Ni kwa nini shughuli za kilimo na ufugaji zimekuwa na changamoto nyingi kuliko matarajio ya watu wengi?

Ni kwa nini shughuli za kilimo na ufugaji zimekuwa na changamoto nyingi kuliko matarajio ya watu wengi?

FAJES

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2017
Posts
720
Reaction score
644
Juzi nikasema nimpigie rafiki yangu mmoja ambaye sijazungumza naye kwa miezi kadhaa sasa. Mingoni mwa mazungumzo yetu ilikuwa kama ifuatavyo:

Mimi: Mambo vipi kaka, habari za siku?
Yeye: Salama kaka, vipi unaendeleaje na mishemishe huko ya maisha?
Mimi: Salama tu kaka, Mungu anajalia uzima, vipi shughuli yako ya ufugaji wa kuku unaendeleaje?
Yeye: Ahh, kaka sina hamu kabisa!
Mimi: Vipi kulikoni?
Yeye: Wale kuku wangu 50 wa kienyeji wote walikufa, yaani pamoja na jitihada zote za kuwapa chanjo na kufuata taratibu zote lakini nimeishia kupata hasara. Kuku walikufa mmoja baada ya mwingine wala sikuamini kabisa.
Mimi: Pole sana kaka.

Hiyo ni sehemu ya maongezo yetu hapo juzi. Feedback aliyoitoa imenifanya kufikiri sana juu ya changamoto za ufugaji na kilimo nchini kwetu. Pamoja na watu wengi kufuata taratibu za kitaalamu juu ya ufugaji na kilimo, ni kwa nini sekta ya kilimo imekuwa ikikumbwa na changamoto nyingi zinazosababisha ufukara badala ya mafanikio? Utasikia kila mtu anakuelezea changamoto hizohizo za hasara kila mahali. Je, katika watu 10 wanaofanya shughuli za kilimo na ufugaji, ni wangapi hufanikiwa? Jitihada zipi tunachukuwa kutatua changamoto hizi maana kilimo ni sekta inayotegemewa na asilimia kubwa ya watu nchini?

Miaka kama minne iliyopita, nilisema nilime mahindi ya kumwagilia, hasara niliyoipata sitaki kuikumbuka. Mahindi yalishambuliwa na wadudu hatari. Nikasema nilime viazi mbatata, nako nikaambulia kipigo cha mbwa koko. Siyo kwamba nilikuwa sifati taratibu za kitaalamu, nilifuata taratibu ila bado nikapigwa na kupotezwa. Ikabidi niwe mpole.

Hapo tunaongelea changamoto za mashambani. Bado zile za masokoni ndio usiseme kabisa. Ni lini mkulima atakuwa na nafuu ya maisha kutokana na kilimo? Pamoja na wataalamu wengi tulionao, ni kwa nini bado kilimo kimekuwa ni tatizo hasa kwa watu wa hali ya chini?

Naomba kujua kama kuna mtu ambaye katika miaka mitano mfululizo, amefanikiwa kupata faida kuanzia shambani hadi sokoni bila ya kukumbana na hizi changamoto? Je, wapo watu hawa? Ni asiliamia ngapi katika wote wanaojihusisha na kilimo?

Naomba kuishia hapa. Nasikia uchungu moyoni!
 
Tatizo sio changamoto, bali tatizo kubwa ni wengi wanao ingia kwenye kilimo na ufugaji hutumia makaratasi na kalamu theory kuanzia kuandaa shamba, kulima, upandaji na hadi kupata faida hata kabla hawajaenda kwenye practical.

Mwisho ndipo wanaenda shambani kwenye practical wakiwa na expectations kubwa kama walivyo jidanganya kwenye theory, na hapo ndipo wanapo kutana na changamoto za "mvua haijanyesha" "wadudu wamekula mazao" na kisha huo ndio unakua mwanzo wa kuanguka kwao.
 
Kabla ya kuingia kwenye mradi wowote fanya utafiti wa huo mradi,soma vitabu,majarida na mtandaoni kuhusu huo mradi, angalia video YouTube.
Tembelea watu wanaofanya huo mradi waulizie faida na changamoto wanazokutana nazo,waulizie wanatatuaje hizo changamoto,waulizie masoko,nk.
Tatizo la Watanzania hatutaki kujifunza kabla ya kuanza mradi.
Pia uzoefu, inabidi uvumilie ili uwe mzoefu na watu wengi hawapendi kuvumilia.Uzoefu unapatikana kwa kufeli mara nyingi.Ukifuga kuku wakifa usikate tamaa,jiulize umekosea wapi na Anza upya.
 
