Ni kweli kuna wanawake wananyota nzuri ukiwa nao au ni dhana tu?

Ukitupia tu ni tag mkuu wimbo wa taifa
 
Hii naona inaandama sana upande wa kikeni, mke akichepuka wengi mambo hukorogeka kuliko mume akichepuka sielewi kuna nini hapo kati
 
na epuka kama ukoma wanawake ambao ukimgusa tu anakukubalia

au anakufanyia vituko mnaita mitego ili tu umle,usione ngekewa chukua maamuzi

ukiwa umetuliza akili yako vizuri kabla hujapokea zawadi unayoita kutunukiwa.

Juzi nilikua natoka makumbusho,naenda zangu Kimara Njiani kufika mlimani city

nikaona dada mmoja anaambaa ambaa pembezoni mwa bara bara taratiibuu kwa maringo na mapozi kama mtu aliechoka sana anaelekea kituo cha dala dala kusubiri dala dala nadhani.

Nikaona huyu ngojea nikatangulia kituo cha daladala nikamsubiri kufika nikamuita akaitika namuuliza unaenda wapi nikusogeze,dada akaniuliza kwani wewe unaenda wapi..

nikamwambia mi naelekea kimara,akasema afadhali na mimi naelekea huko huko,nikamwambia ingia twende,kweli kachoma ndani tukaendelea kwenda.

Sina story nae mimi kimyaaa nae kimya,kufika ubungo mataaa akavunja ukimya,akasema Daaah maisha haya!? nikamuuliza maisha haya yameefanyaje?

basi tu kaka angu hivi unajua sijui hata naenda wapi,nikamwambia dada hujui unapoenda kivipi si umesema unaenda kimara? akasema nimesema tu maana hata sijui sehemu yoyote hili jiji..

namuuliza kwani wewe n mgeni,Akasema hapana n mwenyeji ila sijawahi fika huku naishi masaki (NA KWELI amekaa ki masaki haswa) Nkamwambia sasa huko kimara unaenda wapi? akabaki kimya,akasema ndio maisha yenyewe haya sijui hata naelekea wapi

hapo tunaenda tushafika korogwe akili inawaza nautuaje huu msalaba... Nilivyoutua ni Story ingine...

Baada ya pale yule dada kuachana nae tu nilishikwa kizungu zungu kimoja hicho ni kama mtu kazaba kofi la uso sioni mbele wala nyuma.

Nililala pale pale nilikuja kushtuka ni saa 11 jioni, mkasa wote huu umetokea asubuhi nilidamkia ofisi za TIGO mida ya saa nne hv ndio nmekutana na yule mdada.

Maruenge yaliyonipata baada yakuachana na yule dada sitoyasahau nikasema sasa what if ningesema nipite nae hadi home ile ONE NIGHT STAND si yangenkuta zaidi ya hili?

ki ufupi si kila mwanamke n mwanamke wengine n maroho yaliyovaa umbo la mwanamke yanatafuta watu wao na walengwa n wanaume na sumaku n SEX kupitia sex wanaume tunapotezwa sana.

siamini nikisikia msanii flani anavuta unga,kawa teja,nk ninachojua mimi watu wa namna hiyo wameyakwaa kwenye moja ya aina hyo ya wanawake ambao ndio huwaaachia mikosi.

Kataa kubali,ukiona mwanaume yeyote ana mafanikio yake kweli halali na sio yakijanja janja Wale wanaume wanaitwa Hard working MAN kubali ukatae ila nakwambia Hawa watu SEX sio kipaumbele chao na kama wana mwanamke wanae mmoja na huyo mmoja mwenyewe mpka apate chululuu n kwa mbinde.

SEX ina connection kubwa sana na mafanikio na anguko lako Mwanaume,kubali kataa bisha guna ila fatilia maisha ya wanaume wanaojiita ma player kila mwanamke n wao,fatilia utapata majibu.
 
Umemaliza yote.Unashangaa umesex na limtu kila wakati unahisi kuhukumiwa tu....Mungu nisaidie mm
 
Ni asili yenu zikiendana unapiga pesa mfano mmoja udongo mwingine maji mtafanikiwa ila mmoja asili yake udongo mwingine moto hapo hamna kitu mtafanikiwa kiwepesi
 
Ni kweli
Na wengine ni mitihani mikosi na balaa
Kuna mwanamke bar maid alikuwa misigiri Enzi za njia ya vumbi kila dereva aliye lala nae hupata ajali na kufariki
 
Hapo unaongelea hisia na uhalisia. Katika hali ya kawaida hakuna kitu kinaitwa nyota anatembea nacho mtu, nyota zinakaa angani ila lugha ya nyota hutumika kumaanisha nuru au muongozo anaobeba mtu kuhusu jambo fulani.

Kinachotokea ni kuwa unakutana na mtu ambaye anazielewa harakati zako na anakuelewa wewe potentials zako hata pale ambapo wewe haujielewi.

Imagine unakutana na mwanamke ambaye anajua muziki na anaweza kujua kipaji cha mziki hata kabla haujawahi rekodi, then huyu mwanamke anakukazia uingie studio uimbe nyimbo. Siku ukitoboa kimuziki lazima shukrani zitamuendea huyu mwanamke kwa kuwa msisitizo nyuma ya wewe kumudu kuimba na kufanya muziki vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…