Ni kwa namna gani Julius Nyerere aliwazidi "Ujanja" wazee wa Kariakoo waliompokea kwenye siasa za Dar es Salaam?

Kalamu,
Hakika toka siku ya kwanza nabisha hodi hapa nilinuia kuzungumza na dunia nzima.
Nimefanikiwa sana katika hilo.
Ni kama hujiamini kuwa umefanikiwa, kama inakulazimu kila mara kurudia yale yale ya kuipasha dunia nzima kuhusu habari ile ile.
 
Pengine tutasimamisha shingo zetu na kusema "mzee mohammed ni mdini" lakini hatutathubutu kujiuliza hayo aliyoyafanya nyerere yalimaanisha nin! Hata bila kupepesa macho nyerere alikua na hofu dhidi ya waislam kuwa na nyadhfa za juu katika nchi hasa baada ya uhuru, na pia hakutaka ifahamike wazi kwamba vijana na wazee wengi sana wa kiislamu walikua nae bega kwa bega katika harakati za uhuru. Sababu ya kufanya hivo, anaijua ye mwenyew na pengine amekufa nayo kifuani.
 
Ni kama hujiamini kuwa umefanikiwa, kama inakulazimu kila mara kurudia yale yale ya kuipasha dunia nzima kuhusu habari ile ile.
Kalamu,
Kusomesha katika mtandao ni tofauti na kuwa na darasa ambalo wanafunzi wote unao kwenye chumba kimoja kwa wakati mmoja.

Katika mtandao uko katikati ya ''topic,'' anakuja mwanafunzi mpya kabisa ndiyo kwanza ananisoma.

Hapo ndipo ninaporudia somo ambalo pengine nimeshalisomesha miaka mitatu nyuma.

Bahati ni kama hii yako ya Kariakoo wakati nishaweka hapa historia ya TAA Kenya 1950 na Southern Rhodesia 1953.

Hapo siwezi kumwambia mwanafunzi wangu kuwa mbona somo hilo nishasomesha?

Narejea nyuma na kumwekea asome.
 
Bahati yangu ni kujua darasa lipi la kujifunza na lipi ni la kuvurugana tu akili.
 
Hivi serikalini hawakuwemo waislam, au kuna maana nyingine inayolengwa?
 
Ante...
Hakufanayo.
Prof. Haroub Othman alimkabili Mwalimu na kitabu cha Abdul Sykes.

Bahati nzuri Mwalimu alikuwa kakisoma kitabu.

Prof. Haroub alikwenda kwa Mwalimu kutafuta ukweli wa yale niliyoandika.
Wakawa wanakwenda moja baada ya jingine:
  1. Kweli ipo historia ya Wasilam ambayo haijaelezwa na kwa nini imekuwa hivyo?
  2. Yeye anaingiaje kwa Sykes na yale yaliyomo katika kitabu?
  3. nk. nk.
Prof. Haroub akamweleza Mwalimu kuwa yeye binafsi yale aliyosoma katika kitabu yamemshtua sana kwani Tanzania imejikuta ina historia mpya ya Nyerere na historia mpya ya kupigania uhuru wa Tanganyia kutoka vyanzo ambavyo hakuna anaeweza kuvipinga.

Sasa tunafanyaje?
Prof. Haroub aliuliza.

Haya yanatosha.
 
Yaleyale ya kusimulia habari kama ulikuwepo ukishuhudia mwenyewe!
 

Tafadhari japo kwa uchache tufahamishe majibu ya nyerere juu ya maswali hayo.
 
Ufundi wa "kukoreza chumvi" nao unaweza kuwa kipaji. Katika hili wewe umejaaliwa sana kuwa na kipaji hicho.
 
Bahati yangu ni kujua darasa lipi la kujifunza na lipi ni la kuvurugana tu akili.
Kalamu,
Darasa langu unaweza kulipata Library of Congress
Darasa langu unaweza kulipata ndani ya Dictionary of African Biography
Darasa langu unaweza kulipata Northwestern University, Chicago
Darasa langu unaweza kulipata Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin
Darasa langu unaweza kulipa Cambridge Journal of African History, Cambridge University

Ikiwa madarasa haya yanavuruga akili yako....
Bahati mbaya.


Library of Congress, Washington DC
 
Ufundi wa "kukoreza chumvi" nao unaweza kuwa kipaji. Katika hili wewe umejaaliwa sana kuwa na kipaji hicho.
Kalamu,
''Kukoleza.''

Mimi si mtu wa kubishana.

Lipo tatizo la historia ya Tanganyika ipo hoja imeletwa mimi nitajibu kama ninavyofahamu.

Ikiwa huamini sawa.
Sina ugomvi.

Muhimu nazungumza na dunia wako wengine watasoma na kupima na watajua ukweli.
 
Yaleyale ya kusimulia habari kama ulikuwepo ukishuhudia mwenyewe!

Mkuu, kwani shida iko wapi? Watu wanadadavua na kuhoji maswala mazito ya Mwenyezi Mungu, ndo washindwe na waogope kudadavua na kuhoji mambo ya nyerere? Kama hapakua na tatizo si tuta conclude tu kwamba hakukua na shida, na kama palikua na uwalakini basi tutasema pia, unafki wa nin?
 
Yaleyale ya kusimulia habari kama ulikuwepo ukishuhudia mwenyewe!
Kalamu,
Nimekuonyesha na kukujulisha madarasa yangu.

Mimi nimesoma Nyaraka za Sykes na nimezungumzanao.

Kama yeyote yule angebahatika kuzisoma nyaraka hizi na kuzungumza na watu hawa angezungumza kama mimi.

Unaona baada ya kitabu kuchapwa milango mingapi nimefunguliwa mimi kuingia?


Balozi Abbas Sykes na Mwandishi 2012​
 
Tafadhari japo kwa uchache tufahamishe majibu ya nyerere juu ya maswali hayo.
Antenna,
Mazungumzo ya Prof. Haroub Othman na Mwalimu yalihitimishwa kwa kukubaliana kuwa Prof. Haroub aunde kamati ambayo itaandika kitabu cha maisha yake kwa wao kufanya mazungumzo na yeye.

Mwalimu alikuwa mgonjwa hakuwa katika hali ya kuweza kukaa kitako na kuandika.

Kazi hii ya uandishi haikufanyika.

Nilibahatika kukutana na Prof. Ahmed Muhidin rafiki mkubwa wa Nyerere na mmoja wa watu waliokuwa katika Jopo la Waandishi wa kitabu cha Julius Nyerere.

Prof. Muhidin alinieleza kuwa Mwalimu alimuomba awemo katika jopo hilo:


Nikiwa nyumbani kwa Prof. Ahmed Muhidin, Kikambala Mombasa 2021​
 
Hakuna anayekuzuia kuamini upendavyo, na ni hivyo hivyo kwa wasioamini unayoamini wewe.
Wakiona unasema uongo wanayohaki pia ya kusema hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…