Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Ni kweli kwamba Profesa Janabi hajawahi kusomea wala kuwa Daktari Bingwa wa Moyo?

Huw
Huwezi kufanya fellowship ya kuja kuwa Daktari bingwa wa moyo kama hujawahi kufanya Mmed ya internal medicine. Hiyo ndio standard ya duniani nzima, na ndio standard ya iliyopo MCT mpaka sasa.

Kama huamini, leta status ya MCT yenye kuonyesha Professor Janabi hiyo Fellowship yake imekubalika na MCT.
Kwa hiyo medicine ya Urussi sio internal medicine
 
Uk
Natamani ungesema neno kuhusu sifa/taratibu za kuwa /kusomea Udaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, maana, ndiyo Hoja hasa ya Mleta mada kuhusu Prof.
Ukimaliza miaka mitano ya udaktari unaruhusiwa kwenda kusomea udaktari bingwa

Miaka ya udaktari inatofautiana nchi na nchi

Na ukimaliza sisi tunaita masters in medicine
Mmed
 
Mama yangu alitibiwa moyo na Dr Janabi.
Daktari yoyote anaweza na anaruhusiwa kutibu moyo popote, lakini linapokuja suala la kutibu moyo kwa ngazi ya kibingwa ni daktari bingwa pekee mwenye hayo majukumu.

Ukiona Daktari ambaye sio bingwa anatoa matibabu ya kibingwa basi ujue anafanya hivyo chini ya usimamizi wa daktari bingwa. Tofauti na hapo ni makosa.

Nakuhakikishia kwa 99% kwa elimu ya kutibu moyo aliyonayo Janabi (ya kawaida mnoo) tukisema akae pale JKCI kutibu moyo yeye mwenyewe (bila kusimamiwa na madaktari bingwa waliopo pale) huenda atapaswa kuishia kumpima mgonjwa presha na mapigo ya moyo tu, kwa sababu hana sifa za kutibu moyo kibingwa.
 
Kwa hiyo medicine ya Urussi sio internal medicine
Kuna tofauti kati ya Medicine (Md) na Mmed in Internal medicine, bila kujali ya Urussi, Tz au popote pale duniani.
Moja (Md) ni degree ya kwanza ya udaktari na nyingine (Mmed in internal medicine) ni degree ya pili ya udaktari (ndio udaktari bingwa) ikijikita eneo fulani ya kutibu magonjwa fulani fulani kama moyo, ubongo, figo, maini nk.

Sijui sana, labda wajuzi zaidi watakuja kutupa mwanga zaidi.
 
Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.

View attachment 3173753
Tibalishe dk
 
Daktari yoyote anaweza na anaruhusiwa kutibu moyo popote, lakini linapokuja suala la kutibu moyo kwa ngazi ya kibingwa ni daktari bingwa pekee mwenye hayo majukumu.

Ukiona Daktari ambaye sio bingwa anatoa matibabu ya kibingwa basi ujue anafanya hivyo chini ya usimamizi wa daktari bingwa. Tofauti na hapo ni makosa.

Nakuhakikishia kwa 99% kwa elimu ya kutibu moyo aliyonayo Janabi (ya kawaida mnoo) tukisema akae pale JKCI kutibu moyo yeye mwenyewe (bila kusimamiwa na madaktari bingwa waliopo pale) huenda atapaswa kuishia kumpima mgonjwa presha na mapigo ya moyo tu, kwa sababu hana sifa za kutibu moyo kibingwa.
Ulivyoleta uzi sikukubaliana na wewe ingawa sikuchangia, ila baada ya kufuatili now naungana na wewe
 
Jamaa mjanja mjanja tu.Ndo maana kafuta post ya CV yake kule Twitter.
CV yake aliyokuwa ameiweka kule ilikuwa imejaa uongo na ujanja ujanja mnoo. Sasa wakenya, waganda na waghana walishaanza kuichambua na kuipiga spana kiasi cha kuua the whole professional credibility yake. Na bora kafanya hivyo sasa, japokuwa amechelewa sana maana inaweza kuzaa mengi mnoo.
Watu hawajui tu, academic impersonation ni kosa kubwa mnoo kimataifa, inaweza kukufutia vyeti, titles nk.
 