Mi hua natumiaga maneno haya "Science and art" ya kilimo. Nikiwa namaanisha utaalamu na biashara ya kilimo inavyokwenda. Ni lazima hv vitu viwili uvijue unapoingia kwny sekta ya kilimo especially km utakua mkulima moja kwa moja.
Ni lazima uwe na taarifa za kutosha na sahihi ili kupata faida kwny kilimo mfano mdogo huyo rafiki yako anasema kuku walikufa mmoja mmoja mpaka wakaisha sasa kwa kusema hv kitaalam kuna uwezekano mkubwa ugonjwa wa mdonde / kideri umeua kuku wake. Wakat na yeye anasema amewapa chanjo zote, je ana uhakika aliwapa kweli chanjo? Ilikua ya namna gan ya matone au ya kuchanganya na maji. Aliwapaje? inshort namaanisha ule utaalam (science) yenyewe ya ufugaji anatakiwa awenayo kwa msaada wa afisa mifugo. Na hii inakuja kwa kujifunza na kuptia uzoefu!.
Kwny art (biashara) ya kilimo hapo ndo lile neno "kilimo biashara" huja hapo unatakiwa kua entrepreneur sasa ki kweli kweli kwa jinsi rafik yako navyomuona kuanguka mara moja tu amekata tamaa hiyo sio sifa ya mjasiriamali.
To be OK and comfortable with failure is the top priority for any entrepreneur!
 
Tatizo ni mkulima mwenyewe anaingia ktk kilimo huku amelishwa data za uongo hana muda wa kujifunza yeye anaingia ili apige pesa ndefu apate faida mara 7 ya mtaji wake so akiingia akakuta tofauti basi hukata tamaa kabisa.

Pili ni madalali sokoni hawafai sabab wenyewe ndio wapanga bei

Tatu wakulima wengi ni masikini akivuna anauza kwa bei yeyote ile ili apate pesa za kujikimu na watoto mtu anaelima huku anapesa hua hapati hasara sana sabab anauwezo wa kuweka mazao yake store kusubiri bei ipande

Mwisho jamani kilimo ni kazi kama kazi zingine kinahitaji ujuzi,mapenzi,na usimamiz wa karibu kilimo ni kama mtoto mchanga kinahitajika care ya wewe mwenyewe

Mfano
Nina mashost wangu fulani sasa wao ni wafanyakaz mm niliacha kazi nzur nikajikita ktk kilimo sasa wao walitaka kunitumia mimi ktk kilimo chao yaan walitaka either walime pembeni yangu niwe nawasimamia na kuwapa update wenyewe wakiwa ofisini ama wanilipe waniajili ktk usimamizi wa mashamba yao.kiukweli nilikataa sabab kilimo nakijua fika usipokuwepo mwenyewe lazima utapata dhambi ya kuhisi umepigwa pia niliona nikikubali ni rahisi kuwapoteza kama rafiki so bora nilivyokataa walinuna but baadae maisha yaliendelea

So kwa kila anaetaka kulima chagua either kazi au kilimo sabab its imporsible kufanya vyote pamoja
Juzi nikasema nimpigie rafiki yangu mmoja ambaye sijazungumza naye kwa miezi kadhaa sasa. Mingoni mwa mazungumzo yetu ilikuwa kama ifuatavyo:

Mimi: Mambo vipi kaka, habari za siku?
Yeye: Salama kaka, vipi unaendeleaje na mishemishe huko ya maisha?
Mimi: Salama tu kaka, Mungu anajalia uzima, vipi shughuli yako ya ufugaji wa kuku unaendeleaje?
Yeye: Ahh, kaka sina hamu kabisa!
Mimi: Vipi kulikoni?
Yeye: Wale kuku wangu 50 wa kienyeji wote walikufa, yaani pamoja na jitihada zote za kuwapa chanjo na kufuata taratibu zote lakini nimeishia kupata hasara. Kuku walikufa mmoja baada ya mwingine wala sikuamini kabisa.
Mimi: Pole sana kaka.

