Ni kwanini waliotajwa kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi na CAG, hawachukuliwi hatua za kisheria?

Ni kwanini waliotajwa kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi na CAG, hawachukuliwi hatua za kisheria?

Majaliwa alisema Hazina wanaume wamepiga 2B ndani ya siku 2 akaunda tume mpaka leo haijulikani
 
Matokeo yake ripoti ya CAG siku hizi imekuwa kama mchezo wa kuigiza, inasomwa kwa mbembwe kuonesha tulivyopigwa halafu wapigaji wanalindwa, huu umasikini wa hili taifa utaendelea kuwepo kwa miaka sana mingi ijayo.

Tukiibiwa mapesa mengi na marafiki zao wanakaa kimya, lakini tukiibiwa kidogo na wasio rafiki zao ndio wanawatoa sadaka, hili taifa chini ya utawala wa CCM linaongozwa kisanii sana.
Ripoti ya CAG na mapendekezo yake hayatekelezwi kwa sababu ya udhaifu wa bunge.

Bunge ambalo linaisaidia serikali badala ya kuisimamia.

Hivi wabunge wetu nani aliyewaambia kazi yao ni kuisaidia serikali.
 
Hatua zinachukuliwa

Kama huamini jaribu kufanya upigaji ama tafuta wahusika wa huo upigaji uone kama wako salama


Nadhani labda wawe wanatangaza ili umma ujue
 
Hatua zinachukuliwa

Kama huamini jaribu kufanya upigaji ama tafuta wahusika wa huo upigaji uone kama wako salama


Nadhani labda wawe wanatangaza ili umma ujue
Hatua zipi zinachukuliwa?

Usitugeuze sisi ni watoto wadogo, wa kuweza kutudanganya unavyotaka🥺
 
Labda huwa zinapigwa na kuwekwa kwa ajili ya kampeni who knows?
Labda wamepangiana nani ale wapi na lini
Na Labda kuna Orodha kabisa ya waibaji
Yaani wao wanapewa kwa ajili ya miradi huku wanaambiwa msifanye chochote hizo tumeandika hewa tu

Kwa kweli huwa najiuliza na kutunga mengi kama kichaa vile
Haiwezekani eti kiongozi anakuja anasema
Eti hili ndio jengo la 600m?
Takukuru mchukueni huyo
Hadithi imeishia hapo kapewa lift na taku wakimlinda
 
Watendaji wanaenda kukaangwa kwa moto wa kuyeyusha chuma. Hasa wale waliokuwepo enzi ya jiwe. Tuombe Mungu wasiumizwe wasiohusika na huo upigaji unaotajwa.

MAGUFULI CABAL aka SUKUMA GANG are going to suffer a literal obliteration

God bless you.
 
Tangu lini fisadi anafungwa, jela ni kwa ajili ya watu masikini
 
Miisteeseri
Umepata jibu la Swali lako? au bado ni Porojo kama za wanasiasa wengi?
 
Tusubiri mchakato mzima wa ripoti ili tuweze kuridhika na ukaguzi, unaoendelea
 
Ni jambo lilizoeleka kwa mkaguzi mkuu na mdhibiti wa pesa za Serikali (CAG) kuibuka na ripoti kila mwaka, inayoonyesha namna mabilioni ya pesa ya walipa zinavyotafunwa na "wajanja" wachache walioko Serikalini, pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Lakini tunashuhudia magereza yetu, yakiwa yamefurika wafungwa, wakiwa wamehukumiwa kwa vijikesi, vidogo vidogo, kama vile wizi wa kuku!

Ndiyo hapo ninapouliza, hivi kuna sababu gani ya kutusomea hadharani ripoti hizo za CAG, kama Serikali yetu, haina dhamira ya dhati kuwachukulia hatua za kisheria?

Tumeshuhudia, makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, eti akisema, atamshairi Rais Samia, aweze kuwachukulia hatua za kisheria, wale wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG!

Hivi umewahi kuona wapi watu waliotenda makosa makubwa kama hayo ya kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii, eti mpaka Rais ashauriwe Ili achukue hatua za kisheria?

Mbona hawa wanaotuhumia kwa vijikesi vidogo vidogo, kama vile wezi wa vibasikeli, wakiwa wamejazana magerezani, wakiwa wameshahukumiwa tayari, kutumikia vifungo vyao, je na hao Rais ameshauriwa kabla ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa' vifungo vyao??

Huu mtindo unaotumika na Serikali hii ya CCM, ni wa hatari Sana, unaofanya upendeleo wa wazi kabisa na "kubariki" kwa kuwaona wale wezi wa mabilioni ya Serikali, kama mashujaa na kuachiwa watembee kifua mbele, wakati wezi wa vitu vidogo vidogo, kama wale wanaowakwapua vipochi kwa abiria kwenye daladala, ndiyo wahukumiwe vifungo mahakamani na watuhumiwa wengine hata wakipoteza Maisha yao kwa "kuhukumiwa' vipigo na wananchi wenye hasira kali!

Ndiyo maana nchi hii kodi zinakuwa nyingi mno, kama vile tozo mbalimbali, kwenye miamala ya simu, ambazo zinawakamua watanzania wanyonge, kumbe pesa hizo, zinaliwa na watanzania wachache, tuliowaamini na kuwakabidhi madaraka ya juu, Katika nchi hii!