Ulivyoleta uzi sikukubaliana na wewe ingawa sikuchangia, ila baada ya kufuatili now naungana na wewe
Hata mimi niliposikia hii kitu kwa mara ya kwanza mahali fulani (kutoka kwa hawa wakenya ambayo wanatudharau mnoo sisi waTz) nilipinga mnoo (maana nilikuwa Pro Janabi), lakini nilipochungumza kwa kina na kuuliza baadhi ya madaktari kimya kimya nikagundua kitu tofauti kabisa. Mtazamo ukawa tofauti kabisa.
 
Mimi kilaza wa mambo ya afya naomba nikuelewe hivi mkuu:

1. Msc ya Tropical Medicine sio kigezo sahihi kinachohitajika kwa daktari kwenda ngazi ya kuja kubobea magonjwa ya moyo. Msc hiyo ni hafifu, hata Degree holder wa Pharamacology anaweza soma.

2. Ili mtu akasomee kuwa Cardiologist inabidi kwanza asome Mmed, na sio Msc.

Lakini kwa maelezo ya DR Mambo Jambo ambayo nilichanganya nikadhani Prof. Janabi ana Mmed ya Tropical Medicine kumbe ana Msc ya Tropical Health, je mtu mwenye Msc hiyo (badala ya Mmed) naye ana sifa za kubobea kwenye cardiology?

Wakuu kumbuka mwanzoni hoja ya ndugu Zanzibar-ASP ilikuwa Prof. Janabi hana Mmed ya Internal Medicine hivyo hana sifa. Kwahiyo nikataka kumtetea kuwa hana Mmed ya Internal Medicine ila ana ya Mmed ya Tropical Disease, sasa nazidi kuambiwa pia hana hiyo Mmed bali ana Msc ya Tropical Health.

Nimerudi kwenye CV yake naona MD, Msc. PhD.
Kwahiyo ndugu DR Mambo Jambo nakuuliza tena, Msc ya Tropical Health ya Prof. Janabi inafaa kuwa mbadala wa Mmed ya Tropical Medicine. Ili Zanzibar-ASP aridhike?

Update: Nimekuja kujua hapa kupitia kwa DR Mambo Jambo kuwa Mmed ile ni (Internal medicine Specified In Tropical Medicine). Mwanzoni nilijua Internal Medicine na Tropical Medicine ni vitu viwili tofauti, mnaandika kwa kifupi sana nyie waganga.
Nitakuelewesha hapa hapa baada ya kudadisi na kuhoji watu kadhaa.
Ni kitu rahisi mnoo kuelewa.

Kwa mfumo wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania unaosimamiwa na MCT, udaktari bingwa wa moyo ni ngazi ya tatu (miongoni mwa ngazi za juu kabisa) katika taaluma ya udaktari. Na mhitimu utatambulika kama superspecialist (Cardiologist). Na kufikia hiyo ngazi lazima uwe umepitia ngazi ya degree ya kwanza (bachelor) ya udaktari (Md), halafu ngazi ya degree ya pili (masters) ya udaktari (Mmed), na hapa lazima iwe Mmed in internal medicine (au Mmed in Paeditriac kama utatibu watoto moyo kibingwa)

Sasa Mmed in internal medicine ina uwanja mpana, ina mambo mengi na yote mhusika anajifunza kwa pamoja ikiwemo moyo, figo, ubongo, damu, ini, tumbo nk. Sasa Daktari akishasomea hiyo na kuhitimu anakuwa Daktari bingwa (specialist), na baada ya hapo ikitokea mhusika anataka kuwa mbobezi (super specialist) anachagua eneo moja tu na anakwenda upya kulisomea kwa kina zaidi. Akihitimu anakwenda MCT kule wanampa hiyo status ya kuwa cardiac Superspecialitist (Cardiologist)

Sasa Msc in tropical health sio sawa na Msc in Tropical medicine!. Why? Tropical health haichagui kama wewe ni Daktari (hata muuguzi anasomea) lakini Tropical medicine inajieleza kuweza kusomewa na Daktari tu, yaani Medicine.

Na Msc in Tropical medicine sio sawa Mmed in internal medicine. Kwanini? Tropical medicine ni kipengele kimoja tu katika Mmed in internal medicine ambayo imebeba vipengele vingi huenda zaidi ya vipengele 10.
 
