Ni kweli Papa Wemba kauawa na sumu iliyowekwa kwenye Mic?

Ni kweli Papa Wemba kauawa na sumu iliyowekwa kwenye Mic?

Ni hisia tu zisizo na mashiko....huyo jamaa kama ni fundi wa sound sioni kuna ajabu gani akawa anahangaika na mic zake....

Kuitoa mic baada ya Papaa kuanguka ni labda kuona tu inahitajika nafasi eneo lile......

Isitoshe tumeshaambiwa Papaa alitoka kuumwa muda si mrefu, so sioni kwa nini kunazuka sintofahamu.
 
Ni hisia tu zisizo na mashiko....huyo jamaa kama ni fundi wa sound sioni kuna ajabu gani akawa anahangaika na mic zake....

Kuitoa mic baada ya Papaa kuanguka ni labda kuona tu inahitajika nafasi eneo lile......

Isitoshe tumeshaambiwa Papaa alitoka kuumwa muda si mrefu, so sioni kwa nini kunazuka sintofahamu.
Fundi wa mic ananyata???we huoni akinyata??hata hiyo picha huoni akirudisha mic kwa kunyata???
Huoni anavyoweka mic kwa mashaka??
 
Fundi wa mic ananyata???we huoni akinyata??hata hiyo picha huoni akirudisha mic kwa kunyata???
Huoni anavyoweka mic kwa mashaka??
Hiyo video ipo kwa slow motion kaka....

Na kama umeshahudhuria shughuli mbalimbali utaona huwa wanatembea tu kwa tahadhari kwamba wasisumbue waliopo stejini...nimeshaona hivyo sehemu nyingi tu...

Mwaka jana nilikuwa Zanzibar kwenye tamasha la filamu nilishtuka kuona mtu anatoka nyuma ya steji kwa kuunyata mpaka nilipomuona ameenda ku adjust urefu wa mic pale stejini.
 
Nadhani hii habari wanaikuza Sana ukweli ni Heart failure ndo kilichomuondoa na si kuuliwa.
Papa Wemba alikuwa mgonjwa na Dr.wake ali suggest apumzike lakini alipuuza. Ifike mahali tuangalie mambo mengine kiupana zaidi tuache kuendeshwa na hisia.
 
Pole sana Mkuu kwa kuwa na mashaka ya Kifo cha Jules Shungu Kikumba Pene Wembandio alias PAPA WEMBA na pole pia kwa wale wote walioguswa na huu msiba wa JABALI la Afrika ambalo lilibaki la Kizazi cha kwanza baada ya Franco, Tabu Ley, Kabasele Yampanya PEPE KALLE, Madilu System.

Ukweli wa sababu ya Kifo chake ni MSHTUKO wa MOYO kwani imegundulika kuwa wiki moja kabla ya kwenda Abidjan alikuwa anaumwa sana BP na alipewa tiba ambayo ilimlazimu apumzike kwa angalau wiki mbili ndipo arejee kuendelea na muziki lakini mara baada ya PAPA WEMBA kuona kapata nafuu na huku tena Watu wa Kundi la Muziki maarufu ya nchini Ivory Coast la MAGIC SYSTEM ambao ndiyo walikuwa waandaji wakuu wa lile TAMASHA kumpelekea mwaliko aliona asikose kwenda kwani alitaka kuitumia hiyo siku pia kutambulisha album yake.

Kwa mnaoingia sana katika kumbi za muziki nadhani mnatambua aina ya sauti kubwa ambayo inaambata na mitambo mikubwa kabisa na spika za kufa mtu ambazo zinapiga kiasi kwamba kama una matatizo ya kushtuka kwa moyo au kisukari huwezi kukaa pale hivyo hata Marehemu PAPA WEMBA wakati amepanda pale stejini huku akiwa ana siku tano tu tokea atoke kwa Daktari wake kwa matatizo ya moyo ilikuwa ni dhahiri kuwa ile sound set up ya pale ingemuathiri.

