Mohamed Said, akasema kwa wale waliokuwapo katika 'circle’ ya kupambana na Waingereza hakuna ambae hakuwa anajua kuwa Hamza Mwapachu, ndiye aliyekuwa akisukuma mambo nyuma ya pazia.

Alisema, kazi hiyo aliifanya iwe yuko Nansio au Rungwe, sehemu ambazo ni za mbali alizotupwa na wakoloni ili asiwasumbue kwa kumtoa karibu na miji mikuu ambako ndiko yalipokuwa mashina ya kupinga ukoloni.


Kulia: Abdulwahid Kleist Sykes (1924 - 1968) na Hamza Kibwana Mwapachu (1913 - 1962)


 
Najiuliza! Mkakati huu wa kuhakikisha mashujaa na wapambanaji hawa wa tanganyika yetu, wanafichwa kabisa hata wasisomwe popote kama moja ya watu muhimu katika harakati za uhuru, ni nan aliekuwa anaushughulikia? Mana yote waliokuwa wakiyafanya wao pamoja na nyerere, hayakufanyika gizani wala mafichoni..! Mpaka miaka ya 80's, 90's na mwanzoni mwa 2000's naamini bado palikua na wazee wengi sana waliopata kuyashuhudia yote haya! Sasa nguvu kubwa ya kuwafumba midomo wote hawa ilitoka kwa nani na lengo hasa likiwa ni nin? Yani, lengo la kuwaziba vinywa kiasi asipatikane hata mmoja wa kuyanena haya nin? Ni kitu gan kilihofiwa kutokea endapo history hii ingeachwa wazi? Je kitu hicho ni positive au negative kwa taifa?
 
Huyu Julius alikuwa mjanja sana kupata madaraka na kuweza kuyalinda ndio maana alitawala mpaka akachoka.

Huenda hata mabeberu waliupenda ujanja wake wakati mwingine

Ila kuistawisha nchi kiuchumi hakuwa na huo ujanja kabisa.

Pascal Mayalla JokaKuu zitto junior Kalamu Mohamed Said brazaj
 
Hizi mada zinazomhusu Mwalimu na hili kundi maalum huwa najaribu sana kuiepa nisishiriki kwa sababu najua msukumo wa mijadala hii ni nini hasa.

Sasa unaniita nijadili jambo ambalo ni wazi kabisa kwamba hao wazee wa Kariakoo dunia yao iliishia Magomeni, zaidi ya hapo hawakujuwa uwepo wa Tanganyika nzima na waTanganyika huko kwingine?
Hata hapo Kariakoo penyewe, unaweza kupata nyaraka na kumbukumbu za mikutano walizozifanya kuwa ushahidi wa kupigania uhuru wa Kariakoo?
 
Lakini nikushukuru mkuu'Proved', kwa kuniita hapa. Hii mada ya Mkuu Barafu nilikuwa sijaiona hapa jukwaani ilipoletwa.
 
Ante...
Soma makala hiyo hapo chini:

AFRICA EVENTS (LONDON) ILIVYOFUNGUA UKURASA WA HISTORIA MPYA YA WAZALENDO WALISAHAULIWA KATIKA KUPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

"There is a large body Tanzania's political history which has the effect, if not the avowed goal, of writing down the role of Muslims in the fight for independence. Yet it is a fact that their enterprises were not only crucial but daringly imaginative. Names like Saadan Abdu Kandoro and the Sykes brothers; Abdu and the ever youthful Ali come easily in mind. In a forthcoming book, Mohamed Said concentrates on these forgotten founders, what follows is a chapter from his work."
Mohamed Mlamali Adam

Huo hapo juu ni utangulizi alioandika Mhariri wa Africa Events, Mohamed Mlamali Adam katika makala yangu, ''In Praise of Ancestors,'' Africa Events, London, March/April 1988, pp. 37-41.

Hii ndiyo ilikuwa makala yangu ya kwanza katika gazeti hili.

Mlamali katika utangulizi wake kawataja Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa ujumla wao, kisha akataja majina: Saadan Abdu Kandoro, Abdu na Ali Sykes.

Mlamali Adam akasema katika huo utanguzi kuwa anaweka sura moja katika kitabu alichoandika Mohamed Said kinachotarajiwa kutoka kuhusu waasisi wa harakati za kudai uhuru.

Gazeti hili lilikusanywa lote kuzuia lisiwafikie wasomaji.
Hii ilikuwa mwaka wa 1988.

Mambo yalikuwa moto baada ya makala hii kuchapwa.
Vilifuatia vitisho.

Lakini sikuacha kuandika na AE hawakuacha kuchapa makala zangu.

Mwaka wa 1986 mama mmoja Mwingereza alimtembelea Ally Sykes nyumbani kwake na akamfanyia mahojiano ambayo yalichapwa AE.

Katika mahojiano yale Ally Sykes alieleza vipi yeye na kaka yake Abdul Sykes na Julius Nyerere walivyoasisi chama cha TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Makala ilipochapwa maofisa wa Uhamiaji walimtembelea huyu mama nyumbani kwake na kumuomba aondoke nchini.


 
Kalamu,
Soma makala hapo chini:

KUTOKA MAKTABA: MKUTANO WA SIRI KATI YA ABDUL SYKES NA JOMO KENYATTA NAIROBI 1950

Siku moja katika mazungumzo na Ahmed Rashad Ali akanambia kuwa mwaka wa 1950 yeye akiwa Nairobi wakati wa mashindano ya Gossage Cup Abdul Sykes alifika Nairobi na akawa anakaa Railway Hotel.

Ahmed Rashad alikuwa nahodha wa timu ya Zanzibar.

Abdul alimfuata kwenye kambi yao akamwambia amekuja Nairobi kuonana na Jomo Kenyatta na akamtaka amsindikize.

Leo asubuhi katika pitapita yangu Maktaba nimeikuta taarifa ya Special Branch kuhusu mktano wa Abdul Sykes na Jomo Kenyatta nami nakuwekeeni hapa barzani:



 
Hizi nilishazisoma mara ya kwanza ulipoziweka humu JF; kwa hiyo siyo ngeni kwangu.
Hazina tofauti yoyote na ile habari ya Wakrewe kwenda bandarini kumpokea mtemi wao Lukumbuzya; na badala yake ikawa ni kwenda kumwona mzee wa Kariakoo!
 
Hizi nilishazisoma mara ya kwanza ulipoziweka humu JF; kwa hiyo siyo ngeni kwangu.
Kalamu,
Kwako si mageni haya lakini kuna wengine ndiyo hii leo kwa mara ya kwanza anasoma kuwa Abdul Sykes alikutana na Jomo Kenyata na viongozi wengine wa KAU Nairobi 1950 na anaona kwa macho yake ushahidi wa mkutano ule kutoka taarifa za kikachero za Special Branch.

Abdul hakuwa mzee 1950 alikuwa na miaka 26.
 
Mimi nimejibu kwa niaba yangu, hayo ya wengine siyajui.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…