Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inakuaje mnakuwa na roho ngumu hivyo?😂😂😂 wasituchukulie pouwa
Halafu unapewa maelekezo dawa unafanya mwenyewe, utaona kimtu kinavyoweweseka!!
Kumtoa mpaka umchoke wewe!! Ila la maokoto ndo muhimu, wadada mje msione aibu. Ex kakuacha bado unampenda dawa ipo, wabahili dawa ipo, na wale wa kisasi dawa ipo. Usipofanikiwa narudisha pesa yako 🤣🤣🤣🤣🤣
Unahitaji dawa?Inakuaje mnakuwa na roho ngumu hivyo?
Kuna mbinu za kujidhatiti dhidi ya haya makitu. Maana inatisha sana hizi habari zake.Limbwata lipo sana, huko KAGERA liliibuka Limbwata aina ya SHUNTAMA, acha kabisa wanaume waligeuzwa kama mazuzu , hii kitu ilileta shida miaka hiyo ya 90 mpaka 2000, ilibidi mpaka mapadre na viongozi wa dini waingilie kati na kuhubiri hilo janga makanisani mpaka likatoweka! Nasikia wamama walikuwa wanavizia maji yaliyooshewa na maiti halafu wanafanyia hiyo limbwata basi mwanaume anakuwa hajitambui Kwa mkewe kama maiti!
Kuna mshikaji wangu alipigwa limbwata na mwanamke wa kigoma Mmanyema , daah ofisi nzima ilijua kwamba mwenzetu kakamatika, alikuwa anafua, anapiga deki anachuma kisamvu , siku tukimfuata TWENDE nae viwanja anaweza kupiga hatua kadhaa kuondoka mwanamke akimuuita tu jina jamaa ataghairi safari na kuomba arudi home fasta , Kuna siku tulifanikiwa kumnunulia pombe alipokaliza kunywa alitafuta mapipi na vitu vya kukata harufu ya bia Ili mke asigundue mshikaji kanywa , Yaani mambo yalikuwa mengi , hatukuwa na la kufanya kumnsuru mshikaji ilibidi tumtafute mama yake MZAZI aje amnusuru mwanae, baada ya kunusurika jamaa aliokoka akawa mlokole kabisa,
Tanga kule ni ufundi na mautundu tu. Sina wasiwasi nao. Mbeya huko mhh sina neno.Labda tungepata maoni kutoka kwa watu wa Tanga au Mbeya!
Niroge sweetheart, nipatie limbwata akili inikae sawa kidogo...
Hakuna uchawi ambao hauishi, inabidi uwe unarudi kilingeni kutengeneza mambo upya
Ila kuna vitu vingi vya msingi vya kuvifanyia uchawi kuliko mapenzi. Bora uroge tender zako za serikali zipite, maokoto yatoke kwa wakati, cheo kipande etc kuliko kuhangaika na mtu akupende. Waganga huwa hawasemi tu ila ukiwa unaenda na shida za mapenzi wanakuona msenge sana.
Au hilo la pili ndilo langu maana mi ni kazini then ndaniKuna limbwata tilalila yaan mtu anakua hajitambui kila analoambiwa na mkewe yeye ni yes,kuna limbwata kata mazoea,hili mtu anakua hataki mazoea na ndugu na marafiki,akitoka kazini moja kwa moja ndani!!....