Hiyo ni sehemu ya maongezo yetu hapo juzi. Feedback aliyoitoa imenifanya kufikiri sana juu ya changamoto za ufugaji na kilimo nchini kwetu. Pamoja na watu wengi kufuata taratibu za kitaalamu juu ya ufugaji na kilimo, ni kwa nini sekta ya kilimo imekuwa ikikumbwa na changamoto nyingi zinazosababisha ufukara badala ya mafanikio? Utasikia kila mtu anakuelezea changamoto hizohizo za hasara kila mahali. Je, katika watu 10 wanaofanya shughuli za kilimo na ufugaji, ni wangapi hufanikiwa? Jitihada zipi tunachukuwa kutatua changamoto hizi maana kilimo ni sekta inayotegemewa na asilimia kubwa ya watu nchini?

Miaka kama minne iliyopita, nilisema nilime mahindi ya kumwagilia, hasara niliyoipata sitaki kuikumbuka. Mahindi yalishambuliwa na wadudu hatari. Nikasema nilime viazi mbatata, nako nikaambulia kipigo cha mbwa koko. Siyo kwamba nilikuwa sifati taratibu za kitaalamu, nilifuata taratibu ila bado nikapigwa na kupotezwa. Ikabidi niwe mpole.

Hapo tunaongelea changamoto za mashambani. Bado zile za masokoni ndio usiseme kabisa. Ni lini mkulima atakuwa na nafuu ya maisha kutokana na kilimo? Pamoja na wataalamu wengi tulionao, ni kwa nini bado kilimo kimekuwa ni tatizo hasa kwa watu wa hali ya chini?

Naomba kujua kama kuna mtu ambaye katika miaka mitano mfululizo, amefanikiwa kupata faida kuanzia shambani hadi sokoni bila ya kukumbana na hizi changamoto? Je, wapo watu hawa? Ni asiliamia ngapi katika wote wanaojihusisha na kilimo?

Naomba kuishia hapa. Nasikia uchungu moyoni!
 
Tatizo ni mkulima mwenyewe anaingia ktk kilimo huku amelishwa data za uongo hana muda wa kujifunza yeye anaingia ili apige pesa ndefu apate faida mara 7 ya mtaji wake so akiingia akakuta tofauti basi hukata tamaa kabisa.

Pili ni madalali sokoni hawafai sabab wenyewe ndio wapanga bei

Tatu wakulima wengi ni masikini akivuna anauza kwa bei yeyote ile ili apate pesa za kujikimu na watoto mtu anaelima huku anapesa hua hapati hasara sana sabab anauwezo wa kuweka mazao yake store kusubiri bei ipande

Mwisho jamani kilimo ni kazi kama kazi zingine kinahitaji ujuzi,mapenzi,na usimamiz wa karibu kilimo ni kama mtoto mchanga kinahitajika care ya wewe mwenyewe

Mfano
Nina mashost wangu fulani sasa wao ni wafanyakaz mm niliacha kazi nzur nikajikita ktk kilimo sasa wao walitaka kunitumia mimi ktk kilimo chao yaan walitaka either walime pembeni yangu niwe nawasimamia na kuwapa update wenyewe wakiwa ofisini ama wanilipe waniajili ktk usimamizi wa mashamba yao.kiukweli nilikataa sabab kilimo nakijua fika usipokuwepo mwenyewe lazima utapata dhambi ya kuhisi umepigwa pia niliona nikikubali ni rahisi kuwapoteza kama rafiki so bora nilivyokataa walinuna but baadae maisha yaliendelea

So kwa kila anaetaka kulima chagua either kazi au kilimo sabab its imporsible kufanya vyote pamoja
Ni kweli changamoto za kilimo ni nyingi Sana ila pia wakulima tulio wengi hatuna utaalamu na pia hata tukiupata hatuutumii kwa usahihi,mfano hapo we umesema ulikuwa unafuata utaalamu ila tukikudadisi na ukiwa muaazi utakuwa hukufuata kanunu za zao husika.Mm nalima ila kila mwaka Kuna makosa ya wazi nayafanya (Yani Kama vile Mayeree alivyopaisha penati akiwa Yeye na golia).
Mfano wa kilimo Cha mahindi, wataalam wanatuambia utumie mbegu Bora,upande kwa wakati, mbolea utie Mara 2 au 3 kwa kuzingatia hesabu ya tangia kuota kwa mimea,mimea isiwe ndani ya manyasi n.k ,ukimaliza kazi zote Hadi kufikisha mahindi store lazima uangalie Bei ya faida, mitihani iliyopo unaamua kuuza tu,kisha unaanza kulalamika.Kilimo kinalipa mm ni shahidi kwa upande wangu BINAFSI na Sina mpango wa kuacha Leo Wala kesho In Shaa Allah
IMG_20220403_132658_526.jpg
View attachment 2221699
 
Mimi nitaelezea upande wa changamoto niliyokutana nayo, niliwahi pata mkataba wa ku supply kiwandani ambao kiukweli ulikuwa mzuri kama ungetekelezwa kwa vigezo walivyoainisha wao. Lakini cha kustaajabisha wale watu walikuwa na nia ovu kabisa, walinilipa kiasi cha fedha ili wanipe moyo wa kuendelea, lakini ikafika mahali wale watu hawakunilipa kabisa.

