Msisitizo wangu ni vigezo vilivyotumika. Bila ya vigezo hivyo, orodha nzima inabaki kuwa ni paukwa-pakawa tu. Si tofauti na uteuzi wa mocha bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Unadhani Pluijm atashtuka au kuamini kwamba Mbwana Makata ni kocha bora zaidi yake?
Ila mimi sijapata kujinadi kuwa ni mpenzi wa Yanga. Mimi ni mtetezi wa Yanga na Simba dhidi ya jeuri, kebehi, kejeli na dharau kuwa vilabu hivyo si chochote mbele ya timu zinazoonekana kuchipukia kama Azam. Kadhalika ni mgomvi mkubwa wa hoja zisizokamilika na zinazopotosha. Ndio maana huwa napingana sana na waandishi wetu wa habari, hasa za michezo, sambamba na wachangiaji wapotoshaji humu JF.