Ni kweli TISS hawafahamiani na hawaaminiani?

Ni kweli TISS hawafahamiani na hawaaminiani?

Mbona hata members wa jamiiforums ni tiss kwan humu kuna mtu ananijua naitwa nani? nakaa wapi? umri wangu? Watoto wangapi? Wake wa ngap? Kazi yangu? Tupige kifua wana jf tuseme na sisi tiss
 
Mambo mengine yanawapa shida bureee!! Hebu achana na hao sijui usalama!

Fanya shughuli zako au jadili akina diamond na Tanasha!

Kwanza hawapo hao watu wa usalama [emoji23][emoji23][emoji23][emoji1635][emoji1635][emoji481][emoji1634][emoji482][emoji482]

Sent using Jamii Forums mobile app
..atafute tu hela hata khabari ya daimondi na dona wake aachane nazo hazimsaidii kabsaaa
 
Kuna wanaojuana, kuna wasiojuana, kuna wanao-wafanyia ujasusi wenzao uku nao wakifanyiwa ujasusi bila kuwajua wanaowafanyia ujasusi, kuna wanaofanyishwa kazi za usalama bila wao kujijua, iwe kwenye siasa, biashara, dini kote wapo majasusi.

Tatizo la ujasusi wa bongo umejikita kwenye kukusanya taarifa zaidi za mambo mbali mbali kusaidia utawala uliopo madarakani tofauti na wenzetu ambao wanajikita sana kwenye kuzuia hatari zote mbaya zizazohusu uchumi na siasa bila kuegemea upande wowote wa kisiasa.

TISS wanatakiwa kujikita kwenye ujasusi wa kiuchumi jinsi ya kutengeneza mabilionea, jinsi ya kupigana vita ya kiuchumi na mataifa jirani, kuhakikisha taarifa za kiujasusi wanazokusanya zinafanyiwa kazi haraka bila kuegemea upande wowote.
.....
 
Muundo wa TISS umeharibiwa Sana na CCM , Tz idara hii inayumba Sana undugu na ukabila umejaa Sana, ethics zote zimeporomoka!!

Swala la kujuana inategemea kitengo, si wote wanaojuana inategemea kitengo chako!!!

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
Hii Code ya Mwisho nimeielewa 😂😂
 
TISS imekuja kuharibiwa wakati wa Awamu ya 4. Ukabila na kujuana umeletwa na JK, watu walikuwa wanapewa kazi hata ambao hawana sifa. Baada ya JK kuona ameharibu hii idara ndipo akaanzisha kitengo ambacho alikuwa anawajua yeye tu labda na watu waliokuwa karibu nae ki protocol. Hapo ndipo TISS iligawanyika wakaanza kuogopana.

God save us
Inaitwa Deep State kwa lugha rahisi
 
Wanabodi, weekend hiyooo na kamvua kwa mbali hapa Arusha!

Nipo Triple A hapa. Kuna jamaa yangu ananiambia eti wana usalama/TISS hawafahamiani na hawaaminiani kabisa!

Yaani kila mmoja ana majukumu yake na mahala pa kureport. Hawana mazoea ya mwenzangu uko wapi, unafanya nini!

Hawaaminiani, hawajuani kivile!

Hii kitu ni kweli au ni mfumo kama tu wa TAMISEMI au taasisi zingine?

Sent using Jamii Forums mobile app

hata sisi wakulima hatufahamiani wote na wala hatuaminiani
 
Sasa wakijuana na kutengeneza mtandao usalama utakuwepo kweli? Lazima wasijuane! Na kila mtu anareport kwa bosi wake mmoja na anapokea maelekezo kutoka chanzo kimoja!

Kwenye utendaji wanaweza kujuana lakini wachache sana labda 2 au 3 na tena ujui nani anamchunguza nani?

Tena unakuta mwingine kazi yake ni kuchunguza mienendo ya mwenziwe na kureport basi! Hata hivyo kwa ngazi za chini maslahi hakuna na unatakiwa huwe mzalendo na kujitolea kwasaana!

Ngazi za juu familia yako inaweza kutumiwa kukuwajibisha kama utazingua na unakuwa unajua hilo! Kwa ufupi sio kazi nzuri kama watu wanavyodhani! Sikushauri!
True, sio kaz nzuri kama tunavyo dhania
 
Jamanieee hao usalama ni watu wa kawaida tu (hususani hawa wa hapa kwetu)

Tofauti kubwa iliyopo ni kwamba wanafanya shughuli zao kwa SIRI. Hapo ndio nguvu yao ilipo.

Hata wewe ukiweka maisha yako PRIVATE watu watakuwa wanakuogopa kwa kuwa hawakujui vizuri.

Hata Secret Societies kama Illuminati, Freemasonry, Klu Kla Klux et al zinatumia USIRI kama mbinu mojawapo.

Sababu nyingine: Kwa kuwa CCM inawatumia sana, hivyo imewapa nguvu fulani ( kuwaweka juu ya sheria kwa raia ) kiasi kwamba hata akikuonea huwezi kumfanya chochote.

Suala la kutoaminiana ni kawaida tu kwenye mambo ya ulinzi na usalama, hata walinzi hawaaminiani.

Na kuhusu kutojuana ni kawaida pia, hata mwalimu hajuani na walimu wote nchi nzima unless mmekuwa assigned sehemu moja.

Wanaruhusiwa pia kuwa na vifaa/silaha ambazo wewe raia huruhusiwi kuwa nazo kitu kinachowapa nguvu dhidi ya raia!

Mambo mengine yote ni yale yale.

Kwa kuongeza, nimewahi kuwa lindo moja na Hawa jamaa kwanza walikuwa wanalala tu, maana walikuja na tent na kitanda kikawekwa ndani. Bastola walikuwa wanakabidhiana ( taking and handing over ).
Kumbe wewe ni askari?
 
Si kweli kwamba wote hawajuani, Hata Mwalimu aliyopo Tandahimba anaweza asimjue Mwalimu aliyopo Rorya!
Mifumo yao ya uendaji kazi ndiyo inaweza kuwatenganisha na kuonekana kila mmoja yupo kivyake. Na katika serikali zetu hapa TZ hawa jamaa wapo au wanaweza kuwa wapo katika kila idara, taasisi au kitengo; ndiyo hapo watu huona kama hawajulikani..!
 
Mbona hata members wa jamiiforums ni tiss kwan humu kuna mtu ananijua naitwa nani? nakaa wapi? umri wangu? Watoto wangapi? Wake wa ngap? Kazi yangu? Tupige kifua wana jf tuseme na sisi tiss
Hapa bosi wetu ni Max na timu yake 🤣 🤣 🤣
 
Ni sahihi kabisa mkuu!! Zamani walipenda Sana kutumia special schools kuwapata vijana!!

Siku hizi Ni kujuana na uccm zaidi

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
Mh sasa wanawezaje kutumiki mabwana wawili yaana ccm na state?
 
Back
Top Bottom