Kujibu swali lako kwamba labda aliwekewa SUMU baada ya kuona yule Mtu anakuja kuitoa ile Mic pale na baadae kurudi na nyingine si kweli kwamba ni SUMU bali kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi huwa na Mic yake MAALUM ambayo husetiwa KIUTAALAM sana na Band Sound System Engineer na hufanyiwa test mara kwa mara ili Bwana mkubwa akipanda nayo tu pale mbele isimumsumbue na huwa haiwi moja bali huwa mbili.

Na pia tambua kuwa kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi hasa za Kikongo huwapa jukumu MAALUM watu wanaowaamini sana na mno la kukaa au kutunza hizi mic ili kuepuka hujuma kwani kwa msiojua hakuna Watu ambao huwa Wanarogana katika muziki kama Wakongo na ikumbukwe kuna wakati Werrason alimchezea mchezo JB Mpiana katika TAMASHA ambapo katika huo Uwanja kulinyesha mvua kubwa sana lakini cha kushangaza pembezoni na huo uwanja JUA KALI lilikuwa linawaka ( mfano wake ni kwamba pale ukumbi wa Diamond Jubilee sasa pawe wazi halafu inyeshe mvua kubwa lakini maeneo ya jirani kama Makao Makuu ya SKAUTI, Makao Makuu ya Jeshi, Shule ya Msingi ya Muhimbili na yale maeneo mengine kote kuwe na jua kali na linawaka kisawasawa ) hivyo kupelekea JB Mpiana kutofanya onyesho lake na alipokuja kugundua kuwa alifanyiwa ule mchezo na Werrason na yeye JB Mpiana akalipiza ambapo siku moja Werrason na bendi yake ya Maison Mere walikuwa na onyesho lao na cha kushangaza kila Werrason akishika Mic sauti haitoki lakini akiondoa tu ile Mic sauti inarudi na hata alipobadilishiwa Mic zingine tatizo lilikuwa ni lile lile hali ambayo ilipelekea sasa vipande vyote vya uimbaji vya Werrason aviimbe mwanamuziki wake aitwae Herritier lakini cha moto alikiona.

Mshika Mic mkuu wa Koffi Olomide ni yule Mkewe wa sasa aitwae Cindy ambaye ni Mwanamuziki wake pia japo hapo kabla mshika Mic wake alikuwa ni yule muimbaji aitwae Gibson a.k.a Kardinale huku mshika Mic mkuu wa Werrason ni yule mpiga drums wake maarufu aitwae PAPII KAKOL huku JB Mpiana mshika Mic wake mkuu akiwa ni Rapa wake kipenzi aitwae Gentamycine au Antibiotique Lisimo. Hao washika Mic wao wote ndiyo Watu ambao WANAAMINIKA nao kuliko Mtu yoyote katika bendi zao zote hizo na ndiyo wenye sauti kuu pia ya KIMAAMUZI ndani ya hizo bendi za hao MANGULI wa muziki tajwa hapo hivyo kuwekewa SUMU ni jambo gumu mno Mkuu na hawa jamaa Wakongo wanajilinda na vingi na hasa hasa ni NDUMBA.
Mkuu unaonekana unajua sana mambo ya wanamuziki waki kongo,hivi yule Gibson wa Koffi yupo wapi siku hizi?
 
Kwanza gentamycine hongera zako umeeleza kwa kina unachokijua na uhalisia wa jambo na pana watu wengi wameyaelewa maelezo yako.
Kuhusu hili la kunyata limenikumbusha miaka ya nyuma refarii akiongea na wachezaji wa timu pinzani kisha I katokea timu nyingine kufungwa utasikia wachezaji na mashabiki wao wakisema refa alikuwa anaongea nao kabisa.So kimsingi kama watu wabaya wangekuwa na nafasi nyingi za kumuua nasi pale uwanjani kwa Sumu ambayo hata mletaji ingeanza kumuondoa yeye au alikuwa na patriot?maana sadamu husein alikuwa akitupa scud marekani wanatuma patriot kuizuia.
 