Hivi tunavyoongea nina miaka mitano nafuatilia pesa hizo(kiasi sitataja maana ni kikubwa) ambazo kiukweli ndio ulikuwa mtaji wangu wote. Nimefuatilia mpaka mahakamani na vielelezo vyote vya mkataba. Nilishinda kesi lakini hatua za malipo bado zinaendelea. Wamenipotezea muda mno hawa wenye kampuni yao, lengo lilikuwa baadae ninunua mashine za kilimo kama (Tractors with full set implements,
images.jpeg
combine harvesters) ili niwe mkulima wa kati, lakini ndoto hizo zimefifia kwa sasa.

Kwa changamoto hii ilipunguza sana morali, mpaka sasa nafanya tu lakini malengo si kupata faida kubwa ila ikitokea nimepata basi namshukuru Mungu. Risk ni nyingi na inahitaji uvumilivu wa hali ya juu.
 
Sio kweli kuwa kilimo na ufugaji kinafanya watu wawe maskini, nukulize jambo kila mtaa na kila Kona kuna wafanyabiashara je wangapi wamefanikiwa kupitia biashara, then nikupe udhoefu kidogo, nimefanya kilimo miaka kadhaa , nimerithi mashamba ya familia, wazazi wangu walikuwa wanalima na kufuga, Mimi nilikuwa nalima tu kifupi kazi ya kilimo ilikuwa ngumu,nilipostuka kuchanganya kilimo na ufugaji hali imebadilika sana , siku hizi nikitajiwa millioni siogopi
 
Sio kweli kuwa kilimo na ufugaji kinafanya watu wawe maskini, nukulize jambo kila mtaa na kila Kona kuna wafanyabiashara je wangapi wamefanikiwa kupitia biashara, then nikupe udhoefu kidogo, nimefanya kilimo miaka kadhaa , nimerithi mashamba ya familia, wazazi wangu walikuwa wanalima na kufuga, Mimi nilikuwa nalima tu kifupi kazi ya kilimo ilikuwa ngumu,nilipostuka kuchanganya kilimo na ufugaji hali imebadilika sana , siku hizi nikitajiwa millioni siogopi
Mkuu itapendeza Kama utachangia pia namna ulivyoweza kupiga hatuA ya kimaendeleo kwa shughuli za kilimo,na ni wakati upi na nini kilikushtua ukichanganya na ufugaji
 
Kabla ya kuingia kwenye mradi wowote fanya utafiti wa huo mradi,soma vitabu,majarida na mtandaoni kuhusu huo mradi, angalia video YouTube.
Tembelea watu wanaofanya huo mradi waulizie faida na changamoto wanazokutana nazo,waulizie wanatatuaje hizo changamoto,waulizie masoko,nk.
Tatizo la Watanzania hatutaki kujifunza kabla ya kuanza mradi.
Pia uzoefu, inabidi uvumilie ili uwe mzoefu na watu wengi hawapendi kuvumilia.Uzoefu unapatikana kwa kufeli mara nyingi.Ukifuga kuku wakifa usikate tamaa,jiulize umekosea wapi na Anza upya.
Ndugu ulilo liseme ni kweli kabisa utafiti na uvumilivu na kukubali kufundishika ndio njia iliyo bora kukufanya ufikie malengo yako ktk utendaji wa mradi wowote unaotaka kuanzisha, mf Mimi nafanya ufugaju wa Mbuzi na Mbwa huwa namshauri yeyote anayetaka kuingia ktk ufugaji aje kwanza kunitembelea na kuona ufugaji na aina mbali mbali za Mbuzi nakuzitambua halafuaingie pole pole ktk ufugaji huo huku tukiendelea kuwasiliana kwa ushauri zaidi.
Nakingine kibaya sana watu wanapenda manufaa ya haraka haraka bila kuujua mradi unajiendeshaji na utajizalishaje.
 
Back
Top Bottom