Ni kweli kuonja chakula kwenye mwiko na kulia kwenye sufuria kunafanya mtu achelewe kuoa au asioe kabisa?

Ni kweli kuonja chakula kwenye mwiko na kulia kwenye sufuria kunafanya mtu achelewe kuoa au asioe kabisa?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kwamba ukiwa unaishi geto, hata wale waishio nyumbani kwa wazazi, wewe kijana wa kiume, halafu mathalani wakati unapika chakula chako ukaonja chakula kwa kutumia ule mwiko wa kupikia.

Au wakati unakula chakula, ukawa unakula mulemule kwenye masufuria ya kupikia, badala ya kupakua kwenye sahani, na unakuta mwingne hadi anakunywa kama ni supu ya maharage, rosti maini au nyama, kwa ule utamu wa kukombelezea ananyanyua sufuria na kunywa kilichobakia; sasa tulikua tukiambiwa kwa kufanya hivyo tutachelewa kuoa ama kutokuoa kabisa.

Je, kuna ukweli wowote kwenye hili wajuvi wa mambo na watafiti wa kijamii au ilikua mbinu ya kuchochea vijana kuoa na kufukuzwa nyumbani kiaina?
 
kwamba ukiwa unaishi geto, hata wale waishio nyumbani kwa wazazi.

Kwamba wewe kijana wa kiume, halafu mathalani wakati unapika chakula chako ukaonja chakula kwa kutumia ule mwiko wa kupikia....

au wakati unakula chakula, ukawa unakula mulemule kwenye masufuria ya kupikia, badala ya kupakua kwenye sahani, na unakuta mwingne hadi anakunywa kama ni supu ya maharage, rosti maini au nyama, kwa ule utamu wa kukombelezea ananyanyua sufuRia na kunywa kilichobakia...

sasa tulikua tukiambiwa kwa kufanya hivyo tutachelewa kuoa ama kutokuoa kabisa,

Je, kuna ukweli wowote kwenye hili wajuvi wa mambo na watafiti wa kijamii?🐒

au ilikua mbinu ya kuchochea vijana kuoa na kufukuzwa nyumbani kiaina🐒
Nadhani zilikuwa mbingu za malezi hasa katika kumuandaa mtoto wa kiume kuwa mwanaume imara.

Kijijini kwetu kulikuwa na usemi kuwa ukipigwa na mwiko hutakuja kuowa.

Nakumbuka bibi aliwahi kunitandika mwiko mpaka ukapasuka. Lakini nina mke na watoto na watoto kwa sasa ha ha
 
sasa tulikua tukiambiwa kwa kufanya hivyo tutachelewa kuoa ama kutokuoa kabisa,
Yaan akishaanza kucheza na masufuria tu wewe jiweke kundi la kuchelewa kuoa au kutokuoa kabisa, Mwanaume hachezi na masufuria sijui maflyinpen Mwanaume anavuta Mwali anaanza kucheza na masufuria yeye kazi yake Kula tu
 
Umekulia kijijini if yes
Watu wengi waliolelewa vijijini wanaaamini katika illusion Sana.


Jana mzee mmoja amenambia kuwa kasuku anaongea Kama BINADAMU. Anavyoongea na anatamka maneno.

Hii inafikirisha Sana Wazee wenye age 60+ na 70+ ni kizazi kinachoishi katika illusion kubwa Sana.
 
Nadhani zilikuwa mbingu za malezi hasa katika kumuandaa mtoto wa kiume kuwa mwanaume imara.

Kijijini kwetu kulikuwa na usemi kuwa ukipigwa na mwiko hutakuja kuowa.

Nakumbuka bibi aliwahi kunitandika mwiko mpaka ukapasuka. Lakini nina mke na watoto na watoto kwa sasa ha ha
Yes,
hiyo pia iko :pedroP:
 
Umekulia kijijini if yes
Watu wengi waliolelewa vijijini wanaaamini katika illusion Sana.


Jana mzee mmoja amenambia kuwa kasuku anaongea Kama BINADAMU. Anavyoongea na anatamka maneno.

Hii inafikirisha Sana Wazee wenye age 60+ na 70+ ni kizazi kinachoishi katika illusion kubwa Sana.
Ukichezea sana masufuria jiandae kuchukia kuoa sasa uoe ili ufanye nini wakati unajua kuchezea maflyinpen yako mwenyewe?
 
Umekulia kijijini if yes
Watu wengi waliolelewa vijijini wanaaamini katika illusion Sana.


Jana mzee mmoja amenambia kuwa kasuku anaongea Kama BINADAMU. Anavyoongea na anatamka maneno.

Hii inafikirisha Sana Wazee wenye age 60+ na 70+ ni kizazi kinachoishi katika illusion kubwa Sana.
Umetuweza
 
kwamba ukiwa unaishi geto, hata wale waishio nyumbani kwa wazazi.