Mkuu unaonekana unajua sana mambo ya wanamuziki waki kongo,hivi yule Gibson wa Koffi yupo wapi siku hizi?

Aliachana na Koffi Olomide na kuwa katika mpango wa kuanzisha Bendi yake na bado hajafanikiwa kihivyo na sasa inasemekana anataka kujiunga na Mwimbaji mwenzie aitwae Solei Wanga ambaye anafanya vizuri kiasi. Tatizo la Wanamuziki wa DR Congo wanadhani kila Mtu tu anaweza kuanzisha Bendi yake kwakuwa tu wameshakuwa na majina huku Wakisahau kuwa hao wanaowaiga akina Koffi, JB na Werrason wameingia MAAGANO makali sana ya KISHIRIKINA ambayo nisingependa kuyaweka hapa HADHARANI kwani mnaweza MKAOGOPA na hata KUWACHUKIA. Hata hivyo hao Wanamuziki wote wakishindwa huko waendapo hurudi kwa hawa Wakubwa zao waliowakuza. Kwa mfano Mwanamuziki mwingine wa Bendi hiyo hiyo ya Quarter Latin ya Koffi Olomide aitwae Shela Mputu aliondoka kwa Koffi kwa NYODO sana ila sasa anampigia magoti Koffi arudi kundini ila Koffi kampotezea.
 
Aliachana na Koffi Olomide na kuwa katika mpango wa kuanzisha Bendi yake na bado hajafanikiwa kihivyo na sasa inasemekana anataka kujiunga na Mwimbaji mwenzie aitwae Solei Wanga ambaye anafanya vizuri kiasi. Tatizo la Wanamuziki wa DR Congo wanadhani kila Mtu tu anaweza kuanzisha Bendi yake kwakuwa tu wameshakuwa na majina huku Wakisahau kuwa hao wanaowaiga akina Koffi, JB na Werrason wameingia MAAGANO makali sana ya KISHIRIKINA ambayo nisingependa kuyaweka hapa HADHARANI kwani mnaweza MKAOGOPA na hata KUWACHUKIA. Hata hivyo hao Wanamuziki wote wakishindwa huko waendapo hurudi kwa hawa Wakubwa zao waliowakuza. Kwa mfano Mwanamuziki mwingine wa Bendi hiyo hiyo ya Quarter Latin ya Koffi Olomide aitwae Shela Mputu aliondoka kwa Koffi kwa NYODO sana ila sasa anampigia magoti Koffi arudi kundini ila Koffi kampotezea.
Na allan mpela(afande imeishia vp na jb kuna wakati nilisikia alitaka kurudi bcbg?
 
Na allan mpela(afande imeishia vp na jb kuna wakati nilisikia alitaka kurudi bcbg?

Alain Mpela " Afande " ni kweli anataka kurudi BCBG na alikuwa ni kipenzi mkubwa sana wa JB Mpiana na hata katika nyimbo zote za rhumba ( za taratibu ) za Wenge Musica BCBG kama OMBA na JEANNETE JB Mpiana humuimba mno Alain Mpela huku akitaka hata kulia kwani alimpenda sana na alimkuza mwenyewe. Kikwazo kikubwa sasa cha Alain Mpela kurudi kundini ni kwakuwa tayari nafasi yake imezibwa vizuri mno na Mwanamuziki Bishoo na fundi wa kuchezea sauti aitwae Jean Didier Loko JDL a.k.a Tramendou lakini kama pia haitoshi Alain Mpela wakati akitoka BCBG alikuwa ndiyo Kiongozi wa Wanamuziki wa Bendi ( Directoreire de artiste ) nafasi ambayo sasa JB Mpiana kampa Mwanamuzi Mkongwe na ambaye ndiyo anatunga nyimbo karibia 85% za Wenge Musica BCBG na pia anapanga mashairi na anatengeneza mistari yote ya nyimbo aitwae Jules Kibens a.k.a Le Professeur a.k.a Molongeshi hivyo JB Mpiana anaogopa kumrudisha Alain Mpela Afande asije akaleta chuki za kimadaraka kundini. Kwa faida yako / yenu huyu Mwanamuziki Jules Kibens ni Mwalimu cha Lugha wa Chuo Kikuu cha Kinshasa na ni mtaalam sana wa lugha ya Kifaransa na kile Kifaransa sanifu unachokisia kikiimbwa katika nyimbo nyingi za Wenge Musica BCBG kimetengenezwa na Jules Kibens.
 
