Ni kwanini mpaka sasa hakuna chama cha upinzani kimetoa tamko kufuatia mambo ya Ng'umbi?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Mimi nilitegemea hili jambo lingefungua ukurasa mpya wa hasira za kutaka mabadiliko katika mifumo yetu ya uchaguzi badala yake naona wapinzani wote wapo kimya tu shida Iko wapi!?

Unajua hili jambo limeleta dharau kubwa sana kwa watanzania na nadhani kwa kuwa ushahidi uko wazi kabisa kelele za wapinzani zingewafanya CCM waone aibu waje kwa meza ya mazungumzo ili kufuta huu mfumo.
 
Hawakurupuki hadi wajiridhishe kwanza maana hili swala halihitaji mhemko kujibu
 
Kwani tamko la DC ni la kwanza? Siyo wanasiasa tu wametamka maneno hayo bali hata vyombo vya dola kama polisi na mahakama!

Kwa hiyo hakuna jipya!
 
CCM hawawezi kuona aibu kwa sababu maisha yao yako kidhalimu zaidi.
 
Kwani tamko la DC ni la kwanza? Siyo wanasiasa tu wametamka maneno hayo bali hata vyombo vya dola kama polisi na mahakama!

Kwa hiyo hakuna jipya!
Hata Magufuri aliwahi kutamka kuwa wewe Mkurugenzi ni mtumishi wa Serikali mshahara nikulipe mimi halafu umtangaze mpinzani kuwa ameshionda basi kazi huna.Kwa gia hiyo Serikali ya CCM inaona uchaguzi wa haki siyo kitu ila kulinda chama chao kuna maslahi kuliko maisha ya Watanzania wengi.
 
Hata hapa unapiga kelele,vipi unataka mawe yapige kelele?
 
Ninyi mnamshangaa ng'umbi mbona kuna wakati furani mkuu kabisa akiituma Toti kufanya kampeni, nadhani ilikuwa Zimbabwe au Malawi uko madarakani, kesho aje mtu. Kitoka huko anakotoka umpe nchi kiboya. Jeshi lako serikali yako!!
 
Vyama vya upinzani bado vipo kweli? Kuna enzi zile za akina Wilbrod Silaa, Tl, kabwe, kafulila, Mbowe, wangwe, sugu, heche, msigwa, halima, mbatia nk..sahivi kumepoa hata waliopo wakisema kitu kimyaaa...yani kama chama hakina wabunge bungeni aisee kunakuwa ovyoo..
 
Wapinzani hayo wameshasema sana, kinachofanyika sasa ni hao ccm kukiri tu ukweli hadharani ambao umekuwa ukisemwa siku zote na wapinzani.
 
Matunda ya Magufuri.
 
Lema kapost hii mistari..

Luka 12:2-4

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Hakuna jambo lililofunikwa ambalo halitafunuliwa au siri iliyofichwa ambayo haitajulikana. 3 Kwa hiyo, yote mliyosema gizani yatasikiwa mchana: na yote mliyonong’onezana mkiwa mmeji fungia chumbani, yatatangazwa hadharani.
4 “Nawambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, na halafu basi.
 
Na amesema tayari washamaliza kazi muda mrefu which means uchaguzi wa Nov 2024 kazi ishamalizika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…