Mara baada ya Rais Samia kutangaza kumpigia debe Professor Janabi ili kuiwakilisha Tanzania kwenye kinyang'anyiro cha ukurugenzi mkuu wa WHO kanda ya Afrika, watu wenye akili kubwa ikabidi waingie chimbo kufukua file lenye kubeba wasifu mbali mbali kumhusu Profesa Mohamed Janabi ili kuona ana kipi cha kielimu na kisayansi, na sasa imekuja kugundulika kuwa, kumbe mwamba hakuwahi kusomea udaktari bingwa wowote (Mmed) achilia mbali udaktari bingwa wa moyo (Cardiologist) na wala hana sifa zozote stahiki za kibingwa kutibu moyo.

Na kwa mifumo ya mamlaka za usimamizi wa fani ya utabibu hapa Tanzania (Medical Council of Tanganyika), daktari asiyekuwa na sifa za kibingwa za fani huzika haruhusiwi kutoa matibabu ya kibingwa moja kwa moja kwa mgonjwa, na kwa tafsiri ya moja kwa moja, Professor Janabi hakuwahi popote moja kwa moja kutibu kibingwa moyo, na kama aliwahi kufanya hivyo anastahili kushtakiwa kwenye baraza la madaktari kwa kutenda kosa la kimaadili katika fani ya udaktari.

Hapa chini nimeambanisha wasifu wa Professor Janabi wa kidaktari unaotambulika na mamlaka za usimamizi wa taaluma ya udaktari hapa Tanzania (MCT).

Mwisho kabisa, MCT wanatakiwa kutoa maelezo kwa umma, kwa hicho ulichowahi kusomea Professor Jababi (Masters of tropical health) ambacho hakina sifa yoyote ya udaktari bingwa wa moyo (maana mhitimu yoyote wa fani ya afya anaweza kusomea), kinampaje sifa mhusika kuwa daktari bingwa wa moyo?

NOTE:
Daktari bingwa mbombezi (kama daktari bingwa wa moyo) yoyote mwenye sifa stahiki za kutambulika na baraza la madaktari la Tanganyika (MCT) ni lazima utambulisho wake kwenye ukurasa rasmi wa MCT (Professional Profile status) usomeke SUPER SPECIALIST DOCTOR. Kwa Professor Janabi hakuna hicho kitu.

View attachment 3173753
Huyo ni tapeli kama matapeli wengine tu!!

Na huko WHO wanamjua vizuri. Anakwenda kuangukia pua
 
CV imeondolewa Instagram ingawa watu wamesha download! Kwanini Prof Janabi ameiondoa CV aliyoiweka mwenyewe ktk kuanza kampeni ya safari yake ya WHO! Je! Ni kweli kuna mambo hayako Sawa? Tunasubiri alete mpya tulinganishe!!!

Narudia tena kama TAIFA tunaenda kupambana na Africa nzima! Muda huu wameshachambua kila kitu kwenye taaluma ya mgombea wetu! Ni vyema busara itumike nchi isiingie
Ktk kashfa!!

Huu ni ushauri TUU ktk kuendelea kuiheshimisha mamlaka yetu tukufu! Inawezekana hii CV iliyofutwa ndiyo ilipelekwa kwa Rais na kwa kweli ilikuwa appealing!!

Queen Esther
Tuweke hapa tujifunze jinsi ya kuandika CV
 
Daktari yoyote anaweza na anaruhusiwa kutibu moyo popote, lakini linapokuja suala la kutibu moyo kwa ngazi ya kibingwa ni daktari bingwa pekee mwenye hayo majukumu.

Ukiona Daktari ambaye sio bingwa anatoa matibabu ya kibingwa basi ujue anafanya hivyo chini ya usimamizi wa daktari bingwa. Tofauti na hapo ni makosa.

Nakuhakikishia kwa 99% kwa elimu ya kutibu moyo aliyonayo Janabi (ya kawaida mnoo) tukisema akae pale JKCI kutibu moyo yeye mwenyewe (bila kusimamiwa na madaktari bingwa waliopo pale) huenda atapaswa kuishia kumpima mgonjwa presha na mapigo ya moyo tu, kwa sababu hana sifa za kutibu moyo kibingwa.
Mkuu nilikuwa najibu post uliyoweka kwa maneno yako mwenyewe hii hapa chini. Rudi ukarekebishe huu uzushi ufanye uungwana. 👇🏽👇🏽

Jibu ni NO.
Professor Janabi hajawahi kusomea hicho kitu, hana huo ujuzi, hajawahi kutambuliwa kuwa na hiyo sifa hapa Tz, na huwa hatibu hicho kitu. Kama huamini fika JKCI halafu uulize ni lini alitibu moyo katika level ya kibingwa?
 
Back
Top Bottom