Aliachana na Koffi Olomide na kuwa katika mpango wa kuanzisha Bendi yake na bado hajafanikiwa kihivyo na sasa inasemekana anataka kujiunga na Mwimbaji mwenzie aitwae Solei Wanga ambaye anafanya vizuri kiasi. Tatizo la Wanamuziki wa DR Congo wanadhani kila Mtu tu anaweza kuanzisha Bendi yake kwakuwa tu wameshakuwa na majina huku Wakisahau kuwa hao wanaowaiga akina Koffi, JB na Werrason wameingia MAAGANO makali sana ya KISHIRIKINA ambayo nisingependa kuyaweka hapa HADHARANI kwani mnaweza MKAOGOPA na hata KUWACHUKIA. Hata hivyo hao Wanamuziki wote wakishindwa huko waendapo hurudi kwa hawa Wakubwa zao waliowakuza. Kwa mfano Mwanamuziki mwingine wa Bendi hiyo hiyo ya Quarter Latin ya Koffi Olomide aitwae Shela Mputu aliondoka kwa Koffi kwa NYODO sana ila sasa anampigia magoti Koffi arudi kundini ila Koffi kampotezea.
Nashukuru kwa kunijuza kuhusu Gibson wa Koffi,na Soleil Wanga namfahamu ni yule mrefu mweusi naye huwa anaimba ana kasauti fulani hivi,na kuna wakati alibleach ndevu zake,lakini mkuu mbona umezungumzia wanamuziki vijana kushindwa kutusua kama walivyotusua kina Ngiama Makanda na JB itakua vigumu kwao ,lakini umewasahau watu kama Fally na Ferre Gola mbona wao wametokea hapo hapo kwa kina Koffi na wapo juu hasa Fally kwa mtazamo wangu namuona yupo juu sana,hawa je? na wao wana maagano?.
 
Waswahili banah! Kila kifo lazima atafutwe mchawi. Ndio maana wabibi wanateketea huko Shinyanga na Mwanza kwa sababu za kipumbavu kama huu uvumi unaosambaa kuhusu kifo cha Papa Wemba.
 
Pole sana Mkuu kwa kuwa na mashaka ya Kifo cha Jules Shungu Kikumba Pene Wembandio alias PAPA WEMBA na pole pia kwa wale wote walioguswa na huu msiba wa JABALI la Afrika ambalo lilibaki la Kizazi cha kwanza baada ya Franco, Tabu Ley, Kabasele Yampanya PEPE KALLE, Madilu System.

Ukweli wa sababu ya Kifo chake ni MSHTUKO wa MOYO kwani imegundulika kuwa wiki moja kabla ya kwenda Abidjan alikuwa anaumwa sana BP na alipewa tiba ambayo ilimlazimu apumzike kwa angalau wiki mbili ndipo arejee kuendelea na muziki lakini mara baada ya PAPA WEMBA kuona kapata nafuu na huku tena Watu wa Kundi la Muziki maarufu ya nchini Ivory Coast la MAGIC SYSTEM ambao ndiyo walikuwa waandaji wakuu wa lile TAMASHA kumpelekea mwaliko aliona asikose kwenda kwani alitaka kuitumia hiyo siku pia kutambulisha album yake.