Kwamba wewe kijana wa kiume, halafu mathalani wakati unapika chakula chako ukaonja chakula kwa kutumia ule mwiko wa kupikia....

au wakati unakula chakula, ukawa unakula mulemule kwenye masufuria ya kupikia, badala ya kupakua kwenye sahani, na unakuta mwingne hadi anakunywa kama ni supu ya maharage, rosti maini au nyama, kwa ule utamu wa kukombelezea ananyanyua sufuRia na kunywa kilichobakia...

sasa tulikua tukiambiwa kwa kufanya hivyo tutachelewa kuoa ama kutokuoa kabisa,

Je, kuna ukweli wowote kwenye hili wajuvi wa mambo na watafiti wa kijamii?🐒

au ilikua mbinu ya kuchochea vijana kuoa na kufukuzwa nyumbani kiaina🐒
Asili ya akina mama huwa wanapenda watoto wao wawe na familia. Sasa kwa upande wa watoto wao wa kiume,wakimuona ana mdu kufanya kazi za jikoni wanakuwa na imani ya kwamba ama huyu mpuuzi kwa kujua ama kupata mtelemko kwenye kuchakata na kuandaa mpaka kula chakula huenda kukapelekea asioe au achelewe kuoa.

Sasa ili wafanikishe kumfanya mtoto wao atekeleze jukumu la kuoa au kuwahi kuoa wakatengeza huo mfumo ambao hawata tumia nguvu nyingi kukusimamia bali utajisamamia mwenyewe bila shuruti.

Ni mengi sana hawa wazee wetu waliweza kuyafanya wakafanikiwa pasipo kutumia nguvu kubwa wala kuvuruga amani.

Ongeza na akina mama wajawazito kutokula mayai kwa madai kuwa wangelizaa watoto wasiokuwa na nywele lkn nia ilikuwa ni kwamba ulaji wa mayai kwa mjamzito ungelipelekea kiumbe aliyeko tumboni kunenepa na kuwa na uzito mkubwa hali ambayo ingelileta tabu wakati wa kujifungua wakati hakuna hospital wala huduma za afya.

Wewe dogo,hawa watu walikuwa na hekima kumzidi SELE mmiliki na mpenda madem licha ya kwamba yeye nduguze walifanya hujuma na kumpa medal ya mzee mwenye hekima.
 
Wewe dogo,hawa watu walikuwa na hekima kumzidi SELE mmiliki na mpenda madem licha ya kwamba yeye nduguze walifanya hujuma na kumpa medal ya mzee mwenye hekima.
Kwetu Sisi ni marufuku Mwanaume kufunua Chungu alichopika Mwanamke yaan ni Mwiko kabisa hata kulisogelea Jiko analopika Mwanamke ingawa sasa hivi wamelegeza Miiko Ila kipindi hicho ni marufuku marufuku marufuku hata km una njaa Chungu kile pale aliepika hayupo msubiri mpaka arudi akupakulie sio unachukua Sahani eti unaenda kujipakulia wewe kuoa utakusikia kwenye BOMBA umeshajiroga mwenyewe maana yake umemfunua ukamuongizia Mwiko au Upawa Mwanamke aliepika hicho chakula iwe Mama yako au Dada yako au shangazi yako ni umefanya nae matusi makubwa sana
 
Ukichezea sana masufuria jiandae kuchukia kuoa sasa uoe ili ufanye nini wakati unajua kuchezea maflyinpen yako mwenyewe?


😁😁😁 inafikirisha Sana kuoa huwa ni state of mind plus emotional sasa ukiangalia sufuria au masufuria hayana muunganiko wowote na AKILI zako wala HISIA.

Kuchukia kuoa au kupenda kuoa kunategemea zaidi na unavyoiona PICHA yako kuhusu ndoa.
 
😁😁😁 inafikirisha Sana kuoa huwa ni state of mind plus emotional sasa ukiangalia sufuria au masufuria hayana muunganiko wowote na AKILI zako wala HISIA.

Kuchukia kuoa au kupenda kuoa kunategemea zaidi na unavyoiona PICHA yako kuhusu ndoa.
Usijizoeshe kuchezea masufuria wa Mama wana akili mingi sana kuwahimiza mabinti zao wapike sio vijana wao wa kiume wapike huku mabinti wamekata sebuleni wanachezea remote yaan Dume lipo Jikoni linachezea mimoshi ndio utegemee kuoa labda km upo porini umekamata mnyamapori mbanike kula nyama sio kuchezea masufuria
 
Kwetu Sisi ni marufuku Mwanaume kufunua Chungu alichopika Mwanamke yaan ni Mwiko kabisa hata kulisogelea Jiko analopika Mwanamke ingawa sasa hivi wamelegeza Miiko Ila kipindi hicho ni marufuku marufuku marufuku hata km una njaa Chungu kile pale aliepika hayupo msubiri mpaka arudi akupakulie sio unachukua Sahani eti unaenda kujipakulia wewe kuoa utakusikia kwenye BOMBA umeshajiroga mwenyewe maana yake umemfunua ukamuongizia Mwiko au Upawa Mwanamke aliepika hicho chakula iwe Mama yako au Dada yako au shangazi yako ni umefanya nae matusi makubwa sana



Kuna ndugu yangu yeye akikuwa anapenda kupika Sana na alikuwa wakiume.