Tunaomba viongozi wetu wa Serikali hii ya CCM, wawe "serious" na wachukue hatua mara moja na tuone watuhumiwa wote waliotajwa na CAG kukwapua mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii wanafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.

Hilo ombi likitokea kukubaliwa na hatimaye kufanyiwa kazi ndio utakuwa mwisho wangu wakuja hapa Jamiiforums kuchachafya nisiyoyajua.

Lakini kwa sasa, niulize tu, hiyo Serikali yenye uthubutu wa kufanya hivyo itaongozwa na Chama gani?
ACT, pwaa
CHADEMA, pwaa
CCM, pwaa
...na vile vyama vingine, vivuli, vya hao juu...only time will tell.

Ninayojua hizi Ripoti zikitokea hakuna 'kuu' linalotokea zaidi ya kuimarishwa kwa Vyama vya Kisiasa. Porojo, mihemeko, na vijembe.

Hata Kipanya ana Vijembe! Madenge naye yumo, huko twitani ndiyo usiseme, hata miye Nimo!

CAG,wala, na sintoshangaa nikasikia eti anajiuzulu, kabadilishwa na fedheha wakati hao waliotajwa(kama wametajwa) wanaendelea kupiga ramli za 'kusingiziwa' 'kuonewa'.. kadhalika na kadhalika

Binafsi nitajiuzulu kuingia hapa Jamiiforums na kwenda kuwekeza kilimo cha mihogo Chanika pale tu kuna mtu au watu watafikishwa mahakamani, na kumaliza mchakato huo, halafu kupigwa miaka stahiki Keko. Nitajiuzulu.
Pascal Mayalla naona hawa mchwa toka uhuru wa taifa hili wapo na wanaendelea kula mbao ya taifa na wewe ulionyesha nia ya dhati kugombania ubunge kwenda kuwapa support au kuzima harakati zao
 
Ni jambo lilizoeleka kwa mkaguzi mkuu na mdhibiti wa pesa za Serikali (CAG) kuibuka na ripoti kila mwaka, inayoonyesha namna mabilioni ya pesa ya walipa zinavyotafunwa na "wajanja" wachache walioko Serikalini, pasipo kuchukuliwa hatua zozote.

Lakini tunashuhudia magereza yetu, yakiwa yamefurika wafungwa, wakiwa wamehukumiwa kwa vijikesi, vidogo vidogo, kama vile wizi wa kuku!

Ndiyo hapo ninapouliza, hivi kuna sababu gani ya kutusomea hadharani ripoti hizo za CAG, kama Serikali yetu, haina dhamira ya dhati kuwachukulia hatua za kisheria?

Tumeshuhudia, makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdrahman Kinana, eti akisema, atamshairi Rais Samia, aweze kuwachukulia hatua za kisheria, wale wote waliotajwa kwenye ripoti hiyo ya CAG!

Hivi umewahi kuona wapi watu waliotenda makosa makubwa kama hayo ya kutafuna mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii, eti mpaka Rais ashauriwe Ili achukue hatua za kisheria?

Mbona hawa wanaotuhumia kwa vijikesi vidogo vidogo, kama vile wezi wa vibasikeli, wakiwa wamejazana magerezani, wakiwa wameshahukumiwa tayari, kutumikia vifungo vyao, je na hao Rais ameshauriwa kabla ya kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa' vifungo vyao??

Huu mtindo unaotumika na Serikali hii ya CCM, ni wa hatari Sana, unaofanya upendeleo wa wazi kabisa na "kubariki" kwa kuwaona wale wezi wa mabilioni ya Serikali, kama mashujaa na kuachiwa watembee kifua mbele, wakati wezi wa vitu vidogo vidogo, kama wale wanaowakwapua vipochi kwa abiria kwenye daladala, ndiyo wahukumiwe vifungo mahakamani na watuhumiwa wengine hata wakipoteza Maisha yao kwa "kuhukumiwa' vipigo na wananchi wenye hasira kali!

Ndiyo maana nchi hii kodi zinakuwa nyingi mno, kama vile tozo mbalimbali, kwenye miamala ya simu, ambazo zinawakamua watanzania wanyonge, kumbe pesa hizo, zinaliwa na watanzania wachache, tuliowaamini na kuwakabidhi madaraka ya juu, Katika nchi hii!

Tunaomba viongozi wetu wa Serikali hii ya CCM, wawe "serious" na wachukue hatua mara moja na tuone watuhumiwa wote waliotajwa na CAG kukwapua mabilioni ya pesa ya walipa kodi wa nchi hii wanafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zao.
Ripoti za CAG ni getesha tu ni mpango mwingine wa kutafuna hela
 
Kiuahalisia hawa wakaguzi /wathibiti wetu inabidi nao kuthibitiwa,kukaguliwa na kuhojiwa na Bunge letu. Bunge lenyewe liliondolewa spika na likabaki kimya kabisa.

Naona wanaidhalilisha tu hii ofisi sababu hawaonekani wakiwa serious zaidi ya kutumika kisiasa, maigizo.
Hahahaa
 
Taarifa.
Mchwa ni wafanisi. Piga ua

WanaoEndelea kuwashabikia.

...nao wataendelea kuhuzunika na wivu tu.
.tafuta maharifa ya kweli yasiyo na shurumati halafu utajipenda na kupenda Mchwa.
 
Back
Top Bottom