Kwa mnaoingia sana katika kumbi za muziki nadhani mnatambua aina ya sauti kubwa ambayo inaambata na mitambo mikubwa kabisa na spika za kufa mtu ambazo zinapiga kiasi kwamba kama una matatizo ya kushtuka kwa moyo au kisukari huwezi kukaa pale hivyo hata Marehemu PAPA WEMBA wakati amepanda pale stejini huku akiwa ana siku tano tu tokea atoke kwa Daktari wake kwa matatizo ya moyo ilikuwa ni dhahiri kuwa ile sound set up ya pale ingemuathiri.

Kujibu swali lako kwamba labda aliwekewa SUMU baada ya kuona yule Mtu anakuja kuitoa ile Mic pale na baadae kurudi na nyingine si kweli kwamba ni SUMU bali kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi huwa na Mic yake MAALUM ambayo husetiwa KIUTAALAM sana na Band Sound System Engineer na hufanyiwa test mara kwa mara ili Bwana mkubwa akipanda nayo tu pale mbele isimumsumbue na huwa haiwi moja bali huwa mbili.

Na pia tambua kuwa kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi hasa za Kikongo huwapa jukumu MAALUM watu wanaowaamini sana na mno la kukaa au kutunza hizi mic ili kuepuka hujuma kwani kwa msiojua hakuna Watu ambao huwa Wanarogana katika muziki kama Wakongo na ikumbukwe kuna wakati Werrason alimchezea mchezo JB Mpiana katika TAMASHA ambapo katika huo Uwanja kulinyesha mvua kubwa sana lakini cha kushangaza pembezoni na huo uwanja JUA KALI lilikuwa linawaka ( mfano wake ni kwamba pale ukumbi wa Diamond Jubilee sasa pawe wazi halafu inyeshe mvua kubwa lakini maeneo ya jirani kama Makao Makuu ya SKAUTI, Makao Makuu ya Jeshi, Shule ya Msingi ya Muhimbili na yale maeneo mengine kote kuwe na jua kali na linawaka kisawasawa ) hivyo kupelekea JB Mpiana kutofanya onyesho lake na alipokuja kugundua kuwa alifanyiwa ule mchezo na Werrason na yeye JB Mpiana akalipiza ambapo siku moja Werrason na bendi yake ya Maison Mere walikuwa na onyesho lao na cha kushangaza kila Werrason akishika Mic sauti haitoki lakini akiondoa tu ile Mic sauti inarudi na hata alipobadilishiwa Mic zingine tatizo lilikuwa ni lile lile hali ambayo ilipelekea sasa vipande vyote vya uimbaji vya Werrason aviimbe mwanamuziki wake aitwae Herritier lakini cha moto alikiona.

Mshika Mic mkuu wa Koffi Olomide ni yule Mkewe wa sasa aitwae Cindy ambaye ni Mwanamuziki wake pia japo hapo kabla mshika Mic wake alikuwa ni yule muimbaji aitwae Gibson a.k.a Kardinale huku mshika Mic mkuu wa Werrason ni yule mpiga drums wake maarufu aitwae PAPII KAKOL huku JB Mpiana mshika Mic wake mkuu akiwa ni Rapa wake kipenzi aitwae Gentamycine au Antibiotique Lisimo. Hao washika Mic wao wote ndiyo Watu ambao WANAAMINIKA nao kuliko Mtu yoyote katika bendi zao zote hizo na ndiyo wenye sauti kuu pia ya KIMAAMUZI ndani ya hizo bendi za hao MANGULI wa muziki tajwa hapo hivyo kuwekewa SUMU ni jambo gumu mno Mkuu na hawa jamaa Wakongo wanajilinda na vingi na hasa hasa ni NDUMBA.
Mkuu uko deep, big up!
 
