Ni kweli Vatican wanakataa kumpa Uaskofu Padri Kitima baada ya kupata tetesi anataka kugombea ubunge kupitia CHADEMA?

Mnaosoma hii mada msifikiri mleta mada ni mtu asiejua, bali ni liccm lililopanga tu kumchafua fr. Kitima na Chadema kwa wakati mmoja.
 
Ujinga mtupu. Kanisa Katoliki la Tanzania halijawahi kuruhusu mtumishi wake kushiriki Active Politics. Hilo halina ukweli.
 
La kuhamia Chadema au kuwa Mwana Chadema sina uhakika hata Mimi. Lakini, kwa tunaomjua Father Dr. Kitima ni mtu anayependa sana kudhani yeye yupo sahihi na wengine hawajui. Na hiyo imemfanya kuikosoa sana Serikali mara kwa mara alipokuwa VC wa SAUT. Nakumbuka aliwahi kuinanga vibaya Serikali jukwaani pale Raila Odinga Square Mgeni Rasmi akiwa Waziri wa Miundombinu wakati huo John Pombe Joseph Magufuli. Naye Magufuli alipokuja kuongea hakumkopesha. Alimpa za uso ndio maana Mwamba alipokuwa madarakani Father alitulia kimya, akimjua vyema jamaa!
 
Kanisa Katoliki haligawi u Askofu kama pipi. Wataka haukuwa na Fr kitima bali msimamo wa baraza la maaskofu Tz, yeye kama Katibu Mkuu alitimiza wajibu wake.
 
Vatcan syo lumumba.

over
 
Kwanza mtoe maada unaonyesha dhahiri shahiri una chuki na husda na Fr kitima
1)Mchakato wa kumpata Askofu ni Siri may be anayejuwa cardinal na watu wake wa vetting je? aliyekuambia ni mmoja wa hao watu? Naomba jibu
2)Hakuna kiongozi wa dini yoyote anayekatazwa kuwa mshauri wa kiroho wa kiongozi wa kisiasa au kiongozi wa serikali
3)Fr kitima angejihusisha na siasa hadi sasa asingekuwa padri angevuliwa kama wengine walivofanyia sitaki kutaja Majina RC wako smart sanaa na miongozo yao
4)Fr kitima hana mamlaka yakuandika waraka au kutoa tamko lolote linalohusu kanisa bila baraka ya Baraza la maaskofu(kama ilivyo kwa msemaji wa Raised) ila ana uhuru wakutoa maoni yake personal kwa Serikali au jamii kama wafanyavyo wengine
5)Tuhuma Za kusema yeye ni Chadema hajaaza leo hata mwemyewe Fr kitima aliwahi sema kwenye kongamano la maridhiano nenda u tube utamsikia
NB usipende kusikia maneno yavijiweni na kufanyia kazi fanya utafiti Kwanza,
 
Kumfanya kitima awe mbunge na waziri si ni sehemu ya intelijensia. Wanamuweka serikalini ili wapate kwa urahisi, habari za serikali
 
Mbona huwa anasema kwa msimamo wake watu wanasema anataka kugombea ubunge Chadema na huwa anasema hawezi kufanya kitu cha namna hiyo? Kwani agombee ubunge anakosa nini, posho au heshima?
 
Mzee mbowe ni jitu la ovyo saana ,siku hizi akishiriki msiba wowote ule huwa anasemaga kuwa marehemu alikuwa ni mshauri wake
 
Mnaosoma hii mada msifikiri mleta mada ni mtu asiejua, bali ni liccm lililopanga tu kumchafua fr. Kitima na Chadema kwa wakati mmoja.
Mimi ni Chadema kindakindaki
 
Kama ambavyo wengi hatumjui Kristo vizuri pia hatulijui Kanisa Katoliki.
 
Kwani lazima awe Askofu?
 
Kama kweli anataka kugombea ubunge sidhani kama atajali kupewa uaskofu au la.
Maana akishaamua hivyo hataweza tena kuwa padri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…