Ni kweli Tanga ndipo mapenzi yalipozaliwa au tunapigwa?

Ni kweli Tanga ndipo mapenzi yalipozaliwa au tunapigwa?

Farolito

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
12,001
Reaction score
27,175
Wakuu,

Kumekuwa na nguvu kubwa sana kuwaaminisha watu kwamba Tanga ndipo hasa 'yalipozaliwa mapenzi' au kwa maana nyingine ndio makao makuu ya mapenzi hapa Tanzania.

Hii imekuwa ikichagizwa zaidi na nyimbo za wasanii kama yule Bwana Misosi aliyeimba 'mabinti wa Kitanga' huku akiwapa sifa lukuki kuelezea uwezo wa katika tasnia ya mapenzi.

Pia kumekuwepo misemo kadhaa kama huu wa 'Tanga waja leo kuondoka majaliwa' yote kuonyesha kwamba mwanaume akijichanganya kwa binti wa Kitanga basi hawezi kurudi tena kutokana na kupewa mahaba ya hali ya juu ikiwemo kuogeshwa kwa maji ya Iliki na Mdalasini huku akibebwa mgongoni kwenda bafuni na kurudishwa nakadhalika.

Kwenye kipindi cha Valentine's mwaka huu kuna media fulani walikuwa wakirudia rudia sana kwamba Tanga ndipo mapenzi yalipozaliwa na waliandaa mpaka tour ya kwenda huko.

Je ni kweli mabinti wa Ki-Tanga ndio wanayamudu mapenzi kuliko mikoa yote Tanzania au ni kwamba wao ni wabingwa wa 'kupuliza' ili mwanaume asifurukute?

Ili tujue ukweli wa hili tupate majibu ya maswali haya;

1. Je, Tanga inaongoza kuwa na ndoa zinazodumu hapa Tanzania?

2. Je, mabinti wa Kitanga ndio wanaoongoza kuolewa zaidi kuliko mabinti wa mikoa mingine?

3. Je, mabinti wa Kitanga ndio wanaodumu kwenye ndoa zaidi hapa Tanzania?

4. Je, wanaposema Tanga ndipo mapenzi yalipozaliwa,Je na wanaume wa huko nao ni wajuzi katika mapenzi au ni wanawake tu,maana hatusikii wakizungumzwa?

Kwa Mliowahi kuishi /mnaishi Tanga au mliooa mabinti wa Kitanga tunaomba ukweli wa hili.

Asante.

N:B Jibu kwa namba ya swali.

View attachment 2152729

kanga%2Bmoko.jpg


JamiiForums-427266087.jpg


JamiiForums-1482012616.jpg
 
Ni maneno tu vinginevyo iwe kwa wachache tu. Maana sijawahi ogeshwa wala kupakwa mafuta; kubebwa anabebwa mtoto tu. Hizo chapati kama hapo juu sijawahi ziona kwangu
Aisee,tunaendelea kukusanya ushahidi maana tunaambiwa huko ndio kuna mafundi wa mapenzi eti
 
Overrated kwanza wanawake wa tanga hawanga misambwanda..wengi wamepigwa pass.

Myb mapishi naweza wakubali.

#MaendeleoHayanaChama
Sasa hii kauli kwamba huko ndio mapenzi yalipozaliwa ilitoka wapi?
 
Tanga hamna kitu kipya vinavyopatikana huko vinapatikana kanda yote ya Pwani.
 
Aisee,tunaendelea kukusanya ushahidi maana tunaambiwa huko ndio kuna mafundi wa mapenzi eti
Hizi stori za miaka ya 80 hadi 99 ambapo watu wengi walikuwa hawasafiri-sasa wale wachache waliobahatika kufika huko au kukutana na watanga waliwalisha watu matangopori.
 
Huku ndio kwenyewe washamba na wapumbavu wivu utawaua ndo wanaponda wanawake wanajielewa kwanza kwa nafasi yao hawana mambo sijui 50/50 kama kenge wa bara
 
Sasa kwanini sifa zote ziende Tanga?
Watu wanaotoka bara ndio wakija huku wanaona mambo mapya hivyo huwapaisha, pia inachochewa na jitihada kubwa inayofanywa na wazawa kuisifia Tanga kama chimbuko la mapenzi ila kiuhalisia hakuna jipya huko.
 
Tanga iko overrated alafu mtwara Kwa wamakonde iko underrated..Tukirudi nyuma wamakonde walichukuliwa wakapelekwa Tanga kwenda kulima katani(mkonge),na wengi wao hawakurudi tena mtwara.Kuna uwezekano wamakonde ndy waliwafundisha hao wenyeji hayo mambo

Kwenye chakula nawapa yes..wanawake wa Tanga ni mafundi wa mapishi,sijui majirani zao wa pale mlima mrefu wanakwama wapi!! Si wakapige chabo Tanga?

Mleta mada umewahi kwenda mikoa ya kusini Lindi na mtwara? Huko wanawake wanakatika viuno Feni inasubiri,na ukiwa mzembe kitandani wnakuaibisha

Ndugu yangu ndege JOHN anajua hbr ya wanawake wa Lindi na mtwara,ngoja aje kutoa ushuhuda..karibu shehe wangu ndege JOHN [emoji28]
 
Back
Top Bottom