Kusema ukweli sijapata nafasi ya kuitizama ila kidogo Mkuu wangu nina uzoefu na hawa Wanamuziki hasa wa miziki hii ya dansi ya Kikongo na hata hapa kibongo bongo kwa hizi bendi zetu pia. Sitaki uamini 100% yale maelezo yangu kwani yawezekana ikawa ni Sumu kama usemavyo ila nimekuelezea tu kwa uzoefu wangu na ni ngumu mno kuwekewa SUMU katika Mic anayoenda kutumia isipokuwa ungeniambia kuwa alifanyiwa UCHAWI ningekuamini kwa asilimia zote kwani hakuna Mwanamuziki unayemjua Wewe wa DR Congo ambaye HAROGI. Kuna siku nitakuja na UZI hapa nikuambie UCHAWI wa wote hao hasa hasa Koffi Olomide, JB Mpiana, Werrason, Roga Roga wa Bendi ya Extra Musica, Zaiko Langa Langa, Hayati Pepe Kalle, Hayati Madilu System na hawa vijana wa sasa wawili Fally Ipupa na mwenzake Fere Gola. Mkuu nikikuambia wanayoyafanya unaweza hata ukaogopa kulala au ukazichukua dvd zao hapo ulipo sasa na ukazichoma moto! Wanamuziki ambao najua walikuwa HAWAROGI ni Hayati Franco na Hayati Tabu Ley pekee.
Mkuu gentamycine embu tuambie bana uchaw wa hao jamaa wengine please ama PM mkuu nami nawafatilia ila upande huo sjawah kupagusa ila nlisikaga tena majuz tu juu ya uchaw wa koffi olomide ingawa sjaamini mkuu..
 
Pole sana Mkuu kwa kuwa na mashaka ya Kifo cha Jules Shungu Kikumba Pene Wembandio alias PAPA WEMBA na pole pia kwa wale wote walioguswa na huu msiba wa JABALI la Afrika ambalo lilibaki la Kizazi cha kwanza baada ya Franco, Tabu Ley, Kabasele Yampanya PEPE KALLE, Madilu System.

Ukweli wa sababu ya Kifo chake ni MSHTUKO wa MOYO kwani imegundulika kuwa wiki moja kabla ya kwenda Abidjan alikuwa anaumwa sana BP na alipewa tiba ambayo ilimlazimu apumzike kwa angalau wiki mbili ndipo arejee kuendelea na muziki lakini mara baada ya PAPA WEMBA kuona kapata nafuu na huku tena Watu wa Kundi la Muziki maarufu ya nchini Ivory Coast la MAGIC SYSTEM ambao ndiyo walikuwa waandaji wakuu wa lile TAMASHA kumpelekea mwaliko aliona asikose kwenda kwani alitaka kuitumia hiyo siku pia kutambulisha album yake.

Kwa mnaoingia sana katika kumbi za muziki nadhani mnatambua aina ya sauti kubwa ambayo inaambata na mitambo mikubwa kabisa na spika za kufa mtu ambazo zinapiga kiasi kwamba kama una matatizo ya kushtuka kwa moyo au kisukari huwezi kukaa pale hivyo hata Marehemu PAPA WEMBA wakati amepanda pale stejini huku akiwa ana siku tano tu tokea atoke kwa Daktari wake kwa matatizo ya moyo ilikuwa ni dhahiri kuwa ile sound set up ya pale ingemuathiri.

Kujibu swali lako kwamba labda aliwekewa SUMU baada ya kuona yule Mtu anakuja kuitoa ile Mic pale na baadae kurudi na nyingine si kweli kwamba ni SUMU bali kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi huwa na Mic yake MAALUM ambayo husetiwa KIUTAALAM sana na Band Sound System Engineer na hufanyiwa test mara kwa mara ili Bwana mkubwa akipanda nayo tu pale mbele isimumsumbue na huwa haiwi moja bali huwa mbili.