Mpaka anakuwa MTU mzima 18+ bado alikuwa anapenda Sana KUPIKA Ila mwisho wa siku ameoa na ana mke .

Fortunately , kazi inayomuingizia kipato ni upishi .

So ikiwa mtoto wa kiume anapenda kukaa jikoni na kufunua ,funua masufuria hiyo hutokana na kipaji chake cha mapishi hivyo muache mtoto afunue .
 
Usijizoeshe kuchezea masufuria wa Mama wana akili mingi sana kuwahimiza mabinti zao wapike sio vijana wao wa kiume wapike huku mabinti wamekata sebuleni wanachezea remote yaan Dume lipo Jikoni linachezea mimoshi ndio utegemee kuoa labda km upo porini umekamata mnyamapori mbanike kula nyama sio kuchezea masufuria



Wapishi wakubwa hapa Tanzania katika hotel kubwa za five star na three star ni wakiume.

MTU kupenda kukaa jikoni na kufatilia mapishi ni jambo zuri Sana.


Wamama wa kijijini na wazee wengi AKILI ndogo hutazama jambo katika jicho la ubaya na sio kuangalia FURSA.
 
Kuna ndugu yangu yeye akikuwa anapenda kupika Sana na alikuwa wakiume.

Mpaka anakuwa MTU mzima 18+ bado alikuwa anapenda Sana KUPIKA Ila mwisho wa siku ameoa na ana mke .

Fortunately , kazi inayomuingizia kipato ni upishi .

So ikiwa mtoto wa kiume anapenda kukaa jikoni na kufunua ,funua masufuria hiyo hutokana na kipaji chake cha mapishi hivyo muache mtoto afunue .
Kwetu Sisi Mila na desturi zetu Mwanaume ni Mwiko kumfunua Chungu cha mpishi wa kike ni Mwiko kabisa hio imetuhimiza tusiwe wachezea masufuria
 
Wapishi wakubwa hapa Tanzania katika hotel kubwa za five star na three star ni wakiume.

MTU kupenda kukaa jikoni na kufatilia mapishi ni jambo zuri Sana.


Wamama wa kijijini na wazee wengi AKILI ndogo hutazama jambo katika jicho la ubaya na sio kuangalia FURSA.
Baba yangu mkubwa alikua Mpishi wa Hotel kubwa TU Ila alikua amekiuka Miiko mpaka anafariki alikua hajaoa kafa Hana hata mtoto mmoja
 
Jamii yetu imegawanya majukumu ya utafutaji kwa wanaume, na malezi kwa wanawake.

Ndiyo maana ina-discourage sana wanaume kujihusisha na mambo ya jikoni.

Hiyo yako ni mojawapo tu.
 
Asili ya akina mama huwa wanapenda watoto wao wawe na familia. Sasa kwa upande wa watoto wao wa kiume,wakimuona ana mdu kufanya kazi za jikoni wanakuwa na imani ya kwamba ama huyu mpuuzi kwa kujua ama kupata mtelemko kwenye kuchakata na kuandaa mpaka kula chakula huenda kukapelekea asioe au achelewe kuoa.

Sasa ili wafanikishe kumfanya mtoto wao atekeleze jukumu la kuoa au kuwahi kuoa wakatengeza huo mfumo ambao hawata tumia nguvu nyingi kukusimamia bali utajisamamia mwenyewe bila shuruti.

Ni mengi sana hawa wazee wetu waliweza kuyafanya wakafanikiwa pasipo kutumia nguvu kubwa wala kuvuruga amani.

Ongeza na akina mama wajawazito kutokula mayai kwa madai kuwa wangelizaa watoto wasiokuwa na nywele lkn nia ilikuwa ni kwamba ulaji wa mayai kwa mjamzito ungelipelekea kiumbe aliyeko tumboni kunenepa na kuwa na uzito mkubwa hali ambayo ingelileta tabu wakati wa kujifungua wakati hakuna hospital wala huduma za afya.

Wewe dogo,hawa watu walikuwa na hekima kumzidi SELE mmiliki na mpenda madem licha ya kwamba yeye nduguze walifanya hujuma na kumpa medal ya mzee mwenye hekima.
:pedroP: :ClapHD:
 
Back
Top Bottom