Na pia tambua kuwa kila Mwanamuziki Kiongozi wa Bendi hasa za Kikongo huwapa jukumu MAALUM watu wanaowaamini sana na mno la kukaa au kutunza hizi mic ili kuepuka hujuma kwani kwa msiojua hakuna Watu ambao huwa Wanarogana katika muziki kama Wakongo na ikumbukwe kuna wakati Werrason alimchezea mchezo JB Mpiana katika TAMASHA ambapo katika huo Uwanja kulinyesha mvua kubwa sana lakini cha kushangaza pembezoni na huo uwanja JUA KALI lilikuwa linawaka ( mfano wake ni kwamba pale ukumbi wa Diamond Jubilee sasa pawe wazi halafu inyeshe mvua kubwa lakini maeneo ya jirani kama Makao Makuu ya SKAUTI, Makao Makuu ya Jeshi, Shule ya Msingi ya Muhimbili na yale maeneo mengine kote kuwe na jua kali na linawaka kisawasawa ) hivyo kupelekea JB Mpiana kutofanya onyesho lake na alipokuja kugundua kuwa alifanyiwa ule mchezo na Werrason na yeye JB Mpiana akalipiza ambapo siku moja Werrason na bendi yake ya Maison Mere walikuwa na onyesho lao na cha kushangaza kila Werrason akishika Mic sauti haitoki lakini akiondoa tu ile Mic sauti inarudi na hata alipobadilishiwa Mic zingine tatizo lilikuwa ni lile lile hali ambayo ilipelekea sasa vipande vyote vya uimbaji vya Werrason aviimbe mwanamuziki wake aitwae Herritier lakini cha moto alikiona.

Mshika Mic mkuu wa Koffi Olomide ni yule Mkewe wa sasa aitwae Cindy ambaye ni Mwanamuziki wake pia japo hapo kabla mshika Mic wake alikuwa ni yule muimbaji aitwae Gibson a.k.a Kardinale huku mshika Mic mkuu wa Werrason ni yule mpiga drums wake maarufu aitwae PAPII KAKOL huku JB Mpiana mshika Mic wake mkuu akiwa ni Rapa wake kipenzi aitwae Gentamycine au Antibiotique Lisimo. Hao washika Mic wao wote ndiyo Watu ambao WANAAMINIKA nao kuliko Mtu yoyote katika bendi zao zote hizo na ndiyo wenye sauti kuu pia ya KIMAAMUZI ndani ya hizo bendi za hao MANGULI wa muziki tajwa hapo hivyo kuwekewa SUMU ni jambo gumu mno Mkuu na hawa jamaa Wakongo wanajilinda na vingi na hasa hasa ni NDUMBA.
nimekuelewa Fulani ivi kama ingekuwa we ni wakili wa mtuhumiwa ni dhahir umeshinda kesi mkuu
 
Kusema ukweli sijapata nafasi ya kuitizama ila kidogo Mkuu wangu nina uzoefu na hawa Wanamuziki hasa wa miziki hii ya dansi ya Kikongo na hata hapa kibongo bongo kwa hizi bendi zetu pia. Sitaki uamini 100% yale maelezo yangu kwani yawezekana ikawa ni Sumu kama usemavyo ila nimekuelezea tu kwa uzoefu wangu na ni ngumu mno kuwekewa SUMU katika Mic anayoenda kutumia isipokuwa ungeniambia kuwa alifanyiwa UCHAWI ningekuamini kwa asilimia zote kwani hakuna Mwanamuziki unayemjua Wewe wa DR Congo ambaye HAROGI. Kuna siku nitakuja na UZI hapa nikuambie UCHAWI wa wote hao hasa hasa Koffi Olomide, JB Mpiana, Werrason, Roga Roga wa Bendi ya Extra Musica, Zaiko Langa Langa, Hayati Pepe Kalle, Hayati Madilu System na hawa vijana wa sasa wawili Fally Ipupa na mwenzake Fere Gola. Mkuu nikikuambia wanayoyafanya unaweza hata ukaogopa kulala au ukazichukua dvd zao hapo ulipo sasa na ukazichoma moto! Wanamuziki ambao najua walikuwa HAWAROGI ni Hayati Franco na Hayati Tabu Ley pekee.


mmh! wewe ni mtangazaji wa radio one bisha usibishe tena yule baba wa hawavumi lakini wamo. time will tell
 
Back
Top Bottom